CHADEMA kina wanachama wangapi?

Kamwe cdm isitarajie kuongoza nchi kwa sanduku la kura,kwani in wafuasi wakujaza mikutano lakini si wapiga kura.
HILO TUMELIONA 2010 NA MWEZI WA OKTOBA 2012 KWENYE CHAGUZI ZA MADIWANI.

Sijatoa comment maana nimetoka kutoa comment kwenye mada nyingine niliyoipitia karibuni ikieleza hayo kwa mapana zaidi kama ifuatavyo hapo chini. Inaonekana kuna ukweli mikutano ya Chadema kujaa mashabiki badala ya wapiga kura kama tunavyoona kampeni na matokeo ya chaguzi zinazotokea nchini. Mtoa mada nadhani ni Candid.

 
Hivi tulivyokuwa tunawaambia ukubwa wa pua sio wingi wa makamasi mlikuwa hamtuelewi?

Chadema hakina viongozi wa maana, asilimia kubwa wana matatizo ambayo Watanzania wengi wanayatazama kwa mtazamo hasi.
 
Mbona hamuongelei the fact kuwa chadema haijapoteza nafasi ya udiwani hata moja, na kuwa imepokonya ccm nafasi zake za udiwani japo kwa uchache.
Sio mafanikio makubwa sana lakini.pia sio loss. Ccm is loosing the grip.
 
Hivi tulivyokuwa tunawaambia ukubwa wa pua sio wingi wa makamasi mlikuwa hamtuelewi?

Chadema hakina viongozi wa maana, asilimia kubwa wana matatizo ambayo Watanzania wengi wanayatazama kwa mtazamo hasi.
ohooo!!!! Gaidi ndani ya nyumba
 
Namkubali MM kwa makala zake mbali mbali, anao uhuru wa kimawazo pamoja na uhuru mwingine wowote kama binadamu. Ila kila mwanadamu ana utashi wake na ni vigumu kuwahi kupenda kitu halafu ukakichukia ghafla, labda uwe umefanyiwa kitu ambacho hakisameheki.

MM ni mwana NYINYIEM, hivyo ataendelea kukikosoa chama chake akiwa na ndoto kuwa siku mojakitabadilika. Ni muhimu kwa CDM kuwa na wanchama wake ili kuona inaungwa mkono kwa thati kiasi gani, lakini kwa angalizo kuwa NYINYIEM imekuwa ikipandikiza wanachama upande wa upinzani ili kuwavuruga.

Hivyo hili la wanachama linakuwa na walakini kidogo. Ushindi wa CDM unahitaji ushawishi wa wanachama wa vyama vingine pamoja na wasio na vyama. RE: uchaguzi wa 2010.
 
Wana Bodi hii ni sehemu ya andiko zito sana kwa wana CDM kutoka kwa Dkt. Kitila Mkumbo. Nimeona nilimwage hapa jamvini ili tuone ni kwa kiwango gani CDM inaweza kukata kiu ya Wanamageuzi wengi wanaotaka kuona mwaka 2015 kunakuwa na mabadiliko ya kiuongozi na hatimaye mfumo mbovu uliopo. Ni vema ukalisoma kwa umakini sana na kutafakari.

Chama cha siasa hupitia hatua kuu nne katika kufikia hatua ya kushinda uchaguzi. Hatua ya kwanza ni ya kisheria ambapo chama kinatambulika kisheria kwa kusajiliwa rasmi na kuruhusiwa kufanya shughuli za kisiasa.

Hatua ya pili ni kujulikana kwa wapiga kura, kwamba kuna chama cha siasa na kina viongozi fulani. Juhudi za viongozi katika kukiuza chama chao hukifisha chama hicho katika hatua ya tatu ambayo ni ufuasi. Ufuasi wa chama cha siasa huonekana katika mazungumzo ya kila siku ya wananchi na kwa jinsi wananchi hao wanavyoitikia mikutano na shughuli nyingine za umma kama vile kukichangia chama hicho.

Hatua ya mwisho ni kubadilisha idadi fulani ya wafuasi kuwa wafia chama, ambao ndio wanaoweza kukipatia chama ushindi, hasa katika mazingira makali ya ushindani.

Kwa sasa hivi hakuna shaka kwamba CHADEMA wameweza kupata wafuasi wengi kama inavyoonekana katika mazingira mbalimbali. Katika mazungumzo ya kila siku linapokuja suala la siasa unaona hamasa ya Watanzania kwa CHADEMA.

Kwa wale waliowahi kusafiri na gari mpya za CHADEMA (M4C) watakumbuka jinsi ambavyo wananchi huhamasika barabarani mara wazionapo gari hizi kwa kuonyesha vidole viwili. Madereva wa malori na mabasi ya abiria hawasiti kupiga honi mara wazionapo gari hizi, na hata baadhi ya askari wa barabarani hudiriki kuonyesha vidole viwili mara wazionapo gari hizi zikipita.

Mikutano ya CHADEMA imebadilika kabisa kutoka enzi za akina Mzee Mtei kuhutubia ‘miti' na sasa mikutano hiyo ikijaza maelfu kwa maelfu ya wananchi waliojaa hamasa na hamu kubwa ya mabadiliko.

Hata hivyo, bado CHADEMA hawajifikia hatua ya nne, ambayo ni muhimu sana katika kujihakikishia ushindi. Hatua hii ni ile ya kupata wafia chama. Ili kujihakikishia ushindi ni muhimu kabisa chama cha siasa kiwe na wanachama wafia chama.

Hawa ni aina ya wanachama ambao watakipigia kura wakati wowote iwe mvua, iwe jua. Hili ni kundi muhimu sana kujihakikishia ushindi katika mazingira ambayo wananchi wengi hawajitokezi kupiga kura, ambalo limeanza kuwa jambo la kawaida katika chaguzi zetu.

Ni kundi hili ndilo ambalo limebaki kama mpira wa kupumulia kwa CCM. Hawa ni watu ambao hawatakuja kamwe kugundua ubaya wa CCM hadi kitakapotoka madarakani na ni kundi hili ambalo limeiwezesha CCM kushinda katika uchaguzi wa madiwani uliokamilika wiki jana, ambapo katika baadhi ya kata idadi ya wapiga kura waliojitokeza walikuwa chini ya asilimia 20.

Nahitimisha kwa kutoa wito kwa wapenda mabadiliko. Kwamba kupenda na kutamani tu mabadiliko hakutoshi, inabidi kushiriki katika kuyasaka hayo mabadiliko. Tabia ya baadhi ya wapenda mabadiliko kudhani kwamba kikundi fulani cha watu katika chama fulani ndio wenye jukumu la kuleta mabadiliko itatufanya tukae katika mfumo wa utawala tuliouchoka kwa muda mrefu.

Makala nzima unaweza kuisoma hapa; Raia Mwema - CHADEMA inakua, CCM inasinyaa, lakini kwa kasi ndogo!


My Take
Huu wimbo wa CDM kujipanga mbona umekuwa ukiimbwa muda mrefu sana lakini hatuoni strategies za uhakika na za kudumu? Je kwa muda huu uliobaki nini kitaweza kufanyika ili kuiondoa CCM madarakani kwa maana ya kuifanya CDM kuwa na wanachama wake wa uhakika na kuweza kuipigia kura kiasi cha kuipiku CCM? Si kwambahata wana JF wengi ni wafuasi tu wa CDM na si watu walio tayari kukifia chama? Kazi kubwa inahitajika
 
Majibu ya maswali yako ngojo utokee uchaguzi mgodo utayapata Sumbawanga na Igunga, ama yoyote wa magamba arest in peace ila subri mziki wa 2015...
 
Chadema ni upepo tu kama upepo mwingine na utapita Kama Nccr
 
hata ccm haina wafia chama wa kutosha kama makala inavyotaka tuamini.sidhani kama ni hulka ya mtanzania kuwa mfia chama.wafia chama watatokea baadae na sio sasa.hata kama chadema ingekuwa na wafia chama wa kutosha lazima ungefika wakati wa kushawishi ''wafuasi'' au wasiokuwa na upande,kwa chadema wakati huo ni sasa na hakuna kisingizio wala sababu za msingi za kusema haiwezekani.it is a DO or DIE 2015
 
Majibu ya maswali yako ngojo utokee uchaguzi mgodo utayapata Sumbawanga na Igunga, ama yoyote wa magamba arest in peace ila subri mziki wa 2015...

Mkuu hayo ni maoni ya Kitila Mkumbo na ni mema sana kwa CDM ndiyo maana nimeyaweka hapa jamvini.Anachosisitiza ni haja ya CDM kuwa na wanachama ambao piga ua ni wapigakura wa uhakika dhidi ya CCM. Kwa maneno mengine kwa sasa CCM imechokwa lakini inasafiria nguvu ya wanachama wa aina hiyo (yaani ambao piga ua wataipigia kura tu).

Kazi ya CDM ni kuwa na database hiyo. Chukulia mfano CDM ikiwa na wanachama wa uhakika na watakaoipigia kura Milioni 3.Huu si mtaji mkubwa sana kwa chama? Kitabaki kinatafuta idadi ndogo sana ili kushika dola.
 
mi nawashangaa ccm wanashindwa kuchukua simple logic waliopiga juzi na chaguz zote za hivi karibun ni wale walioandikishwa 2010 tena wengi ni wazee na bado kuna matokeo chanya mengi kwa CDM. subirin daftari jipya na vijana wote hawa wawe kwenye daftari uone mzik wake
 
salaam sana wakuu,

Mimi ni mmoja wa mashabiki wa Chadema na najiita shabiki kwasababu sii mwanachama wa CDM japo naipenda kwa moyo wangu wote baada ya kugundua wana nia ya dhati ya kuleta mabadiliko Tanzania.

Mimi ni mmoja kati ya waliokuwepo Furahisha jana na idadi kubwa ya waliokuwepo pale si wanachama kwani hawana kadi.na wengi walikuwa wanatamani kununua kadi pasipokujua pa kuzipata nimeanzisha uzi huu ili nitoe ushauri kwa chama kuuza kadi na katiba kwa njia ifutayo.

1.katika kila mkutano wa hadhara kuwe na meza mbili au tatu maalum kwa ajili ya kuuza kadi na katiba za chama,na hili linaweza kufanyika kabla na baada ya mgeni rasmi kuhutubia.
naomba kuwasilisha
 
Mkuu nimekusoma, ila natofautiana na wewe kimtizamo; Kama wewe ni shabiki wa CHEDEMA basi hutufai na nashawishika kusema kusema wewe ni masalia au pandikizi.

Ni vyema ukafahamu ndani ya CHADEMA kuna wapenzi wa CHADEMA na siyo mashabiki kama unavyotaka kutuaminisha kwenye post yako. Funguka njomba Mashabiki wapo CCM na ndo maana wapo kima-slahi zaidi.
 
Haya mkuu..wahusika wamekusikia naamini watalifa nyia kazi
Tumaini Makene pita kwa kipande hii uchukue hii........
 
Last edited by a moderator:

cdm ni wajanja sana ,hawa washabiki wanawapa sana viroba mkuu ,ndio maana kwenye mikutano ya cdm vijana wanakuwa hawajitambui
 
Ndio wafanye utaratibu wa kuwafanya mashabiki wawe wanachama na kukusanya wanachama zaidi ili come 2015 wavune kura nyingi.
 
mkuu master peace,kama huna kadi ya chama wewe ni shabiki tu,japo unaweza kupiga kura kwa hicho chama na kuudhuria mikutano na kadhalika,kama mimi ni shabiki wa simba na sikosi kuwashabikia au kuwatetea vijiweni na wote wananijua hivyo ila sina kadi ya uanachama simba.nachotaka chama kiweke utaratibu wa kuuza kadi kwenye mikutano ya hadhara.
 
Kwa jinsi dunia ilivyobadilika kwa sasa naona tuanze kuwaza kuwa uanachama sio lazima kuwa na kadi. Vyama vya siasa vitafute namna ya kusajili wanachama wake na kutunza kumbukumbu. Mfano nina kadi za benki zaidi ya nne, nina kadi ya bima za afya, kitambulisho cha kazi, cha mpiga kura, leseni ya udereva, leseni ya biashara, tin number na mizigo mingine ya kadi kibao,,,, halafu unaongeza na kadi ya uanachama wa chama cha siasa, kadi ya uanachama wa timu ya mpira wa miguu, timu ya mpira wa kikapu, timu ya mpira wa pete,,,,, pia unazo za uanachama wa saccos, vicoba nk... Kwa kifupi unakuwa na mafile kibao.

Ushauri wangu ni kuwa CDM watafute utaratibu wa kupata wanachama wao kwenye ngazi za chini, mtaa au kata ambako ndio mtu unaenda kujiandikisha. Kumbukumbu yako inaweza kuwa namba ya uanachama na namba ya simu ambayo chama kitaitumia kukutafuta kama kuna mkutano au maandamano au kazi za kujitolea au kazi za ujenzi wa taifa, au email adress na hata facebook, twitter account. Unapoenda kununua kadi ya chama kwenye mkutano mkubwa kama ule wa jana Furahisha unakuwa umefuata mkumbo. Mfano wewe unakaa Igoma, badala ya kuchukua kadi yako Igoma unafuata furahisha mkutanoni kwa kuwa Mh Mbowe yupo, then mkutano ukiisha na mwaka mmoja baadaye utailipia wapi hiyo kadi, au utahudhuria mikutano ya tawi gani??

Huu mfumo waasisi wake MaCCM wanasema wana wanachama milioni 7 nchi nzima lakini JK hakufikisha hizo kura milioni 7, umepitwa na wakati. Tena napendekeza uanachama wa chama cha siasa ujumuishwe kwenye kitambulisho cha taifa ambapo kumbukumbu za uanachama zinahifadhiwa halafu unatembea na kitambulisho kimoja kwa matumizi yote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…