Kuna tuhuma kuwa kule Tarime Kamati ya siasa wilaya Tarime ikiongozwa na mwenyekiti wake anaefahamika kama Ngicho, mkuu wa wilaya, wabunge pamoja na viongozi wengine wa chama waliwaamuru vijana wa CCM (Green guard) kuwashambulia walimu wa shule ya msingi Nkende baada kutokea kutokuelewana baina yao na walimu, vile vile kaimu afsa elimu aliyekuwa anapinga walimu hao kushambuliwa na green guard nae alipokea kichapo toka kwa vijana hao.
Kwa mujibu wa chanzo changu cha habari waandishi waliokuwepo katika msafara huo walipigwa stop kuripoti tukio huku walimu hao wakinyimwa PF3 kwa ajili ya kupata matibabu, chanzo changu kinaendelea kutabainisha kuwa walimu hao wamepewa vitisho wasiongee na chombo chochote cha habari, na mkuu wa mkoa wa Mara, Mtanda amefika leo kusawazisha mambo.
Kwa mujibu wa chanzo changu cha habari waandishi waliokuwepo katika msafara huo walipigwa stop kuripoti tukio huku walimu hao wakinyimwa PF3 kwa ajili ya kupata matibabu, chanzo changu kinaendelea kutabainisha kuwa walimu hao wamepewa vitisho wasiongee na chombo chochote cha habari, na mkuu wa mkoa wa Mara, Mtanda amefika leo kusawazisha mambo.