CCM yapasuka? Kinana ang'atuka...

CCM yapasuka? Kinana ang'atuka...

Maswali makuu ambayo waandishi wanatakiwa kujibu ni matano hata utembee pembe gani ya dunia
Candid Scope

Unazungumzia 5W+H?

Am sorry to say that hiyo ni OLD FASHION JOURNALISM!

Today's journalism concentrates on two main aspects, WHY AND HOW!

Hizo zinazobaki (WHO, WHAT, WHEN and WHERE) ni nyongeza tu na sio mambo ya msingi katika uandishi wa habari wa sasa. Journalism ya mwaka 1970s sio journalism ya 2000s mkuu
 
Last edited by a moderator:
Kinana is retiring, he is one of the smartest politician tanzania has, he is a go getter and a hands on man, very respected and he respects everybody. In his campaign he never utters a bad or cheap words.

Lets give him his over due respect in this forum.
 
Hili la kwamba anaenda kufundisha chuo kikuu limenishangaza kidogo. Hivi ana umri gani?
 
Candid Scope

Unazungumzia 5W+H?

Am sorry to say that hiyo ni OLD FASHION JOURNALISM!

Today's journalism concentrates on two main aspects, WHY AND HOW!

Hizo zinazobaki (WHO, WHAT, WHEN and WHERE) ni nyongeza tu na sio mambo ya msingi katika uandishi wa habari wa sasa. Journalism ya mwaka 1970s sio journalism ya 2000s mkuu

Sishangai kwa jibu hilo ndio maana mada tunapata ambazo ni half done.
 
Candid Scope

Unazungumzia 5W+H?

Am sorry to say that hiyo ni OLD FASHION JOURNALISM!

Today's journalism concentrates on two main aspects, WHY AND HOW!

Hizo zinazobaki (WHO, WHAT, WHEN and WHERE) ni nyongeza tu na sio mambo ya msingi katika uandishi wa habari wa sasa. Journalism ya mwaka 1970s sio journalism ya 2000s mkuu

Sishangai kwa jibu hilo ndio maana mada tunapata ambazo ni half done.

Elimu ni bahari, na mwenye kuamini kwamba akiaminicho ndio ukamilifu mwache alivyo vinginevyo ....., lakini kwa mwandishi ridhio ni audience kutoachwa na maswali ya kujiuliza.

Ukiangalia vipengele viwili tu vya mfumo unaouita wa kisasa hujauelewa vizuri, kwani hutakosa kujibu hayo maswali ya msingi ambayo kwangu kwa msingi huo huwa hayamwachi msomaji ye yote na maswali ya kujiuliza. Mtindo unaosema ndio unaotupa wengi hapa maswali kadhaa yasiyojibika kwa maana ya tungo au mada kutojitosheleza kwa kuwa na majibu ya maswali ya msingi, hata useme ni mfumo wa kipengele kimoja lakini hutakwepa maswali hayo ninayokuambia.


Kama WHY AND HOW! ndio msingi wa uandishi wa leo kwa mtazamo wako, je, who, when and where havina nafasi kwako na vitajibiwaje wakati hata kesi za mahakamani ndio msingi? Pole sana, jaribu kurudia tena utagundua kuna kitu hakijakamilika.

Nimekaa darasa la bongo, nimekaa darasa la global nimekutana na uandishi wenye kujibu yote, la sivyo hujakamilisha uandishi wenye kuondoa kiu ya audience. Hata kamwulize aliyekufunza kama unaweza kukwepa
who, when and where halafu uandishi wako ukapokeleka na media na kukidhi matakwa ya wasomaji bila kuwaacha na maswali. Ningekuelewa kama ungesema kuna mantiki (tricky) katika kuyaainisha hayo katika tungo, lakini huwezi kunisadikisha kwamba hayapo. Maana katika uandishi kile tunachokiita critical thinking/critical writting kukipa nafsi zaidi, ndio kinachomfanya msomaji avutike katika uandishi au mada yako lakini hakikisha mwisho wa safari unahitimisha majibu yote pasi shaka kwa msomaji.

Ninacho kijua mabadiliko ya siku hizi katika kuonyesha hayo niyasema yako katika mfumo tofauti ambao hayaonyeshi 1, 2, 3, 4, 5 na 6, bali ni mfumo ambao unapoandika unahakikisha yote yamejibiwa na pengine kipengele cha kwanza ukakiona paragraph ya tatu na mara kadhaa kuunganika etc. Uandishi ambao vyombo vingi vya habari hutumia mara nyingi huanzia na nukuru au mfumo wenye kutoa taswira fulani, uandishi huo kwetu Tanzania sijaona bado, kwani nikisoma tungo mbalimbali za hapa kwetu zingali na mfumo ule wa 1,2,3... Jaribu kupoza kidogo.

Uandishi wa kimataifa na vyombo mbalimbali vilivyokubuhi katika nyanja hizi tazamia zaidi kupata majibu kuanzia katikati na kukamilika mwishoni tofauti na bongo ambapo unaweza kushtukia paragraph ya kwanza na ya pili habari imekamilika na huna haya ya zinazofuata kwa vile unachokitaka kukijua kimeshajibiwa. Uandishi huo wa nchi zilizoendelea unajikita katika kumfanya msomaji amalizie kazi ya mwandishi vinginevyo kwa mtindo wa bongo mwandishi anapoteza umaliziaji wa habari bila kuwa na umuhimu wa msomaji kwa vile kinachohitajika na audience kimeshajibiwa paragraph za awali.

Sishangai kwa jibu lako hili sina haja ya kuendelea kubishana kwani nimeridhika tosha.
 
Kinana is retiring, he is one of the smartest politician tanzania has, he is a go getter and a hands on man, very respected and he respects everybody. In his campaign he never utters a bad or cheap words.

Lets give him his over due respect in this forum.
Unaweza kuniambia manufaa ya kubadili jina la kampuni wakati wa bankruptcy?Je Artumas ilipata manufaa gani kwa kufanya hivyo?
 
Candid Scope

Sishangai kwa jibu hilo ndio maana mada tunapata ambazo ni half done.

Sawa Mkuu, ingawa wanaotoa mada humu sio lazima wawe wanahabari na hawapaswi ama kulazimishwa kutumia A,B,C za Journalism

Ukiangalia vipengele viwili tu vya mfumo unaouita wa kisasa hujauelewa vizuri, kwani hutakosa kujibu hayo maswali ya msingi ambayo kwangu kwa msingi huo huwa hayamwachi msomaji ye yote na maswali ya kujiuliza. Mtindo unaosema ndio unaotupa wengi hapa maswali kadhaa yasiyojibika kwa maana ya tungo au mada kutojitosheleza kwa kuwa na majibu ya maswali ya msingi, hata useme ni mfumo wa kipengele kimoja lakini hutakwepa maswali hayo ninayokuambia.

Hapo kwenye RED, Rejea Comment yangu hapo juu naamini utaelewa

Kama WHY AND HOW! ndio msingi wa uandishi wa leo kwa mtazamo wako, je, who, when and where havina nafasi kwako na vitajibiwaje wakati hata kesi za mahakamani ndio msingi? Pole sana, jaribu kurudia tena utagundua kuna kitu hakijakamilika.

UKisoma vema nilichokujibu, ni kwamba hizo 4Ws zinazobaki ni nyongeza tu lakini kama kuna swala ambalo huwa linawasumbua wasomaji wengi na waandishi wengi wanapuuzia, basi ni kujibu HOW and WHY!


Nimekaa darasa la bongo, nimekaa darasa la global nimekutana na uandishi wenye kujibu yote, la sivyo hujakamilisha uandishi wenye kuondoa kiu ya audience. Hata kamwulize aliyekufunza kama unaweza kukwepa who, when and where halafu uandishi wako ukapokeleka na media na kukidhi matakwa ya wasomaji bila kuwaacha na maswali. Ningekuelewa kama ungesema kuna mantiki (tricky) katika kuyaainisha hayo katika tungo, lakini huwezi kunisadikisha kwamba hayapo. Maana katika uandishi kile tunachokiita critical thinking/critical writting kukipa nafsi zaidi, ndio kinachomfanya msomaji avutike katika uandishi au mada yako lakini hakikisha mwisho wa safari unahitimisha majibu yote pasi shaka kwa msomaji.

Hongera sana kwa kukaa darasa la Bongo na Global, mie nimesoma St Kayumba maana ndo mfumo wetu wa elimu ulivyo na nilichosoma kinanisaidia sana. Critical Thinking/Critical writing? Hahahahahaha Haya ni matatizo ya kukariri masomo darasani. Umeikariri sana Critical Thinking and Argumentation badala ya kuelewa na kudhani iko applicable ktj Journalism tu. U r very wrong

Uandishi wa kimataifa na vyombo mbalimbali vilivyokubuhi katika nyanja hizi tazamia zaidi kupata
majibu kuanzia katikati na kukamilika mwishoni tofauti na bongo ambapo unaweza kushtukia paragraph ya kwanza na ya pili habari imekamilika na huna haya ya zinazofuata kwa vile unachokitaka kukijua kimeshajibiwa. Uandishi huo wa nchi zilizoendelea unajikita katika kumfanya msomaji amalizie kazi ya mwandishi vinginevyo kwa mtindo wa bongo mwandishi anapoteza umaliziaji wa habari bila kuwa na umuhimu wa msomaji kwa vile kinachohitajika na audience kimeshajibiwa paragraph za awali.

Yes indeed, tatizo la kukariri waandishi wa Tanzania mmekaririshwa Inverted Pyramid sio? hiyo ndio niliyosema journalism ya 1970s, News format siku hizi inaweza kuwa kama Champagne glass or Pyramid. Tangu mwanzo hadi mwisho kumeshiba ama kumvuta msomaji aendelee kuona umujhimu wa kusoma kadri anavyomaliza para moja kwenda nyingine. Darasa jipya linatakiwa hapa ili uelewe vema

Sishangai kwa jibu lako hili
sina haja ya kuendelea kubishana kwani nimeridhika tosha.

Very sorry kama ulidhani tunabishana, mie nilijua tunaelimishana na elimu mpya inatakiwa kila siku kwani dunia hii inabadilika kila siku. Tusiendekeze mazoea ya mwaka 47 katika karne hii ya sayansi na teknolojia



Kila la kheri katika taaluma yako ya Habari mkuu. Mie mpitanjia tu, just take it or leave it.
 
Last edited by a moderator:
Kinana is retiring, he is one of the smartest politician tanzania has, he is a go getter and a hands on man, very respected and he respects everybody. In his campaign he never utters a bad or cheap words.

Lets give him his over due respect in this forum.

We all know that, the question is why him why now? Kinana ni mstu muhimu sana kwa Tanzania, inawezakana kuwa yeye pia kwenye ufisadi yumo, lakini he is far better than all who are fighting tooth and nail kubaki NEC na hata kutaka kugombea urais. Believe me ndani ya CCM kwa sasa Kinana ni mmoja wa watu wanaoweza kugombea urais, And believe me in his hands, CCM na Tanzania na watanzania tunaweza kuwa na ahueni kuliko mafisi yanayowania nyadhifa mbalimbali.

Anaheshimiwa na watanzania wengi jeshini, kwenye siasa, uraiani, mashenzini, misikitini na makanisani. Lakini swali ni kwanini yeye na kwanini sasa? wakati watanzania hatuna utamaduni wa kuachia nyadhifa kubwa. Will he be safe au ndio naye watamuua?

Au na yeye ndio anatufanyia kama Mkapa na kutuambia "to hell?"

I am not taking his words so simple. Lazima kuna kitu kikubwa mbeleni, let us wait and see.
 
Kinana, ekinana kiile kyonaaa, kiileee, kiileee niky'eogolaaaa! Wanaojua huu wimbo naomba mniunge mkono. CCM oyee??
 
Mwandishi Wetu

Toleo la 260
26 Sep 2012

UAMUZI wa aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu (CC)na Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kung'atuka katika nafasi za uongozi wa chama hicho umeacha sintofahamu miongoni mwa wakazi wa Arusha na vitongoji vyake.

Kinana alipata kuwa mbunge wa Jimbo la Arusha kati ya mwaka 1985-1995 wakati huo Mkoa wa Arusha ukiwa kitovu cha harakati zake za kisiasa katika kipindi chote cha miaka 25 alichotumikia nafasi mbalimbali ndani ya chama na serikali.


"Nimekuwa Mjumbe wa NEC kwa miaka 25, bila shaka muda huu unatosha, kwani wana CCM wamenipa heshima ya kuwa katika vikao vya juu vya chama kwa robo karne. Sasa ni wakati wa kung'atuka, nimetoa mchango kwa kadri nilivyoweza katika vikao mbalimbali na katika shughuli nyingi," alikaririwa Kinana na vyombo mbalimbali vya habari juzi vikieleza kuondoka kwake.


Alisema anaamini kuachana kwake na siasa hakutakuwa na madhara kwa chama chake, kwani CCM ina hazina kubwa ya viongozi ambao wana sifa na wanaweza kuongoza chama hicho kuelekea Uchaguzi wa 2015.


"Uongozi ni kupokezana vijiti. Wako wana CCM wazuri, walio na uwezo mkubwa na sifa za kutosha kuongoza. Nawashukuru wana CCM na viongozi kwa heshima waliyonipa wakati wote huu," alisema.


Kinana atakumbukwa pia kama meneja mahiri wa kampeni za wagombea urais wa CCM tangu mwaka 1995 hadi mwaka 2000 wakati wa ugombea wa Benjamin Mkapa na kati ya mwaka 2005 na 2010 katika kipindi cha Jakaya Kikwete, vipindi ambavyo vimekipa CCM ushindi mkubwa ukiacha ule wa mwaka 2010 ambao chama hicho kilipata kutikiswa sawasawa na mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Wilbroad Slaa.


Taarifa za kung'atuka kwa Kinana zimepokewa kwa maoni tofauti mjini Arusha ambapo kwa siku mbili mfululizo uamuzi huo ulikuwa mjadala wa kijamii kwa watu wa kada mbalimbali hasa wale waliowahi kufanya naye kazi.


Mmoja wa viongozi wa chama hicho aliyejitambulisha kuwa karibu naye aliliambia Raia Mwema kuwa kiongozi huyo anang'atuka kwa madai kuwa chama hicho tawala kimezidi kukosa mwelekeo baada ya kutafunwa na makundi kwa muda mrefu.


"Ndani ya CCM ya leo ahadi na misingi asilia ya chama vimepuuzwa na badala yake wanachama na viongozi wamekuwa wanaendekeza makundi na fitina za kisiasa ambazo zimeleta mgawanyiko mkubwa," alisema kada huyo.


"Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko" hii ni moja ya ahadi za mwana CCM, na mzee Kinana alisimamia sana ahadi hiyo kila mara alipokuwa anatekeleza majukumu yake sasa ulipofika wakati ambao wanachama na viongozi walipuuza ahadi hiyo basi na yeye akaona kuwa ni muda muafaka wa kuachana na siasa," aliongeza.


Alisema hata hivyo uamuzi huo pamoja na kuwa ni mchungu kwa CCM ni wa busara sana kwa kuwa atabaki na heshima yake tofauti na wazee wengine ambao wameng'atuka kwa aibu baada ya kushindwa kupenya katika chaguzi za nafasi mbalimbali ndani ya chama.


Kada mwingine wa chama hicho Khalifa Mnaro alisema Kinana ameonyesha njia kwa viongozi wengine waliokaa madarakani kwa muda mrefu kuondoka kwa heshima kuliko kusubiri fedheha ya kushindwa katika uchaguzi wa nafasi mbalimbali unaondelea nchini kote.


"Wale viongozi ambao umri umewatupa mkono ni vizuri waige kutoka kwa mzee Kinana ili kuwapisha wenye nguvu na damu changa katika siasa ambao wanaweza kuendana na kasi ya sasa ya siasa za ushindani," alisema Mnaro.


Naye Kada maarufu wa CHADEMA Ally Bananga ambaye aliwahi kufanya kazi na mwanasiasa huyo alieleza kuwa "CCM wameendelea kupoteza ‘vifaa' na simwoni mwingine anayeweza kuwa kama yeye (Kinana) ndani ya Arusha. Nitamkumbuka kwa siasa zake za uwazi zilizokuwa hazina makundi."


Bananga aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali ndani ya CCM kati ya mwaka 2000-2012 alipohamia CHADEMA na miongoni mwa nafasi hizo ni kuwa mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana wa UVCCM Wilaya ya Arusha Mjini 2003-2008, mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Mkoa, mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya na mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa.


Kada huyo wa CHADEMA aliongeza kuwa hata hivyo anampongeza kiongozi kwa kuchukua uamuzi wa busara kuachana na chama hicho ambacho kipo njiani kufa na kuachia madaraka ya dola.


"Ni wazi kuwa CCM ya leo si ile ya miaka 10 au 20 iliyopita. CCM ya leo imechoka mno na viongozi wake hawana jipya la kuwaambia Watanzania, kwa hiyo nampongeza sana Mheshimiwa Kinana kwa kutambua hilo mapema na kuamua kuachia ngazi," alisema.


Hata hivyo, aliongeza kuwa wanasiasa wengi wa upinzani na wale wa chama tawala hasa kutoka Mkoa wa Arusha wana mengi ya kujifunza kutoka kwa Kinana, kama mmoja wa viongozi waliowahi kupigania maendeleo ya Mkoa wa Arusha kijamii, kisiasa na kiuchumi.


"Tutamkumbuka kama mmoja kati ya viongozi waliosimamia ujenzi wa wodi za wazazi na watoto katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru ambayo mpaka leo imekuwa mkombozi wa wanawake wajawazito na watoto wadogo wanaopata matibabu pale," aliongeza Bananga.


Aliongeza kuwa Kinana pia alipigania sana umoja wa kitaifa kwa kushirikiana na makundi tofauti hata viongozi wa vyama upinzani kwa lengo la kulinda maslahi ya Taifa.


Naye Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM Mrisho Gambo alimwelezea Kinana kama kiongozi mwadilifu ambaye amefuata nyayo za Mwalimu Julius Nyerere kwa kung'atuka bila ya kuacha dosari au tuhuma zozote zinazochafua sura yake katika ulingo wa siasa na ndani ya CCM na serikali yake.


"Amekuwa mfano mwingine baada ya Mwalimu Nyerere na uamuzi huo uwe somo kwa viongozi wengine ndani ya CCM ambao wana kashfa lukuki za ufisadi lakini bado wanang'ang'ania kugombea nafasi mbalimbali za u-NEC wilayani, " alisema Gambo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Korogwe.


Kinana mbali ya kushika nyadhifa mbalimbali ndani ya CCM na Serikali, alipata pia kutumikia Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa muda mrefu akipanda cheo hadi kufikia kuwa kanali.


Alipata kuwa naibu waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakati wa rais Ali Hassan Mwinyi na pia amewahi kuwa Spika wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA).











 
Kinana team yake enzi hizo ni LOWASSA, KIKWETE, SAID KIBWANA (GM GENERAL TYRE) na LT. G KARUBI (alikuwa

Mkuu wa Kambi ya OLJORO... alikuwa haishi KAMBINI anakaa MJINI Karibia na Hao Marafiki zao)

Wakati ule 25yrs Ago; Walikuwa na MIKAKATI Mingi ya WAO as a GROUP kuendelea... KIONGOZI alikuwa KINANA

Halafu LOWASSA then KIKWETE na hao Wengine... Na KIMADARAKA ilikuwa hivyo hivyo... MBUNGE

kuwakilisha Wananchi alikuwa ni KINANA pekee ARUSHA MJINI... Sasa naona kwa Siasa za KIKWETE

GROUP LIMEVUNJIKA Kina Karubi yeye alikuwa anaendesha biashara zao especially ya MELI ambazo

KINANA ana JOINT-OWNERSHIP... NDIO WALIKUWA WENYEWE PALE ARUSHA...
 
Mwandishi Wetu



Taarifa za kung'atuka kwa Kinana zimepokewa kwa maoni tofauti mjini Arusha ambapo kwa siku mbili mfululizo uamuzi huo ulikuwa mjadala wa kijamii kwa watu wa kada mbalimbali hasa wale waliowahi kufanya naye kazi.


Mmoja wa viongozi wa chama hicho aliyejitambulisha kuwa karibu naye aliliambia Raia Mwema kuwa kiongozi huyo anang'atuka kwa madai kuwa chama hicho tawala kimezidi kukosa mwelekeo baada ya kutafunwa na makundi kwa muda mrefu.


"Ndani ya CCM ya leo ahadi na misingi asilia ya chama vimepuuzwa na badala yake wanachama na viongozi wamekuwa wanaendekeza makundi na fitina za kisiasa ambazo zimeleta mgawanyiko mkubwa," alisema kada huyo.


Ngoja tumsubiri Nape aje atoe kanusho!
 
Back
Top Bottom