Huyu bila shaka anataka kwenda kwao Somalia kuimarisha lile kundi lake la kigaidi la Al- Shabab maana limeanza kuzidiwa nguvu.
Kwa taarifa yako sasa hivi wamejaa hapa Tanzania, Arusha na kigamboni wanajiandaa kuchukua nchi kupitia CCM.
kwa habari hii iliyo hapa mbele yetu, THIBITISHA kwamba ni uongo! Nape katuthibitishia ni ukweli, haya lete uthibitisho wako wa uongo
Though ntafurah na nina penda sana iwe hivyo, ila nina mashaka kidogo na hii habari.
Moods, Invisible , Paw na wooooote, ikifika J5 na hii habar ikawa ya ukweli, basi mleta uzi apewe Tuzo ya Mleta Nyuzi Tafiti wa Mwaka hapa JF, Otherwise, inabidi mleta uzi, ndugu yetu AL sadat, alimwe a LIFE TIME BANN
Kitendo cha mtu aliyeongoza kwa robo karne kukaa pembeni kinatoa fursa kwa vijana kushiriki katika uongozi. Uamuzi wa Kinana unapaswa kupongezwa na vijana wanaoitakia mema nchi yetu...
Nakumbukuka ulitupa clue mapema.Ukita kujuwa wamechakachua haya mambo,angalia kauli ya Nape kuwa eti mwenyekiti anaweza kuona anafaa na akamteua tena akaingia kwenye NEC.Hiyo statement tu utadunguwa wamewekana sawa hawa magamba.Vurugu zao mara nyingi ni maslahi binafasi,hakuna asiye fisadi miongoni mwao,hapo keshapewa ahadi kibao .......
Siwezi kuchangia sana hadi nipate reliable source
Candid Scope
Kati ya watu ninaowaheshimu humu jamvini, wewe ni mmoja wapo. Najua utakuwa na upeo mkubwa wa kufanya Judgement pale unapokutana na habari na kuamua kuichukua kama ni kweli ama porojo. Pia wewe ni mzoefu SANA ndani ya JF
Unaweza ku-judge according to the credibility ya mtoa uzi hata kama hajatoa source. Kuna watoa uzi ambao ukikuta taarifa yake humu haihitaji wala kuwa na shaka naye kwa mujibu wa historia yake ya kuleta topics.
Unaweza ku-judge according to political affiliation ya mtoa uzi. Naamini anapotoa uzi Rejao (mfano) au anapotoa Mungi au Aweda, na ukisoma maudhui ya uzi wenyewe, moja kwa moja uta-judge usahihi wake accordingly.
Unaweza Ku-judge kutokana na status ya mtoa uzi. kama ni Member na mwingine ni Gold member ama Bronze member, hivyo pia vinaweza kutumika kama kigezo (ingawa sio muda wote) cha usahihi wa habari.
Unaweza kuzoma between the lines na ukaja na conclusion kuwa huo uzi ni sahihi au la hata kama hujawekewa source.
Unaweza ukawekewa source lakini bado uzi ukawa ni uongo, tena source kama haw auliowasema ie. habari toka mjengoni, watu wa karibu na Jk etc.
Cha Muhimu, kama una uhakika uzi sio wa ukweli, hebu jitokeze na kusema kuwa uzi huu sio ukweli kwasababu moja...mbili....tatu..... na wewe uwe na uhakika kuwa ni kweli mtoa uzi kaongopa.
Back to uzi wa leo:
Waliosema kuwa mtoa mada kaongopa, hakuna hata mmoja aliyesema usahihi ni nini. kwakuwa walikuwa hawajui usahihi ni nini, basi ni bora wangechukulia kama tetesi na kukaa kimya na hata kuacha ku-comment maana kwa kufanya hivyo "wangeficha upumbavu wao" (Invinsible). Lakini kwa kusema kuw auzi huu ni uongo wakati wao wenyewe hawaujui ukweli, wamejianika kuwa wao ndio waongo na wasiofikiri.
Yupo mmoja kadiriki kusema huyo mtoa uzi ni mmoja kati ya waliosemwa na JK kuwa wanamilikki kiwanda cha uongo, sasa truth imekuwa revealed. nani anayemiliki kiwanda cha uongo, huyu mtoa uzi ama yule aliyetuhumu wakati hajui ukweli?
Kila niiingiapo JF na kusoma thread zote, najua kabisa hii ni kweli na hii ni porojo na hii ni tetesi bila hata kuuliza source ni nani kwa vigezo nilivyoeleza hapo juu.
Mkuu Mwana Mpotevu na Mag3 mi naomba uthibitisho kwenye red tu hapo juu. Ukinithibitishia baaaaaas sitakuwa na tatizo na nyie otherwise hizi ni Porojo tena yawezekana zimepikwa na wafuasi wa EL
Kwa taarifa yako sasa hivi wamejaa hapa Tanzania, Arusha na kigamboni wanajiandaa kuchukua nchi kupitia CCM.
Tuko pamoja, hatuna maana ya kwamba alisema uongo, la hasha, hapa ni kujaribu kukumbushana, na kama alikuwapo online angetujibu kwamba source ya habari yake ni wapi.
Kwa bahati nzuri Nape alitokeza na kujibu kuhusu habari hiyo, hilo ndilo lilitupa watu uelewa kwamba habari ni ya kweli.
Kwa vyo vyote ni kukumbusha tujitahidi kuweka kitu kinachotuongolewa wasiwasi juuya source, inasaidia, wengine kwa uzoefu wa mambo ya habari, kuleta habari bila kuonyesha source tunajisikia kama dhambi, lakini kwa asiyekuwa na uzoefu katima mambo ya habari vyo vyote ni sawa tu. Ila tunapoandika hapa ambapo kuna watu wa kila aina ambao wengine upeo wao katika habari ni wa juu ni vema kama tutakumbuka kuweka chanzo cha habari, hata kama hakuna hakika ukiandika tetesi tutaijadili kama ilivyo tetesi.
Nashukuru kujua kama kumbe una upeo wa habari. Lakini nikuulize kitu;
Unajua kuhusu Anonymous Sources??
Unajua kuhusu Secret Sources?
Unajua kuhusu Confidential sources?
Unajua kuhusu Unnamed Sources?
Unajua kuhusu Veiled sources and veil information?
Kwakuwa una uzoefu wa habari, utakuwa unaelewa yote haya. na kwakuwa unayaalewa haya, utajua fika kuwa taarifa kama ya mtoa uzi ni sahihi kabisa na haina doubt kwa wanahabari kama mwandishi anajua kuwa it is TRUE!
Wasio na taaluma ya habari ndio wanaweza kuhoji ili wapate truth between the lines lakini sio kwa mtu mwenye ujuzi wa habari kama wewe