CECAFA Kagame Cup 2012 - Live updates

CECAFA Kagame Cup 2012 - Live updates

......ina ashiria nini kama Salim Kinje, Kanu Mbiyavanga na Danny Mrwanda wanaanzia benchi wakati wamesajiriwa kwa dau kubwa kwanini stumikie Club ipasavyo????

Mkuu wape nafsi siyo rahisi kuuzoea mfumo wa timu kwa haraka hivyo...
 
KOCHA Mkuu wa Simba SC, Milovan Cirkovic, ametangaza kikosi kitakachoshuka dimbani leo hii dhidi ya Azam katika Robo Fainali ya Kombe la Kagame ambapo wachezaji Uhuru Selemani na Jonas Mkude wataanza.


Kikosi hicho kinaundwa na Juma Kaseja, Haruna Shamte, Shomari Kapombe, Juma Nyoso, Lino Masombo, Jonas Mkude, Mussa Mudde, Mwinyi Kazimoto, Felix Sunzu, Haruna Moshi na Uhuru.


Benchi watakuwepo; Waziri Hamad, Obadia Mungusa, Kiggi Makassi, Salim Kinje, Kanu Mbiyavanga, Dani Mrwanda na Amri Kiemba.

Kikosi kizuri, ndugu yangu ndetichia naye yuko wapi atuwekee kikosi chake.
 
Yaani yanga baada ya kumchagua manji kuwa wanyekitio wao basi yanajiona kama ndiyo malaika katua jangwani ndiyo maana mimi naomba tukutane nao halafu tuwatandike...

Ajali siyo lazima ugongwe na gari, kwa hali ilivyo Simba kukutana na Yanga ni ajali mbaya sana kwa Mnyama huyo, ni lazima avalishwe shanga nyekundu shingoni (asomaye na afahamu); hivyo Mkuu usi-book ajali, tusubiri dakika 90 zijazo.

Nawaombea sana Watani mvuke kivuko hiki cha wauza mikate yenye fungus, juice na maji yenye typhoid (homa ya matumbo), dysentery (kuhara damu), amoebiasis (hii kwa kiswahili sifahamu) and kichocho (bilhaziasis).
 
Sasa unafurahia,wee Chizi kwelikweli

Yanga=CCM...hivyo hata kuropoka kwenu kunafanana kabisa na mijitu ya pale bungeni....ulisema mechi hii itaenda matuta ukabeza mechi inayofata sasa mechi imeisha ndani ya dakika 90, unasemaje....
 
Hapa Simba tukipita nusu fainali ishakuwa ngumu.

Kama uliuuangalia vizuri ule mpira wa AS Vita na Simba kama tukishinda hawatatusumbua kiivyo tuliwashika sana hasa kipindi cha pili....sema kitendo cha kutufunga mapema ilituchanganya sana.
 
Yanga=CCM...hivyo hata kuropoka kwenu kunafanana kabisa na mijitu ya pale bungeni....ulisema mechi hii itaenda matuta ukabeza mechi inayofata sasa mechi imeisha ndani ya dakika 90, unasemaje....

Mkuu Crashwise mbona unaleta maneno ya uchonganishi? Hivi hilo li Rage si li bunge la Tabora ni la chama kipi? Lile li Sarungi lilezi la Simba ni la chama kipi, li Sumaye je silisemei hili, acha niishie hapa huu upande. Mhe. Mbowe ni shabiki wa Yanga ni wa chama kipi?

Acha Simba ipendwe kama Simba na Yanga ipendwe kama Yanga wanachama wa CCM na upinzani wapo kote kote.

Simba inatumia pesa za Rage zinazotokana na malipo ya mshahara na marupurupu ya ubunge alioupata kupitia CCM, sasa wewe unatuambia nini?
 
Back
Top Bottom