Casual Conversation: DAE struggle to maintain friendships?

Casual Conversation: DAE struggle to maintain friendships?

Nafikiri ni aina fulani ya ubinafsi, kwa kizungu inaweza kuwa na maana nyepesi zaidi tofauti na kiswahili.

Kwa sababu, kuna yule mtu au rafiki unampenda, huyu unaweza hata kuongea naye masaa 2 ujinga ujinga na usione kama unapoteza muda.

Ila wengine hata kujibu SMS tu ukaona kazi.
Exactly, upo sahihi kabisa Don.
 
Ukiwa smart, unafahamu limits zako. Utafahamu umuhimu wa uhuru kwako na kwa hao marafiki. We all need space and only smart people know this. Pia urafiki mwingi unabebwa na drama zisizo za lazima. Ukiwa smart, you can simply tell shit ain't real. Urafiki wa kugandana unapaswa kuishia sekondary sweetheart!

Asante KANA.
Kweli mambo ya kugandana ni secondary. We've got so much to do kadri umri unavyoenda.
Barikiwa sana.
 
Hahaa. Mtu anayeweza kukaa na wa kishua, halafu akakaa uswazi.Akakaa na mabaharia, halafu akakaa na walokole. Akakaa na wabongo, halafu akakaa na wanyamwezi.

Akawa mpenzi wa kujiendeleza kielimu, akajua changamoto za maisha na namna mbalimbali za kuzikabili...

Nafikiri anaweza kusema amepata maksi za kiasi fulani katika kile Wafaransa wanachokiita "savoir faire", uwezo wa kuwa na maadili na ujuzi wa kufanya kitu sahihi, kwa muda sahihi, pahali sahihi.

Sasa hapo ndipo unapokuta mtu kaleta mchango JF kitu ambacho watu washapitia, kinajulikana, mara nyingine hata kumueleza kwamba hilo jambo watu wengi wanalo na ni kawaida inakuwa faraja kubwa. Kwa sababu pengine mtu anaweza kujiona yeye ni wa ajabu, wakati hata nusu ya robo ya ajabu hajafikia.

Kiranga
Umenifurahisha na comment zako na imenikumbusha msemo ukitaka kupata marafiki wa kweli ishi maisha kama ya kinyonga zaidi ni kijifunza kuangalia mazuri ya mwenzako ikiwezekana mpongeze kwa jambo zuli alilanalo na kuwa mwepesi wa kuomba msamaha pale unapokwaza wenzako . Kumbuka Mungu ndiye aliyeumba watu wote mshua, wa uswazi, msomi , baharia , lofa , mdini , mdhambi . Mimi nimejifunza kumfurahia mtu kama alivyo , kila binadamu ana jisikia faraja kuona anathaminiwa .
Urafiki hujengwa au uja wenyewe au waweza amua maisha yako hutaki rafiki labda kwa kujiona unajitosheleza kwa kila kitu , wazungu wa western countries wengi wao kutokana na utoshelevu kimaisha wananiona kinachobaki ni kazi na kutaradadi dunia kukutana na watu wapya maisha mapya maisha yao ya kitajiri , afrika matajiri hasa ni wachache na utamaduni wa afrika kama ndoa na harusi, misiba , maisha kwa ujumla umekaa kirafiki/ kijamaa zaidi.

Mbinu unazoweza kutumia kujenga urafiki imara;

1.Penda na jali watu , misemo kama impressing people endup poor ipotezee
2.Endeleza na furahia career, vipawa, karama zako on the way ukikutana na mtu anatabia kama zako au unavutiwa na maendeleo yake mfurahie usimuonee wivu mtajikuta automatically mnakuwa marafiki .
3.watu unaojisikia furaha kuwa nao waonyeshe hivyo hata kama hamuonani ama kuwasiliana mara kwa mara.
4.Jenga mazoea ya kujichunguza weakness zako mara kwa mara ambazo zinaweza kuudhi watu mfano kama unajiona ni mbinafsi, hasira, chuki, roho mbaya, ugomvi nk tafuta namna ya kuachana na rabia hizo ama kwa kusali na kuombewa au tafuta psychologist au unayemwamini akusaidie ubadilike.
4.Jijengee tabia ya kuwa mtu wa kutoa msaada , kufariji kimawazo, pesa, ujuzi , muda nk usiangalie sana maslai utalipwaje as urafiki sio ajira au fursa kwani changamoto za urafiki ni tofauti na changamoto za ajira / fursa tanguliza sana utu.
5.Jali na wafurahie wenzio zaidi unavyojipenda wewe .

Wale wanaosema wanaona shida kuimarisha urafiki wajaribu mbinu hizi ni uzoefu niliouona kwangu ambao nimeuchunguza kutokana marafiki wengi niilio nao ambao wengi nimedumu nao zaidi ya miaka 30.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nafkiri si mbaya kuwa na marafiki ama kutokuwa nao kabisa inategemea na wewe ni mtu wa namna gani

Lakini kitu nilichogundua pia as we grow old majukumu yanaongezeka na baadhi ya mambo ya kale yanapungua so it might be relation or other stuffs .. Khy mtu unakuwa consisted his daily schedules

Binafsi nafkiri nafahamiana na watu wengi ila sina rafiki and its okay kwa upande wangu ..vitu vyangu najishirikisha mwenyewena Mungu wangu ,vingine vingine bi mkubwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Barikiwa sana Chalii wa ara.
 
Kiranga
Umenifurahisha na comment zako na imenikumbusha msemo ukitaka kupata marafiki wa kweli ishi maisha kama ya kinyonga zaidi ni kijifunza kuangalia mazuri ya mwenzako ikiwezekana mpongeze kwa jambo zuli alilanalo na kuwa mwepesi wa kuomba msamaha pale unapokwaza wenzako . Kumbuka Mungu ndiye aliyeumba watu wote mshua, wa uswazi, msomi , baharia , lofa , mdini , mdhambi . Mimi nimejifunza kumfurahia mtu kama alivyo , kila binadamu ana jisikia faraja kuona anathaminiwa .
Urafiki hujengwa au uja wenyewe au waweza amua maisha yako hutaki rafiki labda kwa kujiona unajitosheleza kwa kila kitu , wazungu wa western countries wengi wao kutokana na utoshelevu kimaisha wananiona kinachobaki ni kazi na kutaradadi dunia kukutana na watu wapya maisha mapya maisha yao ya kitajiri , afrika matajiri hasa ni wachache na utamaduni wa afrika kama ndoa na harusi, misiba , maisha kwa ujumla umekaa kirafiki/ kijamaa zaidi.

Mbinu unazoweza kutumia kujenga urafiki imara;

1.Penda na jali watu , misemo kama impressing people endup poor ipotezee
2.Endeleza na furahia career, vipawa, karama zako on the way ukikutana na mtu anatabia kama zako au unavutiwa na maendeleo yake mfurahie usimuonee wivu mtajikuta automatically mnakuwa marafiki .
3.watu unaojisikia furaha kuwa nao waonyeshe hivyo hata kama hamuonani ama kuwasiliana mara kwa mara.
4.Jenga mazoea ya kujichunguza weakness zako mara kwa mara ambazo zinaweza kuudhi watu mfano kama unajiona ni mbinafsi, hasira, chuki, roho mbaya, ugomvi nk tafuta namna ya kuachana na rabia hizo ama kwa kusali na kuombewa au tafuta psychologist au unayemwamini akusaidie ubadilike.
4.Jijengee tabia ya kuwa mtu wa kutoa msaada , kufariji kimawazo, pesa, ujuzi , muda nk usiangalie sana maslai utalipwaje as urafiki sio ajira au fursa kwani changamoto za urafiki ni tofauti na changamoto za ajira / fursa tanguliza sana utu.
5.Jali na wafurahie wenzio zaidi unavyojipenda wewe .

Wale wanaosema wanaona shida kuimarisha urafiki wajaribu mbinu hizi ni uzoefu niliouona kwangu ambao nimeuchunguza kutokana marafiki wengi niilio nao ambao wengi nimedumu nao zaidi ya miaka 30.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Nakushukuru mkuu, hizo principles watu wanaozifuata ni wachache sana siku hizi.

Umenikumbusha Mzee wangu, yeye ni mtu wa kusaidia watu sana, ile mpaka watu wakawa wanaona atalosti, lakini kauli yake kila siku ilikuwa "sijawahi kuwa masikini kwa kusaidia watu, na sitakuwa masikini kwa kusaidia watu".

Halafu alifanya hivyo kwa busara sana.Yani mara nyingine hata kama si yeye atakayekusaidia, anaweza kutoa neno lake tu, kwa vile watu wanamheshimu, hata kama yeye hana uwezo wa kukusaidia, akitoa neno lake utasaidiwa na watu wengine, kwa maana watu wanamuheshimu sana kwa maisha yake ya mfano.

Watu wa namna hiyo kwa ulimwengu wa sasa si wengi sana.

Na tuliolelewa na watu wa namna hiyo siku zote tunajisikia deni katika kuishi hivyo.

Na kuna watu ana urafiki nao mpaka leo, anakwambia "huyu rafiki yangu kwa miaka 50".

Unaona dah, miaka 50 umri huo mimi sijafika, ina maana hawa wana urafiki tangu mimi sijazaliwa, na bado ni marafiki wakubwa!
 
Nimekuelewa barabaaara.
Tusubiri hapa tupate tiba kutoka kwa wachangiaji.
Usiache kupitia comments kusoma.
Baada ya Kusoma sana Michango ya Wachangiaji nimepata hitimisho..

Haya Mambo ya urafiki tena ule wa Kupigiana simu na Kuchat kila mara kwa dunia yetu ya sasa ni Jambo lisilo la ulazima.

Kuna muda mtu unahitaji kukaa peke yako,Kupangilia mfumo wa Maisha unavyoenda,Majukumu nayo ni mengi sana automatically tunashindwa Ku keep marafiki..

Ni vizuri kuwa na watu ambao tunafahamiana nao ila marafiki wawe wachache na hata hao marafiki ambao kwangu hawajawahi kuzidi wawili..Si lazima kila siku muonane,muongee,mchat...Aisee huo muda wengine hatuna sasa sijui ndiyo Ego lakini wengi tupo hivyo na ndiyo maisha tunayoishi siku zote.

Binafsi kuanzia elimu ya msingi Mpaka elimu ya juu nilifanikiwa kuongeza idadi ya ninaofahamiana nao ila marafiki sikuwapata kabisa na wala sijutii kuhusu hilo.

Ma ofisini ndiyo kabisa tunakutana kwenye majukumu.... Tukitoka kila mtu na la kwake ila mtu akiwa na shida ama Jambo la heri tunajumuika pamoja na huu ndio utaratibu.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ego is still an issue around here..kwa mfano mtu anakutumia message humjibu hii ina maana gan?, ukute huyo mtu hamjawasiliana for days..Selfishness na Ubaguzi pia na kujiona bora kuliko wengine ama una deserve better than others thats why inafikia hatua unashindwa kuji intergrate katika jamii ya watu.Kuna wengine hatafuti watu mpaka atafutwe yeye na hata ukimtafuta anakuwa hatoi ushirikiano hana ubize wala nn na wengine hazikuwa tabia zao ila unakuta ana change ghafla anapoingia katika mazingira mengine km Chuo, Kazini nk.Bila kujua masikini anajikuta hana marafiki mwishowe tunapata nyuzi kama hizi issue sio kwa namna gan una keep friends wala nn jiangalie ww mwenyew tabia zako, and trust me hakuna kitu bora zaidi kama kuwa na loyal friend huyu anaweza kukusaidia kuliko hata hao wanafamilia wako unaowategemea.
Trust me hamna mambo ya Ego wala ubaguzi au kujiona bora kuliko mwingine.
Wala sina kitu chochote cha kunifanya nijione bora kuliko mwingine.

Ndio huwa inatokea, hata nikijibu meseji unakuta sina mambo ya kuandika zaidi ya okay, good nk. Nakosa zile strory za kuendeleza urafiki. Ila kama kuna issue ya kutoka out , kusaidia kwenye tatizo, na mambo mengine nashiriki vizuri sana. Tatizo lipo kwenye kuchat chat na kupigiana simu mara kwa mara siwezi.
 
Wife tuu anatosha Eli?
Kweli utakosa yule "mshikaji " ambaye hata wife akisumbua unaomba ushauri?
Nadhani anatosha, kazii naamini siku nikiacha pale hakuna muendelezo wowote, sioni. Majirani hawa ni obligation kuwa nao, ila tunaonana mara chache sana, kanisani siendi, classmates ni washkaji tu nothing special.
 
Kwanini hao unaotamani wawe rafiki zako hawana nia? Au mnaishi maisha tofauti?.
Unaweza ukawaomba urafiki kama unatamani kuwa rafiki yao. Haujaliwaza hili?
Tuko tofauti unakuta mtu ana maisha mengine kabisa na mimi ni maisha flani nayakubali, au ana characters nazikubali hivo nataka awe karibu zaidi lakini huwa siombi urafiki. Urafiki naamini unatakiwa utokee tu, na mara nyingine unaweza kuwa na rafiki ambaye hamuendani kabisa lakini mnapendana na kuelewana.
 
Asante
Nafikiri ni aina fulani ya ubinafsi, kwa kizungu inaweza kuwa na maana nyepesi zaidi tofauti na kiswahili.

Kwa sababu, kuna yule mtu au rafiki unampenda, huyu unaweza hata kuongea naye masaa 2 ujinga ujinga na usione kama unapoteza muda.

Ila wengine hata kujibu SMS tu ukaona kazi.

Karma
 
Mkuu, jaribu kumwona psychiatric anaweza kukusaidia polepole juu ya tatizo hilo. Utafika wakati katika maisha ambapo hutaweza ku-make friends easily, kwa hiyo utajisikia lonely na kuona afadhali ungekuwa na marafiki wa muda mrefu.
 
Hapo kwenye kuanzisha urafiki kwangu ni tatizo kama mtu asiponisemesha yeye basi ni nakula buyu tu mwanzo mwisho hata nikikaa na mtu seat moja kwenye daladala baada salamu hakuna kinachoendelea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom