Naipendatz
JF-Expert Member
- Jul 27, 2011
- 5,083
- 8,221
Lilishamwangusha, Lowassa alikuwa anamtunishia jamaa akiamini yeye ndiye alimweka ikulu. Sasa hawa wamemwangusha nini Mama? Hivi kuna mtu mtiifu kwa mamlaka kama Majaliwa kwa sasa, kumuondoa Majaliwa ni kumuonea na kuleta taharuki kubwa kwenye chama. Pamoja na mapungufu yake mengine mtu mwingine mtiifu sana kwa mamlaka ni Mwigulu, kumtoa huyo utaonekana una matatizo wewe mtumbuaji.No problem aendelee nao tu, Kikwete hakuwa mjinga kumuondoa Lowassa na baraza lake alipoona litamwangusha.
Unawatoaje watu kama Aweso, Simbachawene, Marehemu Kwandikwa, Kabudi, Kitila? Hawana makuu wala makundi yeyote chamani. Miiba ilikuwa ile miwili, Bashiru na Polepole, akawachomoa fasta, hilo hulioni? Ukija kwenye wakuu wa vyombo vya usalama utaanzaje kumtoa Mabeyo, Sirro? Ni watu wenye utiifu uliopitiliza, ila wale vimeo si kawaondoa, especially yule jamaa wa TAKUKURU.