Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,952
- 10,037
Mkuu ni kweli hili ni suala la kujadili na wala siyo la kushabikia tu ati CCM imejivua gamba. Mimi sioni muktadha wa kujivua gamba ni upi. Nimetatizika sana na hili suala la kujivua gamba. Mimi nadhani kujivua gamba kunge translate kwenye utendaji thabiti wa serikali na kushuka kwa gharama za maisha kwa watanzania. Watanzania wanalalamikia maisha magumu ya serikali ya CCM sasa gamba hili lililovuliwa hatuambiwi kama litaleta maisha bora kwa Watanzania. Kuwashughulikia mafisadi, sawa japo ukiangalia huko kuna mafisadi wengi Chamani na serikalini, lakini je hii secretariati mpya ya CCM ambayo ni gamba jipya inatuambiaje kuhusu ugumu wa maisha na utendaji wa serikali? Nadhani serikali nayo ijivue gamba, najua ina gamba nene tu na lililokomaa!