Heshima sana wanajamvi.
Nimekaa pale natafakari na kujiuliza mambo mengi sipati majibu.
Natazama hizi kesi za michongo na hukumu za michongo naiona chadema inapitia mkondo ule ule wa NCCR-MAGEUZI.
Ngongo kwasasa Tanga Michungwani.
Mkuu Ngongo heshima kwako.
Bila shaka wewe ni mdau mkubwa wa CHADEMA uliyeshiriki kujenga chama hicho kwa dhamira kubwa kivitendo tofauti na baadhi ya wadau wanavyokuhisi hapa. LAKINI sidhani kama umepatia kulinganisha mkondo inaopitia CHADEMA hivi leo na ule iliopitia NCCR-Mageuzi enzi zile. Labda kama unataka kuonesha kutofurahia kwako jinsi chama kilivyo na kinavyoenenda nyakati hizi.
Muhimu kwako katika uzi wako huu ni kutoa mawazo na mikakati jinsi CHADEMA inavyoweza kuepuka kwenda shimoni (kama unavyoona). Usipoteze muda kujibu michango yenye jazba.
Be positive. Umeleta uzi, utendee haki; toa hitimisho lenye tija.
***********
Binafsi, tangu dola iamue kukamilisha michakato yote ya chaguzi mezani/ofisini na wananchi kutangaziwa matokeo tu, sioni kama CHADEMA wala chama chochote cha siasa kinaweza kufanya shughuli za siasa kwa haki nchini. (Hata CCM wamenywea). Wawakilishi wa wananchi ni wale wanaopitishwa na dola pekee. Ushahidi ni 2019, 2020, na 2024.
Katika mazingira haya, sioni kingine wanachoweza kufanya CHADEMA labda nao waamue kuwasaliti wananchi kama wanavyofanya CCM na vyama vingine washirika wao. Yaani waache kudai marekebisho (reforms) badala yake wapange foleni ya kuomba huruma ya dola kugawiwa viti vya uwakilishi!
Ni mwehu tu ndiye anayeweza kuamini kuwa 2020 CHADEMA ilipata mbunge mmoja (1) tu! Kama ni kuwa shimoni basi CHADEMA ilitumbukia tangu Oktoba 2020. (Linganisha matokeo ya 2015 na 2020).
Nilishangaa baada ya Oktoba 2020 kusikia CCM na serikali bado inatambua CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani nchini huku kikiwa na mbunge mmoja tu na halmashauri 0! Halafu 2021 yanaanzishwa mazungumzo ya "maridhiano" kati ya serikali na CHADEMA! Sitashangaa baada ya Oktoba CHADEMA bado ikiendelea kutambuliwa kama chama kikuu cha upinzani huku Msajili akiendelea kujiumauma kuhusu kuifuta kwenye rejesta!