CCM yatoa maelekezo sakata la mgomo wafanyabiashara Kariakoo, Katiba Mpya

“Kamati Kuu baada ya kujadili imeielekeza Serikali kufanya uchambuzi wa kina wa masuala yaliyoibuliwa na kulalamikiwa na wafanyabiashara wa Kariakoo ili kutafuta kiini cha tatizo halisi na kuyapatia ufumbuzi wa kudumu,”imesema taarifa ya chama hicho iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu Taifa, Itikadi na Uenezi,

Zote hizo ni buying time tu ,kiini cha tatizo wafanyabiashara waliweka wazi ,kodi nyingi sana hadi nyingine zinajirudia rudia(Double taxation) ,Futeni kodi ya store ,kodi itozwe mara moja tu kwa mzigo ukiingia ,mlolongo mrefu wa kupata leseni na matozo kibao!! Kodi zinakusanywa nyingi halafu kina mwigulu wanaenda kuzipiga(mfanyabiashara alitoa maoni hayo ,akashauri wathibiti wizi ili wasiwe wanaumizwa wao kwenye kodi).
 
Yaani kwa lugha rahisi ni kwamba,Mwenyekiti wa CCM Taifa Mh Samia Suluhu Hassani ,amemuagiza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kwamba mgogoro wa Kariakoo, unadhibitiwe na kujua kiini cha tatizo...tena ndiye alikuwa Mwenyekiti wa Kikao...CCM Oyeee!
 
Yaani kwa lugha rahisi ni kwamba,Mwenyekiti wa CCM Taifa Mh Samia Suluhu Hassani ,amemuagiza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kwamba mgogoro wa Kariakoo, unadhibitiwe na kujua kiini cha tatizo...tena ndiye alikuwa Mwenyekiti wa Kikao...CCM Oyeee!
CCM wanajiona kuwa wanavyopeana PhD basi na akili wanazo, Kumbe umewasoma vituko vyao
 
Dar es Salaam. Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) leo Jumapili Mei 21, 2023 imeingiza mguu katika sakata la mgomo wa wafanyabiashara Kariakoo huku ikiitaka Serikali kutafuta kiini cha tatizo na kukitafutia ufumbuzi.

Kamati hiyo imetoa maelekezo hayo katika kikao chake maalum kilichoongozwa na Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan baada ya kupokea na kujadili taarifa kuhusu mgogoro wa wafanyabiashara wa soko hilo la kimataifa.

“Kamati Kuu baada ya kujadili imeielekeza Serikali kufanya uchambuzi wa kina wa masuala yaliyoibuliwa na kulalamikiwa na wafanyabiashara wa Kariakoo ili kutafuta kiini cha tatizo halisi na kuyapatia ufumbuzi wa kudumu,”imesema taarifa ya chama hicho iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu Taifa, Itikadi na Uenezi,

Vilevile, Kamati Kuu imeielekeza Serikali kuhakikisha inatengeneza utaratibu wa kutatua changamoto mapema kabla hazijaleta madhara katika jamii kama ilivyokuwa katika mgogoro wa soko la Kariakoo.

Kamati Kuu imetoa maelekezo hayo kwa Serikali ikiwa ni siku nne zipite tangu wafanyabiashara wa soko la Kariakoo wamalize mgomo wao ambao ulifanyika kwa siku tatu mfululizo kwa kufunga maduka yao kushinikiza kutolewa kwa kodi ya stoo na kukomeshwa kwa kile walichokiita kamatakamata inayofanywa na Mamlaka ya Mapato (TRA).

Hata hivyo, mgomo huo ulitamatika baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kufanya vikao viwili na wafanyabiashara hao huku kikao cha kwanza kilichofanyika Mei 15, 2023 kisifue dafu na baadhi ya wafanyabiashara waliendelea na mgomo hivyo kulazimika tena Mei 17, 2023 kufanya kikao kingine cha wazi katika viwanja vya Mnazi Mmoja.

Katika kikao cha pili kilichohudhuriwa na mamia ya wafanyabiashara wa soko hilo maarufu nchini lenye kila aina ya pilikapilika kilifanikisha kumaliza mgogoro huo baada ya Majaliwa pamoja na Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba na Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Ashatu Kijaji kuwasikiliza wafanyabiashara hao wakitema nyongo kuhusu kero zinazowasibu na baadaye kuunda kamati ya watu 14 kushughulikia matatizo hayo ikiwahusisha wafanyabiashara na watumishi wa Serikali.

Kwa upande mwingine, Kamati Kuu imempongeza Rais Samia kwa kuanzisha mchakato wa Katiba Mpya na kukamilisha ujenzi wa Ikulu Mpya ya Chamwino iliyozinduliwa rasmi Jumamosi Mei 20, 2023.
Kwahiyo wanajiagiza wenyewe au Kuna misukule Wana iagiza? Au kwenye hiyo kamati kuu mwigulu hayupo pumbafu zenu
 
CCM huwa inawadanganya na kuwa tapeli wananchi:

Kamati kuu wajumbe ni Wale Wale walioko kwenye serikali sasa kamati kuu inaiagiza serikali ipi !!!

Mfano Waziri mkuu, makamu wa Rais na Rais wote ni viongozi wa kiserikali na ni members wa Kamati kuu sasa ni ccm ipi inaiagiza serikali ifanye wakati ni hao hao wanaoshindwa kufanya au kutekeleza wakigeuka upande wa pili wanajiagiza tena wanasema chama kimesema?

Mfano, Tulia Akson ni spika wa bunge, wakati huo huo ni mjumbe wa Kamati kuu ya ccm Taifa, ni mjumbe wa mkutano mkuu wa ccm Taifa, mkoa,wilaya, ni mjumbe wa kamati Za siasa kata, wilaya,mkoa, Taifa Ana vyeo 42.

Ushauri : viongozi wa kamati kuu wasiwe viongozi wa serikali na viongozi wa serikali wasiwe wajumbe wa kamati kuu.
Mkuu meshawahi hata kuwa Class Monitor?
 
CCM huwa inawadanganya na kuwa tapeli wananchi:

Kamati kuu wajumbe ni Wale Wale walioko kwenye serikali sasa kamati kuu inaiagiza serikali ipi !!!

Mfano Waziri mkuu, makamu wa Rais na Rais wote ni viongozi wa kiserikali na ni members wa Kamati kuu sasa ni ccm ipi inaiagiza serikali ifanye wakati ni hao hao wanaoshindwa kufanya au kutekeleza wakigeuka upande wa pili wanajiagiza tena wanasema chama kimesema?

Mfano, Tulia Akson ni spika wa bunge, wakati huo huo ni mjumbe wa Kamati kuu ya ccm Taifa, ni mjumbe wa mkutano mkuu wa ccm Taifa, mkoa,wilaya, ni mjumbe wa kamati Za siasa kata, wilaya,mkoa, Taifa Ana vyeo 42.

Ushauri : viongozi wa kamati kuu wasiwe viongozi wa serikali na viongozi wa serikali wasiwe wajumbe wa kamati kuu.
Wanacheza sana na akili za wananchi hawa CCM
 
Tatizo linalioonekana hapa, na ninavyolisoma, nikuwa, haya madhara yaliyotokea n yametokea Lumumba. Sasa kwaavile limewagusa kwa ukaribu kabisa,ndii wanajifanya wanafanyia kazi manung'uniko au Njaa za mitaani.

Hatahivyo, nastaajabishwa. Kwamba katika karne hii hawana mkakati wa kuangaza na kuchukua hatua stahiki wakati kuna hali kama hiyo?,(mgomo)kwa sababu ilikuwa dhahiri hali hiyo ingetokea na walikuwa na Taarifa mapema.
Walipuuza?
Walifikiri tisha toto😂😂😂😁
Nimeandika humu marakadhaa kwamba serikali hutumia muda mwingi na pesa nyiongi kujifungia kutangeneza sheria, miongozo na tozo bila kuwashirikisaha wadau, (wafanyabiashara), matokeo yake huwa hayana tija ndiyo hicho kilichotokea kariako na kwingineko hili swala litakuwa endelevu kwasabu jamii yetu ni mfu ambayo haiwezi kuhoji
 
Dar es Salaam. Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) leo Jumapili Mei 21, 2023 imeingiza mguu katika sakata la mgomo wa wafanyabiashara Kariakoo huku ikiitaka Serikali kutafuta kiini cha tatizo na kukitafutia ufumbuzi.

Kamati hiyo imetoa maelekezo hayo katika kikao chake maalum kilichoongozwa na Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan baada ya kupokea na kujadili taarifa kuhusu mgogoro wa wafanyabiashara wa soko hilo la kimataifa.

“Kamati Kuu baada ya kujadili imeielekeza Serikali kufanya uchambuzi wa kina wa masuala yaliyoibuliwa na kulalamikiwa na wafanyabiashara wa Kariakoo ili kutafuta kiini cha tatizo halisi na kuyapatia ufumbuzi wa kudumu,”imesema taarifa ya chama hicho iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu Taifa, Itikadi na Uenezi,

Vilevile, Kamati Kuu imeielekeza Serikali kuhakikisha inatengeneza utaratibu wa kutatua changamoto mapema kabla hazijaleta madhara katika jamii kama ilivyokuwa katika mgogoro wa soko la Kariakoo.

Kamati Kuu imetoa maelekezo hayo kwa Serikali ikiwa ni siku nne zipite tangu wafanyabiashara wa soko la Kariakoo wamalize mgomo wao ambao ulifanyika kwa siku tatu mfululizo kwa kufunga maduka yao kushinikiza kutolewa kwa kodi ya stoo na kukomeshwa kwa kile walichokiita kamatakamata inayofanywa na Mamlaka ya Mapato (TRA).

Hata hivyo, mgomo huo ulitamatika baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kufanya vikao viwili na wafanyabiashara hao huku kikao cha kwanza kilichofanyika Mei 15, 2023 kisifue dafu na baadhi ya wafanyabiashara waliendelea na mgomo hivyo kulazimika tena Mei 17, 2023 kufanya kikao kingine cha wazi katika viwanja vya Mnazi Mmoja.

Katika kikao cha pili kilichohudhuriwa na mamia ya wafanyabiashara wa soko hilo maarufu nchini lenye kila aina ya pilikapilika kilifanikisha kumaliza mgogoro huo baada ya Majaliwa pamoja na Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba na Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Ashatu Kijaji kuwasikiliza wafanyabiashara hao wakitema nyongo kuhusu kero zinazowasibu na baadaye kuunda kamati ya watu 14 kushughulikia matatizo hayo ikiwahusisha wafanyabiashara na watumishi wa Serikali.

Kwa upande mwingine, Kamati Kuu imempongeza Rais Samia kwa kuanzisha mchakato wa Katiba Mpya na kukamilisha ujenzi wa Ikulu Mpya ya Chamwino iliyozinduliwa rasmi Jumamosi Mei 20, 2023.
Nina mashaka na uwezo wetu wa akili
 
Yaani kwa lugha rahisi ni kwamba,Mwenyekiti wa CCM Taifa Mh Samia Suluhu Hassani ,amemuagiza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kwamba mgogoro wa Kariakoo, unadhibitiwe na kujua kiini cha tatizo...tena ndiye alikuwa Mwenyekiti wa Kikao...CCM Oyeee!
Yaani hii sijui imekaaje!! Walewale wenye migogoro na wafanyabiashara/kazi ndiyo Hao Hao wa nakaa na kujiagiza watafute suluhisho!!!! WOTE CHEKENI KWA SAUTI KUBWA HADI NEMC WAWAFUNGIEEEE
 
Back
Top Bottom