Casual Conversation: DAE struggle to maintain friendships?

Casual Conversation: DAE struggle to maintain friendships?

Rafiki wengine kama kunguni watakuganda kwa maslai yao na hawatakuachia mpaka wakunyonye damu.

Waswahili wanasema "ni bora uwe na urafiki na mbuzi, unaweza kunywa japo mchuzi".

Siyo kila anayekunja kwenye maisha yako ni lazima kumpokea , maana wengine wapita njia, ni vizuri kuwa makini unapo teua/chagua/pata rafiki,hata yesu alikuwa na marafiki wengi ila ila aliteua first Twelve (12) yake ila bado alitokea Snitch,

By the way mada nzuri P²(Paula Paul)
 
Kwamba huna familia... Huna mchumba... Bado unaishi home..

Yani kifupi bado 'UPOUPO'!??!??
 
Nina Rafiki zangu inaweza pita hata miezi miezi mitatu hatujawasiliana lakini still bado ni marafiki.

Ukikwama anakusaidia bila ugumu wowote na akikwama unamsaidia bila ugumu wowote.

Haya maisha yetu, tena kwa sisi vijana, harakati nyingi sana. Ukijiona unapata muda wa kuzogoa mwingi sana ujue kuna sehemu unakosea.

Baada ya kusema hayo yote, naunga mkono hoja kwa asilimia 100.
 
Dah! Wewe kama mimi tu.. Mpaka sahv kwenye my early 20's najiona kama cna rafiki wa kudumu.. mara nyingi nakua mpweke..nashindwa hata kuingia kwenye mahusiano.. kuzoeana na wa2 its a talent

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe umenipita mimi. Kama hata hauwezi kuingia kwenye mahusiano ni hatari.
Inabidi uwe na mpenzi ambaye ni Extrovert ndio mtaendana.
 
Mkuu, jaribu kumwona psychiatric anaweza kukusaidia polepole juu ya tatizo hilo. Utafika wakati katika maisha ambapo hutaweza ku-make friends easily, kwa hiyo utajisikia lonely na kuona afadhali ungekuwa na marafiki wa muda mrefu.
Asante kwa ushauri. Nitalifanyia kazi
 
Hapo kwenye kuanzisha urafiki kwangu ni tatizo kama mtu asiponisemesha yeye basi ni nakula buyu tu mwanzo mwisho hata nikikaa na mtu seat moja kwenye daladala baada salamu hakuna kinachoendelea
Hata ukikaa na mdada?
 
Rafiki wengine kama kunguni watakuganda kwa maslai yao na hawatakuachia mpaka wakunyonye damu.

Waswahili wanasema "ni bora uwe na urafiki na mbuzi, unaweza kunywa japo mchuzi".

Siyo kila anayekunja kwenye maisha yako ni lazima kumpokea , maana wengine wapita njia, ni vizuri kuwa makini unapo teua/chagua/pata rafiki,hata yesu alikuwa na marafiki wengi ila ila aliteua first Twelve (12) yake ila bado alitokea Snitch,

By the way mada nzuri P²(Paul Paul)
Huo mfano wa snitch kwenye first twelve ya Yesu nimecheka sana.
Asante Cognition kwa ushauri. Asante kwa kuipenda mada.
 
Nina Rafiki zangu inaweza pita hata miezi miezi mitatu hatujawasiliana lakini still bado ni marafiki.

Ukikwama anakusaidia bila ugumu wowote na akikwama unamsaidia bila ugumu wowote.

Haya maisha yetu, tena kwa sisi vijana, harakati nyingi sana. Ukijiona unapata muda wa kuzogoa mwingi sana ujue kuna sehemu unakosea.

Baada ya kusema hayo yote, naunga mkono hoja kwa asilimia 100.
Asante sana Stan.
 
Hiyo itakuwa kawaida tu hata mi nipo hivyo na wala sijishtukii, tena tulio Single simu zetu hata siku nzima unaweza usipokee call wala text yoyote. Tena kwa stress hizi za maisha ndo kabisa marafiki inabidi hata tusameheane tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada ya Kusoma sana Michango ya Wachangiaji nimepata hitimisho..

Haya Mambo ya urafiki tena ule wa Kupigiana simu na Kuchat kila mara kwa dunia yetu ya sasa ni Jambo lisilo la ulazima.

Kuna muda mtu unahitaji kukaa peke yako,Kupangilia mfumo wa Maisha unavyoenda,Majukumu nayo ni mengi sana automatically tunashindwa Ku keep marafiki..

Ni vizuri kuwa na watu ambao tunafahamiana nao ila marafiki wawe wachache na hata hao marafiki ambao kwangu hawajawahi kuzidi wawili..Si lazima kila siku muonane,muongee,mchat...Aisee huo muda wengine hatuna sasa sijui ndiyo Ego lakini wengi tupo hivyo na ndiyo maisha tunayoishi siku zote.

Binafsi kuanzia elimu ya msingi Mpaka elimu ya juu nilifanikiwa kuongeza idadi ya ninaofahamiana nao ila marafiki sikuwapata kabisa na wala sijutii kuhusu hilo.

Ma ofisini ndiyo kabisa tunakutana kwenye majukumu.... Tukitoka kila mtu na la kwake ila mtu akiwa na shida ama Jambo la heri tunajumuika pamoja na huu ndio utaratibu.




Sent using Jamii Forums mobile app
Asante kwa hii summary.
Hata mimi nimeona maoni mengi yame-base hapa.
 
Sasa mimi sio introvert, shy wala anti social.
Napenda kujichanganya na watu, kupiga strory, kutoka out na ni mchangamfu sana mpaka wanatamani kila siku niwepo.

Lakini tatizo langu ni kuuendeleza urafiki niliouanzisha. Kwa mfano tunaweza kula bata leo pamoja, au tukasafiri pamoja tukakaa hata wiki pamoja. Ila tukishaachana napata ugumu wa kuuendeleza huo urafiki.
hyo n kawaidah

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante KANA kwa maoni yako.

"Pia kadri unavyokua smart upstairs, ndio unavyozidi kua na marafiki wachache" kwanini?
I would say "because there aren't that many smart people out there." so your interactions are somewhat limited.

Honestly though....it's not easy being friends with someone you don't have much in common with maana mwisho wa siku unakuwa huna chakuongea nae. Ndo mnaishia na "niambie...niambie" wakati hamna chakuambiana.

I have the same issue and for me this applies to family aswell. It's not that i don't love them or miss them. I might even be thinking about them quite alot but what are we gonna talk about all the time??? The best thing is....my people get me. Kila mtu anafanya mambo yake, siku kukitokea issue ya msingi ya kuongea ama tukikosana sana tunatafutana, tunahang out for a bit then kila mtu anaendelea na mambo yake. If a friendship (any relationship for that matter) is legit...it'll survive a little pause here and there

Kwa upande mwingine...UMRI!! With all the responsibilities that comes with growing up how can we be talking and chatting 24/7??? Like most of us I did my share of that when I was a teen all the way to my early 20s(talking on the phone 'till early mornings, chatting like I worked for MSN back then etc. etc.)....sasa hivi tuwaachie generation Z nao.
 
Hali hii husababishwa na vitu vitatu ambavyo nataka Paula Paul uangalie wewe utakua umedondokea kundi gani kati ya haya matatu nitakayoyachambua kulingana na upeo wangu

1.Makuzi yako utotoni

Wakati ukiwa mdogo ulikuwa na kulelewa katika aina gani ya mazingira,kuna wale wamezaliwa mtoto m1 tu kwenye familia then mama na baba wapo busy na mishe zao hivyo kupelekea huyu mtoto kukua ktk hali ya upeke ake peke ake na mwisho anazoea hii hali,na matokeo yake akikua Hawezi dumu na marafiki kamwe.

au mwingine kazaliwa kisha wazazi wake baba na mama wakaachana hivyo mzazi m1 kaamua kumchukua mtoto na kuondoka nae au kumpeleka kwa ndugu,huyu mtoto kwakua tyr kashaelewa haya sio mazingira yangu,lazima atajitenga tenga na mwisho ataanza kuwa pekeake na baadae atazoea maisha hayo,ila effect zinakuja onekana ukubwani,hatoweza dumu na marfiki,mifano ya kundi hili ipo mingi.

2.Waliotendwa/kuumizwa (na marafiki)

Hawa ni wale sio kwamba hawawezi kuwa na marafiki au kudumu nao,hawa ni wale kwanza wanapenda marafiki sana sana ila shida yao ni moja "yalishawakuta" walifanyiwa umafia,au jambo baya lolote kiasi kwamba sasa hivi muda wa kufatana fatana au kuwa intouch saaaana na mtu hawawezi,hujikuta wakikumbuka nyuma na mwisho hujisemea "sihitaji yanikute tena" matokeo yake hushindwa kudumu na marafiki.

ila kutokudumu kwao na marafiki haimaanishi wamewachukia hao wengine hapana,Upendo upo ila wanaishi maisha ya wasi wasi ya kutoamini tena mtu mwngine na effect zake ndio hizo kwenye thread yako Paula Paul (kundi hili ndio lina watu wengi hata kwnye hi thread wengi wanatoka kundi hili.

3.Nature

Hawa ni wale waliozaliwa hivi,ki ufupi ni aina ya watu hat kama wamezaliwa kwenye familia yenye watoto 7,ila yeye ni mt wa kujitenga tenga mkimya mkimya mfata mambo yake,ndugu zake wakicheza game wakibadilishana Pad yeye Hana time na game muda huo,atasubiri wamalize kucheza wakiondoka wote yeye ataenda atashika Pad atacheza mwenyewe au atachagua mtu anaemtaka yeye acheze nae,akimaliza hapo HUYOOO anaondoka zake.

huyu yeye siku zote n mpole mpole,mkimya mkimya,sio kwamba anachuki na wengine Hapana huyu ndio alivyoumbwa,mfano wa huyu mtu ni kama jamaa anaitwa PROFESSOR kwenye season inaitwa MONEY HEIST huyu kiumbe ni mtu wa peke ake pake ake,lipo kama jinga jinga flani,ila Ana upendo wa hali ya Juu kwa wenzake sema ndio huwezi mgundua.(ana akili huyo acha kabisa)

watu wa aina hiii wakiwa watu wazima ndio effect zao huonekana kwasababu hatoweza dumu na rafiki na haoni shida kukaa bila rafik kwasababu ndivyo alivyoumbwa.

Tukirudi kwenye swali lako la Je Ni tatizo au si tatizo?

Jibu nadhani linategemea wewe upo kundi gani hapo juu.
 
Inaonekana wewe ni mtu wa maombi sana Suriya. Inapendeza sana. Huo urafiki unaitwa "wapendwa".
Asante sana.
Napenda kujifunza neno,
😔😣 Lakini kwenye maombi nimekua nyuma sana, nipo nalifanyia kazi jambo hilo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom