Kichwa cha mada kinapotosha sana. CCM maarufu au umaarufu wa CCM umeporomoka? Chama tawala kuwa na acceptance level ya 52% sio jambo la kushangilia kwa chama hicho. It is a huge huge thing. By the time elections come CCM will have less than 30% and end this corrupt regime
Kaka unajidanganya sana.,tena unajitia upofu wa macho na akili.,upofu ambao hautaleta afya nzuri ya kisiasa kwako na kwa Chama chako.
Naomba usome hapa;
Kushindwa kwa CDM;
Kulingana na yanayoendelea hivi sasa ndani ya CDM kikiwa kama chama kikubwa cha upinzani kunaonyesha dhairi kushindwa kwake katika kufikiri juu ya njia sahihi na mbinu piganizi katika kuyashughulikia matatizo yanayowakabili watanzania kiuchumi, kiutawala, pamoja na kijamii.
Na nitayazungumza machache na kwa mifano ili watu wapate kuelewa kiunaga ubaga
1: Katika ufisadi, CDM haijaonesha mipango thabiti juu ya kulishughulikia suala la ufisadi nchini zaidi ya kuitisha maandamano yasiyo na tija na kudai kuwa mafisadi wanabebwa na mahakama na kusahau kuwa wao ndio wanatoa mawakili wa kwenda kusimamia mafisadi mahakamani (Mabele Marando), lakini ni wazi kuwa kama CDM wangelikuwa na nia thabiti ya kulisimamia hili wanao uwezo wa kisheria kama chama cha siasa na haki ya kikatiba ya kupendekeza mchakato wa namna ya kuwakamata na kuwashughulikia wala rushwa na mafisadi na hata kutoa direction ya adhabu na kanuni zinazosimamia utekelezaji wa mikakati hiyo ya kupambana na rushwa bali tumeona kuwa wapo viongozi katika CDM ambao wanapropagate ufisadi katika nafasi walizonazo hali inayotoa ishara ni kwa kiasi gani wanaweza kuwa pindi wakipata nafasi kubwa, kumbuka ya Mshahara wa Dk Slaa, kumbuka Magari ya Mbowe, kumbuka ukwepaji wa kodi wa chama, yale ya diwani kule Mara, na sasa kashfa ya Dr slaa kuchukua fedha ya ruzuku kwa matumizi yake binafsi.
2: Katika nchi ambayo demokrasia ni msingi na daraja la kuendea utawala wa sheria, wananchi (wapiga kura) lazima wawe na ufahamu wa kutosha juu ya maamuzi wanayotakiwa kuyachukua pindi wanapotumia fursa yao ya kupiga kura, Katika hili CDM wamekuwa mbele kulalamika na kupinga matokeo bila kufanya study yakinifu juu ya uhalisia wa wapiga kura Tanzania, wakiwa wanatumia sample space ambayo ni irrelevant kwa wakazi wa mijini na watumiaji wa mitandao pekee katika kufanya tathmini zao za ushindi ama kushindwa., katika uchaguzi mkuu uliopita na zingine ndogondogo kama igunga, Mwanza na (hata chaguzi za hivi karibuni za kata 29 ambazo CCM ilishinda kata 24 kati ya hizo) tathmini za kwenye mitandao zilionyesha kuwa CDM itashinda kwa kishindo na matokeo yamekuja tofauti mara zote katika chaguzi zote, na ni baada ya matokeo ndipo CDM hukakamaa na kunadi kuibiwa kura baada ya kutulia na kujifanyia tathmini yakinifu. UKWELI NI KUWA..,wapiga kura walio wengi ni watu waishio vijijini ambako CDM hawakubaliki na propaganda zao hazifiki huko, Siasa za CDM ni za mlalo na zimeegemea upande mmoja , zipo jamiiforums zikiipiga vijembe CCM, zipo Arusha wakiandamana kila uchao na kulala nje, wakiamasisha kujitenga na kujitawala, wakiunadi ukanda na kupinga utaifa, lakini kuigawa siasa ya Tanzania kwa kigezo cha kanda na kuimarisha baadhi ya watu Fulani kwa kuwapa stahili kubwa katika chama, na nafasi za uongozi, hayana mvuto wala uhalisia wa siasa za Tanzania,CDM ipo Arusha kwa kila nguvu kana kwamba hakuna maeneo yenye kuhitaji usimamizi wa karibu wa kisiasa na kiuchumi bali ni Arusha pekee.
Lakini kama hayo hayatoshi, ni kuwa wakati wakiibeza na kuishutumu serikali ikishindwa kusimamia fedha na miradi inayoelekezwa katika maeneo ya vijijini CDM inashindwa kuweka mkakati wa ufuatiliaji na taasisi ya kuhoji matumizi na utekelezaji ( hili linawezekana kisheria) ambapo kupitia taasisi hiyo usimamizi utaimarika lakini pia wapiga kura watapata mrejesho na kushuhudia nia ya kweli ya wanasiasa wao ya kuwaletea maendeleo.
3: Kulingana na mfumo wa sasa wa kiuchumi wa soko holela ambapo wenye nacho hupata fursa ya kujitajirisha zaidi, CDM inayofursa ya kutoa muelekeo wa uchumi na mfumo unaojali na kugusa pande zote kwa kushauriana na wachumi walionao (kama ZITTO) na kuandaa proposal ya sera zenye kulenga mabadiliko chanya kwenye sekta ya fedha,kodi, biashara, mishahara,na miamala mbalimbali katika sekta tofauti za kiuchumi hususani kilimo, ambapo watanzania walio wengi wamejiajiri huko. Na hili lazima lifanyike chini ya wataalamu wa uchumi na fedha.
4: katika mambo ambayo wapinzani (hasa CDM) wanayapigia kelele ni pamoja na undugunization katika ajira na mgawanyo wa vyeo na madaraka, katika hili CDM tuliamini watakuja na mbinu tofauti ya kuhakikisha kuwa vyeo na madaraja ya kazi yanagawanywa kulingana na uwezo, elimu na nafasi ya mtu,lakini tofauti na matarajio ya wengi bado ipo system ya kulimbikiziana vyeo ndani ya CDM, watu kama mnyika na wengineo wanavyo vyeo zaidi ya vitano wakati mmoja kana kwamba hakuna vijana wengine katika CDM walio na uwezo na elimu ya kushika nafasi hizo. Lakini pia upo upendeleo wa dhahiri wa kupeana vyeo kwa nasabu na ukoo, ipo mifano katika hili, Tundu lissu na dada yake, Slaa na hawara yake,Ndesamburo na mwanae,mbowe na familia ya Mtei n.k
5: kupoteza umaarufu na kushindwa ushawishi kwa jamii.,hivi sasa kwa mtu aliye makini na siasa za ndani ya nchi, anaweza kugundua kwa urahisi na kukubaliana moja kwa moja na ripoti ya synovate (ambayo kwangu ni sahihi) kuwa CDM wamepoteza umaarufu na ushawishi kwa watanzania makini, umaarufu ambao ulipatikana kwa gharama kubwa na akili nyingi, hii inatokana na kauli za kibaguzi za viongozi wa CDM kama Mzee Mtei (Muasisi CDM), Joshua Nassar (Mb, Arumeru) na Wenje (Mb, Nyamagana) na kupoteza uelekeo kwa media outlet zinazotumiwa na chadema, mfano wa magazeti kama mwanahalisi,mtanzania,Tanzania daima,mwananchi na social medias kama jamii forums ama jambo forums,amua sasa blog n.k ambazo kwa mara ya kwanza zilikuwa na mvuto mkubwa kwa watanzania wapenda habari lakini kutokana na kuandika kwa mlengwa mmoja na kwa muda mrefu bila kubadilika zimepoteza ladha na thamani yake kwa watanzania, upendeleo, uzushi, upotoshaji wa dhahiri pamoja na uchochezi vimechangia kuondoa hadhi na heshima ya vyombo hivi kwa watanzania wanahabari na wapenda habari.
6: Migogoro ndani ya chama.,CDM kikiwa chama kilichojitokeza mbele ya watanzania kama chama cha wapenda mabadiliko, wapenda vijana na wanaharakati wenye kutaka Tanzania yenye neema ipatikane, bahati mbaya CDM kimekuwa kikijiingiza ndani ya migogoro ya mara kwa mara tena kwa viongozi wake wa ngazi za juu., ili linatokana na ukweli kuwa wapo wapenda madaraka wasiotaka kupisha wenzi wao katika nafasi za kiutawala ndani ya chama, wenye kutaka kutoa kauli za mwisho zisizopingwa wala kukosolewa.,wenye ukanda, udini na ukabila hali hii inatia mashaka kwa watanzania walio wengi hivyo kupoteza ari na hamasa katika kukipenda na kukiamini CDM. Kisa cha Zitto na Slaa kipo dhahiri katika kutoa picha ya suala hili. Shibuda, Arfi, Mwanpamba, Shonza etc against godfathers ndani ya CDM.
Haya na mengine mengi yamewafanya watanzania wapoteze imani kabisa na chama hiko cha siasa kulingana na mfumo huo mbaya wa siasa zao.