Cecil Mwambe: Nimeshindwa kwenye uchaguzi Mkuu wa CHADEMA kwa kuwa uwanja haukuwa sawa

Besta Mlagila

Senior Member
May 29, 2018
101
191
1576841831355.png

Ikiwa ni siku moja imepita tangu kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi wa kitaifa wa CHADEMA na viongozi hao kupatikana, aliyekuwa mgombea wa nafasi ya mwenyekiti na kushindwa Mhe. Cecil Mwambe amesema kuwa, ameshindwa kwenye uchaguzi huo kwa kuwa 'uwanja haukuwa sawa'.

Amesema "Mhe. Mwenyekiti (Freeman Mbowe) aliongoza vikao mfululizo kwa nafasi yake(Mwenyekiti), na muda wote vikao hivyo vilikuwa ni sehemu ya kampeni, kuongea na wanachama kwa nyakati tofauti, halafu mimi nikapewa dakika 5 niombe kura na maswali matatu, jumla dakika 8"
 
Cha kujifunza hapo ni kwamba kutokukubali kushindwa iko kwenye DNA ya chadema na wao kila siku wakishindwa husingizia kuibiwa kura, sijui ni nani aliwadanganya kwamba kukubali kushindwa ni udhaifu?
Sasa huyo jamaa wa Mtwara alitegemea kiukweli kabisa Wachaga wamkabidhi Chama?
 
Mwambe nakuomba utulie kakà, uliambiwa juu ya kufanyiwa mizengwe ukawa mbishi. Tunajua umeonewa na wewe ndio mshindi halali lakini ungefanya Nini kama SACCOS imemtaka huyo.

Nakushauri urudi CCM au uendelee kubaki ufukuzwe kama mbwa kama mwenzako Zitto na Sasa mwenyekiti kapata fimbo ya kuadhibu wote waliokuwa wanataka uenyekiti. Mark my words: Mnyika ndio fimbo ya mwenyekiti kuwatoa hapo
 
Sifahamu sheria na kanuni za CDM zimekaaje wakati wa mchakato wa kugombea uenyekiti haliyakuwa mwenyekiti aliyopo ni mgombea pia wa nafasi hyo,binafsi naona kama vikao hvyo Vngeongzwa na makamu mwenyekiti au mtu mwingine tu ambaye si mgombea
 
Cha kujifunza hapo ni kwamba kutokukubali kushindwa iko kwenye DNA ya chadema na wao kila siku wakishindwa husingizia kuibiwa kura, sijui ni nani aliwadanganya kwamba kukubali kushindwa ni udhaifu?
Sasa huyo jamaa wa Mtwara alitegemea kiukweli kabisa Wachaga wamkabidhi Chama?
Wizi wa kura uko kwenye mfumo wa damu wa ccm hivyo hata ukiwapima Kwa DNA wizi wa kura utaonekana tu maana ccm imejengwa kwa misingi ya wizi uliokubuhu!!
 
Back
Top Bottom