CCM kujivua ‘gamba’ Dodoma

CCM kujivua ‘gamba’ Dodoma

it reflects reality at ground! ccm has long way to go!! tanzanians have lost their trust on ccm governing!
 
Kinachoendelea ndani ya CCM ni vita ya makundi, yaani kundi la Lowassa na kundi la kina Sitta. Kwa nje CCM inaonekana imejivua gamba yaani imevaa uupya kitu ambacho hakipo.

Ukitaka kuja hali hiyo wasikilize wakiwa majukwani, ni vijembe, kupayuka, propaganda sana. Kujisifu sana kwamba wana serikali sikivu kitu ambacho hakipo. Wanalumbana na wapinga ufisadi nje ya CCM.

Naona kinachoendelea ni furaha ya kundi moja ndani ya CCM kupewa nafasi kupiga vita kundi lingine.

Ni vita kati ya mafisadi wakubwa na wadogo.
 
CCM wasipoangalia ndo itakuwa mbaya zaidi kwa sababu hao wafisadi kwenye majimbo Yao wamefanya vitu vingi vya maendeleo wakitamka chochote wapiga Kira wake pia wanawezakukihama cha na kwenda upinzani hasara itakuwa kwa ccm, ngoja tusubiri siku 90 maana hakuna mtu atakayekiri kwamba yeye ni fisadi hadi afukuzwe.
 
Nimeipenda hii ya "gamba kukomaa tena!" CCM wamekosea kweli kutumia mfano wa "kujivua gamba" maana inaonesha kwamba hawana nia ya kumaliza kabisa ufisadi isipokuwa wanataka watu wakishtukia ufisadi wao wanawapa watu siku 90 eti wajiondoe kwenye chama! Kama ingekuwa ni mimi nisingeondoka! Wanachotakiwa ni kuwakamata na kuwafikisha mahakamani, as simple as that! Otherwise CCM kwa ujumla wake ni gamba linalotakiwa kuvuliwa na si baadhi ya wanachama!
 
Hao ccm nia yao kubwa ni kututoa kwenye mjadala wa msingi ambao ni hali mbaya za kimaisha kwa watu, wao wanataka kutuzuga na bla bla zao za kujivua gamba wakati ukweli ni kwamba ccm ni chama kilichoshindwa kabisa kujenga taifa bora kwa maana ya kujenga watu wenye ustawi unaoeleweka na kiwango na taifa la kujitegemea.
Sasa Rais na Waziri mkuu hawajui kwanini taifa bado ni masikini, sasa kwamfano hapo gamba linahusikaje...? Hebu nisaidieni wanajamii!
 
Matokeo ya kura kutoka IPP-Media:

Kubadilika kwa safu ya Sekretarieti ya CCM. Unapongeza?

Napongeza sana
28%

Kawaida tu
47%

Hapana.
25%
Total number of votes: 502
 
mbona kauli ya mwenyekiti wao kukataa kura za wafanyakazi hawakuliweka kama ni chnzo cha kupunguza kura zao?
 
Mafisadi wataka Kikwete ang’oke
• Wadai naye ni gamba, chama kitamfia mikononi

na Salehe Mohamed


amka2.gif
HOFU kubwa imezuka ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya hatua ya uongozi wa chama hicho kuwapa muda wa siku 90 wanachama wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Sasa baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi wanataka na mwenyekiti wao aondoke nao kwenye uongozi wa chama.
Uchunguzi wa Tanzania Daima Jumapili umebaini kuwa makada wa chama hicho, ambao wanatuhumiwa kwa ufisadi, na ambao wamepewa siku 90 wajiondoe, wanasema ufisadi wa CCM unamgusa hata mwenyekiti wao.
Wanadai naye ametuhumiwa mara kadhaa, kama wao, na kwamba amechangia kukipa chama sifa mbaya.
Wanamshangaa Rais Jakaya Kikwete, kwamba amekuwa kigeugeu, kwani alishaweka wazi kuwa kamwe hawezi kumfukuza, kumuwajibisha kiongozi wa serikali au wa chama bila ya kuthibitika kwa tuhuma zinazomkabili, ili kuepusha serikali kulipa mabilioni ya fedha iwapo mhusika atakwenda mahakamani na kushinda.
Wanadai kwamba kama ni kuwajibika au chama kujivua gamba, hata Rais Kikwete alipaswa kuwa ni miongoni mwa wale wanaotakiwa kuwajibika, kwa sababu alishatajwa mara kadhaa kuhusika na ufisadi mbalimbali, ukiwemo ule wa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL).
Na wanadai kutajwa kwake huko ndiko kumeshusha heshima yake kwa umma, na hata kumfanya apite kwa shida katika uchaguzi mkuu uliopita, huku akiwa rais aliye madarakani.
Wanasema kuwa kama kutajwa mara nyingi katika kashfa za ufisadi ni kukichafua chama na ndicho kigezo kilichotumiwa na CC, NEC, Rais Kikwete hapaswi kupona kwa kuwa alishawahi kutajwa katika orodha ya mafisadi 11 na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, alipokuwa akihutubia wananchi katika viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam.
Septemba 15, 2005, Dk. Slaa aliwataja baadhi ya makada wa CCM na watendaji wa serikali akiwamo Rais Kikwete kuwa ni mafisadi wanaochangia umaskini wa taifa kwa kutumia rasilimali zilizopo kwa manufaa yao.
Wachambuzi hao wanasema kuwa hicho kilikuwa kipimo tosha kwa wana CCM kuwaadhibu makada wao lakini haikufanya hivyo na badala yake kikajikita katika kukanusha kuhusika na kuhusishwa kwa makada wao hasa Rais Jakaya Kikwete.
Miongoni mwa watuhumiwa wa ufisadi wameliambia Tanzania Daima Jumapili kuwa tatizo lilipo ndani ya CCM si wao kama inavyoelezwa na kushabikiwa, kwani kama wangekuwa tatizo wasingeweza kushinda uchaguzi katika majimbo yao kwa asilimia kubwa kuliko hata zile alizopata Rais Jakaya Kikwete kwenye uchaguzi uliofanyika Oktoba 30, mwaka jana.
Alisema ana uhakika watuhumiwa wa ufisadi wakitoka ndani ya CCM na kuwania ubunge kupitia vyama vya upinzani watarejea bungeni wakiwa mashujaa kama ilivyo kwa wenzao walioshinda ubunge baada ya kufanyiwa zengwe kwenye chama hicho tawala.
“Sisi si tatizo ndani ya CCM… kuna matatizo lakini NEC, CC hawakuyaangalia hayo, kimsingi naona maamuzi yaliyofanyika yaliwalenga watu zaidi kuliko hoja, tusipokuwa makini chama kitaendelea kupoteza umaarufu,” alisema.
Kada huyo alibainisha kuwa tatizo lililopo hivi sasa ni la kimfumo zaidi na wala si la mtu mmoja mmoja.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaweka bayana kuwa uamuzi wa kujiondoa chamani kwa watuhumiwa wa ufisadi unaweza pia kuyumbisha shughuli za utendaji wa serikali pamoja na kuimarisha upinzani ambao umepata umaarufu zaidi baada ya kuonekana ndiyo unaosimamia masilahi ya wananchi.
Wanasema kuwa uamuzi wa CCM unaweza kuwa na madhara zaidi kwa kuwa chama hicho hakijapata kuwaadhibu wanachama wengi kwa wakati mmoja kama ilivyo hivi sasa kwa sababu huko nyuma kilikuwa kikitoa adhabu kwa mtu mmoja moja.
Kwa sababu hiyo, hivi sasa wanachama wamegawanyika juu ya uamuzi huo, huku kundi moja likiona umefanywa kwa fitna, majungu na chuki, hasa kwa lengo la kuwavunja nguvu vigogo wanaodaiwa kuanza mbio za kuwania urais.
Gazeti hili limedokezwa kuwa uamuzi huo wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) umeanza kukimega chama katika mapande makubwa mawili kuelekea 2015.
Iwapo moja litajiondoa na kujiunga na upinzani utakuwa mwanzo wa utabiri wa hayati Baba wa Taifa, Julius Nyerere ambaye aliweka bayana kuwa upinzani wa kweli na utakaokiangusha chama tawala utatoka ndani ya chama hicho.
Nyerere alisema iwapo CCM haitabadilika kwa viongozi kuacha kuendekeza majungu, fitna, kujilimbikizia mali na kuwanyenyekea watu wachache (matajiri) huku ikiwatupa wananchi walio wengi, kingekumbwa na hatari ya kumegeka.
Lakini yeye alisisitiza pia kwamba mmeguko utakaokisaidia chama hicho ni ule wa kiitikadi. Wachambuzi wa kisiasa wanasema CCM ya sasa inaelekea kumeguka kwa majungu na fitna.
Baadhi ya makada wenye hofu ya kumeguka kwa chama hicho wanahoji ushahidi uliotumika kuwataka watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi waachie nyadhifa zao ilhali hawajawahi kuhojiwa na taasisi yoyote ya dola na kufikishwa mahakamani kama ilivyo kwa wengine ambao mpaka sasa kesi zao zinaendelea kusikilizwa.
Tanzania Daima Jumapili, imedokezwa kuwa makada wa CCM wana hofu kuwa wanaotuhumiwa kwa ufisadi wakiamua kukihama chama hicho na kujiunga na upinzani wana uwezo wa kuondoka na wafuasi wengi wanaowaunga mkono, hivyo kuinyong’onyeza CCM.
Sababu kubwa inayotolewa na wanaodai hivyo ni kwamba kwa kuwa viongozi wanaoendekeza majungu si waadilifu, lakini wana madaraka, wale wanaodhani wameonewa ni rahisi kupata wafuasi wanaowaonea huruma, hasa wanaoamini kwamba uongozi wa sasa wa CCM hauna uadilifu wala uwezo wa kukivusha kwenye mapambano na upinzani unaokua, hasa CHADEMA.
Wasiwasi huo unachagizwa zaidi na kuwapo kwa tetesi kuwa watuhumiwa hao, Edward Lowassa (Monduli), Andrew Chenge (Bariadi Mashariki), na Rostam Aziz (Igunga) hawakuridhishwa na uamuzi wa CC, NEC ambao unadaiwa kuamuliwa kifitna zaidi kuliko kuangalia uhalisia wa tuhuma za wahusika.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wameweka wazi kuwa wameshangazwa na uamuzi wa CCM kutaka kuwatosa watuhumiwa wa ufisadi kwa kusikiliza maneno ya watu, huku naye (mwenyekiti) akituhumiwa kwa ufisadi kama wao, bila ya kupata ushahidi wa namna walivyoshiriki kwenye ufisadi unaotajwa.
Wakati huo huo, Mwenyekiti Mwenza wa Taasisi ya Utafiti na Elimu ya Demokrasia (REDET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Benson Bana, anasema bila ya mabadiliko ya kisela, kifalsafa na kiitikadi, CCM haiwezi kusalimika katika hatari ya kung’oka madarakani.
Dk. Bana alisema katika mfumo wa vyama vingi ambapo wananchi wanapata fursa kubwa ya kusikia na kuona ushindani wa sera, itikadi, falsafa za vyama mbalimbali ni lazima CCM iviangalie vitu hivyo ili kutimiza matakwa ya wananchi na wanachama wao, kinyume na hapo mabadiliko yoyote yatakayofanyika hayatoweza kukiepusha na hatari ya kung’oka madarakani.
Na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema matatizo waliyonayo CCM ni sawa na saratani (kansa) iliyopo damuni ambayo kamwe hayawezi kupona, hivyo jitihada zinazofanywa na chama hicho kujinusuru na kifo haziwezi kuzaa matunda.
Naye Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Dayosisi ya Mjini Kati, Askofu Thomas Laizer, wakati akiwa katika mazishi ya mama yake, alimtaka Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, atulie kwani walichokifanya wenzake wa CCM ni kutoa boriti kwenye jicho la mwenzao wakati macho yao yana magogo.
Kauli hiyo inaonyesha wazi kuwa kiongozi huyo wa dini hakubaliani na kilichofanywa na CCM, kwa kuwa wapo viongozi wengi ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa wakinyooshewa kidole kwa kuhusika na ufisadi lakini NEC na CC hawajawachukulia hatua zozote.
Wachambuzi wa mabo wamebainisha kuwa hivi sasa wanatarajia CCM itawaandikia barua kujiondoa kwenye chama hicho makada wengi zaidi, kwa kuwa Dk. Slaa ametaja orodha nyingine ya watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Wanabainisha kuwa mabadiliko yaliyofanywa na chama hicho hayawezi kutoa matunda mazuri, kwa kuwa kwa kiasi kikubwa yametokana na hoja ya ufisadi waliyoiteka kutoka kwa wapinzani, hasa baada ya kutangaza orodha ya mafisadi mwaka 2007 katika viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam.
 
Slaa apasua jipu
• Ataja orodha mpya ya mafisadi, wafikia 17

na Waandishi wetu


amka2.gif
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ametaja orodha mpya ya vigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Vigogo hao ni Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, John Samwel Malecela, aliyekuwa Waziri Mkuu, Fredrick Sumaye, na aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Philip Mangula, kwa kuhusika na wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) kupitia Benki Kuu.
Dk. Slaa alitangaza majina hayo jana mjini Tabora alipokuwa akiwahutubia wanachama na wananchi waliofurika kwenye viwanja vya Chipukizi.
Alisema majina hayo ni muendelezo wa yale ya vigogo wanaotuhumiwa kwa ufisadi aliyoyataja Septemba 15, 2007 katika viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam ambayo ni 11 akiwemo Rais Jakaya Kikwete.
Katika orodha ya mwaka 2007, Dk. Slaa aliwataja aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), ambaye sasa ni marehemu, Dk. Daudi Balali, Mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge (CCM) na Basil Mramba aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Rombo (CCM).
Wengine ni Gray Mgonja aliyekuwa Katibu Mkuu mstaafu, Hazina, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Patrick Rutabanzibwa, kada wa CCM, Nazir Karamagi, Mbunge wa Musoma Vijijini Nimrod Mkono (CCM), Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM), Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa (CCM), Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, na Rais Jakaya Kikwete.
Alisema katika orodha hiyo mpya Magufuli amehusika na kashfa ya uuzaji wa nyumba za serikali ambazo ziliuzwa kwa watu wasiostahili na nyingine hazikutakiwa kuwekwa sokoni.
Alibainisha kuwa katika kashfa hiyo, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa naye alihusika kwenye uamuzi huo mbovu uliosimamiwa na Magufuli, ambaye hivi sasa amepewa Wizara ya Ujenzi.
Mangula na Malecela, alisema wao walikuwa wakitoa ‘vimemo' vilivyokuwa vikitoa maagizo ya kwenda kuchotwa fedha za EPA ambazo zilikisaidia Chama Cha Mapinduzi katika kampeni zilizomuwezesha Rais Kikwete kuingia madarakani.
Alisema Mangula alikuwa akitumia kofia yake ya ukatibu mkuu wa chama na Malecela alikuwa akitumia wadhifa wa umakamu mwenyekiti wa Bara kwa wakati huo.
Aliongeza kuwa Sumaye naye alihusika kwa kuwa alikuwa waziri mkuu na alikuwa akijua kila kilichokuwa kikiendelea lakini aliamua kunyamaza kimya na kushirikiana na wabadhirifu hao.
Katika hatua nyingine, Dk. Slaa ametoa siku 90 kwa Rais Kikwete, kuueleza umma zilipo sh bilioni 70 zilizorejeshwa na wezi wa EPA.
Alisema Rais Kikwete aliahidi kuwa fedha hizo zitapelekwa katika Benki ya TIB, ambako kumeanzishwa dirisha la kuwakopesha wakulima.
Alibainisha kuwa kwa mujibu wa taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), fedha hizo hazionekani zilipo kwa kuwa hakuna akaunti yoyote inayoonyesha zimewekwa.
Slaa, pia ametoa tuhuma kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwamba kuna upotevu wa sh bilioni 220 kwa mujibu wa taarifa ya CAG.
Alisema mfanyabiashara mwenye malori kadi za magari yake zimekuwa zikishikiliwa na TRA kwa muda wa miaka 10 sasa na ameishitaki serikali na imeamriwa kumlipa kiasi hicho cha fedha.
"Sioni sababu ya serikali kulipa kiasi hicho cha fedha wakati aliyesababisha hasara hiyo yupo na bado anaendelea kufanya kazi TRA," alisema.
Slaa alitumia fursa hiyo kumtaka Spika wa Bunge, Anne Makinda, asitumie nafasi ya uspika kama jukwaa la kisiasa kwa sababu yeye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi.
Alisema Makinda anatumia nafasi hiyo kuwa mwanasiasa badala ya kufanya kazi za uspika zilizoingiliana na kazi za siasa.
Slaa, ameahidi kuwa CHADEMA itazirudisha hoja zote za ufisadi kwenye mjadala ili zijadiliwe upya kwa kuwa Kikwete ameshindwa kuchukua hatua.
Naye Mwasheria wa CHADEMA, Mabere Marando, aliwataja wafanyakazi wawili wa kampuni ya Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM) ya Caspian Ltd, ambao walighushi majina yao na nyaraka ili kufanikisha wizi wa sh bilioni 40.
Wafanyakazi hao ni John Kato, ambaye alijulikana kwa jina la Kamando William, na Bharaeti Goda, alijulikana kwa jina la Francis William, waliofanikiwa kuiba kiasi hicho cha fedha kupita Kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd.
Alisema anao ushahidi wa jambo hilo na yuko tayari kuisaidia serikali kama ikiwapeleka mahakamani wahusika.
Naye Fred Mpendazoe, alisema kilichofanywa na CCM kujidai kujivua gamba ni usanii mtupu, kwani katika uchaguzi mkuu uliopita Kikwete mwenyewe aliwanadi watuhumiwa wa ufisadi huku akiwasifu kuwa ni viongozi bora na hakuna kama hao.
"Kama alivyo kuhani kanisani ndivyo walivyo waumini wake na kama alivyo sheikh msikitini ndivyo walivyo waumini wake…Kikwete hawezi kutenganishwa na hao waliovuliwa gamba", alisema Mpendazoe.
 
Chomoa, chomeka itainusuru CCM?
ban.maswali.jpg

Ansbert Ngurumo

amka2.gif
SAKATA la CCM kujivua gamba limezaa maswali mengi ambayo hayajajibiwa. Na limetusaidia kujua zaidi upeo wa watawala wetu, na uwezo wa kukabiliana na misukosuko ya ndani na nje ya chama tawala.
Na kwa kuwa wanapima upeo wa Watanzania kwa mizani ya upeo wao wenyewe, watawala wetu wamediriki kujitapa kwamba CCM imezaliwa upya. Wengine wanasema CCM imefufuka. Wamekosea!
Ni fursa kwa CCM ya Kikwete kujiuliza au kuulizwa. Kama CCM ya Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa ilionekana imara, ni nani ameidhoofika CCM ya Kikwete?
Mtu mmoja alinieleza miezi mitatu iliyopita, kwamba Rais Jakaya Kikwete alisikika akimweleza rafiki yake mmoja wa Iringa kwamba anavyoona chama kimeanza kumfia mikononi, na hilo ni jambo analoogopa sana. Je, mabadiliko haya ya kuchomoa na kuchomeka sura ndiyo yanaweza kuinusuru CCM inayokufa?
Tumesikia wanajitapa kwamba wameondoa mafisadi kwenye Kamati Kuu, na sasa wanataka waliobaki kwenye Halmashauri Kuu na vyombo vingine vya chama wajiondoe wenyewe, la sivyo watafukuzwa! Jambo jema.
Lakini CCM wameanza lini kukiri kwamba chama chao ni cha mafisadi au kina mafisadi? Si hawa hawa ndio walibeza na kulaani kauli ya wapinzani, iliyotolewa na Dk. Willibrod Slaa Septemba 2007, Mwembeyanga, Dar es Salaam, alipotaja orodha ya mafisadi na kufafanua ufisadi wa kila mmoja wao?
Si ndio hawa waliotishia, na baadaye wakaogopa kumshitaki Dk. Slaa, lakini wakaendelea kuwatumia mawaziri na makada wengine kuzunguka mikoani kushambulia wapinzani kwa kile walichoita ‘uzushi?'
Hoja ya ufisadi si ndiyo ilimfanya Rais Kikwete awabeze na kuwakejeli wapinzani akidai kelele za mlango hazitamzuia mwenye nyumba (yeye) kulala?
CCM hii si ndiyo iliwatuma Yusuph Makamba, Kingunge Ngombale-Mwiru, Jaji Joseph Warioba, Sofia Simba na makada wengine kubeza na kudhihaki wapinzani na vyombo vya habari, wakidai wanaendekeza habari za ufisadi badala ya masuala ya maendeleo?
Kama Rais Kikwete na wenzake wanasema kuwa umefika wakati chama kiondokane na mafisadi, basi wamethibitisha kwamba Dk. Slaa na wenzake walikuwa sahihi. Sasa tuwaamini CCM au akina Dk. Slaa?
Pili, dhana hii ya kujivua gamba bado ni tata hata kwa wenyewe wanaoipigia debe. Mwenyekiti mwenyewe aliyeianzisha alidhani CCM ina gamba moja tu inalopaswa kujivua; na akadhani inatosha tu kuvua gamba. Inasikitisha kwamba yeye anaishia hapo, lakini hata sisi tusio wana CCM tunajua kuwa CCM haikuhitaji kuvua gamba, bali kuwa na moyo mpya.
Lakini wale waliopenda kuendelea kuchambua hoja ya gamba wameshaorodhesha magamba ya CCM. Na wengine wamesisitiza kwamba Rais Kikwete, kwa staili yake ya uongozi, na baada ya kutathimni alikokitoa na alikokifikisha chama, naye ni gamba.
Kwa bahati mbaya, inavyoonekana, hata watawala wenyewe bado hawajajua idadi, na aina ya magamba wanayopaswa kukivua chama chao. Vile vile, hawajajua kwamba hata kama wangefanikiwa kuyatambua na kuyavua mgamba hayo, bado chama chao hakitaweza kuwa kipya.
Tatu, na hili ndilo la msingi kwangu, hivi watawala wanadhani kwamba nyoka anapojivua gamba anabadilika na kuwa mjusi au kinyonga?
Tunaona, na tunasema wazi kwamba CCM ya Kikwete, yenye gamba na isiyo na gamba, ni ile ile. Wanachofanya sasa ni kujaribu (na kufanikiwa kwa sehemu kubwa) kuwafukuza 'wabaya wao' wa sasa na kuingiza marafiki wapya. Na bahati mbaya, ni sura zile zile tulizozizoea, tunazozifahamu, na ambazo tunapata shida kuzitenganisha na ufisadi uliowakumba kina Yusuph Makamba, Rostam Aziz, Andrew Chenge na wenzao.
Kikubwa zaidi ni mamlaka ya kimaadili yanayotumika kuwafukuza wengine na kuingiza wengine. Maana kama tunaendelea kukuza na kusisitiza hoja ya Mwembeyanga, waliotajwa kwenye orodha ya mafisadi ni hawa hapa:
1. Daudi Balali
2. Andrew Chenge
3. Basil Mramba
4. Gray Mgonja
5. Patrick Rutabanzibwa
6. Nazir Karamagi
7. Nimrod Mkono
8. Rostam Aziz
9. Edward Lowassa
10. Benjamin Mkapa
11. Jakaya Kikwete

Chama kinachojivua gamba, kwa mfano, kitajitapaje kwamba kimeondokana na mafisadi, wakati hata mwenyekiti mwenyewe yumo kwenye orodha?
Si hilo tu. Kwa misingi ya kikatiba, kihistoria na kitamadumi, CCM inaongozwa na mwenyekiti. Na hii ndiyo asili ya kaulimbiu ya siku nyingi ya CCM ya ‘zidumu fikra za mwenyekiti.'
Kwa mantiki hiyo, chama kinapofanikiwa au kinapokwama, mtu wa kwanza ambaye wana CCM wanapaswa kumhoji si katibu mkuu (maana utendaji wake unasimamiwa), bali mwenyekiti.
Sekretariti na Kamati Kuu ni zao la mwenyekiti. Ni mikono ya kazi anayotumia kuendesha chama. Ni kweli, Yusuph Makamba, kwa elimu na upeo wake, alibebeshwa mzigo mzito. Lakini ndiye huyo ambaye mwenyekiti aliridhika naye kwa miaka mitano.
Kwa hiyo, mwenyekiti ndiye aliyepaswa kubeba udhaifu wa katibu na chama kwa ujumla. Maana wana CCM walipohoji na kubeza uteuzi wa Makamba mwaka 2006 kurithi nafasi ya Philip Mangula, mwenyekiti hakujali.
Hata ilipopatikana fursa ya kubadilisha uongozi wa chama hapa katikati, Rais Kikwete aliridhika na utendaji wa Makamba. Huyu huyu hawezi kuibuka leo na kusema Makamba na sekretarieti yake hawajamsaidia kazi.
Nionavyo mimi, yaliyomkuta Makamba na Sekretarieti na Kamati Kuu yake ni sawa na yaliyomkumba Lowassa na Baraza la Mawaziri lililokuwa chini yake mwaka 2008.
Uamuzi wa kuondokana na Lowassa ilikuwa njia pekee ya kumnusuru Kikwete na anguko la kisiasa akiwa madarakani, kwa maana kashfa yenyewe iliyomsomba Lowassa iliwahusu wote.
Na hili la Makamba limeharakishwa na vuguvugu la mapinduzi ya ndani, baada ya mwenyekiti kuletewa taarifa kwamba kuna watu wananadi uenyekiti wake kwa maelezo kuwa ameshindwa kuongoza vema chama. Walitaka (na bado wanataka) abaki na urais, aachie uenyekiti.
Wanajua kuwa kwa utamaduni wao, mwenyekiti ndiye kiongozi wa chama. Anakotaka chama kiende, ndiko kinakokwenda. Na wandhani kuwa wakipata mwenyekiti mzuri watakuwa na chama kizuri.
Katika mazingira haya, njia pekee ya mwenyekiti kujinusuru ilikuwa kuwashughulikia walio chini yake ili ajipange upya, abadili hoja, na apate pa kuning'iniza propaganda za CCM mpya.
Na kwa maana hiyo, kujiuzulu kwa wajumbe wa Kamati Kuu na Sekretarieti (kwa shinikizo la mwenyekiti) ilikuwa faraja kwake binafsi si kwa CCM. Na ndiyo maana sisi wengine tunakataa kukubaliana na propaganda za akina Nape Nnauye eti chama kimezaliwa upya!
Nne, upya wa chama hauletwei na upya wa sura za wajumbe. Kama muono wa chama ni ule ule; itikadi ni ile il; sera zake ni zile zile; i wapi CCM mpya inayozungumzwa?
Bahati nzuri Katibu Mkuu mwenyewe ameshakiri kwamba hana jipya, bali anataka kurejesha na kusimamia misingi ile iliyokiasisi chama. Mwisho wa fikra!
Zaidi ya yote, kama huyu anayeteua, kupendekeza na kufukuza wajumbe wa kamati ndiye aliyesimamia waliopita, amepata wapi njozi mpya za kusimamia wapya kwa ufanisi? Au ni yale yale tuliyozoea kuona kila anapoteua baraza la mawaziri? Kama ndivyo, je, udhaifu wa uteuzi na utendaji tunaoshuhudia serikalini hautaendelezwa kwenye chama?
Kumwondoa Makamba na kumwingiza Mukama ni mabadiliko ya mwelekeo? Kumwondoa John Chiligati na kumwingiza Nape Nnauye ni kukipa chama dira mpya?
Kumwondoa Amosi Makala na kumwingiza Mwigulu Nchemba ni kukipa chama moyo mpya? Kumwondoa Bernard Membe na kumwingiza January Makamba ni kukipa chama katiba mpya? Kurejeshwa kwa Zakia Meghji kunakipa chama itikadi mpya?
Lililo wazi ni kwamba CCM ni chama kinacho kufa. Kina sura zile zile na mawazo yale yale. Na kwa sababu wameishiwa mapya, wamebaki katika siasa za kuwindana na kumalizana. Wanachomoa hawa na kuchomeka wale. Inatosha kuwanusuru?
 
CCM na mabadiliko, gamba jipya ‘sumu' ile ile!
ban.nundu.jpg

Deus Bugaywa

amka2.gif
"NI muhimu kusisitiza kuwa pamoja na maandishi ya chama yaliyo sahihi na ya kimapinduzi, pamoja na upeo na uwezo mkubwa alionao Mwenyekiti, Mwalimu
Julius Nyerere, wa kutafakari na kuchambua masuala mbali mbali kwa kina na ufasaha au wa kiongozi mwingine yeyote, lakini kwa kuwa chama ni wanachama na viongozi wote kwa pamoja katika mshikamano wao wa nadharia na vitendo, basi ni hatari kwa maendeleo ya chama na ya siasa yake ya ujamaa kuiachia hali ambapo kiwango cha kuielewa nadharia ya chama kinahitilafiana mno kati ya wana CCM na hata kati ya viongozi wa ngazi moja ya uongozi". Mwongozo wa CCM 1981, ukurasa wa 14.

Nimelazimika kunukuu sehemu hii ya mwongozo wa CCM wa mwaka tajwa hapo juu ambao ulikuwa na lengo la kujichambua na kujikosoa kama chama, pamoja na mambo mengine mengi ambayo chama kilikuwa kinajikosoa wakati huo, nukuu hiyo iko chini ya kichwa cha habari kinachozungumzia umuhimu wa nadharia sahihi kwa wanachama.
Ni kweli kwamba uhai wa chama ni nadharia na misngi ambayo chama kina itikadi kwayo, na hii siyo tu inatakiwa iwe kwa inajulikana kwa viongozi tu lakini pia kwa wanchama wote ambao kimsingi ndiyo chama chenyewe.
Kwamba unapuzungumzia chama maana yake siyo jina au nembo tu, lakini zaidi sana ni misingi ya chama na itikadi yake kinayoisimamia, na ambayo inatakiwa siyo tu ijulikane kwa viongozi wachache lakini pia wanachama wote.
Hivi karibuni tumeshuhudia chama tawala CCM kikichukua maamuzi ya kujivua gamba, kimeamua kuondokana na ufisadi au kuwakana watuhumiwa wote wa ufisadi, kinataka kuwaeleza wanachama wake kwamba sasa chama hicho kina gamba jipya, kimevaa sura mpya na hivyo wale waliopoteza imani nacho sasa waanze kukiamini kwa kuwa tu Yusufu Mkamba siyo tena Katibu Mkuu wa chama na Wilson Mukama ndiye Katibu Mkuu mpya wa chama.
Tumesikia mipango ya kuanza kutembea nchini nzima kwa ajili chama hicho kuukana ufisadi, ni wazi kuwa ufisadi ni kitu halisi na chama chenyewe kimesaidia sana kuthibitisha kilio cha wananchi wengi walichokuwa wakikielekezea chama kwa siku nyingi kwamba kinalea ufisadi.
Kwa hatua hizi sasa inaashiria kuwa hata wao wanakubali kwamba yapo makosa yaliyofanywa na chama katika kuukumbatia ufisadi, kwa hatua hiyo ni kweli wanastahili pongezi siyo kwa kubadili viongozi, lakini kwa kuwa kitendo hicho kinaashiria kukubali na kukiri udhaifu wao katika utendaji kichama.
Pamoja na kwamba ni kweli kuwa kuwa kutambua na kukiri udhaifu wako ni hatua moja kubwa kuelekea kuondokana na udhaifu huo, lakini udhaifu hauwezi kuondoka kwa kuutambua na kuukiri tu, ni lazima hatua mahsusi zichukuliwe kuonyesha dhahiri shahiri kuwa umekerwa na matatizo uliyoyatambua.
Na hapa linazaliwa tatizo jingine ambalo ni hatari waliyoiona wana CCM mwaka 1981 walipoamua kujikosoa, hatari hii ni "kuiachia hali ambapo kiwango cha kuielewa nadharia ya chama kinahitilafiana mno kati ya wana CCM na hata kati ya viongozi wa ngazi moja ya uongozi". Kumuiga nyoka kujivua gamba kumedhihirisha tofauti hizi.
Kama kuna vitu ambavyo vinakigharimu Chama Cha Mapinduzi ni pamoja na kukosa mwelekeo na kuachana na msingi yake iliyokiasisi chama hicho, kulea na kukumbatia vitendo vinavyoonekana machoni pa jamii kuwa ni vya kifisadi na ambavyo havina manufaa kwa jamii.
Chama kimefanya juhudi kubwa kukataza mijadala ya mambo makubwa na ambayo yana athari kubwa kwa mustakabali wa taifa ambayo yanahusishwa na ufujaji mkubwa wa mali ya umma.
Kwa hiyo chama kinaposema kinajivua gamba, na kuwa na gamba jipya masuala kama tuhuma za Meremeta ambalo serikali mpaka hivi majuzi tu wakati waziri mkuu anajibu maswali ya papo kwa papo, alikwepa na kutotaka kulizungumzia kwa kisingizo kwamba gamba inalojivua CCM ni gamba la ndani ya chama kwa hiyo Meremeta ni kitu tofati sana.
Hii tafsiri yake ni moja na ya wazi kabisa kwamba, kukerwa na ufisadi kulikoonyeshwa na CCM ndani ya chama na kuamua kuchukua hatua, hakuwezi kutafsirika ndani ya serikali hasa kwa kushughulikia masuala mbali mbali ya ufisadi katika serikali.
Na hapa ndipo hatari kwa chama hiki ilipo. Kama kimekubali kwamba kimepoteza mvuto na hasa kwa vijana wa kizazi hiki kinapaswa pia kuingia ndani kwa kina na kujiuliza kwanini watu wanakosa matumaini nacho na kuamua kuyawekeza kwenye vyama vingine ambavyo wanaona vinaweza kuwarejeshea matumaini yaliyopotea.
Mojawapo ni hali ngumu ya maisha, inayochangiwa kwa kiasi kikubwa na kukosekana kwa ajira hasa miongoni mwa vijana, kukosekana kwa mikakati au mipango mibovu ya serikali ya CCM ya kuratibu shughuli za vijana wasio katika ajira rasmi, hasa wamachinga kwa kushughulikia matatizo yao kwa staili ya zimamoto, hali ambayo inazidi kuwaweka vijana hawa katika hali ngumu ya maisha.
Kutelekezwa kwa wakulima wa nchi hii kwa kisingizo cha uhuru wa biashara na hivyo kuwaacha wakiwa wahanga wa wawekezaji wakubwa wanaowanyoya katika kuuza mazao yao huku serikali ikiwa katika usingizi mzito na hata ikishtuliwa inajitetea kwa visingizio ambavyo havimsadii chochote mkulima badala ya kuwa kero tu.
Mfano mzuri ni mvutano usio na tija kwa wakulima wa pamba kati ya wakuu wa wilaya na bodi ya pamba juu ya nani ana haki ya kusimamia na kuratibu zoezi la ugawaji pembejeo, wakati wakulima wanakula hasara kwa kuuziwa dawa ‘feki' za kuua wadudu serikali na vyombo vyake wako ‘bize' wanavutana nani ni mwamba zaidi ya mwingine kwenye usimamizi wa pamba, hili ni tatizo la msingi.
Kitu kingine kilichokipotezea mvuto CCM kwa wananchi na hata baadhi ya wanachama wake waadilifu na waaminifu ni usimamizi usioridhisha wa rasilimali za taifa.
Moja ya jukumu kubwa la serikali yeyote makini duniani ni kuhakikisha kuwa rasimali za taifa zinatumika kwa manufaa ya wananchi wake.
Bahati mbaya sana kwa serikali ya CCM ni kukosa uzalendo au uwezo wa kusimamia tunu za taifa hili kwa manufaa ya wananchi wote, unapozungumzia madini, mtu mwingine anayeijua Tanzania kwa kuisoma kwenye ramani na takwimu za uzalishaji madini anaweza kusema watanzania wamebarikiwa kweli na hawana matatizo.
Lakini ukienda North Mara, kwa wananchi wanaoishi kwenye bonde la Mto Tigithe, watakwambia maana ya laana ya kuwa na madini jirani na kwao, ukienda Buzwagi ukimwangalia yule bibi aliyesafiri kwenda Dodoma kwenye bunge la Aprili mwaka huu, ili kupaza sauti ya malalamiko yake dhidi ya wamiliki wa mgodi huo kuhusu fidia yake, utajua nini maana ya utajiri wa Tanzania .
Mifano ni mingi na kila mahali, Nenda Loliondo (siyo kwa Babu) utaona jinsi wananchi wa huko wanavyoona laana badala ya fahari kuwa jirani na moja ya urithi mkubwa wa dunia, kwa jinsi tunawaoita wawekezaji wanavyowanyanyasa katika ardhi pekee wanayoijua kuwa ni kwao tangu kuumbwa ulimwengu.
Haya na mengine ya namna hiyo ndiyo yanayoifanya CCM leo ikose mvuto kwa sababu kimekiuka misingi yake mikuu na muhimu ya kuwa chama mtetezi wa wanyonge na kuwa mtetezi wa ‘wawekezaji' na wananchi wa tabaka la juu.
Haya yote hayawezi kuondoka kwa kumfanya Nape Nnauye kuwa Katibu wa NEC, Uenezi na Habari au January Makamba kuwa Katibu wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa wa halmashauri kuu ya chama hicho.
Na wala siku tisini walizowapa watuhumiwa wa ufisadi kujiuzulu wenyewe haziwezi kufanya muujiza wa kuyamaliza matatizo haya yaliyosababishwa kwa kiasi kikubwa na serikali ya chama hicho.
Kama hakitachukua hatua zaidi za kusafisha serikali kinayoiongoza na kujisahihisha, mfano wao wa kumuiga nyoka kujivua gamba utakuwa mfano halisi kwa maana halisi ya nyoka anayejivua gamba, ambaye hata kama atajivua magamba mengi namna gani anabaki kuwa ni nyoka na sumu yake inabaki ile ile.
 
Makamba tangulia ukaandae makao
ban.nasema.jpg

Christopher Nyenyembe

amka2.gif
FALSAFA aliyoizoea aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, ya kutumia maneno yenye hekima kutoka kwenye maandiko ya vitabu vitakatifu Kurani na Biblia kwa kiasi kikubwa hayakuweza kabisa kuwatisha mafisadi.
Makamba katika kipindi chake chote cha uongozi tangu alipovaa kwa mara ya kwanza viatu vilivyoachwa na Katibu Mkuu aliyemtangulia, Philip Mangula, hakuna hata jambo moja aliloweza kurithi kutoka kwa kiongozi huyo ili kuweza kuinusuru CCM na anguko la aibu.
Wengi walikuwa wamemzoea, mzee Makamba aliyesifika kwa semi, mafumbo na misamiati mizito aliyokuwa akiibua hadharani, kwenye vikao vya ndani vya chama hicho na kwenye mikutano kadhaa ikiwamo ile ya kampeni pale alipotumia mvuto na ushawishi wa kutumia Biblia akinukuu jambo analoona linafaa ili kuweza kuwafikishia watu ujumbe.
Uamuzi mzito na mgumu uliofanywa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete wa kuwavua gamba la zamani makada maarufu wa chama hicho na kuwavika wengine kwa maana ya kuvaa gamba jipya kamwe hakuwezi kuwanusuru wale waliobaki kwa kuwa wenzao waliojiuzulu wanatangulie mbele kwenda kuwaandalia makao.
Katika salamu zale za kuwashukuru wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) mjini Dodoma , Makamba alisema wazi kuwa wao wanaondoka na wale waliobaki wajue fika kuwa walioondoka wanakwenda kuwaandalia makao wenzao ambao wapo ndani ya CCM iliyojivika gamba jipya.
Makamba alionekana kunukuu maandiko matakatifu kutoka kwenye Biblia kama ilivyoandikwa na Yohana Mtakatifu, Yesu alipokuwa akiwaaga mitume wake 11 kuwa wasifadhahike mioyoni mwao kwa kuwa wanamuamini Mungu wamuamini na yeye, kwa kuwa nyumbani kwa baba kuna makao mengi.
"Kama sivyo nisingaliwaambia maana naenda kuwaandalia mahali basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali nitakuja tena niwakaribishe kwangu ili nilipo mimi na nanyi muwepo, nami niendako mwaijua njia, mimi nimekuwepo nanyi siku zote, tumetangulia ili kwenda kuwaandalia makao ili siku ya kustaafu kwenu ikifika tutawakaribisha," hayo ni maneno ambayo sehemu yake Makamba alinukuu vifungu vya Biblia.
Kwa tafsiri rahisi, katibu mkuu huyo mstaafu anaonyesha ni kwa kiasi gani alivyokuzwa na kulelewa katika maadili ya kidini bila kujali dhehebu analotoka lakini kwa bahati mbaya makuzi yake ya kidini yameshindwa kufungamana kabisa na watendaji wengine ndani ya CCM na kwenye serikali ya chama hicho kutokana na ufisadi iliokithiri na kusababisha wengine wabatizwe jina jipya kuwa ni gamba la zamani.
Ikumbukwe kuwa kwa falsafa hiyo hata Nabii Isa alipokuwa akiwaaga mitume wake 11 baada ya kufufuka, Tomaso hakuamini na hata Filipo nae hakumjua baba ambako Yesu anataka kwenda kuandaa makao, akamtaka aonyeshwe baba alipo kabla hajaenda kuwaandalia makao kwa kuwa hawaijui njia atakayopita ili nao waweze kumfuata siku ikifika.
Kwa maana hiyo nia ya Makamba ya kwenda kuwaandalia makao wana CCM wenzake waliowaacha kwenye kamati kuu na sekretarieti mpya iliyoundwa ndani yake bado wamo kina Tomaso na Filipo ambao hawamwamini Makamba kwa jambo lolote na hawajui hayo makao anayokwenda kuandaa ni kwa manufaa ya nani.
Ikumbukwe kuwa ni kazi kubwa na ngumu kwenda kuwandalia makao watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi ambao jamii ya CCM imejiwekea mikakati mikubwa ya kuwamaliza mafisadi wote ndani yake na muda wa siku tisini waliopewa ili kupima, kubaki CCM au kuondoka huo ni mtihani mkubwa na kimsingi hawatakuwa tayari kuungana na Makamba katika makao hayo mapya baada ya kujivua gamba la ufisadi.
Lakini jambo kubwa ninalotaka kulisema hapa ni kuhusu dharura aliyonayo mzee Makamba ya kwenda kuwaandalia wenzake makao, lazima awe na tahadhari kubwa kuwa makao hayo lazima yawatenganishe, mafisadi na waadilifu wachache waliobakia ndani ya CCM, vinginevyo makao hayo yanaweza kuwa kambi jipya la majeruhi wa kisiasa waliojivua gamba huku roho zikiwauma.
Kama dhamira ya kuandaa makao mapya itafanywa kwa lengo la kukiponya chama hicho na mafisadi, basi ipo haja Rais Kikwete akaugeukia upande wa pili wa watendaji wa serikali ambao bado wamevaa magamba ya ufisadi na ndio ambao wananchi wanawategemea kwa karibu.
Kwa kauli ya Makamba serikali haiwezi kuwa salama sana kama wale waliobaki serikalini wataendelea kuwa na makao yasiyoandaliwa na wana CCM waliojiuzulu ili kupisha damu mpya ndani yao, nikiamini wanaomuangusha Rais Kikwete na dhana nzima ya ufisadi bado wapo serikalini.
Wana CCM waliojiuzulu kutoka kwenye kamati kuu kamwe hawawezi kuaminiwa na wenzao na hawana nguvu za kuandaa makao ya kuweza kuhifadhi kundi kubwa la mafisadi walioshindwa kukitii chama hicho na serikali yake kiasi cha kujijenga na kubobea zaidi katika vitendo vya rushwa.
Jambo la busara ambalo naliona mbele ya wateule wachache wa CCM waliojipambanua kuwa wamesafishwa upya na hawafanani kabisa na wale walioondoka, nia ya kujisafisha ingeanzia kwa watendaji wote ndani ya CCM yaani mwenyekiti na timu yake yote walipaswa kujiuzulu.
Kujiuzulu huko kungetoa nafasi kwa wajumbe wote wa halmashauri kuu ya CCM (NEC) wapige kura ya kuwa na imani au ya kutokuwa na imani na uongozi wote wa chama hicho sambamba na kumpigia kura Mwenyekiti wao wa taifa ili kupima ni kiasi gani hawajajeruhiwa na nguvu za mafisadi.
Naamini yaliyowakuta akina Makamba akiwa Katibu Mkuu wa CCM hakuwezi kumponya Mwenyekiti wao Kikwete na doa la ufisadi na uchafu wa rushwa iliotanda kila kona ya chama hicho, hakuna kiongozi aliyeweza kuchaguliwa bila rushwa kuanzia mchakato wa chini hadi juu.
Viongozi wa CCM waliovua gamba bado watakuwa wanasutwa na dhamira ya kuwaona wenzao waliobaki ni safi na waadilifu, si mafisadi, sio wala rushwa wala watoa rushwa na kwamba kuchaguliwa kwao hakuna doa la ufisadi na mtandao wa rushwa, doa hilo kila mtu limemchafua waliobaki si salama sana.
Kwa mantiki hiyo, naamini fika kile alichokisema Makamba kuwa anakwenda kuwaandalia makao wana CCM wenzake ambao nao siku yao ya kung'atuka itakapofika awakaribishe huko, haiyamkiniki kuwa nia ni njema lakini hao walioachwa kama wamemsahau Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na fikra zake zote watazikumbuka kweli fikra za Makamba?
Viongozi wa CCM wamesahau kuwa Nyerere na Abeid Aman Karume wametangulia mbele ya haki ili kwenda kuwaandalia makao wengine na kama hao wamedharaulika ni nani anayeweza kuamini kuwa makao ya Makamba ni muafaka kwa wana CCM waliopo madarakani, ni lini mafisadi waliobaki ndani ya chama hicho na serikali yake wataiamini njia aliyopita Makamba?
Ndiyo maana Nasema Hivi inakuwa vigumu sana kuifanya jamii iamini uadilifu wa viongozi walioondoka na kusadiki kuwa hawa waliobaki ni waadilifu, si mafisadi na hawakuchaguliwa kwa hongo wala ulaghai, basi kwa kuwa waliondoka wapo ndani ya CCM na wanaobaki ni CCM kama makao ya Dodoma hayafai ni wapi ambapo CCM itazaliwa upya?
 
h.sep7.gif
master.gif

Hongera Kikwete kuizika CCM
ban.blank.jpg

Walter Sawe

amka2.gif
BABA wa Taifa hayati Julius Nyerere aliwahi kusema: "Upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM''. Kauli hii sikuielewa na sikujua lengo la kusema vile wakati yeye ni miongoni mwa waasisi wa chama hicho tawala.
Lakini kadiri muda ulivyokwenda sasa maneno yale tayari yanapiga hodi, kelele katika mawazo yangu na kuweka mwangwi mkuu katika fikra hata kwenye njozi zangu.
Binafsi nakumbuka kipindi kile cha Mwalimu Nyerere kama pakitokea migawanyiko au migongano yoyote ile iwe ndani ya chama au nje ya chama chake TANU/CCM, alitumia busara na hekima kwa kuitisha vikao mapema na kulizungumzia tatizo husika.
Leo hii baada ya yeye kufariki dunia, mambo yamekuwa vuluvulu, busara zimekuwa haba, siasa nazo zimegeuzwa vijiko vya kuliibia taifa, sasa kuna nyufa kwenye chama chake alichokiacha.
Rejea kuibuka kwa matabaka ya walionacho na wasiokuwa nacho pia kuwepo makundi (mitandao) ndani ya chama na nje ya chama.
Ninachopenda kusema kupitia makala hii ni kwamba hali ya chama hicho kikongwe barani Afrika leo kama ni kweli na kilichofanyika mjini Dodoma (kujivua gamba).
Naomba nikiri kwamba nilivyoangalia mchakato mzima na kufuatilia mwenendo ulivyokuwa, ndipo nilipoyakumbuka yale maneno ya Nyerere alivyousia kuwa upinzani wa kweli utakaoifurumusha CCM utatoka ndani ya cha hicho tawala.
Leo nikubali kwamba hayawi, hayawi, sasa yamekuwa ndani ya CCM baada ya kuyazika yaliyokuwa mienendo (dira) maadili ya uongozi, dalili zilizopo sasa na huko tuendako kama ndivyo tulivyoshuhudia, ilivyotangazwa na vyombo vya habari mjini Dodoma (kuvunjwa sekretarieti).
Naweza kusema kuwa kazi ya kuisambaratisha CCM sasa imeshaanza, aliyeianzisha ni Rais Jakaya Kikwete ingawa najua ni jambo la bahati mbaya sana kwamba rais wetu halijui hilo na pengine niseme anaweza kudhani ni hadithi za kufikirika.
Najua waliomsifia Kikwete kuwa yeye ni ‘Chaguo la Mungu' walifanya hivyo kwa kubembeleza masilahi na kujikomba, walishindwa kujua upande wa pili wa shilingi kuwa alichaguliwa kubomoa si kujenga. Nani leo atabisha? Rejea serikali yake kukumbwa na utitiri wa kashfa na asizishughulikie!
Nasema anakuja kubomoa kwani kadiri siku zinavyozidi kwenda ndivyo ugumu wa maisha kwa mwananchi unavyoshamiri na bei za bidhaa zinapaa mithiri ya ndege ya rais iliyonunuliwa kwa gharama za wavuja jasho walioambiwa wale majani ili usafiri huo ununuliwe.
Rais anayekiri kuwa mambo ni magumu na wananchi wake wawe wavumilivu lakini viongozi na watendaji wengine wakitafuna (ufisadi) wa rasilimali za taifa kwa faida yao bila kuchukuliwa hatua za kisheria ua kinidhamu, tumuweke kwenye kundi gani?
Ufisadi hivi sasa ndiyo imekuwa sifa kubwa kwa kiongozi, kutumikia wananchi hivi sasa hakupo tena kila anayepata wadhifa hufikiria kujinufaisha badala ya kuwaangalia wale waliompigia kura.
Uteuzi wa viongozi wa ngazi mbalimbali umekuwa ukifanyika kwa lengo la kulindana, kulipana fadhila, kirafiki na vigezo vinginevyo ambavyo kimsingi havipaswi kuangaliwa wakati wa uteuzi.
Rais Kikwete, haonekani kubadilika kwa kutowachagua watu kwa sifa na vigezo walivyonavyo, uswahiba, umtandao umekuwa ukiendelezwa kwa kificho au kwa uwazi.
Nakumbuka aliyewahi kuwa Rais wa Kenya, Daniel arap Moi, kipindi kile ama kwa kujua au kutojua alijikuta akipigilia misumari ya mwisho kwenye jeneza la chama chake cha KANU kilichokuwa kikitawala pale alipolazimisha Uhuru Kenyatta agombee urais badala ya Mwai Kibaki aliyekuwa akionekana ndiye chaguo la watu wengi.
Moi alionywa kuwa uamuzi wake huo unalenga kukiua chama chake lakini hakusikia, matokeo yake KANU ilianguka na Kibaki akafanikiwa kuwa rais kwa kupitia muungano wa vyama vya upinzani (NARC)
Kilichotokea Kenya ndicho ninachokiona kwa CCM ambapo baadhi ya wanaosema ukweli na kukosoa ufisadi ndio wanaoshughulikiwa kwa madai ya kukiyumbisha chama na wengine walishughulikiwa kwenye michakato ya chaguzi mbalimbali za chama na zile za kitaifa.

Ninachopenda kusema baada ya kulisoma somo lile la Kenya, nikaangalia mambo yalivyo CCM ninaona dalili za kifo cha chama hicho chini ya Rais Kikwete kimewadia na upinzani wa kweli utatoka humo.
Leo hii CCM wanapowaadhibu wakemea ufisadi ambao wamejizolea umaarufu mkubwa inategemea nini? Makada hao wakiamua kujiengua chamani na kujiunga na upinzani nina uhakika huo ndio utakuwa mwanzo wa kubomoka kwa chama hicho tawala.
Ni ulevi wa madaraka na kutosoma alama za nyakati ndiko kunakowafanya baadhi ya makada wa CCM kuimba wimbo kuwa chama hicho kitatawala milele pasi na kuungalia ukomavu wa vyama vya upinzani unaoonekana sasa.
Nawaomba Watanzania wenzangu wale wote wapenda mabadiliko na maendeleo, Tumwombe Mungu huko tuendako walioenguliwa CCM wajiunge na upinzani ili tupate mabadiliko kwenye nyanja mbalimbali.
CCM inaweza kuwa kwenye benchi la upinzani kama KANU au UDF ya Malawi, yote haya yanawezekana kama wale waonaofanyiwa fitna ndani ya chama tawala wataamua kuchukua maamuzi magumu na kujiunga na upinzani ili waendelee kupigania mgawanyo sawa wa rasilimali za taifa.
Najua makada wa CCM wasingependa kusikia chama chao kitakuja kuwa cha upinzani na hivi sasa wanajifariji kuwa wamejivua gamba lililokuwa likiwapa sifa mbaya kwa wananchi, wanajidanganya.
Nasema wanajidanganya bure kwani ile migawanyiko, matusi,kuvuana nguo tulikoshuhudia siku za hivi karibuni ndani ya chama hicho na jumuiya zake ni cheche za kukimaliza chama hicho.
Ukweli ni kuwa saratani inayoitafuna CCM ipo ndani ya damu, hivyo kujivua gamba hakutaweza kukinusuru chama hicho, kwani rais ni yule yule, watu ni wale wale, sitarajii mambo mapya baada ya uamuzi huo unaoitwa ni mgumu.
CCM na serikali yake watazidi kuumizwa na kushindwa kutekeleza ahadi ilizozitoa kwa wananchi katika kampeni za uchaguzi wa mwaka 2005, 2010 hasa ile ya maisha bora kwa kila Mtanzania. Hii ni saratani.
Rejea pia vigogo wengi wa CCM hadi leo wanakabiliwa na tuhuma za wazi zikiwemo zile za kughushi hata vyeti vya taaluma, kukwapua mabilioni ya fedha kupitia Kampuni za Meremeta, Kagoda, Deep Green.
Chama hicho pia kinadaiwa kuhusika na wizi mkubwa wa Fedha za Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) zilizokuwa zimehifadhiwa Benki Kuu, fedha hizo inasemekana ndizo zilizompa Rais Kikwete ushindi mwaka 2005.
Niseme kuwa hata kuhusishwa kwa kada wa CCM na aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali, Andrew Chenge, kuhusishwa na ufisadi mkubwa wa rada lakini bado ni mbunge!
Pia aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kuhusishwa na ufisadi wa kutisha wa Kampuni ya kufua umeme ya Ricmond/Dowans, ambao unatikisa nchi hadi leo halafu eti ni mbunge wa chama kile kile! (‘Tushajivua gamba bwana')
Rejea kauli ya Rais Kikwete hivi karibuni kwenye NEC, "katika kipindi hiki cha mazongo mazongo yetu, wananchi wamekata tamaa na ninyi ndio wenye mamlaka ya hali hiyo''.

Nilishituka nikajiuliza hapa rais wetu anampiga chenga nani au anamdanganya nani wakati mambo yote ndani ya serikali na chama ni lazima yapitie mezani kwake, maana yeye ni mwenyekiti wa chama na kiongozi wa baraza la mawaziri?
Rais Kikwete amesahau kuwa yeye ndiye aliyewapigia kura mwaka jana tena kwa kuwanadi kuwa hao ni hazina ya chama, mapanga ya zamani yenye makali mapya, sasa anapotoa muda wa kupima wenyewe ana lengo gani?
Naomba kwa faida ya Watanzania na wale wote waliopewa miezi mitatu kama wapo au wanatarajia kuondoka, nitanukuu katiba yetu ya mwaka 1977 ambayo yeye (Rais) anailinda sehemu ya ibara ndogo ya (4)ya ibara ya 132 inasema hivi:
"Katiba inapiga marufuku viongozi wasio waaminifu, wanaopendelea au wasio waadilifu, wachochezi wa rushwa katika shughuli za umma, wanaohatarisha masilahi ya taifa na ustawi wa jamii. Katiba inawataja hao viongozi ni kuanzia; Rais, Makamu wa Rais,Waziri Mkuu, mawaziri, spika, waziri kiongozi (Zanzibar),wakuu wa mikoa, mabalozi, makatibu wa wizara,wabunge na wengine wote. Bila kusahau kile kifungu cha sheria ya maadili ya umma namba 13 ya 1995 kinachoweka wazi hatua za viongozi wezi na mafisadi kuchukuliwa.
Mmeisikia katiba hiyo mliyojivua gamba na ambao mnasubiri kuvuliwa? Msomaji wangu na Mtanzania mwenzangu leo ukiulizwa mantiki ya Rais Kikwete kushindwa hata kutaja mali zake au awabane wenzake wataje, wewe utajibu nini?
Rejea kila mtu leo ni msemaji ndani ya awamu ya nne, yako wapi yale maisha bora tuliyoahidiwa miaka sita sasa tangu Kikwete aingie madarakani? Yako wapi ikiwa leo mama zetu wanapewa bajaji au kujifungulia nje ya hospitali huku watawala wakishindana kununua mashangingi kwa fedha za masikini?
Ushahidi wa kushindwa kwake Kikwete leo upo, kuna jambo moja kubwa na la maana sana ameshaanza kulifanya, anakiua chama chake, tumsaidie kwa sababu ni ukombozi kwa Watanzania.
Wakati tukimuunga mkono Rais Kikwete kwa kuiua CCM, tuwape changamoto wale wote walioondolewa kwenye sekretarieti kwa kuwaambia ‘wasiogope kujiondoa ndani ya chama hicho tawala.
 
Hawana Jipya kwa Watanzania zaidi ya siasa za Maji Taka zao hivyo ni wakati wa Watanzania kuamka sasa
 
Tusitegemee kumuona uchi aliyekwenda kununua nguo mpya dukani
ban..jpg


amka2.gif
CHAMA tawala nchini, Chama Cha Mapinduzi (CCM), hivi karibuni kiliahidi kufanya mabadiliko katika muundo wake ili kukabiliana na changamoto zinazotolewa na vyama vya upinzani.
Mabadiliko hayo yaliahidiwa na Mwenyekiti wa taifa wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete, wakati wa sherehe za mwaka huu za kumbukumbu ya kuzaliwa kwa chama hicho mjini Dodoma.
Rais Kikwete, alitumia neno "chama kujivua gamba" kumaanisha mabadiliko makubwa yaliyokuwa yanatazamiwa kufanyika ndani ya chama hicho.
Mabadiliko hayo yalionekana kushinikizwa na ushindani wa kisiasa ambao CCM ilikuwa haikuuzoea kutokana na chama hicho kuhodhi siasa za nchi yetu tangu kilipozaliwa.
Baada ya mfumo wa vyama vingi kurudishwa nchini CCM kimejikuta kikishindwa kwenda sambamba na kasi ya vyama vipya vya upinzani na hivyo chenyewe kulazimika kuegemea kwenye dola muda wote wakati vyama vingine vikijihimili vyenyewe na wakati mwingine dola likijaribu kuviingilia ili kuvipunguza kasi.
Katika hali kama hiyo naweza kusema CCM ni chama kisichojiamini, ndiyo maana kinakosa moyo wa uthubutu. Daima uthubutu hutokana na kujiamini, pasipo kujiamini uthubutu ni muhali.
Kwa nini uthubutu kufanya kitu mahali usipo na uhakika kama utapata au utapoteza? Maana kuthubutu bila kujiamini ni kukubali kupoteza.
Ni kwa sababu hiyo kauli ya CCM kujivua gamba ikachukuliwa kama mchezo wa kisanii.
Pamoja na hiyo kitu kilichojitokeza kuishtua zaidi CCM ni matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana. Hata kama CCM iliibuka na ushindi lakini ujumbe uliotokana na ushindi huo wa mbinde uliifanya ilazimike kujitazama upya.
Mwenyekiti wake akaona kwamba kuna umuhimu wa chama chake kujivua gamba, kwa maana ya kujibadilisha muonekano ili kuweza kuyahimili zaidi mazingira ya sasa ya kisiasa nchini.
Mabadiliko hayo yaliyoahidiwa na mwenyekiti wa CCM, kujivua gamba, yalichukuliwa na baadhi ya watu kwamba yatakuwa mabadiliko ya kukifanya chama hicho kujiweka katika muonekano ulio sawa na wa vyama vingine na hivyo kukifanya chama hicho kuwa katika ushindani ulio sawa wa kisiasa katika kuvipunguzia vyama vya upinzani huruma viliyokuwa vinaipata toka kwa wananchi.
Maana kwa kiasi kikubwa ilichukuliwa kwamba pengine CCM ilihisi kwamba ni huruma hiyo iliyokisababisha kufanya vibaya katika uchaguzi uliopita.
Kwahiyo wengi tulitegemea kwamba chama hicho kujivua gamba ni pamoja kuacha kuwa chama dola, kuachia mambo mengi kinayoyahodhi kama mali zake wakati mambo hayo yalitokana na nguvu za wananchi wote walio wanachama wa chama hicho na waliokuwa si wananchama wake.
Pia tulitegemea kwamba kutakuwepo mabadiliko makubwa ya kimfumo na kimuundo katika chama ambayo yangeweza kukionyesha kama chama kipya kilichokusudia kuvuta hisia za wananchi.
Katika kufanya hivyo tulitegemea kuona baadhi ya makada wake waliokisababisha kuchujuka na kupoteza mng'ao wake kwa wananchi wakiondolewa kwenye nafasi zao na hata kunyang'anywa kadi.
Sababu watu hao ambao wamekifikisha chama chao katika hali ya umahututi hatukutegemea waendelee kuitwa "wenzetu" ndani ya chama hicho.
Hao ni watu ambao walistahili adhabu ya chama, kama kweli chama hicho kilikuwa kimedhamiria kufanya kile kilichokuwa kinakieleza kwa wananchi.
Ni kwa mtazamo huo tulitegemea CCM kijitenge kabisa na ufisadi uliogeuzwa nembo yake ya biashara.
Si kwamba chama hicho kinaukubali ufisadi kwa kauli, kilichopo ni vitendo vinavyoonyesha ukaribu wa chama hicho na shetani ufisadi.
Watu wanaoshukiwa kwa tabia hiyo ya hatari kwa jamii wamekuwa vipenzi wakubwa wa chama hicho.
Kwahiyo tulitegemea kwamba katika kujivua gamba chama hicho kingejaribu kujitenga na watu hao. Lakini ajabu kimeshindwa kukidhi kiu hiyo.
Wapo watu waliokuwa vipenzi wa Chama Cha Mapinduzi lakini baadaye wakawa wamekatishwa tamaa na chama hicho kiasi cha kuamua kwenda kwenye vyama vingine na wengine kuachana kabisa na mapenzi ya vyama vya siasa.
Watu hao wana sababu zao, nazo ni kuchefuliwa na mambo yalivyokuwa yakiendeshwa ndani ya chama chao kikongwe.
Ni vigumu watu hao kuwashawishi kuwa chama hicho kwa sasa kimebadilika, kimejivua gamba, bila kuwaonyesha adhabu walizochukuliwa wale waliokifanya chama kuvaa gamba hilo chafu.
Naliita gamba chafu kwa maana lingekuwa gamba safi sidhani kama lingejitokeza wazo la kukitaka chama kulivua gamba hilo.
Kitu kisafi hutunzwa na sio kuvuliwa na kutupwa. Kwahiyo wazo la kwamba chama kijivue gamba limesukumwa katika vitendo na uchafu wa gamba hilo.
Ili kukirudishia chama imani ya wanachama na wananchi kwa ujumla ulikuwepo umuhimu wa kuwatambua wale waliokisababisha chama kupoteza imani kwa wanachama na wananchi.
Wakishatambulika zionekane hatua za kinidhamu zilizochukuliwa dhidi yao . Bila ya hiyo ni vigumu kabisa kujenga ushawishi wa kwamba chama kimebadilika.
Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika juzi kimehitimisha mawazo ya kufikirika tuliyokuwanayo wengi wetu.
Tumesikia kwamba yamefanyika mabadiliko ya kawaida ndani ya chama hicho, kujiuzulu kwa sekretarieti ya chama hicho si kipimo tosha kuweza kuona kama chama hicho kimebadilika.
Kujiuzulu kwa watu hao kunamaanisha kwamba watu hao walikuwa na madhambi, kwahiyo kujiuzulu peke yake hakutoshi kuwarudishia imani wale walioishiwa na imani ya chama hicho.
Sababu mtu akifanya kosa hawezi kuambiwa toka kimbia na potea, hiyo ikakubalika kuwa ni adhabu. Mtu akiiba, kwa mfano, ni lazima apewe adhabu inayolingana na kosa la kuiba ambayo mara nyingi ni kutengwa na wanajamii wenzake kwa muda fulani huku akitumikia kazi ngumu.
Baada ya hapo wanajamii wenzake wanaweza kurudisha imani kwamba adhabu hiyo itakuwa imemfundisha kitu fulani na hivyo kumrudisha katika nafasi ya raia mwema.
Lakini yule anayeambiwa toka kimbia na potea hawezi kuaminika kama anaweza kurudia wema wake, atabaki anawatia shaka wanajamii na kuwafanya waishi wasiwasi.
Kibaya zaidi ni kwamba katika mabadiliko ya juzi yaliyofanyika ndani ya CCM bado majina yale yalioonekana kukipaka chama hicho matope yanaendelea kujitokeza katika safu inayodaiwa ni mpya yakiwa ni ya watu walewale au warithi wao.
Hilo linatia shaka kama chama hicho kimedhamiria kujivua gamba kikweli kweli.
Kutokana na mabadiliko hayo yanayomtoa mtu na kumweka mrithi wake au kumzungusha mtu yule yule na kumbakiza pale pale au kumsogeza katika nafasi ya jirani, kunajitokeza mawazo ya kwamba chama kinavua gamba na kuvaa gamba jipya au kuliimarisha gamba la awali.
Haileti picha ya chama kujivua gamba kwa lengo la kujilegeza na kuojiondolea mkakamao utakaowawezesha watu kukisogelea kwa wepesi.
Chama Cha Mapinduzi kina wananchama wasiopungua milioni tano nchi nzima, haiingii akilini hata kidogo chama hicho kidhamirie kufanya mabadiliko halafu tuendelee kuziona sura zilezile tulizozioea kwa takriban miaka 30 katika uongozi wa chama ngazi ya kitaifa.
Chama chenye wananchama milioni 5 kinawezaje kushindwa kubadilisha sura za watu wasiozidi mia tatu?
Kwani hawa wana hisa gani katika chama kiasi cha kuendelea kuzishikilia nafasi hizo wao tu bila kuwajaribu wanachama wengine?
Neno kujivua gamba linaleta maana kwa vitu viwili kama nilivyoonyesha mwanzo. Kubadilisha muundo na mfumo wa chama pamoja na kubadilisha kabisa sura katika safu ya uongozi wa chama.
Lakini kubadilisha tu nafasi za ukaaji katika vikao vya chama wakati sura ni zile zile hakuwezi kukubalika kama chama kujivua gamba, sana sana kutaonekana kama chama kuliimarisha gamba lake chafu.
Siku chache zilizopita niliandika nikiuliza kama nchi yetu imerudi katika utaratibu wa kuendeshwa kiufalme ambapo nyadhifa za utawala zinakwenda kwa kurithishana kiukoo.
Niliuliza vile kwa sababu niliona kwamba kama baba alikuwa katika safu ya utawala ni lazima ahakikishe mtoto wake naye anakuja kwenye safu ileile ya utawala.
Inaleta maana gani iwapo baba amelazimika kujiuzulu kutokana na kufanya madudu katika nafasi nyeti anayokuwa amekabidhiwa halafu na mwanae ndiye aje kurithi nafasi hiyo iliyomshinda baba yake?
Haya yalikuwa yanafanyika katika taratibu za kifalme peke yake.
Kwa hali yoyote ile hii dhana ya CCM kujivua gamba, kwa mwenendo huu, si ya kushangilia hata kidogo.
Kuna uwezekano CCM ikawa inajivua gamba jepesi, ambalo pengine imeona kuwa vyama pinzani vinalipenya kiurahisi, ili kuvaa gamba la chuma litakalokiwezesha chama hicho kufanya madudu yake bila bughudha yoyote kutoka kwa vyama vya upinzani.
Mtu anayekwenda kununua nguo mpya dukani haina maana kwamba ile nguo yake ya zamani ni lazima aitupe, kwahiyo wanaotegemea kumuona akiwa uchi kwa vile kasema kwamba nguo yake ya siku zote kaichoka wanakuwa wamejidanganya.
Kwahiyo kulishangilia hilo la CCM kujivua gamba tutakuwa tunachekelea kifo kama kicheche, huo ni usemi wa Wahaya ambao kikwao wanatamka "Okushekelela orufu nk'omunyima".


h.sep3.gif

prudencekarugendo@yahoo.com
 
Hivi ndivyo CCM inavyocheza na akili za Watanzania
ban.tafakuri.jpg

Deogratius Temba

amka2.gif
HABARI mpya za kuwalainisha Watanzania waliokwisha kuamka na kuuona uozo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na uchafu wake ndani ya serikali kwa miongo kadhaa zinaenezwa nchi nzima.
Habari ni kwamba "imezaliwa CCM mpya" kunahitajika kazi kubwa kuthibitisha kama kweli kuna CCM mpya ambayo imezaliwa tofauti na ile tunayoifahamu ya mwaka 1975.
Kama kweli kuna tofauti kati ya CCM iliyokuwa inaongozwa na Luteni mstaafu Yusuf Makamba na Jakaya Kikwete.
Kunahitajika uchunguzi na uchambuzi wa kina kujua kama kweli, kuna CCM mpya ambayo haina mafisadi, haina kashfa mbalimbali za ukwapuaji wa mabilioni ya fedha katika akaunti ya madeni ya nje (EPA) pale Benki Kuu.
Tayari timu ya wajumbe wa Halmahauri Kuu na Kamati Kuu ya CCM (CC), imeshasambaa nchi nzima kuwatangazia wananchi kuwa ufisadi umeisha ndani ya CCM.
Majina matatu ya wanachama wa CCM waliokuwa wajumbe wa Kamati Kuu ambao bado ni wajumbe wa Halmashauri Kuu yametajwa, chama kikashindwa kuwawajibisha kisheria, hata kinidhamu kwa wakati huo.
Chama kikabakia kuwaogopa kwa kuwataka wapime uzito wenyewe. Hii kauli ya kupima uzito ni kauli ya kuogopana, kama umeona mtu ni mwizi au anakwenda kinyume na maadili, kukosa uaminifu kwanini usimchukulie hatua.
Je, chama chenye serikali ambacho hakiwezi kuwawajibisha wananchama wake wakorofi kina sababu gani ya kuendelea kuaminiwa na kuongoza nchi?
Haiwezekani mkutano wa halmashauri Kuu umemalizika ndani ya siku saba, maazimio yaliyotoka hayatajatekelezwa, watuhumiwa wa ufisadi waliotuhumiwa kuchezea rasilimali za taifa hawajachukua au kuchukuliwa hatua tunatangaza kuwa ufisadi umeisha ndani ya CCM.
Kwa mtu mwenye akili timamu, busara na hekima, tena mchanganuzi wa mambo na mwenye kusoma alama za nyakati kwa haraka hawezi kukubali kutumika na CCM kuwadanganya wananchi kuwa imezaliwa upya.
Kauli hizi ni sawa na kutangaza kuwa Watanzania wana maisha bora na hawana tatizo. Tujipe muda, tuangalie kama CCM imejivua gamba kweli, tuone mabadiliko ya kweli, tuone mwelekeo wa kile kilichokataliwa ndani ya chama.
Vinginevyo hatua inayochukuliwa na CCM kwa sasa ni ya kukurupuka na kujihami kwasababu kinajua kimechafuka, kudhalilika, kimepoteza mvuto, kiko mahututi na kinaelekea kufa.
Tena kibaya zaidi, timu mpya ya sekretarieti inayojigamba kusambaa nchini kukisafisha chama ambayo inaongozwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye, imeanza kuonesha dalili za wazi kuwa itashindwa kazi mapema na ionawezekana ikaelekea kubaya kuliko sekretarieti ya Yusuf Makamba iliyojiuzulu.
Nape anatumia kasi ya kukimbizana na mafisadi kama vile mtu aliyemwona paka mwizi akimendea kula vifaranga cha kuku, akifikiri kuwa atamkamata kwa mbio za miguu bila kuweka mitego.
Nape na CCM wanapaswa kujua kuwa mafisadi ni wanasayansi kwa nafasi yao, wamejengwa, wamepikwa, wamekulia na kuzeekea ndani ya CCM. Hicho ni chama chao na hawana pa kukimbilia.
Kuwatoa au kuwaadhibu kunahitaji uchambuzi yakinifu na sayansi ya aina yake pia. Vinginevyo Nape na wenzake watalipana posho za safari kwa miezi kadhaa na mwishowe wataishia kuzomewa na wananchi mikoani.
Kasoro nyingine CCM wanadhani tatizo ni kubadilisha sura za watu ndio ufumbuzi wa tatizo; wakati tatizo ni mfumo wa kutumia rasilimali na vyombo vya usalama vya umma kulinda CCM na ufisadi wake halafu wanakurupuka na kuondoa kamati kuu na sekretariati pamoja na watu watatu wanaodhani ni mafisadi pekee.
Ufisadi kwa CCM uko kitaasisi (institutionalized), mpaka ndani ya serikali. Kwa hiyo kinachotakiwa ni kufumua mfumo na sio kubadilisha sura, lakini wanajidanganya wao kwanza halafu wanadhani watawadanganya na Watanzania wapatao milioni 40.
CCM wanakumbuka kosa la heri walilolifanya mwaka 2008, wakati mawaziri wa Rais Jakaya Kikwete walipojaribu kwenda mikoani kuitangaza bajeti ya mwaka wa fedha 2008/09 iliyokuwa ikiendelea kuwabana wananchi masikini. Mawaziri walizomewa na kupigwa mawe na wananchi waelewa.
Wanachokiita " kujivua gamba" CCM wasitegemee kwamba Mtanzania mwenye akili timamu ataamini akiambiwa kwamba sasa ufisadi umekwisha CCM.
Muda wa kuwadanganya watu kwa kukubali kila kinachosemwa umepita, sasa hivi watu wanaelewa na wanaona hivyo wanataka matendo zaidi kuliko porojo na ngonjera.
CCM wangefanya jambo la heri kama wangezunguka nchi nzima kuwashtaki mafisadi kwa wnaanchi kwa kuwataja majina waziwazi na kutangaza adhabu ambayo chama kitawachukulia ikiwa ni pamoja na kuwafilisi kwa kuliibia taifa na kuwakabidhi mikononi mwa vyombo vya dola kwa hatua za kisheria.
Wawataje nani ni mmiliki wa Kagoda, Dowans, Richmond, Meremeta, Deep Green, na makampuni mengine ya kifisadi yaliyotuingiza kwenye umaskini wa kutupwa.
Hakuna CCM mpya bila mabadiliko ya kweli. Sheikh yule yule kanzu nyingine kuna mabadiliko?
 
Serikali inakimaliza CCM kupitia katiba mpya
ban.bamdogo.jpg

Innocent Nganyagwa

amka2.gif
KAMA Chama Cha Mapinduzi (CCM) kisipokuwa makini, kinaweza kuathirika sana kiasi cha kung'olewa madarakani kutokana na jinsi ambavyo serikali inalishughulikia suala la mchakato wa uandikaji wa Katiba mpya.
Tumeshuhudia mambo ya ajabu sana kuhusiana na suala hilo hadi hivi sasa.
Inavyoelekea, kuna watu ndani ya serikali ambao wana lengo la kukihujumu chama tawala. La sivyo, wasingefanya hivi wanavyofanya. Ndio maana nakishauri CCM kuwa makini sana na watendaji wa serikali maana inaonekana hawakitakii mema chama hicho.
Serikali inadhani kuwa Watanzania wa leo bado ni wale wa mwaka 47. Haijajua kuwa wameamka na si tu kuwa wanazijua haki zao, bali pia wanajua jinsi ya kuzidai.
Yaliyotokea katika uchaguzi mkuu uliopita yalipaswa kuwa funzo kwa serikali kuwa Watanzania wamebadilika. Hata kama si wizi, nani alitarajia kuwa wananchi wanaweza kuvipa vyama vya upinzani kura nyingi kiasi cha kushusha kwa kiasi kikubwa wigo wa ushindi wa CCM.
Hivi sasa CCM na serikali zina kazi kubwa sana ndani na nje ya Bunge. Ingawa idadi ya wabunge wa upinzani si kubwa sana, lakini hao wachache waliopo wameonyesha umakini wa hali ya juu na wasio na woga wa kuiwajibisha serikali. Wanajua nguvu yao inatokana na nini na wapo tayari kuitumia.
Huku nje nako mambo si mazuri. Mwamko wa wananchi, kama ulivyoshuhudiwa katika maadamano na mikutano ya vyama vya upinzani, ni uthibitisho kuwa wananchi nao wameshafamu nguvu waliyonayo na wapo tayari kuitumia. Serikali na CCM tayari wameshataharuki.
Ukiangalia jinsi Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) ulivyochanganyikiwa kiasi cha kuanza kuwatafuta wachawi miongoni wa wana CCM wenyewe, na jinsi ambavyo chama kwa ujumla wake kimeshindwa kudhibiti malumbano baina ya taasisi na makada ndani ya chama hiho, ni dhahiri kuwa kutaharuki kwa CCM kumefikia hatua mbaya sana.
Kwa upande mwingine, midahalo miwili juu ya katiba mpya iliyoandaliwa na Udasa, imetoa picha ya nini ambacho wananchi wanakitaka. Midahalo hiyo ilipaswa kuwa somo zuri na kubwa kwa CCM.
Walitakiwa kuangalia kilichosemwa na kutokea kwenye midahalo hiyo, na mijadala iliyoibuka baada ya midahalo, na kuchanga vema karata zake.
Kama ingekuwa CCM bado ina watu wanaofikiria vema, midahalo hiyo ilikuwa ni fursa ya kupanga mikakati ya kuhakikisha kuwa inajipanga nayo kuhakikisha kuwa inatoa ushawishi katika mchakayo wa kuandika katiba mpya kwa kutumia mwelekeo wa wananchi waliouonyesha.
Ni dhahiri kuwa wananchi wengi wameonyesha kuchoshwa na katiba iliyopo. Hata serikali nayo imeshadhihirisha kuwa baada ya mika 50 ya uhuru, umefika wakati wa Tanzania kujipatia katiba mpya ambayo uandaaji wake utahusisha wananchi wengi iwezekanavyo.
Ni Rais Jakaya Kikwete aliyetanga kuanzisha mchakato wa uandikaji wa katiba mpya. Yeye ni mwenyekiti wa CCM. Sijui kumetokea nini kiasi kwamba serikali inaonyesha kana kwamba inataka kuichongea CCM kwa wananchi.
Ukianglia mambo aliyotokea kuhusiana na mchakato wa Katiba mpya, ni dhahiri kuwa serikali haiitakii mema CCM.
Kwanza, serikali iliamua kuandaa muswada wa mabadiliko ya katiba iliyopo kimya kimya bila kuhusisha wananchi.
Muswada huo, kimsingi, unataka kuleta mabadiliko katika katiba iliyopo ili kuingiza vipengele vinavyohusiana na mchakato wa uandikwaji wa katiba mpya ili kuwezesha kuanza kwa mchakato huu ukiwa na misingi ya kisheria. Hili wa si jambo baya.
Lakini serikali, kana kwamba ina nia mbaya, haikuhusisha wananchi na wadau wengine katika mchakato wa kuandaa muswada huo. Serikali ilitangaza kuwa muswada huo ungewasilishwa kwenye vikao vya Bunge vinavyoendelea hivi sasa mkoani Dodoma.
Wananchi wakakaa mkao wa kusubiri kualikwa kutoa maoni yao kuhusiana na muswada huo. Hawakuipata nafasi hiyo na walikuja kushtuka kuwa muswada huo umeshaandaliwa.
Ni ajabu kuwa serikali iliamua kufanya hivi wakati wananchi walishaonyesha kupitia mijadala mbalimbali kuwa hawatakubaliana na mchakato wa uandikaji wa Katiba mpya ambao hauwashirikishi.
Serikali, kana kwamba haikusikia maoni hayo, ikaamua kuandaa muswada wa kwanza kabisa katika mchakato kuelekea uandikwaji wa katiba mpya bila kuwashirikisha!
Wananchi walipogundua hilo, wakapaza sauti zao wakitaka kupewa nafasi ya kuingiza maoni yao kwenye muswada huo. Bunge likaamua kufanya majadiliano ya kitaifa ili kukusanya maoni ya wananchi kuhusiana na muswada huo.
Majadiliano hayo yalipangwa yafanyike kwa siku mbili, Dar es Salaam na Dodoma. Wazanzibari nao wakaja juu kwa nini wameachwa, kikaongezwa kituo cha tatu, Zanzibar.
Siku ilipofika, wananchi waliojitokeza Dodoma wakazuiwa kuingia kwenye ukumbi. Wale wa Dar es Salaam walipigwa butwaa walipofika ukumbini na kukuta umejaa watoto!
Ni ajabu kuwa zinaweza kutolewa siku mbili tu kwa wananchi kuujadili muswada huo. Ni ajabu zaidi kuwa kunaweza kuwekwa vituo vitatu tu vya kuujadili muswada huo.
Hii ina maana kuwa wananchi wa mikoa mingine zaidi ya 23 ya Tanzania, wamenyimwa haki ya kutoa maoni yao kuhusiana na muswada huo.
Ajabu nyingine ni kuwa baada ya kufahamu kuwa wananchi wengi wanapenda kutoa maoni yao kuhusiana na muswada huo, vikao vya kupokelea maoni ya wananchi vikapangwa kufanywa kwenye kumbi ndogo!
Lakini, cha kushangaza kingine ni kuwa wale walioruhusiwa kuingia, hivi walitarajiwa watoe mchango gani wa maana kwa muswada ambao hata hawaujui?
Matokeo yake pale Dodoma watu walipigwa mabomu ya machozi kwa sababu tu wanadai haki yao ya kutaka kusikilizwa na serikali waliyoiweka madarakani. Sasa kama serikali haitaki kuwasikiliza wale ambao wameiweka madarakani, hivi watu hawa wataendelea kuipenda tena serikali hii?
Na hiki ndicho kitakachokiponza CCM. Wananchi wameshagundua kuwa serikali ndiyo inayowawekea kizingiti kushiriki katika mchakato wa kuandika kwa katiba mpya.
Kama wataipata au hawataipata katiba wanayoitaka au wasioitaka hadi kufikia 2015, ni dhahiri kuwa wananchi wengi watakuwa wameshashtuka kiasi cha kutothubutu kuichagua tena serikali inayohusisha watu ambao wapo hivi sasa.Wataikataa.
Na kwa sababu serikali hiyo inaundwa na CCM, ni dhahiri kuwa chama hicho litaanguka pamoja na serikali yake.
CCM inapaswa kufahamu kuwa matendo yake yanahatarisha ushindi wa chama hicho kwenye uchaguzi ujao. Kisije kusema kuwa sikukionya.
 
Serikali inakimaliza CCM kupitia katiba mpya
ban.bamdogo.jpg

Innocent Nganyagwa

amka2.gif
KAMA Chama Cha Mapinduzi (CCM) kisipokuwa makini, kinaweza kuathirika sana kiasi cha kung’olewa madarakani kutokana na jinsi ambavyo serikali inalishughulikia suala la mchakato wa uandikaji wa Katiba mpya.
Tumeshuhudia mambo ya ajabu sana kuhusiana na suala hilo hadi hivi sasa.
Inavyoelekea, kuna watu ndani ya serikali ambao wana lengo la kukihujumu chama tawala. La sivyo, wasingefanya hivi wanavyofanya. Ndio maana nakishauri CCM kuwa makini sana na watendaji wa serikali maana inaonekana hawakitakii mema chama hicho.
Serikali inadhani kuwa Watanzania wa leo bado ni wale wa mwaka 47. Haijajua kuwa wameamka na si tu kuwa wanazijua haki zao, bali pia wanajua jinsi ya kuzidai.
Yaliyotokea katika uchaguzi mkuu uliopita yalipaswa kuwa funzo kwa serikali kuwa Watanzania wamebadilika. Hata kama si wizi, nani alitarajia kuwa wananchi wanaweza kuvipa vyama vya upinzani kura nyingi kiasi cha kushusha kwa kiasi kikubwa wigo wa ushindi wa CCM.
Hivi sasa CCM na serikali zina kazi kubwa sana ndani na nje ya Bunge. Ingawa idadi ya wabunge wa upinzani si kubwa sana, lakini hao wachache waliopo wameonyesha umakini wa hali ya juu na wasio na woga wa kuiwajibisha serikali. Wanajua nguvu yao inatokana na nini na wapo tayari kuitumia.
Huku nje nako mambo si mazuri. Mwamko wa wananchi, kama ulivyoshuhudiwa katika maadamano na mikutano ya vyama vya upinzani, ni uthibitisho kuwa wananchi nao wameshafamu nguvu waliyonayo na wapo tayari kuitumia. Serikali na CCM tayari wameshataharuki.
Ukiangalia jinsi Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) ulivyochanganyikiwa kiasi cha kuanza kuwatafuta wachawi miongoni wa wana CCM wenyewe, na jinsi ambavyo chama kwa ujumla wake kimeshindwa kudhibiti malumbano baina ya taasisi na makada ndani ya chama hiho, ni dhahiri kuwa kutaharuki kwa CCM kumefikia hatua mbaya sana.
Kwa upande mwingine, midahalo miwili juu ya katiba mpya iliyoandaliwa na Udasa, imetoa picha ya nini ambacho wananchi wanakitaka. Midahalo hiyo ilipaswa kuwa somo zuri na kubwa kwa CCM.
Walitakiwa kuangalia kilichosemwa na kutokea kwenye midahalo hiyo, na mijadala iliyoibuka baada ya midahalo, na kuchanga vema karata zake.
Kama ingekuwa CCM bado ina watu wanaofikiria vema, midahalo hiyo ilikuwa ni fursa ya kupanga mikakati ya kuhakikisha kuwa inajipanga nayo kuhakikisha kuwa inatoa ushawishi katika mchakayo wa kuandika katiba mpya kwa kutumia mwelekeo wa wananchi waliouonyesha.
Ni dhahiri kuwa wananchi wengi wameonyesha kuchoshwa na katiba iliyopo. Hata serikali nayo imeshadhihirisha kuwa baada ya mika 50 ya uhuru, umefika wakati wa Tanzania kujipatia katiba mpya ambayo uandaaji wake utahusisha wananchi wengi iwezekanavyo.
Ni Rais Jakaya Kikwete aliyetanga kuanzisha mchakato wa uandikaji wa katiba mpya. Yeye ni mwenyekiti wa CCM. Sijui kumetokea nini kiasi kwamba serikali inaonyesha kana kwamba inataka kuichongea CCM kwa wananchi.
Ukianglia mambo aliyotokea kuhusiana na mchakato wa Katiba mpya, ni dhahiri kuwa serikali haiitakii mema CCM.
Kwanza, serikali iliamua kuandaa muswada wa mabadiliko ya katiba iliyopo kimya kimya bila kuhusisha wananchi.
Muswada huo, kimsingi, unataka kuleta mabadiliko katika katiba iliyopo ili kuingiza vipengele vinavyohusiana na mchakato wa uandikwaji wa katiba mpya ili kuwezesha kuanza kwa mchakato huu ukiwa na misingi ya kisheria. Hili wa si jambo baya.
Lakini serikali, kana kwamba ina nia mbaya, haikuhusisha wananchi na wadau wengine katika mchakato wa kuandaa muswada huo. Serikali ilitangaza kuwa muswada huo ungewasilishwa kwenye vikao vya Bunge vinavyoendelea hivi sasa mkoani Dodoma.
Wananchi wakakaa mkao wa kusubiri kualikwa kutoa maoni yao kuhusiana na muswada huo. Hawakuipata nafasi hiyo na walikuja kushtuka kuwa muswada huo umeshaandaliwa.
Ni ajabu kuwa serikali iliamua kufanya hivi wakati wananchi walishaonyesha kupitia mijadala mbalimbali kuwa hawatakubaliana na mchakato wa uandikaji wa Katiba mpya ambao hauwashirikishi.
Serikali, kana kwamba haikusikia maoni hayo, ikaamua kuandaa muswada wa kwanza kabisa katika mchakato kuelekea uandikwaji wa katiba mpya bila kuwashirikisha!
Wananchi walipogundua hilo, wakapaza sauti zao wakitaka kupewa nafasi ya kuingiza maoni yao kwenye muswada huo. Bunge likaamua kufanya majadiliano ya kitaifa ili kukusanya maoni ya wananchi kuhusiana na muswada huo.
Majadiliano hayo yalipangwa yafanyike kwa siku mbili, Dar es Salaam na Dodoma. Wazanzibari nao wakaja juu kwa nini wameachwa, kikaongezwa kituo cha tatu, Zanzibar.
Siku ilipofika, wananchi waliojitokeza Dodoma wakazuiwa kuingia kwenye ukumbi. Wale wa Dar es Salaam walipigwa butwaa walipofika ukumbini na kukuta umejaa watoto!
Ni ajabu kuwa zinaweza kutolewa siku mbili tu kwa wananchi kuujadili muswada huo. Ni ajabu zaidi kuwa kunaweza kuwekwa vituo vitatu tu vya kuujadili muswada huo.
Hii ina maana kuwa wananchi wa mikoa mingine zaidi ya 23 ya Tanzania, wamenyimwa haki ya kutoa maoni yao kuhusiana na muswada huo.
Ajabu nyingine ni kuwa baada ya kufahamu kuwa wananchi wengi wanapenda kutoa maoni yao kuhusiana na muswada huo, vikao vya kupokelea maoni ya wananchi vikapangwa kufanywa kwenye kumbi ndogo!
Lakini, cha kushangaza kingine ni kuwa wale walioruhusiwa kuingia, hivi walitarajiwa watoe mchango gani wa maana kwa muswada ambao hata hawaujui?
Matokeo yake pale Dodoma watu walipigwa mabomu ya machozi kwa sababu tu wanadai haki yao ya kutaka kusikilizwa na serikali waliyoiweka madarakani. Sasa kama serikali haitaki kuwasikiliza wale ambao wameiweka madarakani, hivi watu hawa wataendelea kuipenda tena serikali hii?
Na hiki ndicho kitakachokiponza CCM. Wananchi wameshagundua kuwa serikali ndiyo inayowawekea kizingiti kushiriki katika mchakato wa kuandika kwa katiba mpya.
Kama wataipata au hawataipata katiba wanayoitaka au wasioitaka hadi kufikia 2015, ni dhahiri kuwa wananchi wengi watakuwa wameshashtuka kiasi cha kutothubutu kuichagua tena serikali inayohusisha watu ambao wapo hivi sasa.Wataikataa.
Na kwa sababu serikali hiyo inaundwa na CCM, ni dhahiri kuwa chama hicho litaanguka pamoja na serikali yake.
CCM inapaswa kufahamu kuwa matendo yake yanahatarisha ushindi wa chama hicho kwenye uchaguzi ujao. Kisije kusema kuwa sikukionya.
 
Nchi inatikisika sasa kwani kundi linalotaka kung"oka lina mizizi mingi
 
Ni mnyukano wa ndani au mabadiliko ya kweli?
ban.wazo.jpg

Juvenalis Ngowi

amka2.gif
JUMA lililopita katika makala yangu niliangalia upungufu wa Muswada wa marejeo ya Katiba na nikaahidi kuendelea kujadili upungufu wa muswada huo, hata hivyo, kwa sababu kubwa mbili nitasitisha kwa muda kujadili upungufu ule.
Sababu ya kwanza ni ukweli kwamba serikali imeshaanza kuona mapungufu yenyewe na imeanza kuyafanyia kazi ikiwemo kutoa tafsiri ya Kiswahili ya muswada husika. Sababu ya pili nimeona ni vema nijadili tukio linaloitwa kujivua gamba kwa CCM.
Macho ya wengi yalielekezwa huko Dodoma kuangalia nini kinachoendelea. Wakati wa kumbukumbu ya uzao wa CCM, mwenyekiti wa chama hicho alisema kwamba CCM inahitaji kujivua gamba mithili ya nyoka.
Wengi walicheka kimoyomoyo wakijua kwamba hata nyoka akijivua gamba, hubakia nyoka yule yule tena mwenye tabia zile zile. Ukitaka unaweza kusema kwamba ni mvinyo ule ule kwenye bilauri tofauti.
Inaweza kuwa hatua ya kwanza nzuri kwa chama hicho na wananchi. Hata hivyo kwa tunaofuatilia siasa ni lazima kupokea kwa uangalifu kilichotokea maana isije ikawa ni adakadabra za kisiasa tu au ni vita ya kisiasa ya wenyewe kwa wenyewe huku wengine wakishangilia wakidhani saa ya ukombozi imewadia.
Muda ni hakimu wa kweli. Muda ndio utatuthibitishia kama kweli CCM wamekiri wamechoka na kuchoshwa kiasi cha kuamua kujiumiza kwa kujichuna ngozi! Wamejichuna ngozi kweli na wasipokuwa makini maumivu haya yanaweza kuwachosha zaidi.
Ukweli ni kwamba tatizo la watanzania sio sura za watu. Kwamba ubovu wa CCM haukuanza walipoingia wale waliojiuzulu. Ubovu wa CCM ulianza pale walipopiga teke misingi ya kuasisiwa kwake. Pale walipolipa kisogo Azimio la Arusha. Pale walipokubali kubadilika na kuwa chama cha wafanyabiashara badala ya kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi. Hapo ndipo CCM ilipoanza kutembea mithili ya kuku aliyekatwa kichwa. Misingi ya matatizo yote ya leo ni CCM kushindwa kusimamia maadili ya kitaifa. Waliposhindwa hili ndipo pesa ikawa roho na nguvu ndani ya chama. Na pesa ikatafutwa na kutumiwa kwa namna yoyote. Matokeo tumeyaona.
Ili mabadiliko haya yawe na maana ni lazima hatua nyingine ifuate. Kurudi katika maadili na kuliweka taifa katika njia sahihi.
Kinachowafanya watu leo wawe hawana uhakika wa kesho sio sura za kina Yusuf Makamba na wengine waliojiuzulu. Sura za viongozi hazina maana yoyote kwa Mtanzania asiyejua tonge linalofuata la mlo wake litapatikana lini.
Sura za viongozi hazina msaada wowote kama kesho haitakuwa na nafuu kuliko leo. Hicho ndicho wanachopaswa kutuletea ili tutulie, watuletee kesho yenye afadhali.
Kinyume cha hapo vijana wa kileo wanatumia lugha ya mtaani kwamba uongozi usioleta mabadiliko chanya ni sawa na kuuza sura.
Unaweza usikubaliane na mtazamo wangu, lakini wahenga walishasema siku nyingi kwamba mazoea huzaa tabia. CCM hii imekuwa na mazoea ambayo sasa ni tabia. Kama wanajibadilisha ina maana wataturudishia zile nyumba za serikali walizouziana? Watarudisha yale mashirika yaliyobinafsishwa katika hali ya uzembe kama vile tuliamua kutoa sadaka?
Kwenye sadaka ni muhali kuuliza kiwango kinachotolewa, na wengi hutumbukiza humo sarafu za thamani haba. Benki yetu iliuzwa bei gani?
Kusikia sekretarieti imebadilika sio sababu ya kupiga mayowe na vigelegele vya furaha, tunahitaji zaidi. Wanajibadilisha kwa lengo la kutoka wapi kwenda wapi? Isije ikawa haya ni mabadiliko ambayo yamelenga manufaa kwa makundi ndani ya chama na si kuleta mabadiliko ya kweli. Kumbuka watu hawa wamekuwa wakinyukana wao kwa wao kwa muda mrefu. Wako katika maandalizi ya kusaka nafasi za ulaji ndani ya chama mwakani na kiserikali 2015. Kila kitu kiangaliwe kwa tahadhari ya kutosha.
Kuna msemo kwamba huwezi kumfundisha mbwa mzee ujanja mpya. Lakini pia kuna msemo usemao kwamba shetani akizeeka hufanana na malaika. Hawasemi shetani akizeeka anakuwa malaika. La hasha, hufanana na malaika. Yawezekana CCM ni shetani anayetaka kufanana na malaika? Baada ya kuona maandamano Kanda ya Ziwa sasa wana wasiwasi kwamba hawapendwi? Au ni ushindi usiovutia uliopatikana katika uchaguzi uliopita?
Ni kipi hasa kinachowafanya leo sekretarieti ijiuzulu? Lakini kama nilivyoanza aya hii, mbwa mzee hawezi kufunzwa ujanja mpya. CCM ambayo imekuwa kinara wa rushwa katika chaguzi zake za ndani leo hii wanaweza kujifunza ujanja mpya na kutupatia siasa safi? Mazoea haya ya kutumia fedha hayajawa kilema kwao? Hayajajenga desturi kwao? Hivi kweli kuna kipya kinatokea hapa au ni sarakasi tu za kisiasa?
Kama tutaamua kwamba serikali ni taasisi. Na kwamba CCM inajibadilisha baada ya kuona serikali haifanyi inavyotakiwa kufanya, swali linakuja, ni nani aliyetufikisha hapa tulipo? Jibu moja sahihi ni CCM.
Taja ufisadi wa aina yoyote ile kwenye taifa letu, utang'amua kwamba umefanyika katika serikali ya CCM. Wataalamu wa mambo ya utawala wanatuambia kwamba huwezi kutumia wale walioingusha taasisi kuinyanyua taasisi hiyo hiyo. CCM iliyotufikisha hapa haiwezi kututoa hapa! Mwenyekiti wake taifa ni yule yule na serikali iliyopo ni ile ile. Viongozi wa CCM katika ngazi nyingine zote ni wale wale na sera za CCM ni zile zile walizoziibua baada ya mauti ya Azimio la Arusha.
Kama kuna mabadiliko ya kweli yanayotaka kuletwa, hebu hii CCM mpya isababishe serikali ianzishe mchakato huru wa kuandaa katiba mpya. Kuondoa hati ya dharura kwenye muswada husika ni hatua moja lakini hatua ya pili ni kukubali mapungufu yaliyopo katika muswada husika na kututengenezea sheria ambayo kwayo watu watajiundia katiba yao na sio mwenyekiti wa CCM atawatengenezea watu Katiba. Tuwape jaribio hhili la kwanza tuone kama watashinda!
Kama kweli CCM inataka tuamini imejibadilisha, ije hadharani na ripoti ya kila aina ya ufisadi uliofanyika. Ifufue madudu yaliyozikwa kama vile Richmond ili tujue ukweli. Kama madudu ya serikali hayabadilishwi tukabaki na sura mpya tu, tutakuwa hatuna jipya la kufurahia. Itakuwa kama ule mfano unaotolewa kwenye maandiko matakatifu wa kaburi lililopakwa chokaa nje kumbe ndani ni uozo mtupu.
Kuna chochote kwamba huko mbele ya safari kuna mabadiliko yatakayotokana na mabadiliko ya nyuso za sekretarieti ya CCM? Siku wakithubutu kufanya mabadiliko ya kweli, ni wachache watabaki wamesimama ndani ya chama na ndani ya serikali. Magamba ni mengi.
Wote wako pamoja kwa kuwa wana kinachowaunganisha.
Ndiyo maana hata wanaotuambia kwamba wanapinga ufisadi wapo humo humo na hawathubutu kutoka. Kwa nini wanalalamika mtumbwi umetoboka lakini hawabadili mtumbwi?
Ni ngumu kwa chama hiki kubadilika kwa sababu tayari wanaokimiliki sio wale waliokusudiwa. Ni mfanyakazi au mkulima gani leo anathubutu kusema atagombea ubunge kupitia chama hiki? Nani ataweza kuturudisha enzi zile ambapo kura hazikuwahi kuwekwa kwenye mnada?
Ubovu wa CCM hauko kwenye sekretariti tu, uko kwenye mfumo mzima waliojiundia. Kwa maneno mengine, tatizo halikuwa gamba bali damu na roho ya chama hicho. Kama inaweza kubadili damu na roho yake, basi tunaweza kuwa na matumaini kwamba mabadiliko ndani ya chama yatatuletea tija.
Kama wamejivua gamba tu, basi huo ni mnyukano wa wenyewe kwa wenyewe. Sekretarieti ni sehemu ndogo sana ya chama hicho.
Kinachotakiwa kubadilika ni mfumo na mtazamo mzima wa chama. Je, magamba mengine yatavuliwa lini? Nani ambaye si gamba ndani ya CCM?
 
Back
Top Bottom