CCM kujisafisha Juni 2016, mafisadi kutimuliwa

CCM kujisafisha Juni 2016, mafisadi kutimuliwa

Chama cha Mapinduzi kimedhamiria kujisafisha kwa kutimua mafisadi wote chamani kuanzia mwezi Juni mwaka huu. Nyaraka za ndani ya chama zinaonesha kuwa mwezi Juni ni mwezi unaotazamiwa kuwa mwezi wa 'mabadiliko makubwa chamani'. Rais Magufuli anatazamiwa kukabidhiwa Uenyekiti wa CCM mwezi huo wa Juni.

Nyaraka za kimaandalizi zinaonesha kuwa CCM imepania kujisafisha kwa kuwatimua mafisadi wote chamani ili kuendana na dhamira ya Rais na Mwenyekiti mtarajiwa wa CCM, Rais Magufuli, katika vita dhidi ya ufisadi. Nyaraka nzitonzito zinaendelea kuandaliwa na kuwabaini wanaofaa kutimuliwa chamani.

CCM inataka kuwa na sura mpya. CCM inataka kuwa mpya. Nyaraka za kichama zinaonesha kuwa huo utakuwa ni muendelezo wa Operesheni ya Kujivua Gamba, ambayo sasa itaitwa Operesheni ya Kutumbua Majipu,iliyoasisiwa wakati Mukama akiwa Katibu Mkuu wa CCM.

Safishasafisha hiyo ya kichama, kama ikifanyika kweli, itawakumba Wabunge na vigogo mbalimbali chamani ambao kwa miaka nenda rudi wamekuwa wakisemwa kuwa ni mafisadi. CCM isirudi nyuma. Ifanye kweli. Isije ikawa kama vile ambapo 'Gamba liliishia kiunoni'. Ukifika muda wa kutaja na kutoa ushahidi wa ufisadi, nitafutwe!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Ina maana hazta katibu mkuu wa sasa atatimuliwa? kwani huyu naye ni mtuhumiwa wa ufisadi na ujangili kwa muda mrefu.
 
kuwatosa wala rushwa na mafisadi toka nafasi ya uongozi na hata chama inawezekana chini ya uongozi wa magufuli.wala rushwa na mafisadi wanajua pa kwenda. chadema inawapokea na kuwaosha kama wakitoa hela.
Cdm haipo tayari kumpokea magufuli
 
N
Sio kazi yake kufuta. Kila mwenye akili timamu anatambua amefukuzwa au hajafukuzwa. Uliza Lowassa alipojitambua alifanya nini.

Najua mna machngu ila kumbukeni si kila msemalo lazma litimie maana humu duniani hamuishi wenyewe. mmesema wenyewe ngoja tusubiri maana Juni si mbali kivile
 
Nape kila siku analalamika Lowassa fisadi lakini walishindwa kumfukuza, watamuweza joka la makengeza na mama pesa ya mboga?
JK (kama ni yeye) alipiga mahesabu vizuri sana kutomfukuza Lowassa wakati ule! Hivi umeshapata kujiuliza; kaenda CHADEMA July 2015 lakini damage ambayo ameifanyia CCM ilimfanya Magufuri aambulie 58%! Sasa sidhani kama CCM wangeweza kumzuia Lowassa ingekuwa ameingia CHADEMA tangu 2012 au hata 2013/2014. Kwanza hata ule mtafaruku na Dr. Slaa usingetokea... with time, Dr. Slaa angemkubali tu EL!! Na infact, kama EL angefukuzwa mapema na kujiunga CDM; basi yeyote ambae angesimamisha bendera; iwe Slaa au EL; CCM wasingefurukuta hata kama wangeiba kura!
 
kuna kitu kinaitwa TERMINATION na kingine FORCED TERMINATION

TERMINATION ni pale ambapo "wenyewe" wanakufukuza ... (refer mzee Moyo)

FORCED TERMINATION ni pale yanapetengenezwa mazingira "rafiki" ili wewe mwenyewe uachie ngazi.
 
Mimi ngoja nirudie kuisoma avator yangu ,maana nimesahau sijui inasemaje? Na huu uzee sioni vizuri. Yeyote anaeweza aikuze aiweke hapa.
 
Chama cha Mapinduzi kimedhamiria kujisafisha kwa kutimua mafisadi wote chamani kuanzia mwezi Juni mwaka huu. Nyaraka za ndani ya chama zinaonesha kuwa mwezi Juni ni mwezi unaotazamiwa kuwa mwezi wa 'mabadiliko makubwa chamani'. Rais Magufuli anatazamiwa kukabidhiwa Uenyekiti wa CCM mwezi huo wa Juni.

Nyaraka za kimaandalizi zinaonesha kuwa CCM imepania kujisafisha kwa kuwatimua mafisadi wote chamani ili kuendana na dhamira ya Rais na Mwenyekiti mtarajiwa wa CCM, Rais Magufuli, katika vita dhidi ya ufisadi. Nyaraka nzitonzito zinaendelea kuandaliwa na kuwabaini wanaofaa kutimuliwa chamani.

CCM inataka kuwa na sura mpya. CCM inataka kuwa mpya. Nyaraka za kichama zinaonesha kuwa huo utakuwa ni muendelezo wa Operesheni ya Kujivua Gamba, ambayo sasa itaitwa Operesheni ya Kutumbua Majipu,iliyoasisiwa wakati Mukama akiwa Katibu Mkuu wa CCM.

Safishasafisha hiyo ya kichama, kama ikifanyika kweli, itawakumba Wabunge na vigogo mbalimbali chamani ambao kwa miaka nenda rudi wamekuwa wakisemwa kuwa ni mafisadi. CCM isirudi nyuma. Ifanye kweli. Isije ikawa kama vile ambapo 'Gamba liliishia kiunoni'. Ukifika muda wa kutaja na kutoa ushahidi wa ufisadi, nitafutwe!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Huyo magu si ndo aliyempa wizara fisadi? Au ccm ya zimbabwe
 
Mzee Tupatupa nilifikiri Lowasa aliondoka na genge lake la mafisadi kuhamia CHADEMA na kuiacha CCM safi. Rejea pia kauli ya Dr. Slaa kuhusu "choo kuhamia chumbani". Kumbe bado kuna mafisadi CCM! Kila la heri katika kuwang'oa.
 
Hii naona imekaa vizuri lakini itakuwa vizuri zaidi kama wakiwafukuza na kuwakamata mafisadi wote kuanzia Mkapa, Mwinyi, Kikwete, Mzee wa Majungu Makamba. Inabidi wawakamate hawa watu na kuwafunga pamoja na bakora si chini ya 50 kila mmoja.

Naona mkuu umesahau kauli ya mtoto wa mkulima a.k.a mkulima wa nyuki kuwa mafisadi wakiendewa ovyo nchi itatikisika!
 
Kwahiyo tujiandae na kutimuliwa kwa 90% ya wanachama??
 
CCM hi ya Tanzania au CCM nyingine? Yaani wamfukuze nanihii? Hahahaa au eti kabisa wamfukuze yule Jamaa? By the way, nani atamfukuza nani? Labda uniambie waamue kuondoka wote! Tunajua tumeamua kukaa kimya
Huu ndiyo Ukweli harisi bila Ubishi ccm hakuna Msafi wote wamechafuka Kama ni kuanza upya waanze na wengine maana wapo Watanzania kibao wapo tu hawana chama.
 
Hii kazi ni ngumu sana mfano ikaonekana marais wastafu nao ni wachafu je watatimuliwa? Mbona naona kama wataonewa vidagaa tu, tena huyo Magufuli ajiangalie atafika ukingoni na yeye atajikuta anatakiwa kuwa nje ya chama maana majipu atakayoyatumbua yatampaka usaha na kuchafuka
 
H
Nape kila siku analalamika Lowassa fisadi lakini walishindwa kumfukuza, watamuweza joka la makengeza na mama pesa ya mboga?
hata Nape mwenyewe ni bonge la mwizi anapiga pesa nyingi za chama na pesa za kampeni alizitafuna vizuri ccm hakuna msafi.
 
Back
Top Bottom