CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga!

CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga!

Wanabodi,

Nikiwa hapa Dom, nimebahatika kukutana baadhi ya wabunge wapya wa CCM na wa kambi ya upinzani, kujaribu kufahamiana, sio siri, baadhi yao hawana hata substance ya ni nini kilichowafanya washinde, na kwa viti maalum ndio usiseme kabisa!, wengi wao kama si makapi tuu, basi ni vidumu, basi ni kwa ajili ya kutoa huduma na kibinaadamu!, na hili litathibitishwa na michango yao kikao cha Januari.

Nilipoongea na baadhi ya wale makamanda waliokata magogo kanda ya ziwa, nimewaona ni wa kawaida tuu, hivyo nimefikia jibu moja la uhakika, kuwa CCM katika baadhi ya maeneo, imechokwa mpaka basi!, upinzani hata ungesimamisha jiwe, lingechaguliwa!, nadhani ni moja ya sababu kuu iliyopelekea wengi hawakujitokeza waliona kujitokeza kupiga kura ni kujisumbua tuu!.

Nasisitiza CCM imechokwa, na ule ushindi wa kishindo wa toka Asilimia 80% niliyohakikishiwa na mwana CCM mwandamizi mpaka asilimia 60% ni uthibitisho tosha, Watanzania wameichoka CCM ila pia hawakuwachagua wapinzania kwa wingi zaidi, kwa sababu wapinzani hawajaonyesha wako tayari kukamata dola.

Najua kwa dhati, japo JK anafurahia ushindi kwa furaha ya machoni, lazima atakuwa na huzuni moyoni kwa kukataliwa na hiyo asilimia 20% kukataliwa ni kukataliwa tuu, kunauma. Hivyo CCM lazima watakaa na kujiuliza kulikoni, huenda wakajipanga upya na kuja kwa mbinu mpya, ila kwa vile CCM imechokwa, hata ijipange upya vipi, safari ya kwaheri ndio imeanza, there is nothing to stop it from failing down!.

Dawa pekee ya kuitibu CCM, ni kuirevamp CCM completely, task nambari moja ni Makamba should go first with his old guards team. Msisubiri mpaka uchaguzi mkuu wa chama chenu, miaka miwili ijayo (2012), itakuwa too late. If you are to du anything, doi it now and fast!. Leteni fresh blood kina January type, Kippi, Nape type and the like ambao wanaweza siasa za kisasa za dot com type.

Hakuna ubishi, Chadema imenyanyuka, toka wabunge 5 mpaka 22 wa kuchaguliwa tena majimbo ya haja, huku sio kukua bali ni kupaa, tatizo kubwa la Chadema, bado hawajipanga.

Kichama, wanachadema mkubali msikubali, chama chenu japo kipo juu, lakini bado hamjajipanga kwa sura ya kitaifa.
Kwa vile CCM imekaa mkao wa kifo, hii ndio opportunity yenu kujipanga muwe na sura ya kitaifa, Watanzania wawamini wawakabidhi nchi mwaka 2015.

Kwanza Freeman Mbowe, ajiuzulu uenyekiti, ampishe Dr. Slaa kwenye Usukani, Katibu Mkuu mpeni Zitto, hii itaifuta ile dhana ya nepotisim kwenye chama chenu, ili Walioichoka CCM wawafungulie mikono kwa kujitokeza kuwapigia kura 2015.

Kitendo cha kuihodhi kambi ya upinzani Bungeni, huu ni udhaifu mkubwa ambao hautawafikisha mbali. Pamoja na kanuni za bunge kuruhusu Chadema kuunda kambi rasmi ya upinzani, Chadema peke yenu hamuwezi!.

Kama CCM iko ICU na Chadema haijajipanga, spika ndio huyo mama ma over confidence na over reaction, 2015 tutegemee nini?.

Angalizo: Pasco wa Jamii Forums ni political commentator ambaye yuko objective, bila kuegemea chama chochote, upande wowote na hufanya kazi kwa wote, ila ni muumini wa demokrasia ya kweli ndani ya bunge for the balance of power, hivyo nashangilia sana kambi ya upinzani kuingiza vichwa 100 bungeni, ni matumaini yangu, 2015 kazi itakamilishwa!

Angalizo la nini sasa, Chadema imejipanga vizuri sana. You are just not objective as you claim.
 
Hakuna ubishi, Chadema imenyanyuka, toka wabunge 5 mpaka 22 wa kuchaguliwa tena majimbo ya haja, huku sio kukua bali ni kupaa, tatizo kubwa la Chadema, bado hawajipanga.

Kichama, wanachadema mkubali msikubali, chama chenu japo kipo juu, lakini bado hamjajipanga kwa sura ya kitaifa.
Kwa vile CCM imekaa mkao wa kifo, hii ndio opportunity yenu kujipanga muwe na sura ya kitaifa, Watanzania wawamini wawakabidhi nchi mwaka 2015.

Kitendo cha kuihodhi kambi ya upinzani Bungeni, huu ni udhaifu mkubwa ambao hautawafikisha mbali. Pamoja na kanuni za bunge kuruhusu Chadema kuunda kambi rasmi ya upinzani, Chadema peke yenu hamuwezi!.
Hayo maneno kwenye bold, niliyasema 2010, leo ni 2015, tayari Chadema imeishawashirikisha wapinzani ndani ya Kambi rasmi ya upinzani bungeni, na Chadema iko ndani ya UKAWA. Swali sasa linabaki kuwa Jee UKAWA peke yao bila ACT wataweza?!. IKULU ndio ile pale, yule mpangaji anamaliza mkataba wake wa upangaji mwezi October, jee tunamrudisha, au tunampangisha mpangaji mpya!,

Pasco
 

Hayo maneno kwenye bold, niliyasema 2010, leo ni 2015, tayari Chadema imeishawashirikisha wapinzani ndani ya Kambi rasmi ya upinzani bungeni, na Chadema iko ndani ya UKAWA. Swali sasa linabaki kuwa Jee UKAWA peke yao bila ACT wataweza?!. IKULU ndio ile pale, yule mpangaji anamaliza mkataba wake wa upangaji mwezi October, jee tunamrudisha, au tunampangisha mpangaji mpya!,

Pasco

Mbowe aliwapayukia CUF na kuwaita CCM B na kuwaita mashogo lakini mwisho wa siku akaja kuwapigia magoti na kuwashirikisha kambi ya upinzani. Hata hili la ACTasipoomba mbeleko na ACT basi ACT itamuomba aje aungane nao katika jeshi lao kambi ya upinzani, kama sio 2015 itakuwa 2020 au mbele kidogo.
 
Kwa sababu wametuibia sana mpaka tumewachoka.
 
Nimejaribu kufuatilia kwa kina nini hasa watanzania wanahitaji, nimegundua kwamba, wengi walikuwa na tumaini na Ukawa, lakini baada ya kutokea migongano ya kimaslahi ukawani(kila chama kutaka kutoa rais) , wananchi wameachwa njia pande, pia kukosekana kwa siasa za uwazi(transparency) kwenye vyama vikuu vya upinzani(chadema & CUF) kumevunja kabisa matumaini ya wengi
 
Nimejaribu kufuatilia kwa kina nini hasa watanzania wanahitaji, nimegundua kwamba, wengi walikuwa na tumaini na Ukawa, lakini baada ya kutokea migongano ya kimaslahi ukawani(kila chama kutaka kutoa rais) , wananchi wameachwa njia pande, pia kukosekana kwa siasa za uwazi(transparency) kwenye vyama vikuu vya upinzani(chadema & CUF) kumevunja kabisa matumaini ya wengi

So, what's the way forward?
 
Kwa hiyo matumaini yote yamehamia ACT Kwa sababu.
1/Ni chama cha wazalendo.
2/Ni chama cha kijamaa na kufuata Azimio la Arusha.
3/Ni chama kinachoongozwa na Zitto Kabwe(Mfalme)
4/Ni chama kinachotaka kutuwachukie watu wa Kilimanjaro na Arusha kwa kuwa wananyonya rasilimali zetu.
5/Ni chama rafiki na CCM.
 
Kwa hiyo matumaini yote yamehamia ACT Kwa sababu.
1/Ni chama cha wazalendo.
2/Ni chama cha kijamaa na kufuata Azimio la Arusha.
3/Ni chama kinachoongozwa na Zitto Kabwe(Mfalme)
4/Ni chama kinachotaka kutuwachukie watu wa Kilimanjaro na Arusha kwa kuwa wananyonya rasilimali zetu.
5/Ni chama rafiki na CCM.

Mmmmh! Hii kali
 
Nimejaribu kufuatilia kwa kina nini hasa watanzania wanahitaji, nimegundua kwamba, wengi walikuwa na tumaini na Ukawa, lakini baada ya kutokea migongano ya kimaslahi ukawani(kila chama kutaka kutoa rais) , wananchi wameachwa njia pande, pia kukosekana kwa siasa za uwazi(transparency) kwenye vyama vikuu vya upinzani(chadema & CUF) kumevunja kabisa matumaini ya wengi

mivutano ni jambo la kawaida ukiona hakuna mvutano basi ujue kuna dictatorship kwahiyo hiyo isikutishe watapatia maana wana hekima na busara za kutosha kufikia muafaka wa kitaifa kwani wanajua gharama ya kuiacha ccm iendelee kutawala ni kubwa kuliko tofauti zao.
 
Duuuhh kumbe wewe umefuatilia, wenzio huwa wanafanya utafiti. Hii ni karne ya 21 mambo yamekuwa ya "kidigitali zaidi". Fanya utafiti utakuja na hoja zenye mashiko.
 
Duuuhh kumbe wewe umefuatilia, wenzio huwa wanafanya utafiti. Hii ni karne ya 21 mambo yamekuwa ya "kidigitali zaidi". Fanya utafiti utakuja na hoja zenye mashiko.
siyo habari ya utofauti wa Idea zao sisi tunataka chama kingine siyo makapi ccm we are tired
 
Mmmmh! Hii kali
wala hatusikii la mtu kijijini kwetu hatujaisikia ACT tena hatuitaki kwani Zito Haaminiki, Ukiungana naye mbele atakusaliti na kukuuza kwa ccm.si kosa lake ndivyo alivyozaliwa kuwa kigeugeu
 
Nimejaribu kufuatilia kwa kina nini hasa watanzania wanahitaji, nimegundua kwamba, wengi walikuwa na tumaini na Ukawa, lakini baada ya kutokea migongano ya kimaslahi ukawani(kila chama kutaka kutoa rais) , wananchi wameachwa njia pande, pia kukosekana kwa siasa za uwazi(transparency) kwenye vyama vikuu vya upinzani(chadema & CUF) kumevunja kabisa matumaini ya wengi

Huyu ana taka na yule ana taka wakichanganywa pamoja wakashindanishwa kwa vigezo hatima yake ni kupatikana kwa kiongozi bora na hiyo ndiyo demokrasia yenyewe.
 
Nimejaribu kufuatilia kwa kina nini hasa watanzania wanahitaji, nimegundua kwamba, wengi walikuwa na tumaini na Ukawa, lakini baada ya kutokea migongano ya kimaslahi ukawani(kila chama kutaka kutoa rais) , wananchi wameachwa njia pande, pia kukosekana kwa siasa za uwazi(transparency) kwenye vyama vikuu vya upinzani(chadema & CUF) kumevunja kabisa matumaini ya wengi

Nenda act kwani mnajulikana
 
umetumwa ww na umeshindwa na umefeli kufikisha ujumbe
 
Back
Top Bottom