Wengi tunashindwa kutofautisha kufahamiana na urafiki. Ndio maana mtu anakwambia naomba tuwe marafiki.
Kwangu inakua ngumu sana kwa sababu urafiki ni kitu kinatokea kutokana na vitu au mambo yanayoweza kuwaleta pamoja.
Kiranga ameweka vizuri sana, kuwa rafiki yako mzuri wewe mwenyewe kwanza. Hapo haitakusumbua kwamba una rafiki mwingine au hauna kwa sababu tayari unae rafiki wa kudumu ambae ni wewe binafsi.
Unaweza ukawa na rafiki sio lazima uwasiliane nae au uchati nae kila wakati kumaanisha urafiki wenu upo kwenye kiwango bora, lakini ni pale ambapo ibapobidi au panapokua na uhitaji.
Ikumbukwe pia kuwa rafiki kuna gharama zake, inahitaji trust, muda na kujali. Hii sio kila mtu anaweza, ndio maana sio kila mtu anaweza kuwa na rafiki.
Kwa upande wangu naweza kuelewana na mtu kwa urahisi na haraka sana lakini haimaanishi turakua marafiki, inachukua muda sana na hii ni kwa vile nikishakua rafiki na mtu, mara nyingi inadumu sana. Nna rafiki nimesoma nae O level, tukaenda A level na hadi leo tuko marafiki na imekua kama ndugu lakini hatuwasiliani au kuonana mara kwa mara.
Rafiki mwingine niliyempenda ni kwa kuwa sio mnafiki. Ananiambia ukweli inapobidi kitu ambacho wengi wetu ni wanafiki, atakupamba au kukwambia vitu unavyopenda kusikia.
Mwisho wa siku usijilazimishe sana kufanya mambo ili kupata au kudumisha urafiki, acha vile ulivyo ndio iwe sababu ya mtu kukufaham na ijenge msingi wa urafiki wenu.
Bottom line, "Be your own best friend" (
Kiranga, 2020) .