No problem aendelee nao tu, Kikwete hakuwa mjinga kumuondoa Lowassa na baraza lake alipoona litamwangusha.
Lilishamwangusha, Lowassa alikuwa anamtunishia jamaa akiamini yeye ndiye alimweka ikulu. Sasa hawa wamemwangusha nini Mama? Hivi kuna mtu mtiifu kwa mamlaka kama Majaliwa kwa sasa, kumuondoa Majaliwa ni kumuonea na kuleta taharuki kubwa kwenye chama. Pamoja na mapungufu yake mengine mtu mwingine mtiifu sana kwa mamlaka ni Mwigulu, kumtoa huyo utaonekana una matatizo wewe mtumbuaji.

Unawatoaje watu kama Aweso, Simbachawene, Marehemu Kwandikwa, Kabudi, Kitila? Hawana makuu wala makundi yeyote chamani. Miiba ilikuwa ile miwili, Bashiru na Polepole, akawachomoa fasta, hilo hulioni? Ukija kwenye wakuu wa vyombo vya usalama utaanzaje kumtoa Mabeyo, Sirro? Ni watu wenye utiifu uliopitiliza, ila wale vimeo si kawaondoa, especially yule jamaa wa TAKUKURU.
 
Acheni ramli chonganishi, CCM huwa wanajua kushughulikia mambo yao ya ndani kwa weledi mkubwa! Kuna migogoro ilishaibuka huko mikubwa mnoo, ikatulizwa, mojawapo ni ule mgogoro wa 2015 ambao mwishowe waliwatupia takataka lao huko kwenu mkalimeza mazima, likawamaliza nyinyi. Hamna mgogoro CCM kwa sasa.
Hawajui CCM ni taasisi siyo individuals kama ilivyo kwingine
 
1628677493921.jpeg
 
Uongozi wa nchi upo kwenye autopilot

Mama alianza na kujitofautisha na Magufuli akatengeneza split loyalty.

Kadri siku zinavyoenda anarudi kwenye njia ileile ya Magufuli tofauti ni team ya wachezaji tu.

Wapi bandari ya Bagamoyo, wapi LNG plant, wapi mikutano ya hadhara na wapi uhuru wa habari usio na mipaka.

Ndio waelewe hiyo miradi ni interest ya taifa hakuna asieitaka isipokuwa terms ndio zilikuwa shida na hakuna demokrasia isiyokuwa na mipaka.

Hayo ndio mambo aliyokuwa akilenga Magufuli na sio jambo raisi kubadili tabia za watu.

Mama alidhani inawezekana kupendwa na kila mtu; the good thing anaanza kurudi kwenye mstari na kuelewa kwanini miradi ambayo alipoingia alikuja na mikwara itekelezwe sasa hivi atumsikii tena kuiongelea na hiyo demokrasia isiyo na mipaka.

Kukopa maneno ya waingereza ‘it’s only easy if you know it’.
 
alisema au hakusema. hatutaki agombee. she is not a presidential material. aliuokota tu ndomana hana plan wala vision anapuyanga tu.

na hii ikawe fundisho kwa yeyote anaepata kuwa rais ahakikishe anateua the right person for the vp position.
 
alisema au hakusema. hatutaki agombee. she is not a presidential material. aliuokota tu ndomana hana plan wala vision anapuyanga tu.

na hii ikawe fundisho kwa yeyote anaepata kuwa rais ahakikishe anateua the right person for the vp position.
..alikuwa na nia nzuri ya kurudisha haki na utu miongoni mwa Watanzania.

..tatizo amezidiwa nguvu na kundi lililokuwa likifanya udhalimu wakati wa magufuli.

..inawezekana ni kweli hataki kugombea 2025.
 
Back
Top Bottom