CCM yanguruma Busanda; Wapinzani chali!


Si uje wewe utoe habari vizuri unapenda kupewa tu. Dawa kama unaona kuna tatizo basi jitahidi ulitatue sio kuomba jirani akutatulie
 
So what is your point here bwana mkubwa? Kukua kwa chadema kunakukera au namna gani? Sijakupata kabisa unachojaribu kusema!
Kitila,

Kazi mnayo Biharamulo. Naamini unaweza kutumia busara yako kuwashauri kina Freeman wafanye nini kabla ya kuhamisha kambi toka Busanda. Mkumbuke hata hao waliowapa kura walikuwa na mapenzi na chama chenu, watieni moyo!

BTW, hongera CCM kwa ushindi mwingine...
 

Kweli kabisa hapa umeongea kisagarani. ndiyo maana walimchagua mnyika kuwa mbunge wao ubungo!
 
...bila ya Malecela huu uchaguzi wangebwagwa tena...nafikiri yule mzee ni asset kwa CCM.


Unajipunguzia heshima ndugu, kuwa objective na uache kujikomba. Hufanani na maneno uliyoandika hapo.

Ukweli ni kwamba CCM wamejimaarisha maeneo ya vijiji kuliko vyama vya upinzani. Hii ni changamoto kwa upinzani kujiandaa vyema kwa uchaguzi 2010 katika maeneo ya vijijini. Operesheni wanazozifanya bado haziwaamsha wananchi kiasi wawe na imani ya kunyakua viti vingi vya ubunge au hata urais katika miaka mwakani au hata 2015.
 
Si uje wewe utoe habari vizuri unapenda kupewa tu. Dawa kama unaona kuna tatizo basi jitahidi ulitatue sio kuomba jirani akutatulie

Acha kunifuata fuata. Toa hoja zako badala ya kunifuata fuata mimi.

Mimi si natoa habari za Mbeya ambazo ndio zimekukoroga kichwa chako mpaka unaanza kunifuata fuata? Jibu hoja zangu na achana na kufuata mtu.

JF kila mtu ana maeneo yake ya kujidai; maeneo ambayo ana data zake.
 
Last edited by a moderator:
Hakuna cha kufika hapo NCCR mwaka 1995 ilikuwa chachu kuliko leo 2010 CHADEMA. Huwezi kusema watu ndio wanaanza kuamka wakati 1995 tuliona wabunge wengi wa upinzani.Kusema hivyo nikujaribu kujidaganya tu.

Ya NCCR ilikuwa ni ushabiki wa MREMA na KUITIKA UPEPO WA MABADILKO DUNIANI..

Ya CHADEMA yanaendana na hali ya sasa nchini, kukuwa kimtazamo kuhusu umuhimu wa vyama vya upinzani na pia kukuwa kiasasi kwa chama hicho.....ni wazi kuwa kuna kila ya uwezekano wa mabadiliko haya kuwa ni endelevu......

omarilyas
 
Uwiano Maalum,

kwa nilivyoona mimi, tofauti kati ya Tarime na Busanda ni Malecela.

Unaweza usikubaliane na mimi lakini ndio conclusion yangu. Sisemi niko sahihi maana haya mambo huwezi kujua kama uko sahihi au la, lakini naamini Malecela kaisaidia CCM ishinde.
 
mabadiliko yanaanzia mjini na ndio maana ccm wanaishikilia dar hata kwa nini hawata iachia
siasa haina tofauti na mambo mengine kama matangazo na new products, zikiwa kiboko mijini basi hata vijijini pia..

population puzzle, kuna mtu anaweza kunielezea hii vizuri
population statistics zinaonyesha mjini kuna watu wengi sana lakini ikifika wakati wa uchaguzi mambo yanabadilika na kuanza kusema vijijini kuna watu wengi... mimi sielewi kabisa
 


Malecela kaisaidiaje CCM kushinda?
 
Acha kunifuata fuata. Toa hoja zako badala ya kunifuata fuata mimi.

Mimi si natoa habari za Mbeya ambazo ndio zimekukoroga kichwa chako mpaka unaanza kunifuata fuata? Jibu hoja zangu na achana na kufuata mtu.

Wewe si umetoa hoja yako ya kutufundisha na mimi nimesema kuwa sisi sio wanafunzi wako hivyo hayo unayotufundisha fanya wewe mwenyewe! unafura du! . sawa mimi ni mshamba nimekubari

By the way Dr anaendele vyema!
 

Chadema imezaliwa lini Chama karibu zaidi ya miaka 17 hakijaweka matawi huo ndicho nini Ruzuku wanazipeleka wapi?

Huwezi niambia kazi ya kuikombowa TZ sio CHADEMA,CUF na CCM ukasema ni yangu hizo ruzuku za nini? wanipe hizo ruzuku wanazopata ili nipigane uhuru wetu.

Kifupi Hii nchi ni yetu sote lakini ktk upiganaji lazima kuwe na model ambayo iko ktk hierachy yani ya kwamba kila layer fulani inafanya kazi fulani mimi LAYER yangu ni kutoa pesa yani kama kodi ili CHADEMA wapate RUZUKU kwa hizo ruzuku wajidhatiti na uhuru upatikane.

Kusema eti nisiwalaumu wakati mimi ROLE yangu ktk Layer yangu nimeikamilisha na ROLE yao imewashinda ktk layer yao UNANITUSI kwa namna moja ama nyingine.
 
Kushinda mmeshinda,lakini cha moto mmekiona.Kwa ufupi niwape hongera CHADEMA kwani ni chama ambacho kinakuwa kwa haraka,na CCM kimedumaa.Big up viongozi wa CHADEMA.
 
Wewe si umetoa hoja yako ya kutufundisha na mimi nimesema kuwa sisi sio wanafunzi wako hivyo hayo unayotufundisha fanya wewe mwenyewe! unafura du! . sawa mimi ni mshamba nimekubari

By the way Dr anaendele vyema!

Shalom,

Please ondoa ujinga wako hapa!

Dr kuendelea salama kuna uhusiano gani na thread hii?

Waambie wana JF unachotaka kusema; waambie ile ajali ulikuwa mkono wa Mtanzania.

Pure nonsense! Inatakiwa ukapimwe akili yako.
 
FMES na Williams wameishakusoma mkuu.....

Guys!!! for once we have to be true.... aliyechangia chachu ya yote ni magufulu

Can we have a little repsect to JOHN POMBE MAGUFULI.... wa ndani mnanisoma vilivyo!!!!!
 

Mjini CHADEMA wana majimbo mangapi? acha hizo
 
Samahani Busanda hakuna umeme na ki E90 changu kilichemsha sasa ndio nimerudi hewani na matokeo ndio hayo mliyoyasikia.
Nakuomba uendelee kuniaminia kwa sababu ni hakika bila mashaka mimi sio mshabiki wa chama chochote bali ni pro-democracy ambaye ningependa kuona upinzani unashinda ili kuongeza wigo wa demokrasia ndani ya bunge.
Naamini pia kuna wana CCM ma pro-democracy hawafurahii bunge la upande mmoja.
Nililisisitiza niliyoaandika ndiyo niliyo yashuhudia kwa kumbukumbu yangu ya jana, Mji mzima wa Katoro ulimezwa na Chadema na CCM walikuwa wanatilisha huruma.
Ukiweza kuyasoma yale masaa yangu 48 ya juzi na jana, ukijumlisha na matokeo ya leo, huna sababu za kuwa na mashaka na impartiality yangu na bado nasisitiza mimi ni realist tatizo ambalo nalikubali, visio yangu ilikuwa myopic iliyoishia mijini kumbe vijijini it was the other way round.
 
Shalom,

Please ondoa ujinga wako hapa!

Dr kuendelea salama kuna uhusiano gani na thread hii?

Waambie wana JF unachotaka kusema; waambie ile ajali ulikuwa mkono wa Mtanzania.

Pure nonsense! Inatakiwa ukapimwe akili yako.

Samahani nilikuwa ninakupa habari tu wa port nilizani hujui maana nimetoka kumtembelea muda sio mrefu kama umekwazika samahani sana. Mimi nilifikiri utashukuru kwa update hiyo na si wewe umetufundisha muda siyo mrefu kuwa tuwe tunaleta habari ambazo ni za uwakika. Hiyo habari ni ya uwakika na ni ya kushuhudia kwa macho.

Mimi akili yangu iko salama kabisa asante kwa ushauri wako port. Vipi utagombea Kyela?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…