Kama tunataka kuwaandaa viongozi wa CHADEMA kuwa viongozi wa taifa wawajibikaji, ni LAZIMA tuwawajibishe kuanzia sasa kwa maamuzi yao yote yanayokosa busara.
Ndugu wasomaji,
Tumeshuhudia jinsi nchi yetu ilivyokumbwa na vurugu za kisiasa jijini Arusha. Katika vurugu hizo damu ilimwagika. Ni wakati wa masikitiko makubwa kwa nchi yetu na vilevile ni wakati wa tafakuri na mafunzo muhimu. Je, ni nini kilichopelekea vurugu na kumwagika kwa damu?
Kimsingi mgogoro wa kisiasa ulisafirishwa kwenda Arusha. Chanzo chake ni halmashauri ya Hai. Katika halmashauri hiyo CHADEMA kiliwaorodhesha Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) kuwa wapiga kura katika uchaguzi wa mwenyekiti wa halashauri hiyo. Kuorodheshwa kwao kulikipa CHADEMA nafasi kubwa ya kuweza kushinda uchaguzi huo. Tukumbushane tu, kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Freeman Mbowe (MB) ni mjumbe katika halmashauri hiyo ya Hai. Kwa kutokuelewa sheria ipasavyo wajumbe kutoka CCM walipinga ushiriki wa wabunge hao wa CHADEMA katika uchaguzi wa mwenyekiti wa halmashauri. Hata hivyo wabunge hao wa CHADEMA waliruhusiwa kupiga kura na kumpa ushindi mgombea toka chama hicho. Hivi sasa halmashauri ya Hai inaongozwa na CHADEMA.
Tujifunze katika hili kuwa mwenyekiti wa CHADEMA anatambua kuwa wabunge wa viti maalum wanaweza kusajiliwa katika halmashauri fulani na kukipa chama chao "advantage" katika maamuzi yatakayofanywa katika vikao vya halmashauri hiyo. Katika kufahamu hili ndipo mwenyekiti huyu akawachukua wabunge wake hao wawili ili waweze kushinda uchaguzi. Pingamizi kutoka CCM kisheria halikuwa na nguvu yoyote.
Je, CHADEMA walifanya nini baada ya kukutana na changamoto huko Hai?
Walichokifanya CHADEMA ni kupinga uamuzi wa mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Arusha wa kumruhusu Mh. Mary Chatanda (MB) toka CCM kushiriki katika uchaguzi wa meya wa jiji la Arusha. Kigezo walichokitoa ni kwamba swala hilo si sahihi kisheria.
Tujiulize;
iwapo swala hilo si sahihi kisheria, ni kwanini Mh. Freeman Mbowe (MB) aliwasajiri Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) toka CHADEMA kwenye uchaguzi wa Hai?
Je Mh. Freeman Mbowe (MB) alikuwa anajaribu kuvunja sheria?
Kwa vile waliopinga ushiriki wa wajumbe hao toka CHADEMA huko Hai ni wajumbe toka CCM, je CHADEMA inawatumia wajumbe wa CCM kuwajulisha sheria ya nchi inaruhusu vitu gani?
Iwapo CHADEMA hawajaridhishwa na maamuzi ya mkurugenzi wa Hai, je, ni sahihi kukataa maamuzi halali ya mkurugenzi wa jiji la Arusha kama majibu kwa mkurugenzi wa Hai?
Kwanini CHADEMA hawakuandamana Hai?
Kimsingi, maamuzi ya mkurugenzi wa jiji la Arusha ni maamuzi sahihi. Na wale wote waliowakatalia Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) kushiriki uchaguzi wa mwenyekiti wa halmashauri huko Hai hawakuwa sahihi - na kwa vitendo, mwenyekiti wa CHADEMA amedhihirisha kulitambua hili.
Kitendo cha wajumbe kutoka CHADEMA kukataa kuchiriki uchaguzi kwa kisingizio cha kuwepo kwa Mh. Mary Chatanda (MB) kama mjumbe kingepelekea jiji la Arusha kushiindwa kupata meya, iwapo mkurugenzi angeendelea kusubiri wajumbe wafikie theluthi mbili. Je, ni kwanini CHADEMA waliona sawa kwa jiji la Arusha kushindwa kufanya uchaguzi wa meya ilhali wakijua kuwa maamuzi ya mkurugenzi kumruhusu mjumbe huyo toka CCM ni sahihi?
Ninaamini CCM hawatajibu tukio hili kwa kuongeza mbunge mwingine wa viti maalum, kwa sababu kwa kufanya hivyo watakuwa wanaweka wananchi wa Arusha katika "political roller-coaster"
Hivi karibuni imeripotiwa kuwa CHADEMA kimeamua kumsajili Mh. Anna Komu (MB) kama mjumbe wa halmashauri ya jiji la Arusha. Maamuzi haya ni sahihi kisheria na yanathibitisha kuwa viongozi wa CHADEMA wanatambua kuwa Mh. Mary Chatanda (MB) ni mjumbe halali kwa sheria za nchi. Hata hivyo viongozi hao hawajaonyesha tabia ya kiung'wana ya angalau kuomba radhi kwa kuupotosha umma wa Arusha. Hii imedhihirisha kuwa viongozi hawa sio watu wawajibikaji.
Wito: CHADEMA kisisikilizwe tena mpaka viongozi wake wakuu waliochochea vurugu zilizosababisha vifo huko Arusha (Dr. Wilbroad Slaa, Mh. Freeman Mbowe, Mh. Ndesamburo, ) watangaze kujiuzuru/ kuomba radhi umma kwa upotoshaji walioufanya.
Kwa nini kisisikilizwe?
CHADEMA kimekuwa chama ambacho viongozi wake wamekuwa wakifanya maamuzi bila kuyafanyia utafiti na tafakuri ya kutosha na inapodhihirika kuwa maamuzi hayo si sahihi wamekuwa wakitafuta lugha za "longolongo" za "ujanjaujanja".
1.Tumeshuhudia wakianzisha mchakato wa kutokumtambua Rais. Walipgundua kuwa uamuzi huo hautekelezeki/ hawawezi kuutekeleza, wakachezacheza na maneno bila kuwaomba radhi wananchi waliowapa support.
2. Tumeshuhudia viongozi wa CHADEMA wakisema kura zao za urais zimeibiwa na mgombea wao akiahidi kuleta vidhibiti vya kuhujumiwa kwenye uchaguzi. Mpaka sasa mgombea huyo wa CHADEMA hajatoa kidhibiti chochote wala hakuomba radhi kwa kutoa ahadi hewa.
3. Tumeshuhudia viongozi na waasisi wa CHADEMA wakiwanyima wanachama wao haki yao ya kikatiba ya kugombea nafasi za uongozi ndani ya chama hicho.
4. Tumeshuhudia viongozi wa CHADEMA wakiwanyima wanawake wanachama wa chama hicho kuchagua wabunge wao wa viti maalum.
5.Tumeshuhudia viongozi wa CHADEMA wakichangamkia kupeleka mchakato wa katiba bungeni. Walipokumbushwa na mwanazuoni Prof. Issa Shivji kuwa kufanya hivyo ni kuukabidhi mchakato huo kwa CCM wamekosa moyo wa kukiri upungufu kwenye mkakati wao huo/ angalau kumshukuru Prof. Shivji kwa angalizo hilo muhimu.
6.Leo tunashuhudia CHADEMA ikipeleka mbunge katika halmashauri ya jiji la Arusha jambo ambalo walipinga lisifanywe na CCM.
Je ni lini tutaanza kuwawajibisha viongozi wa CHADEMA?
Kama tunataka kuwaandaa viongozi wa CHADEMA kuwa viongozi wa taifa wawajibikaji, ni LAZIMA tuwawajibishe kuanzia sasa kwa maamuzi yao yote yanayokosa busara.
crap
Upupu? Unawasha.
REAL CRAAAAAPPPPPP!!!!! - Umekosa kabisaaa kitu cha kuandika, c'mmon! on a serious note why have you spent so much time doing crazy type of analysis instead of using your precious time to do some productive work?????? - PSE PSE usirudie tena!!!! :frusty:
Kweli mtu anatumia muda mwingi na nguvu nyingi sana kuandika upupu na isitoshe ametumia saa nzima kufanya editing ya hiyo crap yake.
crap
mtu anayetoa maoni kama haya ya propaganda kuilinda ccm bila kuangalia upande mwingine ama amepewa vihela vya kujikimu na kuuza utu wake au ana mtindio wa ubongo maana haelewi. wewe umepata hela au upo mentally challenged?
Pombe bila chakula ni noma!Kwanza ni upuuzi anaandika huyu bwana! halina hata uhakika na vitu linaandika bc tu akishalewa yanayokuja anaangukia keyboard! HAI waandamane kwa ajili gani? madiwani wa CHADEMA HAI walidanganywa kuwa kuna kikao sehemu flani wakaenda alafu wa ccm wakafanya uchaguzi?? maandamano ya arusha ni pamoja na huo unyama wa kuwaadaa wabungge na madiwani wa CHADEMA kuwa kuna kikao olasiti na madiwani wa ccm kufanya uchaguzi wa meya bila hata aibu!! alafu unakuja kutuandikia LOVE STORY huku! naomba msichokoze watu
MANY HANDS MAKE THE LOAD LIGHTER
Inawezekana wewe hujui kuwa wajumbe toka CHADEMA walisusia mkutano wa kuchagua meya. Jambo hilo maana yake ni kwamba jiji la Arusha lisiwe na meya. Mkurugenzi hakuruhusu hali ya jiji la Arusha kushindwa kuwa na meya. Nampongeza kwa uamuzi huo. Je, wajumbe wa CHADEMA walikuwa na sababu ya msingi kususia uchaguzi huo wa meya?Kwanza ni upuuzi anaandika huyu bwana! halina hata uhakika na vitu linaandika bc tu akishalewa yanayokuja anaangukia keyboard! HAI waandamane kwa ajili gani? madiwani wa CHADEMA HAI walidanganywa kuwa kuna kikao sehemu flani wakaenda alafu wa ccm wakafanya uchaguzi?? maandamano ya arusha ni pamoja na huo unyama wa kuwaadaa wabungge na madiwani wa CHADEMA kuwa kuna kikao olasiti na madiwani wa ccm kufanya uchaguzi wa meya bila hata aibu!! alafu unakuja kutuandikia LOVE STORY huku! naomba msichokoze watu
MANY HANDS MAKE THE LOAD LIGHTER
Ndugu wasomaji,
Tumeshuhudia jinsi nchi yetu ilivyokumbwa na vurugu za kisiasa jijini Arusha. Katika vurugu hizo damu ilimwagika. Ni wakati wa masikitiko makubwa kwa nchi yetu na vilevile ni wakati wa tafakuri na mafunzo muhimu. Je, ni nini kilichopelekea vurugu na kumwagika kwa damu?
Kimsingi mgogoro wa kisiasa ulisafirishwa kwenda Arusha. Chanzo chake ni halmashauri ya Hai. Katika halmashauri hiyo CHADEMA kiliwaorodhesha Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) kuwa wapiga kura katika uchaguzi wa mwenyekiti wa halashauri hiyo. Kuorodheshwa kwao kulikipa CHADEMA nafasi kubwa ya kuweza kushinda uchaguzi huo. Tukumbushane tu, kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Freeman Mbowe (MB) ni mjumbe katika halmashauri hiyo ya Hai. Kwa kutokuelewa sheria ipasavyo wajumbe kutoka CCM walipinga ushiriki wa wabunge hao wa CHADEMA katika uchaguzi wa mwenyekiti wa halmashauri. Hata hivyo wabunge hao wa CHADEMA waliruhusiwa kupiga kura na kumpa ushindi mgombea toka chama hicho. Hivi sasa halmashauri ya Hai inaongozwa na CHADEMA.
Tujifunze katika hili kuwa mwenyekiti wa CHADEMA anatambua kuwa wabunge wa viti maalum wanaweza kusajiliwa katika halmashauri fulani na kukipa chama chao "advantage" katika maamuzi yatakayofanywa katika vikao vya halmashauri hiyo. Katika kufahamu hili ndipo mwenyekiti huyu akawachukua wabunge wake hao wawili ili waweze kushinda uchaguzi. Pingamizi kutoka CCM kisheria halikuwa na nguvu yoyote.
Je, CHADEMA walifanya nini baada ya kukutana na changamoto huko Hai?
Walichokifanya CHADEMA ni kupinga uamuzi wa mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Arusha wa kumruhusu Mh. Mary Chatanda (MB) toka CCM kushiriki katika uchaguzi wa meya wa jiji la Arusha. Kigezo walichokitoa ni kwamba swala hilo si sahihi kisheria.
Tujiulize;
iwapo swala hilo si sahihi kisheria, ni kwanini Mh. Freeman Mbowe (MB) aliwasajiri Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) toka CHADEMA kwenye uchaguzi wa Hai?
Je Mh. Freeman Mbowe (MB) alikuwa anajaribu kuvunja sheria?
Kwa vile waliopinga ushiriki wa wajumbe hao toka CHADEMA huko Hai ni wajumbe toka CCM, je CHADEMA inawatumia wajumbe wa CCM kuwajulisha sheria ya nchi inaruhusu vitu gani?
Iwapo CHADEMA hawajaridhishwa na maamuzi ya mkurugenzi wa Hai, je, ni sahihi kukataa maamuzi halali ya mkurugenzi wa jiji la Arusha kama majibu kwa mkurugenzi wa Hai?
Kwanini CHADEMA hawakuandamana Hai?
Kimsingi, maamuzi ya mkurugenzi wa jiji la Arusha ni maamuzi sahihi. Na wale wote waliowakatalia Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) kushiriki uchaguzi wa mwenyekiti wa halmashauri huko Hai hawakuwa sahihi - na kwa vitendo, mwenyekiti wa CHADEMA amedhihirisha kulitambua hili.
Kitendo cha wajumbe kutoka CHADEMA kukataa kuchiriki uchaguzi kwa kisingizio cha kuwepo kwa Mh. Mary Chatanda (MB) kama mjumbe kingepelekea jiji la Arusha kushiindwa kupata meya, iwapo mkurugenzi angeendelea kusubiri wajumbe wafikie theluthi mbili. Je, ni kwanini CHADEMA waliona sawa kwa jiji la Arusha kushindwa kufanya uchaguzi wa meya ilhali wakijua kuwa maamuzi ya mkurugenzi kumruhusu mjumbe huyo toka CCM ni sahihi?
Ninaamini CCM hawatajibu tukio hili kwa kuongeza mbunge mwingine wa viti maalum, kwa sababu kwa kufanya hivyo watakuwa wanaweka wananchi wa Arusha katika "political roller-coaster"
Hivi karibuni imeripotiwa kuwa CHADEMA kimeamua kumsajili Mh. Anna Komu (MB) kama mjumbe wa halmashauri ya jiji la Arusha. Maamuzi haya ni sahihi kisheria na yanathibitisha kuwa viongozi wa CHADEMA wanatambua kuwa Mh. Mary Chatanda (MB) ni mjumbe halali kwa sheria za nchi. Hata hivyo viongozi hao hawajaonyesha tabia ya kiung'wana ya angalau kuomba radhi kwa kuupotosha umma wa Arusha. Hii imedhihirisha kuwa viongozi hawa sio watu wawajibikaji.
Wito: CHADEMA kisisikilizwe tena mpaka viongozi wake wakuu waliochochea vurugu zilizosababisha vifo huko Arusha (Dr. Wilbroad Slaa, Mh. Freeman Mbowe, Mh. Ndesamburo, ) watangaze kujiuzuru/ kuomba radhi umma kwa upotoshaji walioufanya.
Kwa nini kisisikilizwe?
CHADEMA kimekuwa chama ambacho viongozi wake wamekuwa wakifanya maamuzi bila kuyafanyia utafiti na tafakuri ya kutosha na inapodhihirika kuwa maamuzi hayo si sahihi wamekuwa wakitafuta lugha za "longolongo" za "ujanjaujanja".
1.Tumeshuhudia wakianzisha mchakato wa kutokumtambua Rais. Walipgundua kuwa uamuzi huo hautekelezeki/ hawawezi kuutekeleza, wakachezacheza na maneno bila kuwaomba radhi wananchi waliowapa support.
2. Tumeshuhudia viongozi wa CHADEMA wakisema kura zao za urais zimeibiwa na mgombea wao akiahidi kuleta vidhibiti vya kuhujumiwa kwenye uchaguzi. Mpaka sasa mgombea huyo wa CHADEMA hajatoa kidhibiti chochote wala hakuomba radhi kwa kutoa ahadi hewa.
3. Tumeshuhudia viongozi na waasisi wa CHADEMA wakiwanyima wanachama wao haki yao ya kikatiba ya kugombea nafasi za uongozi ndani ya chama hicho.
4. Tumeshuhudia viongozi wa CHADEMA wakiwanyima wanawake wanachama wa chama hicho kuchagua wabunge wao wa viti maalum.
5.Tumeshuhudia viongozi wa CHADEMA wakichangamkia kupeleka mchakato wa katiba bungeni. Walipokumbushwa na mwanazuoni Prof. Issa Shivji kuwa kufanya hivyo ni kuukabidhi mchakato huo kwa CCM wamekosa moyo wa kukiri upungufu kwenye mkakati wao huo/ angalau kumshukuru Prof. Shivji kwa angalizo hilo muhimu.
6.Leo tunashuhudia CHADEMA ikipeleka mbunge katika halmashauri ya jiji la Arusha jambo ambalo walipinga lisifanywe na CCM.
Je ni lini tutaanza kuwawajibisha viongozi wa CHADEMA?
Kama tunataka kuwaandaa viongozi wa CHADEMA kuwa viongozi wa taifa wawajibikaji, ni LAZIMA tuwawajibishe kuanzia sasa kwa maamuzi yao yote yanayokosa busara.
Hili Baraza limevamiwa na malimbukeni wa siasa!
wewe ni m*w*ehu tu.
umechelewa.
WaTz tunajua muyawazayo hata kabla hamjayatamka.
haturudi nyuma!!
REAL CRAAAAAPPPPPP!!!!! - Umekosa kabisaaa kitu cha kuandika, c'mmon! on a serious note why have you spent so much time doing crazy type of analysis instead of using your precious time to do some productive work?????? - PSE PSE usirudie tena!!!! :frusty:
Kiongozi,kwa nini hoja zake zisijibiwe kwa hoja. Je ni kweli cdm waliwatumia wabunge wateuli kule katika halimashauri ya hai, na ilikuwa halali kisheria ama la. Na ccm walikuwa na nafasi gani kisheria kumtumia mbunge wao wa kuteuliwa.
Kubwa sheria inasemaje kuhusiana na sakata hili??
Hili Baraza limevamiwa na malimbukeni wa siasa!
ilikuwa siku haijaisha kabla ya wewe kuja kujaza mahaba upofu yako hapa.
Ndugu wasomaji,
Tumeshuhudia jinsi nchi yetu ilivyokumbwa na vurugu za kisiasa jijini Arusha. Katika vurugu hizo damu ilimwagika. Ni wakati wa masikitiko makubwa kwa nchi yetu na vilevile ni wakati wa tafakuri na mafunzo muhimu. Je, ni nini kilichopelekea vurugu na kumwagika kwa damu?
Kimsingi mgogoro wa kisiasa ulisafirishwa kwenda Arusha. Chanzo chake ni halmashauri ya Hai. Katika halmashauri hiyo CHADEMA kiliwaorodhesha Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) kuwa wapiga kura katika uchaguzi wa mwenyekiti wa halashauri hiyo. Kuorodheshwa kwao kulikipa CHADEMA nafasi kubwa ya kuweza kushinda uchaguzi huo. Tukumbushane tu, kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Freeman Mbowe (MB) ni mjumbe katika halmashauri hiyo ya Hai. Kwa kutokuelewa sheria ipasavyo wajumbe kutoka CCM walipinga ushiriki wa wabunge hao wa CHADEMA katika uchaguzi wa mwenyekiti wa halmashauri. Hata hivyo wabunge hao wa CHADEMA waliruhusiwa kupiga kura na kumpa ushindi mgombea toka chama hicho. Hivi sasa halmashauri ya Hai inaongozwa na CHADEMA.
Tujifunze katika hili kuwa mwenyekiti wa CHADEMA anatambua kuwa wabunge wa viti maalum wanaweza kusajiliwa katika halmashauri fulani na kukipa chama chao "advantage" katika maamuzi yatakayofanywa katika vikao vya halmashauri hiyo. Katika kufahamu hili ndipo mwenyekiti huyu akawachukua wabunge wake hao wawili ili waweze kushinda uchaguzi. Pingamizi kutoka CCM kisheria halikuwa na nguvu yoyote.
Je, CHADEMA walifanya nini baada ya kukutana na changamoto huko Hai?
Walichokifanya CHADEMA ni kupinga uamuzi wa mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Arusha wa kumruhusu Mh. Mary Chatanda (MB) toka CCM kushiriki katika uchaguzi wa meya wa jiji la Arusha. Kigezo walichokitoa ni kwamba swala hilo si sahihi kisheria.
Tujiulize;
iwapo swala hilo si sahihi kisheria, ni kwanini Mh. Freeman Mbowe (MB) aliwasajiri Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) toka CHADEMA kwenye uchaguzi wa Hai?
Je Mh. Freeman Mbowe (MB) alikuwa anajaribu kuvunja sheria?
Kwa vile waliopinga ushiriki wa wajumbe hao toka CHADEMA huko Hai ni wajumbe toka CCM, je CHADEMA inawatumia wajumbe wa CCM kuwajulisha sheria ya nchi inaruhusu vitu gani?
Iwapo CHADEMA hawajaridhishwa na maamuzi ya mkurugenzi wa Hai, je, ni sahihi kukataa maamuzi halali ya mkurugenzi wa jiji la Arusha kama majibu kwa mkurugenzi wa Hai?
Kwanini CHADEMA hawakuandamana Hai?
Kimsingi, maamuzi ya mkurugenzi wa jiji la Arusha ni maamuzi sahihi. Na wale wote waliowakatalia Mh. Lucy Owenya(MB) na Mh. Grace Kihwelu (MB) kushiriki uchaguzi wa mwenyekiti wa halmashauri huko Hai hawakuwa sahihi - na kwa vitendo, mwenyekiti wa CHADEMA amedhihirisha kulitambua hili.
Kitendo cha wajumbe kutoka CHADEMA kukataa kuchiriki uchaguzi kwa kisingizio cha kuwepo kwa Mh. Mary Chatanda (MB) kama mjumbe kingepelekea jiji la Arusha kushiindwa kupata meya, iwapo mkurugenzi angeendelea kusubiri wajumbe wafikie theluthi mbili. Je, ni kwanini CHADEMA waliona sawa kwa jiji la Arusha kushindwa kufanya uchaguzi wa meya ilhali wakijua kuwa maamuzi ya mkurugenzi kumruhusu mjumbe huyo toka CCM ni sahihi?
Ninaamini CCM hawatajibu tukio hili kwa kuongeza mbunge mwingine wa viti maalum, kwa sababu kwa kufanya hivyo watakuwa wanaweka wananchi wa Arusha katika "political roller-coaster"
Hivi karibuni imeripotiwa kuwa CHADEMA kimeamua kumsajili Mh. Anna Komu (MB) kama mjumbe wa halmashauri ya jiji la Arusha. Maamuzi haya ni sahihi kisheria na yanathibitisha kuwa viongozi wa CHADEMA wanatambua kuwa Mh. Mary Chatanda (MB) ni mjumbe halali kwa sheria za nchi. Hata hivyo viongozi hao hawajaonyesha tabia ya kiung'wana ya angalau kuomba radhi kwa kuupotosha umma wa Arusha. Hii imedhihirisha kuwa viongozi hawa sio watu wawajibikaji.
Wito: CHADEMA kisisikilizwe tena mpaka viongozi wake wakuu waliochochea vurugu zilizosababisha vifo huko Arusha (Dr. Wilbroad Slaa, Mh. Freeman Mbowe, Mh. Ndesamburo, ) watangaze kujiuzuru/ kuomba radhi umma kwa upotoshaji walioufanya.
Kwa nini kisisikilizwe?
CHADEMA kimekuwa chama ambacho viongozi wake wamekuwa wakifanya maamuzi bila kuyafanyia utafiti na tafakuri ya kutosha na inapodhihirika kuwa maamuzi hayo si sahihi wamekuwa wakitafuta lugha za "longolongo" za "ujanjaujanja".
1.Tumeshuhudia wakianzisha mchakato wa kutokumtambua Rais. Walipgundua kuwa uamuzi huo hautekelezeki/ hawawezi kuutekeleza, wakachezacheza na maneno bila kuwaomba radhi wananchi waliowapa support.
2. Tumeshuhudia viongozi wa CHADEMA wakisema kura zao za urais zimeibiwa na mgombea wao akiahidi kuleta vidhibiti vya kuhujumiwa kwenye uchaguzi. Mpaka sasa mgombea huyo wa CHADEMA hajatoa kidhibiti chochote wala hakuomba radhi kwa kutoa ahadi hewa.
3. Tumeshuhudia viongozi na waasisi wa CHADEMA wakiwanyima wanachama wao haki yao ya kikatiba ya kugombea nafasi za uongozi ndani ya chama hicho.
4. Tumeshuhudia viongozi wa CHADEMA wakiwanyima wanawake wanachama wa chama hicho kuchagua wabunge wao wa viti maalum.
5.Tumeshuhudia viongozi wa CHADEMA wakichangamkia kupeleka mchakato wa katiba bungeni. Walipokumbushwa na mwanazuoni Prof. Issa Shivji kuwa kufanya hivyo ni kuukabidhi mchakato huo kwa CCM wamekosa moyo wa kukiri upungufu kwenye mkakati wao huo/ angalau kumshukuru Prof. Shivji kwa angalizo hilo muhimu.
6. Tumeshuhudia viongozi wa CHADEMA wakitoa tamko la kutokuhudhuria mahakamani kusikiliza kesi waliyoshitakiwa. Viongozi wanaotegemewa kuonyesha mfano wa kutii utawala wa sheria wanaonyesha dharau kwa mahakama!
7.Leo tunashuhudia CHADEMA ikipeleka mbunge katika halmashauri ya jiji la Arusha jambo ambalo walipinga lisifanywe na CCM.
Je ni lini tutaanza kuwawajibisha viongozi wa CHADEMA?
Kama tunataka kuwaandaa viongozi wa CHADEMA kuwa viongozi wa taifa wawajibikaji, ni LAZIMA tuwawajibishe kuanzia sasa kwa maamuzi yao yote yanayokosa busara.