CCM Maarufu: Utafiti wa Synovate wabainisha!

CCM Maarufu: Utafiti wa Synovate wabainisha!

Hawa Synovate walikodiwa na CCM kufanya huu utafiti CHADEMA wameichomeka hapo kutimiza malengo ya CCM, lakini mimi sioni shida acha waendelee kujidanganya! Maswali karibia yote yanaihusu CCM, kama Dr. Slaa ndo atakayeshinda ukifanyika uchaguzi, inakuwaje chama chake kisiwe maarufu umaarufu wa chama uwe kwa ccm! Uongo mtupu!

Hii kampuni ni ya kitapeli na wala rushwa wakubwa. Msikubali kuingizwa chaka. Hakuna utafiti hapa ni maandalizi ya kumbeba mtu fulani na kumwangamiza mtu fulani. Dili lote kuna jamaa amesema analifuatilia na akifanikiwa kupata info atawaumbua. Habari za kuaminika ni kuwa hizi ni fedha za mzee mamvi zinaongea. Deal ni kwamba baada ya muda yatatolewa tena matokeo mengine ya kuonyesha Dr. Slaa/wagombea wengine wameshuka kwa percentage fulani na mzee mamvi ameongeza pcg fulani, halafu uchaguzi ukikaribia ndio Mamvi ''atapaishwa'' kwa kasi na kumpita Dr Slaa/wagombea wengine. Tuombe uzima jamaa akifaniwa atatuletea kwa undani na vielelezo vyote.
 
Watu 2∅∅∅ ndo wamefanyiwa utafiti dah wa acheni utani nyie
 
Tatizo humu ndani JF hamkubali labda na nyie mfanye takwimu zenu.
CDM sasa hivi imepoteza mwelekeo, babu hana mvuto tena, asipoangalia atapotea kama alivyopotea Augustine Mrema.

 
Watu 2∅∅∅ ndo wamefanyiwa utafiti dah wa acheni utani nyie

Mie sina tatizo na watu 2000 kuulizwa maswali, halafu utafiti uchapwe na kusema habari hizi zimetokana na utafiti uliofanywa kwa watu 2000. Utafiti huu utakuwa na upungufu wa kuwa na idadi ndogo ya watu lakini matokeo yatakuwa yametolewa in context, unayachambua kwa kujua ni sample ya watu 2000. Tunaona hata kwenye ma articles ya The New York Times, Washington Post na Wall Street Journal wakitoa tafiti kama hizi, with full "caveat emptor".

Tatizo linakuja pale utafiti unapofanywa kwa watu 2,000 , watafiti wakatoa hizo habari, halafu waandishi vilaza wanapoandika "asilimia 52 ya Watanzania wote" kama vile Watanzania wote ndio hao 2000.

Hivi kulikuwa na kazi gani kusema "asilimia 52 ya Watanzania 2000 waliochaguliwa katika utafiti huu...."?

Najiuliza.

Kupindishwa habari huku kumetokea by a malevolent intent or pure ignorance?

Muandishi alijua kwamba utafiti ni wa watu 2000 tu na akataka kupindisha habari isomeke kama utafiti umehusisha Watanzania wote? Inaonekana ni hivyo. Kama muandishi anajua uandishi ilibidi apitie analysis yote na kujua utafiti umefanyika kwa watu 2000 tu, na sio "Watanzania wote"

La, muandishi hajui misingi ya tafiti, na tofauti kati ya "Watanzania 2000" na "Watanzaniawote".

Either way, tatizo letu kubwa sana.

What's next? Tutawaachia watafiti wa ague "Watanzania wote wanataka kiongozi gani" in some Asimovian twist, complete with a Multivac computer reminiscent of "Franchise" na tuahirishe kura kabisa?

Itapunguza sana gharama.
 
Nitakuwa wa mwisho kukubali matokeo ya utafiti huu, hata kama wakisema waliohojiwa ni wafanyakazi wa zile ofisi za pale Lumumba street (DSM) na Chamwino/Chimwaga (Dodoma) bado hakuna reality/uhalisia.

Hii inanikumbusha utafiti wa REDET pale UDSM kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010, baada ya matokeo hata waliokuwa wafadhiri wakuu wa REDET walijitoa maana waliona wanatoa pesa zao nyingi watu/watafiti wanajifungia vyumbani kwa masilahi kikundi fulani wanapika matokeo na mwisho wa siku inakuwa aibu tupu.

Hawa nao hawana jipya, wanafungama na CCM na hata 2010 tafiti zao zilikuwa ovyo. Endeleeni hivyo hivyo ili mwisho wa siku mnakuta chama chenyewe mnachohangaika kukibeba kwa sababu ya njaa zenu mnakuta hakipo, mtakufa njaa maana mtakosa kazi ya kufanya.
 
Kwanza nawasalimu ndugu zangu wote humu JF! Mwenzenu huwa mzimu wa REDET na tafiti zake unaniandama kila nisikiapo neno utafiti.Kuna viji taasisi vinaibuka na kushika kasi kila tunapoelekea kwenye uchaguzi nchini.

Unaweza kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa au uchaguzi mkuu ambapo vitaasisi hivyo hujifanya kutoa tathmini za kisiasa bila kuainisha 'objectives of the study, population size,area of study e.t.c) Kama hutakuwa makini unaweza kuaminishwa ujinga nawe ukapoteza muda kujadili kitu ambacho hakipo ukiacha mambo muhimu kuhusu gesi, uranium, kushuka kwa kiwango cha elimu, migogoro ya ardhi, katiba mpya,vitambulisho vya taifa,vazi la taifa,kilimo na teknolojia eti tunajadili CCM kimekuwa maarufu.

Nahoji, kati ya chama cha zamani na vyama vipya kipi kinaweza kupanda kuwa maarufu? Utafiti wa Synovate ulilenga nini,wametumia vigezo gani kupima umaarufu na wamewahoji watanzania wangapi?

Nielewesheni!
 
Kitu cha kwanza kuangalia katika hizi tafiti ni reputation ya watafiti.

Watafiti wana credibility gani?

Kuna mambo kibao ya kuangalia, lakini ukishathibitisha watafiti wana issues za "conflict of interest" au washanunuliwa huna hata haja ya kuendelea.

Credibility ya watafiti ikoje? Track record? Tafiti zao za nyuma zime pan out vipi with time?

Kabla hata ya kuingia kwenye methodology na sample huko.
 
Hawa ni watafiti njaa tu.Mwaka 2010 walisema CCM ingeshinda kwa 80%.Hawa ni wa kupuuzwa tu
 
Hawa Synovate ni matapeli na wala rushwa wakubwa.
 
Makala Jr

Hawa ni njaa kali tu. Tafiti zao zinaongozwa na matumbo yao. Wasitubabaishe na tafiti pori. Wanakolalia sisi ndiko tulikoamkia. Nimeambiwa utafiti wao mwingine unaofuata Mamvi na Zitto watapanda kidogo halafu Slaa atashuka tena kidogo....
 
Last edited by a moderator:
Molemo. Umenena mkuu,nadhani hawa watu wanatafuta ulaji.Ni vema kwa taifa kuwa na taasisi za utafiti wa kisiasa ambazo ni huru kabisa.CCM ni maarufu siku zote ila siyo imara kama 2000-2010.Labda ndugu zetu wana tafsiri nyingine ya umaarufu.Lakini pia najiuliza,CCM kimekuwa maarufu kwenye nyanja gani na kivipi?
 
Last edited by a moderator:
Ni taarifa muhimu ili kuweza kujipima.
tatizo nilionalo ni sample iliyotumika kujibu na kutoka mawazo. Taarifa AMA utafiti huu ulitakiwa uwe representative. Huwezi kutunisha kifua mbele kwa mawazo ya watu 2000 (N=2000) na kuamini matokeo hayo.
Sensa iliyopita inaonyesha watanzania tuko 40+mil ambapo kama 20% ni watu wazima.
sasa huwezi kusema kuwa raia 2000 wakitoa mawazo yao, wanawakilisha wenzao 20mil.
huu ni upuuzi mtupu!
 
Kumbe hawa ni wakenya, si wangeenda kufanya utafiti wa uchaguzi wao? Tz wanatafuta nini?
 
Watu 2∅∅∅ ndo wamefanyiwa utafiti dah wa acheni utani nyie
 
Mmmh! Hz tafiti sasa tuna mashaka nazo. Lkn yote kwa yote ccm haina mvuto tena nyie kaeni mkijidanganya na hizo tafiti zenu za kijipendekeza na kuibeba ccm. Na umaarufu wa jk vp mbona hatuuoni?.
 
Vibaraka wa CCM. 2fanye utafiti we2 FB. Wanao ipenda CCM wa coment 1. Wanaoipenda CHADEMA WANA LYK THE UONE ZIPI NYINGI. Lyk? Au coment za 1. Let go
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom