1000 digits
JF-Expert Member
- Oct 16, 2012
- 7,802
- 10,304
Nimeelezwa na mnyetishaji wangu kuwa kimbunga cha vijukuu wawili wa Mungu, Tundu Lissu na John Heche kimeleta tafrani isiyo ya kawaida huko CCM.
Support kubwa waliyopata CHADEMA kwenye mikutano waliyofanya Kanda ya Nyasa tu inasemwa kusababisha watu kulala na viatu huko CCM.
Kujitokeza kwa wananchi wengi hadi vijijini ambao wameweka nadhiri ya kuzuia uchaguzi imeelezwa kuwatisha sana CCM ambao kiuhalisia hawana majeshi ya kutosha kuwazuia wananchi endapo wakiamua kuuzuia uchaguzi.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Kwa mujibu wa mnyetishaji wangu, CCM imemwagwa hela nyingi sana kwa mapandikizi yao yaliyopo CHADEMA ili tu wafanye lolote liwezekanalo Chama kisiendelee na ajenda ya NO REFORM NO ELECTION. Pamoja na hela CCM pia imetoa ahadi ya ajira kwa mapandikizi hayo ambayo inasemwa kuwa hawana uwezo wowote ule wa kufanya lolote lile kwa sasa kwa sababu wananchi wa Tanzania kwa sasa huwezi kuwaambia chochote juu ya Lissu na Heche kutokana na umahiri wao na misimamo yao thabiti.
Baadhi ya maelekezo waliyopewa mapandikizi hao ni kuleta fujo na kuibua hisia za mifarakano kwenye chama pamoja na kuibua maneno ya kumuondoa Mwenyekiti Madarakani.
Kutokana na kuwa desperate sana, nimeelezwa pia kuwa CCM imetoa amri zitoke ajira zaidi ya 5000 Jeshi la Polisi ili tu wadhibiti Uchaguzi.
Mnyetishaji wangu kamaliza kwa kuniambia, vyovyote vile lazima mwaka huu ajenda ya No Reform No Election ifanikiwe maana hata wenye akili kwenye system wameshawachoka CCM na upuuzi wao.
Mungu wabariki na kuwalinda Tundu Lissu na John Heche.
Polisi 5000 kati yao 2500 toka Kongo na 2500 toka Burundi .
Sio fair kabisa . Tatizo la Ajira kwa Kongo sio kubwa kama kule Kongo kulingana na uwiano wa idadi ya watu.
Wakati huo huo watawala wa Burundi wanauza Ardhi yote ya Kongo kwa wageni ili badae Wakongo wawe watumwa wa wageni kwenye nchi yao .Rais wa Kongo ambaye ni Mrundi akipewa miaka mitano tena ataliangamiza taifa la Kongo.