CCM: Tuna madiwani 16 Arusha

Haya mkuu huyu aliye defect anahesabika upande upi? Umeeeleza vizuri

Mimi nimeongelea mgawanyo wa madiwani baada ya uchaguzi.

Huyu aliyejiuzulu ina maana kata haina diwani mpaka hapo uchaguzi utakapofanyika. Kwahiyo CCM itakuwa na madiwani 9 wa kuchaguliwa, CHADEMA 8 na TLP 1.

Ukiacha wabunge wa viti maalum bado CCM itakuwa na madiwani 13 na CHADEMA 12.
 
Wewe ni hopeless kabisa eti tumuulize Mwanakijiji inavyoonekana hata ukipigwa na mkeo huwa unamshitaki kwa MKJJ hovyoooo, kwanza takwimu zako feki hujui wabunge nao ni madiwani kwenye mikoa yao.

Uzuri wa dunia hii time ndio mwamuzi wa mambo mengi. Nina uhakika sio muda mrefu kila mtu atajua kati ya mimi na wewe nani ni hopeless.
 
Uzuri wa dunia hii time ndio mwamuzi wa mambo mengi. Nina uhakika sio muda mrefu kila mtu atajua kati ya mimi na wewe nani ni hopeless.
Mna nyimbo tamu sana nyie na akina Makamba eti time, tuliambiwa hivyo hivyo Kigoma Mjini, time ikafika, wakatuambia hivyo hivyo Mwanza time akawatembelea huko, wakatuambia mzee time hajafika Hai walifikiri hatakuja milele jana kafika huko, yaleyale unatuambia Arusha eti time itafika unafikiri ni mbali sana, mtakimbia mmoja mmoja humu.
 
Naulza: Hivi Hizza anaposema CCM ina Wabunge 3 ambao ni madiwani, ni wa wapi hao? bila shaka ni kutoka majimbo ya uchaguzi yale mengine ya mkoa wa Arusha yaani wilaya nyingine ambazo zina halmashauri zao na hivyo wanakuwa madiwani wa huko. Kadhalika hao wabunge wa chadema ambao pia ni madiwani kisheria.

Au tuseme 'madiwani' wa namna hii ambao ni wabunge hujichagulia wenyewe waende halmashauri gani wakapige kura?

Lazima kuna kanuni kuhusu hili ama sivyo mambo yatakuwa shghala baghala.

Nawasilisha

Marksman,

Hili la wabunge watatu nafikiri Tambwe kakosea kama ninavyofahamu mimi ni sahihi (naweza kuwa wrong). Nafikiri CCM ina wabunge wa viti maalum wawili ambao ni huyo mtoto wa Sokoine pamoja na mama huyu wa Tanga. Ila ina madiwani wa kuteuliwa wanne na sio watatu kama alivyosema. Ila namba ya mwisho kweli ni 16. Hiyo ilikuwa kabla ya yule aliyejiuzulu na ambaye kwa sheria itabidi uchaguzi urudiwe kwenye kata yake.

Kinachowachanganya watu ni kwamba huyu mama Chatanda aligombea ubunge ndani ya CCM kupitia mkoa wa Tanga. Huo ulikuwa ni uchaguzi ndani ya CCM. NEC haina wabunge wa mikoa kwenye viti maalum. Kwa mfano mtu anaweza kunitajia hapa wabunge wa CHADEMA wa mikoa ni akina nani?

Wakati CHADEMA walitumia vigezo vya elimu na ushiriki kwenye chama, CCM waligawa viti kwenye makundi mbalimbali na kisha kupigiwa kura kwenye kundi. Sio kweli kwamba kwasababu huyo mama ndani ya CCM alichaguliwa kupitia kundi la mkoa wa Tanga basi yeye ni viti maalum Tanga. Hapana, NEC hawalijui hilo na wote wanajulikana kama wabunge wa viti maalum CCM, au CHADEMA au CUF. Hivyo wapi anashiriki inategemea zaidi anakoishi.

Sheria inasema chama ndio kinaiambia halmashauri kwamba tuna mbunge wetu kwenye mji wako ambaye atatimiza majukumu yake kama diwani kwenye mji huu. Kikawaida hao wabunge viti maalum wanashiriki udiwani kwenye sehemu wanazoishi. Sasa huyo mama anaishi Arusha kabla ya uchaguzi na mpaka sasa, mnataka awe anaenda Tanga kila wiki kuhudhuria vikao kule?

Kama hii sheria ni mbovu basi ibadilishwe, lakini kwa sheria iliyopo huyo mama ana sifa zote za kuwa diwani Arusha.
 
Quinine,

Ninakuaminia sana kwa mambo ya Chadema. Ila kama mnataka kuwa tofauti na CCM, kama mnataka kuwa tofauti na POLISI WA TZ, kama mnataka kuwa tofauti na Kikwete, kama mnataka kuwa tofauti na Makamba nk basi ni LAZIMA muwe mnasikiliza wengine.

Mkulima kaweka POINT nzito na ushahidi wa waziwazi. Kuanza tu kurusha matusi ya mtu kupigwa na mkeo, inanikumbusha Makamba zaidi kuliko Quinine ninayemfahamu siku nyingi hapa. Tuwe tunatofautisha CCM aina ya akina MS na watu wanaokuja na POINT nzito.

Nimesoma na kufuatilia maneno ya Mkulima na kwa mbali naanza kukubaliana naye. Kwanza ni kweli CCM waliwazidi CDM kwenye Madiwani wa kuchaguliwa. Pili kama utakumbuka maneno ya Regia, aliamua KUIWAKILISHA Chadema kwao kilombero ingawa anaishi Dar. Angeliweza kabisa kuwa mbunge wa kuteuliwa na kuwa anafanya kazi zake Dar ila (kumbuka maneno yake), yeye ALIAMUWA kuwa KILOMBERO.

Labda hapa Chadema walifanya makosa. Wangeliweza kuwachukua akina Regia na kuwaandikisha kama wakazi wa Arusha.

Kuna haja ya KUWAONDOA hawa wabunge wa kuteuliwa kwenye mambo ya MADIWANI maana watakuwa wanaleta MATATIZO kila mwaka. Kwa mfano kwa Mwanza, wangeliweza kuwachukua wabunge kibao wa kuteuliwa Mwanza ili washinde kwenye uchaguzi wa madiwani na mwisho wawe na Meya wa Mwanza.

Katika Mabadiliko ya KATIBA, kuna haja ya hii kitu pia ibadilishwe ili KUPUNGUZA vyama vya siasa KU-FIX matokeo.

MKULIMA: Labda tu niseme kuwa SI KWELI kuwa unawakilisha TU sehemu unayokaa. Regia anaishi Dar ila anawakilisha Kilombero. Nafikiri inategemea baada ya kuchaguliwa, unataka kuwakilisha wapi. Nakubaliana na wewe kuwa inabidi kuandikisha utawakilisha jimbo lipi maana kuna wale hawakugombea kabisa ubunge na wamechaguliwa. Sasa hawa watawakilisha wapi zaidi ya sehemu wanayotaka wao kuwakilisha (na mara nyingi ili kurahisisha maisha - SEHEMU WANAZOISHI.)

Wewe ni hopeless kabisa eti tumuulize Mwanakijiji inavyoonekana hata ukipigwa na mkeo huwa unamshitaki kwa MKJJ hovyoooo, kwanza takwimu zako feki hujui wabunge nao ni madiwani kwenye mikoa yao.
 
Sio kweli kwamba kwasababu huyo mama ndani ya CCM alichaguliwa kupitia kundi la mkoa wa Tanga basi yeye ni viti maalum Tanga. Hapana, NEC hawalijui hilo na wote wanajulikana kama wabunge wa viti maalum CCM, au CHADEMA au CUF. Hivyo wapi anashiriki inategemea zaidi anakoishi.

Mkulima with the quoted argument ina maana basi wabunge say wa viti maalum wa CDM wangeamua wote kulundikana say Ilala ili wapate Meya wao ingewezekana? na ingekuwa sahihi? Kwa nini kipindi kile kuna mvutano wa umeya Kigoma (Nadhani huundiyo ulikuwa mvutano wa kwanza) CCM haikupeleka wabunge viti maalum kutoka majimbo mengine kuokoa jahazi?

Above all kwa nini uchaguzi wa Meya Arusha ulikuiwa na vizia vizia iliyopelekea hali hii kutokea. If what u have just said is right na mshindi anapatikana kwa simple majority assuming madiwani wote wa CCM ni loyal kwa chama chao kulikuwa na haja gani ya kuwa na huyo Chitanda maana with numbers bado CCM ingeshinda tu?
 
Quinine,

Ninakuaminia sana kwa mambo ya Chadema. Ila kama mnataka kuwa tofauti na CCM, kama mnataka kuwa tofauti na POLISI WA TZ, kama mnataka kuwa tofauti na Kikwete, kama mnataka kuwa tofauti na Makamba nk basi ni LAZIMA muwe mnasikiliza wengine.

Mkulima kaweka POINT nzito na ushahidi wa waziwazi. Kuanza tu kurusha matusi ya mtu kupigwa na mkeo, inanikumbusha Makamba zaidi kuliko Quinine ninayemfahamu siku nyingi hapa. Tuwe tunatofautisha CCM aina ya akina MS na watu wanaokuja na POINT nzito.

Nimesoma na kufuatilia maneno ya Mkulima na kwa mbali naanza kukubaliana naye. Kwanza ni kweli CCM waliwazidi CDM kwenye Madiwani wa kuchaguliwa. Pili kama utakumbuka maneno ya Regia, aliamua KUIWAKILISHA Chadema kwao kilombero ingawa anaishi Dar. Angeliweza kabisa kuwa mbunge wa kuteuliwa na kuwa anafanya kazi zake Dar ila (kumbuka maneno yake), yeye ALIAMUWA kuwa KILOMBERO.

Labda hapa Chadema walifanya makosa. Wangeliweza kuwachukua akina Regia na kuwaandikisha kama wakazi wa Arusha.

Kuna haja ya KUWAONDOA hawa wabunge wa kuteuliwa kwenye mambo ya MADIWANI maana watakuwa wanaleta MATATIZO kila mwaka. Kwa mfano kwa Mwanza, wangeliweza kuwachukua wabunge kibao wa kuteuliwa Mwanza ili washinde kwenye uchaguzi wa madiwani na mwisho wawe na Meya wa Mwanza.

Katika Mabadiliko ya KATIBA, kuna haja ya hii kitu pia ibadilishwe ili KUPUNGUZA vyama vya siasa KU-FIX matokeo.

MKULIMA: Labda tu niseme kuwa SI KWELI kuwa unawakilisha TU sehemu unayokaa. Regia anaishi Dar ila anawakilisha Kilombero. Nafikiri inategemea baada ya kuchaguliwa, unataka kuwakilisha wapi. Nakubaliana na wewe kuwa inabidi kuandikisha utawakilisha jimbo lipi maana kuna wale hawakugombea kabisa ubunge na wamechaguliwa. Sasa hawa watawakilisha wapi zaidi ya sehemu wanayotaka wao kuwakilisha (na mara nyingi ili kurahisisha maisha - SEHEMU WANAZOISHI.)

Mkuu Sikonge If this is the case, Conclusion inayonijia haraka haraka in my own opinion ni kwamba hawa wabunge wa viti maalumu hawaiwakilishi demokrasia period!!
 
Uzuri wa dunia hii time ndio mwamuzi wa mambo mengi. Nina uhakika sio muda mrefu kila mtu atajua kati ya mimi na wewe nani ni hopeless.
Mkulima;

kwanza sio kweli kama Mbunge wa viti maalum hawana sehemu wanazotambuliwa ndani ya mamlaka zao;kwa mfano mbunge wa viti maalum Hilda Ngoye yeye anapiga kura yake kumchagua meya wa Mbeya tu kama ilivyo Zabida Masaburi kwa Dar;Mama Chitanda alipita kama Mbunge Maalum CCM Tanga na anapaswa kupiga kura yake Tanga tu kama ilivyo kwa Ms Bilal kupiga kura yake ZNZ.

Mkulima;

CCM ilikuwa na wapiga kura 17 kwenye uchaguzi ule wa kinyemela.Ukimtoa Mamluki Mama Mary Chitanda wa Tanga aliyekuja kupiga kura ARusha basi CCM itabaki na wapiga kura halali 16.Ukimtoa diwani wa TLP aliyeshiriki na CCM kabla ya kujizuru basi CCM inabaki na wapiga kura halali 15 tu na ukimtoa diwani wa CCM aliyejizuru juzi basi CCM inabaki na wapiga kura 14 tu halali!

Mkulima;

Kwa mtiririko huo basi ni wazi unajua sasa kwa nini CCM inamleta mamluki toka Tanga kuja kupiga kura Arusha!
 
Na ofcourse kama this is the case ile vizia vizia ya kufanya uchaguzi ilikuwa ya nini. Na kwa nini waligoma kurudia uchaguzi wakati wao wana madiwani wengi?

hapakua na vizia vizia ila chadema ndo waligoma kufanya uchaguzi tarehe 17 kwa madai yao wenyewe ukaahirishwa siku ya pili chadema hawakuonekana unataka CCM wafanye nini. CHADEMA inaona yenyewe ndo wanajua sana na wanahaki sana ndo kitu kinachowa gharimu
 
Dunderheads........

accm03.JPG
 
This is all confusing.... please anayejua naomba anijibu Je ni kweli mbunge wa Viti maalumu anaruhusiwa kuwakilisha Jimbo lolote???, Na CCM na Chadema wana Viti Vingapi??? please HELP am now more confused after reading this topic than I was before :A S confused::kev:
 
MKULIMA: Labda tu niseme kuwa SI KWELI kuwa unawakilisha TU sehemu unayokaa. Regia anaishi Dar ila anawakilisha Kilombero. Nafikiri inategemea baada ya kuchaguliwa, unataka kuwakilisha wapi. Nakubaliana na wewe kuwa inabidi kuandikisha utawakilisha jimbo lipi maana kuna wale hawakugombea kabisa ubunge na wamechaguliwa. Sasa hawa watawakilisha wapi zaidi ya sehemu wanayotaka wao kuwakilisha (na mara nyingi ili kurahisisha maisha - SEHEMU WANAZOISHI.)

Mkuu Sikonge,

Achana na hao watukana matusi na ndio wanafanya watu wengi wenye info wakae kimya na mwisho wake watu wanabaki kushangilia jambo kumbe ni makosa.

Regia yeye ndiye ameamua atumie haki yake ya kikatiba kuwa diwani kule Kilombero. Angeweza kuamua kutumia haki hiyo Dar. Kwenye viti maalum CHAMA ndio kinaijulisha halmashauri kwamba mbunge wao fulani anaishi kwenye hiyo halmashauri na atakuwa diwani hapo.

Kwa mheshimiwa Regia ina make sense kuamua kuwa Kilombero kwasababu ana interest na Kilombero na si ajabu anataka kugombea tena huko 2015.

Kikatiba angeliweza kabisa kuwa diwani wa manispaa za Dar kama angelipenda.

Cha kufurahisha CHADEMA wametumia kifungo hicho kibovu wanachokipinga kushinda umeya kule Hai. Kama una muda nenda kasome gazeti la Mtanzania Daima. CCM wamejitetea wee lakini wakaambiwa sheria ni msumeno. CHADEMA wameamua wanawake wao wawili viti maalum wawe madiwani Hai.
 
This is all confusing.... please anayejua naomba anijibu Je ni kweli mbunge wa Viti maalumu anaruhusiwa kuwakilisha Jimbo lolote???, Na CCM na Chadema wana Viti Vingapi??? please HELP am now more confused after reading this topic than I was before :A S confused::kev:

Jibu ni NDIYO. Hiyo sheria haikuwa na utata huko nyuma kwasababu CCM ilikuwa na viti vingi muda wote.

Hiki kifungu hata CHADEMA wenyewe wamekitumia kule Hai na hata Arusha. Iweje katika wabunge wao 30 wa viti maalum waweke 2 katika halmashauri moja wakati kuna halmashauri zaidi ya 200? Jibu ni kwamba wamewaweka kule ambako wanajua inawasaidia zaidi.

CHADEMA wana around 30 na CCM around 67.
 
Mkulima with the quoted argument ina maana basi wabunge say wa viti maalum wa CDM wangeamua wote kulundikana say Ilala ili wapate Meya wao ingewezekana? na ingekuwa sahihi? Kwa nini kipindi kile kuna mvutano wa umeya Kigoma (Nadhani huundiyo ulikuwa mvutano wa kwanza) CCM haikupeleka wabunge viti maalum kutoka majimbo mengine kuokoa jahazi?

Above all kwa nini uchaguzi wa Meya Arusha ulikuiwa na vizia vizia iliyopelekea hali hii kutokea. If what u have just said is right na mshindi anapatikana kwa simple majority assuming madiwani wote wa CCM ni loyal kwa chama chao kulikuwa na haja gani ya kuwa na huyo Chitanda maana with numbers bado CCM ingeshinda tu?

Kwa katiba iliyopo hilo lingewezekana. Ingawaje mpaka sasa vyama vimekuwa responsible kidogo kwa kupanga hawa wabunge kule wanakoishi au kule wanakotoka.

Mbunge wa viti maalum wapi anaenda kuwa diwani inategemea yeye mwenyewe na chama cheke. NEC haina habari huyo mbunge anawakilisha nini.

Mara nyingi hawa wabunge wanakuwa na interests zao sehemu fulani na huko ndiko wanawakilisha.

Kwasasa hii sheria ni mbovu na inabidi ibadilishwe ili wajanja wasiitumie vibaya.

Kama huyo mama Chatanda, yeye anaishi Arusha, na alikuwa anaishi huko hata kabla ya uchaguzi, kweli mnataka akatumie haki yake ya udiwani Tanga? Hiyo ina maana kusafiri masaa mengi sana kwenda kwenye vikao.
 
Mkulima;

kwanza sio kweli kama Mbunge wa viti maalum hawana sehemu wanazotambuliwa ndani ya mamlaka zao;kwa mfano mbunge wa viti maalum Hilda Ngoye yeye anapiga kura yake kumchagua meya wa Mbeya tu kama ilivyo Zabida Masaburi kwa Dar;Mama Chitanda alipita kama Mbunge Maalum CCM Tanga na anapaswa kupiga kura yake Tanga tu kama ilivyo kwa Ms Bilal kupiga kura yake ZNZ.

Mkulima;

CCM ilikuwa na wapiga kura 17 kwenye uchaguzi ule wa kinyemela.Ukimtoa Mamluki Mama Mary Chitanda wa Tanga aliyekuja kupiga kura ARusha basi CCM itabaki na wapiga kura halali 16.Ukimtoa diwani wa TLP aliyeshiriki na CCM kabla ya kujizuru basi CCM inabaki na wapiga kura halali 15 tu na ukimtoa diwani wa CCM aliyejizuru juzi basi CCM inabaki na wapiga kura 14 tu halali!

Mkulima;

Kwa mtiririko huo basi ni wazi unajua sasa kwa nini CCM inamleta mamluki toka Tanga kuja kupiga kura Arusha!

Malafyale,

Mama Ngoye anatumia haki yake Mbeya kwasababu ndiko anakoishi. Angeweza kuamua kutumia hiyo haki Dar wala asingelikuwa amevunja sheria.

Unachagua halmashauri moja na huwezi kuwa na halmashauri mbili. Wengi wanachagua kwao kwasababu either wanaishi huko na hivyo rahisi kuhudhuria vikao au wana interests zao huko.

Kwa mfano mama Ngoye anajua ndani ya CCM kapata hiyo nafasi kupitia mkoa wa Mbye; ina make sense kuwa diwani Mbeya ili awe karibu na waliompa nafasi maana miaka mitano sio mingi.

Kwa Chatanda kwasababu kikazi yuko Arusha nafikiri alikuwa hana ujanja isipokuwa kuchagua Arusha maana huko Tanga angelikuwa anaenda mara ngapi?

Soma CHADEMA walichofanya Hai na utaelewa zaidi juu ya sheria hii. Huko mbele itabidi ibadilishwe ili kuzuia chama kimoja kisihamishie wabunge wake wote kwenye halmashauri moja.

Lakini ujanja kama huo unaweza usifanye kazi. Kwa mfano kule Hai kama sikosei CHADEMA wana madiwani 8 na mbunge na viti maalum 2 jumla 11. CCM wana madiwani 11. Vikao vya halmashauri mara nyingi vinaenda sambamba na vikao vya bunge. CCM wakitaka wanaweza kukwamisha kabisa shughuli za halmashauri ya hai maana wao watakuwa 11 huku CHADEMA wako 8. Wabunge haitawezekana kila wiki kukimbilia Hai kwenda kuokoa jahazi.

Tunapoteza muda mwingi kutumia kila mbinu kupata meya lakini pia tuangalie je ni rahisi kuongoza hiyo miji kama namba hazikubali? mahali ambapo wamekaribiana sana, wangetumia walichofanya Kigoma baada ya uchaguzi wa 2005.
 
hapakua na vizia vizia ila chadema ndo waligoma kufanya uchaguzi tarehe 17 kwa madai yao wenyewe ukaahirishwa siku ya pili chadema hawakuonekana unataka CCM wafanye nini. CHADEMA inaona yenyewe ndo wanajua sana na wanahaki sana ndo kitu kinachowa gharimu

Nasikia kuna issue ya "quorum" kwenye kanuni za uchaguzi inayohitaji wapiga kura (madiwani) wawe 2/3 ya wapiga kura ndio uchaguzi uendeshwe....Hili vipi kuna ukweli kwenye hili? Ukichukua 16( CCM) na 14(CDM) unapata 30, 16/30 X100 = 57% haifiki 66% inayotakiwa ili uchaguzi uendelee.
 
Mkuu Sikonge,

Achana na hao watukana matusi na ndio wanafanya watu wengi wenye info wakae kimya na mwisho wake watu wanabaki kushangilia jambo kumbe ni makosa.

Regia yeye ndiye ameamua atumie haki yake ya kikatiba kuwa diwani kule Kilombero. Angeweza kuamua kutumia haki hiyo Dar. Kwenye viti maalum CHAMA ndio kinaijulisha halmashauri kwamba mbunge wao fulani anaishi kwenye hiyo halmashauri na atakuwa diwani hapo.

Kwa mheshimiwa Regia ina make sense kuamua kuwa Kilombero kwasababu ana interest na Kilombero na si ajabu anataka kugombea tena huko 2015.

Kikatiba angeliweza kabisa kuwa diwani wa manispaa za Dar kama angelipenda.

Cha kufurahisha CHADEMA wametumia kifungo hicho kibovu wanachokipinga kushinda umeya kule Hai. Kama una muda nenda kasome gazeti la Mtanzania Daima. CCM wamejitetea wee lakini wakaambiwa sheria ni msumeno. CHADEMA wameamua wanawake wao wawili viti maalum wawe madiwani Hai.
Mkulima

Nitaendelea kukuita mpuuzi na hopeless kama utakuwa ukijitetea kwa kuomba usaidizi kwa MKJJ kwani yeye ndiye kipimajoto chako kwanini usijiamini 'inferiority complex', ndiyo maana nikakuambia inawezekana hata ukipigwa na mkeo utakimbilia kwa MKJJ.

Usifikiri mimi ni sawa na MS huwa nabadilika kuendana na wakati na kuendana na mtu ukijifanya kichaa nakuwa kichaa huwa sifichi kwa hilo.

Nevertheless, utetezi wako wa madiwani nimekuamba ni feki umebase kwa takwimu za kina Makamba na Tambwe ambazo ndizo zinazolalamikiwa na wewe unachukulia ni za ukweli kama hivyo kwanini hawakuitisha uchaguzi halali wa wazi wakakimbilia vifichoni.

Mbali ya kukiukwa kanuni za uchaguzi yaani 2/3, CCM walikuwa na jumla ya wapigakura madiwani halali 15 tu ukiondoa mamluki wa Tanga ambaye wewe unamhesabu. Juzi kajiuzulu mmoja wamebaki 14.

Mambo ya Sikonge yaache wengine tunamjua anajifanya kubeba bendera ya CDM na signature nzurinzuri lakini hana lolote, kwenye issue muhimu yeye huingiza regae zake ku deflect tension za watu.
 
Mkulima

Nitaendelea kukuita mpuuzi na hopeless kama utakuwa ukijitetea kwa kuomba usaidizi kwa MKJJ kwani yeye ndiye kipimajoto chako kwanini usijiamini 'inferiority complex', ndiyo maana nikakuambia inawezekana hata ukipigwa na mkeo utakimbilia kwa MKJJ.

Usifikiri mimi ni sawa na MS huwa nabadilika kuendana na wakati na kuendana na mtu ukijifanya kichaa nakuwa kichaa huwa sifichi kwa hilo.

Nevertheless, utetezi wako wa madiwani nimekuamba ni feki umebase kwa takwimu za kina Makamba na Tambwe ambazo ndizo zinazolalamikiwa na wewe unachukulia ni za ukweli kama hivyo kwanini hawakuitisha uchaguzi halali wa wazi wakakimbilia vifichoni.

Mbali ya kukiukwa kanuni za uchaguzi yaani 2/3, CCM walikuwa na jumla ya wapigakura madiwani halali 15 tu ukiondoa mamluki wa Tanga ambaye wewe unamhesabu. Juzi kajiuzulu mmoja wamebaki 14.

Mambo ya Sikonge yaache wengine tunamjua anajifanya kubeba bendera ya CDM na signature nzurinzuri lakini hana lolote, kwenye issue muhimu yeye huingiza regae zake ku deflect tension za watu.

Quinine,
Mimi siko interested kujua nani kashinda umeya Arusha au kama uchaguzi ulikuwa halali au sio halali. Nilichofanya ni kuweka facts ambazo mimi nazijua.

Sasa kama unaona ninachosema sio kweli basi lete facts zako.

Kwenye ujumbe wangu niliongelea facts mbili tu. Kwanza ni hiyo ya kwamba CCM walikuwa na madiwani 16 wanaotambuliwa kisheria wakati CHADEMA walikuwa na 14 na TLP 1.

Pili, kulingana na katiba huyo mama wa Tanga ni mjumbe halali wa hilo baraza la jiji la Arusha.

Suala la kujiuzulu ni mpaka mkurugenzi wa jiji akitangaza na baada ya hapo uchaguzi utaitishwa.

Sasa kama una facts ambazo zinaonyesha nilichoandika hapo juu si sawa basi leta na tutajadili. Nilitumia Mwanakijiji au Mbunge wa CHADEMA kama reference; kwenye mijadala ya kisomi reference ni kitu kinachokubalika. Nategemea hao watu kwasababu ya kazi ambazo wanafanya au wamewahi kufanya huko nyuma wawe na uwezo wa kuzielewa sheria zetu kuliko mtu wa kawaida. Kama kwa kuandika hivyo nakuwa hopeless, well, that is your opinion sir na haitanikosesha usingizi hata tone.
 
Malafyale,

Mama Ngoye anatumia haki yake Mbeya kwasababu ndiko anakoishi. Angeweza kuamua kutumia hiyo haki Dar wala asingelikuwa amevunja sheria.

Unachagua halmashauri moja na huwezi kuwa na halmashauri mbili. Wengi wanachagua kwao kwasababu either wanaishi huko na hivyo rahisi kuhudhuria vikao au wana interests zao huko.

Kwa mfano mama Ngoye anajua ndani ya CCM kapata hiyo nafasi kupitia mkoa wa Mbye; ina make sense kuwa diwani Mbeya ili awe karibu na waliompa nafasi maana miaka mitano sio mingi.

Kwa Chatanda kwasababu kikazi yuko Arusha nafikiri alikuwa hana ujanja isipokuwa kuchagua Arusha maana huko Tanga angelikuwa anaenda mara ngapi?

Soma CHADEMA walichofanya Hai na utaelewa zaidi juu ya sheria hii. Huko mbele itabidi ibadilishwe ili kuzuia chama kimoja kisihamishie wabunge wake wote kwenye halmashauri moja.

Lakini ujanja kama huo unaweza usifanye kazi. Kwa mfano kule Hai kama sikosei CHADEMA wana madiwani 8 na mbunge na viti maalum 2 jumla 11. CCM wana madiwani 11. Vikao vya halmashauri mara nyingi vinaenda sambamba na vikao vya bunge. CCM wakitaka wanaweza kukwamisha kabisa shughuli za halmashauri ya hai maana wao watakuwa 11 huku CHADEMA wako 8. Wabunge haitawezekana kila wiki kukimbilia Hai kwenda kuokoa jahazi.

Tunapoteza muda mwingi kutumia kila mbinu kupata meya lakini pia tuangalie je ni rahisi kuongoza hiyo miji kama namba hazikubali? mahali ambapo wamekaribiana sana, wangetumia walichofanya Kigoma baada ya uchaguzi wa 2005.

Nisahihishe
Katibu wa Chama ngazi ya mkoa ni mtendaji na hivyo ni kazi ya ujira wa mwezi. Mbunge nayo ni kazi ya ujira wa mwezi, kwanini asiachane na Ukatibu wa Chama na kwenda kuwahudumia wale aliowatumia kama ngazi ya kupatia ubunge?
 
CCM huwa wanapenda kutumia watu fulani kama puppets wao one of them ni huyu TAMBWE and the other one is MAKAMBA

Unajua katika maisha hakuna kitu muhimu kama kujitamba wewe ni nani na nafasi yako katika jamii... huyu bwana (TAMBWE) hajitambui yeye ni nani na anatumika vipi katika ccm
 
Back
Top Bottom