CHADEMA imemkosea nini huyu mwandishi?

CHADEMA imemkosea nini huyu mwandishi?

Hamna vijana wapuuzi kama wafuasi wa CDM japo nami nimfuasi tu sio mwanachama.

Wanajiona wao Ndio wanahaki ya kutoa maoni, kukosoa, kuhoji, kutukana na kusikilizwa, ila hawana uvumilivu kabisaaaaa endapo watu wasioamini wanachoamini wao wakitoa maoni, wakikosoa, wakihoji, wakitukana wao hawako tayari kusikiliza.

Yule askofu aliyekomaa yuko upande wao hapo ni sawa kabisaaaaa hakuna shida, Wapo waandishi wako upande wao hapo ni sawa hakuna shida. Ila ikitokea askofu anaonekana yuko upande tofauti nao hilo kwao ni tatizo. Ikitokea mwandishi anawakosoa hilo kwao ni tatizo.

Sijui uhuru wa kutoa maoni wanaoulilia kila siku humu wanaufahamu Kweli Au wengi wanafata tu mkumbo na mihemko.
Kama mtu anafikia hatua kuita chadema ni chama cha Mungu na ccm ni chama cha shetani, mpaka utaona utaona jinsi tatizo lilivyo kubwa.

Umeeleza ya kweli kabisa, kuna wengine wao wanaona anayefaa kukosolewa ni chama tawala tu na huwezi kukosoa chama pinzani kwa sababu hakijashika dola na wengine ni kama hawaamini kama chadema hufanya makosa.
 
Jaribu kusoma swali na kulielewa ..jaribu kusoma mfano wa utangulizi nilioweka.. Tuna tofautiana itakadi ni kweli lakini hatuwezi kuzusha hata yasiyo ya kweli kwa kisingizio cha uhuru wa demokrasia.. Huo utakuwa ni upuuzi ujue
Tunakosoa penye shida
Tunasifu panapostahili hizo ndio siasa za ushindani
Huu Sasa ni uongo wa wazi kabisa kwamba chadema inakosoa penye kasoro na kusifia panapostahili? Hii si kweli chadema wanapinga na kuponda kila kitu
 
Maana wafuasi wa Chadema mnaongoza kumtukana Magufuli huku mkijua hawezi kujibu kwasasa
[emoji15][emoji3064][emoji848][emoji848][emoji2827] Nadhani hizi ni tuhuma mpya zisizo na ithibati
Hivi yeyote anayemtukana Magufuli ni mfuasi wa Chadema?.
Kuna wafuasi wa vyama tofauti tofauti humu,hivi unawatofautishaje?.
Kwa sababu hata wafuasi wa CCM sio wote walifurahishwa na Magufuli,kama ambavyo wapo wanaomnanga Samia.
 
Dah, kamanda nenda katubu na ufunge kabisa kwa wiki nzima kupata radhi ya M/Mungu.

Kusema cdm ni chama cha Mungu ni sawasawa na kusema Mungu anapenda wivu, upendeleo, uongo, hila, chuki, ubaguzi, matusi na utengano. Hili si sawa labda km kuna 'mungu' mwingine unamzungumzia tofauti na huyu tunayemuabudu.

Ushauri; tuepuke kumtumia Mungu km fursa au daraja katika kutafuta kuungwa mkono katika usheitwani wetu,...........hasira zake ni kali sana!!
Kuna kauli watu wanaziongea bila kupima uzito wake, kumuhusisha Mungu na hivi vyama vya upinzani sijui huyo mtu anafikiria nini au anamchukulia vp huyo Mungu? Ubaya humu kuna watu hawaamini Mungu hivyo pengine ndio maana inakuwa rahisi kwao kutoa kauli kama hizo.
 
Huu Sasa ni uongo wa wazi kabisa kwamba chadema inakosoa penye kasoro na kusifia panapostahili? Hii si kweli chadema wanapinga na kuponda kila kitu
Chadema akiponda kila kitu ndio wanasema ni kwa sababu ni wapinzani ila wewe ukiponda kila kitu chadema unaonekana una tatizo binafsi na cdm haubalance.

Kiongozi wa dini akiponda ccm na serikali muda wote anaonekana ni kiongozi wa kweli na mchamungu haswa ila akisifia serikali hata mara moja huonekana ni mchumia tumbo.
 
Tangu niingie humu kama mahali Pa kupass time mke Wangu akinizingua sijawahi ONA WANACHADEMA Wamekuwa unbiased. Matusi. Kkashfa Ndo maandiko yao. Sawa wewe umeona haya? Mnalazimisha uwingi kwa kujipanga na kupeana sifa hata kama hoja za kijinga ili Mradi Huyu Ni wa kwetu. Hamuwezi Ona kosa la mtu mpaka tu awe sio CHadema.
Kwanza jifunze Adabu , kwamba kwako jf ni sehemu ya kupotezea muda baada ya kugombana na mumeo hayo ni matusi , kuweni na heshima na jukwaa hili nyie vijana .
 
Back
Top Bottom