nyakubonga
JF-Expert Member
- Apr 5, 2015
- 4,598
- 7,172
Hii nchi ina wasomi wengi sana, wataendesha hao.Hiyo mijadala iendeshwe na nani sasa ?
Hii nchi ina wasomi wengi sana, wataendesha hao.Hiyo mijadala iendeshwe na nani sasa ?
Katiba ina sura mbili ya kisheria na kisiasa.Hii nchi ina wasomi wengi sana, wataendesha hao.
Mchango mzuri asante sana kiongozi kwa maono mazuri juu ya maendeleo ya taifa letu kwa ujumla.Hoja: la muhimu zaidi ni heshima kwa sheria, na kwa vile Katiba ni sheria mama, basi heshima husika iwe kwenye sheria zilizomo kwenye katiba.
Hali ilivyo sasa: ni kweli katiba iliyopo ina mapungufu mengi. Na ni kweli kuwa mapungufu hayo yanaathiri maeneo mbalimbali hususan haki za kisiasa/kidemokrasia.
Katiba yote ya sasa ina mapungufu?: Hapana. Kuna sheria nyingi tu katika katiba ya sasa ambazo ni mwafaka. Tatizo ni kwamba heshima kwa sheria ni changamoto kubwa kwa Watanzania. Kwahiyo hata sheria hizo "nzuri" zaishia kuonekana "mbaya" kwa sababu zinapuuzwa
Case study: kwa mujibu wa maelezo ya Chadema, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilifoji majina wa wabunge 19 wa viti maalum wa chama hicho. Kufoji ni kosa la jinai. Hadi muda huu Chadema hawajafungua mashtaka dhidi ya tume ya Taifa ya Uchaguzi kutokana na forgery hiyo.
Tatizo lipo wapi? Ukisikiliza mjadala kuhusu Katiba mpya, focus ipo kwa watawala. Nguvu kubwa za Rais, Tume ya uchaguzi kutokuwa huru, nk. Lakini pengine kwa makusudi au kutojua, hakuna mjadala kuhusu "mapungufu ya watawaliwa." Mfano hai hapa ni huo wa NEC kuvunja sheria lakini wahanga wa uvunjifu huo wa sheria, Chadema hajachukua hatua za kisheria. Sasa hapo tatizo si katiba bali ni kupuuza sheria inayoweza kutoa haki stahili.
Logic ya wakati huo kwa Chadema: zama za Mwendazake, ingekuwa sawa na kupoteza muda kwa Chadema kwenda mahakamani kudai haki yao.
Logic ya sasa: huhitaji kuwa na upeo mkubwa wa kinachoendelea Tanzania kubaini kuwa zama zimebadilika haswa. Japo utaambiwa "kutenguliwa hukumu ya Mbowe na Mdude kuachiwa huru ni suala la kimahakama," ukweli wa wazi ni kuwa haya yasingewezekana katika zama za Mwendazake.
Kwa maana hiyo: kwa vile mazingira yaliyopo ni rafiki kudai haki, angalau kwa kigezo cha kesi hizo mbili, kwanini Chadema wasiiburuze mahakamani Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kosa la kufoji majina 19 ya wabunge wa viti maalum?
Katiba mpya inaingiaje hapa?: Naam kuna haja ya marekebisho ya sheria mbalimbali kandamizi. Endapo mabadiliko hayo ni lazima yafanyike kwa njia ya Katiba mpya, ni sawa. Endapo badala ya katiba mpya tunaweza kufanya marekebisho tu ya katiba, ni sawa pia. However, iwe ni marekebisho ya katiba au ujio wa katiba mpya, kasumba ya kupuuza sheria itafanya marekebisho ya katiba/katiba mpya kuwa tatizo kama ilivyo sasa.
Kama alivyosema Askofu Bagonza kuwa wanaovunja Katiba hii wanaweza pia kuvunja katiba mpya, nami nahitimisha kuwa wanaopuuzia kudai haki zao kipindi hiki cha "katiba yenye mapungufu" wanaweza pia kupuuzia kudai haki zao katika zama za "Katiba mpya."
Na mwisho kabisa, kama hatuwezi kuheshimiana sie wenyewe katika mjadala huu muhimu kwa mustakabali wa taifa letu, hiyo katiba mpya itaheshimiwa vipi maana asiye na heshima kwa mtu ana nafasi kubwa ya kutokuwa na heshima kwa kitu/vitu (eg Katiba).
Mfano hai wa "kukoseana heshima" ni pale nguli wa sheria Prof Issa Shivji alipotoa angalizo kuhusu katiba mpya na kutanabaisha kuwa sio mwarobaini wa kutatua changamoto mbalimbali, baadhi ya "wasiopenda mawazo tofauti na yao" wamedai profesa huyo anazeeka vibaya. Wengine wameenda mbali na kumtusi kuwa "nafasi za u-DC zimejaa."
I stand to be corrected 🙏
Katiba kutoka kwa mwanasiasa ni ile inayompa favour yeye kwanzaKatiba ina sura mbili ya kisheria na kisiasa.
Huwezi kuitenganisha katiba na siasa kutengeneza katiba siyo Caesarean Section procedure kwamba unahitaji technocrats.
Wanasiasa ndiyo chimbuko la mabadiliko mengi ya mifumo ya kiutawala siyo hao wasomi wako au unataka kusema wanasiasa siyo wasomi ?
Sheria inasema maamuzi ya tume yanaweza kupingwa mahakamani? Au umesahau kuwa matokeo ya uchaguzi hayawezi kupingwa mahakamani?Hoja: la muhimu zaidi ni heshima kwa sheria, na kwa vile Katiba ni sheria mama, basi heshima husika iwe kwenye sheria zilizomo kwenye katiba.
Hali ilivyo sasa: ni kweli katiba iliyopo ina mapungufu mengi. Na ni kweli kuwa mapungufu hayo yanaathiri maeneo mbalimbali hususan haki za kisiasa/kidemokrasia.
Katiba yote ya sasa ina mapungufu?: Hapana. Kuna sheria nyingi tu katika katiba ya sasa ambazo ni mwafaka. Tatizo ni kwamba heshima kwa sheria ni changamoto kubwa kwa Watanzania. Kwahiyo hata sheria hizo "nzuri" zaishia kuonekana "mbaya" kwa sababu zinapuuzwa
Case study: kwa mujibu wa maelezo ya Chadema, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilifoji majina wa wabunge 19 wa viti maalum wa chama hicho. Kufoji ni kosa la jinai. Hadi muda huu Chadema hawajafungua mashtaka dhidi ya tume ya Taifa ya Uchaguzi kutokana na forgery hiyo.
Tatizo lipo wapi? Ukisikiliza mjadala kuhusu Katiba mpya, focus ipo kwa watawala. Nguvu kubwa za Rais, Tume ya uchaguzi kutokuwa huru, nk. Lakini pengine kwa makusudi au kutojua, hakuna mjadala kuhusu "mapungufu ya watawaliwa." Mfano hai hapa ni huo wa NEC kuvunja sheria lakini wahanga wa uvunjifu huo wa sheria, Chadema hajachukua hatua za kisheria. Sasa hapo tatizo si katiba bali ni kupuuza sheria inayoweza kutoa haki stahili.
Logic ya wakati huo kwa Chadema: zama za Mwendazake, ingekuwa sawa na kupoteza muda kwa Chadema kwenda mahakamani kudai haki yao.
Logic ya sasa: huhitaji kuwa na upeo mkubwa wa kinachoendelea Tanzania kubaini kuwa zama zimebadilika haswa. Japo utaambiwa "kutenguliwa hukumu ya Mbowe na Mdude kuachiwa huru ni suala la kimahakama," ukweli wa wazi ni kuwa haya yasingewezekana katika zama za Mwendazake.
Kwa maana hiyo: kwa vile mazingira yaliyopo ni rafiki kudai haki, angalau kwa kigezo cha kesi hizo mbili, kwanini Chadema wasiiburuze mahakamani Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kosa la kufoji majina 19 ya wabunge wa viti maalum?
Katiba mpya inaingiaje hapa?: Naam kuna haja ya marekebisho ya sheria mbalimbali kandamizi. Endapo mabadiliko hayo ni lazima yafanyike kwa njia ya Katiba mpya, ni sawa. Endapo badala ya katiba mpya tunaweza kufanya marekebisho tu ya katiba, ni sawa pia. However, iwe ni marekebisho ya katiba au ujio wa katiba mpya, kasumba ya kupuuza sheria itafanya marekebisho ya katiba/katiba mpya kuwa tatizo kama ilivyo sasa.
Kama alivyosema Askofu Bagonza kuwa wanaovunja Katiba hii wanaweza pia kuvunja katiba mpya, nami nahitimisha kuwa wanaopuuzia kudai haki zao kipindi hiki cha "katiba yenye mapungufu" wanaweza pia kupuuzia kudai haki zao katika zama za "Katiba mpya."
Na mwisho kabisa, kama hatuwezi kuheshimiana sie wenyewe katika mjadala huu muhimu kwa mustakabali wa taifa letu, hiyo katiba mpya itaheshimiwa vipi maana asiye na heshima kwa mtu ana nafasi kubwa ya kutokuwa na heshima kwa kitu/vitu (eg Katiba).
Mfano hai wa "kukoseana heshima" ni pale nguli wa sheria Prof Issa Shivji alipotoa angalizo kuhusu katiba mpya na kutanabaisha kuwa sio mwarobaini wa kutatua changamoto mbalimbali, baadhi ya "wasiopenda mawazo tofauti na yao" wamedai profesa huyo anazeeka vibaya. Wengine wameenda mbali na kumtusi kuwa "nafasi za u-DC zimejaa."
I stand to be corrected 🙏
Hata mahakama zitakuwa huru zitaanza kutenga hakiMojawapo ya umuhimu mkubwa wa Katiba mpya ni kwamba kutakuwa hakuna tena uporaji wa chaguzi. Chaguzi ziitakuwa za HAKI na HURU si za kupora kutumia Tume FAKE na mtutu wa bunduki kwani kupitia Katiba mpya tutakuwa na Tume huru ya uchaguzi na kama taratibu za uchaguzi zikiukwa na chama kilichoshinda basi matokeo yanaweza kabisa kufutwa na kuitishwa uchaguzi mpya kama ilivyotokea Kenya 2017.
KENYA: Mahakama yatengua matokeo ya Uchaguzi wa Rais. Kurudiwa upya ndani ya siku Sitini(60)
Mahakama imempa ushindi mwombaji yaani Odinga hivyo uchaguzi umeonekana ulikuwa na kasoro na utarudiwa ndani ya siku sitini. Nchi za Afrika zijifunze hasa Tanzania Hivi punde,Mahakama ya Juu ya Kenya imeridhika na hoja za Umoja wa Vyama vya Upinzani (NASA) kuwa uchaguzi haukufuata Katiba na...www.jamiiforums.com
Mahakamani kwenye unamkuta Mganga ndiyo Jaji unategemea nini?Sheria inasema maamuzi ya tume yanaweza kupingwa mahakamani? Au umesahau kuwa matokeo ya uchaguzi hayawezi kupingwa mahakamani?
Nakushangaa chadema ni chama cha siasa nimetoa kauli hawahusiki na hiyo barua ya wabunge 19,na imetoa hukumu kama chama kuwafukuza walio forge,kaa kwenye kiti jiuulize vizuri nani mwingine inatakiwa kuchukua hatua dhidi ya fojali hiyo.Hoja: la muhimu zaidi ni heshima kwa sheria, na kwa vile Katiba ni sheria mama, basi heshima husika iwe kwenye sheria zilizomo kwenye katiba.
Hali ilivyo sasa: ni kweli katiba iliyopo ina mapungufu mengi. Na ni kweli kuwa mapungufu hayo yanaathiri maeneo mbalimbali hususan haki za kisiasa/kidemokrasia.
Katiba yote ya sasa ina mapungufu?: Hapana. Kuna sheria nyingi tu katika katiba ya sasa ambazo ni mwafaka. Tatizo ni kwamba heshima kwa sheria ni changamoto kubwa kwa Watanzania. Kwahiyo hata sheria hizo "nzuri" zaishia kuonekana "mbaya" kwa sababu zinapuuzwa
Case study: kwa mujibu wa maelezo ya Chadema, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilifoji majina wa wabunge 19 wa viti maalum wa chama hicho. Kufoji ni kosa la jinai. Hadi muda huu Chadema hawajafungua mashtaka dhidi ya tume ya Taifa ya Uchaguzi kutokana na forgery hiyo.
Tatizo lipo wapi? Ukisikiliza mjadala kuhusu Katiba mpya, focus ipo kwa watawala. Nguvu kubwa za Rais, Tume ya uchaguzi kutokuwa huru, nk. Lakini pengine kwa makusudi au kutojua, hakuna mjadala kuhusu "mapungufu ya watawaliwa." Mfano hai hapa ni huo wa NEC kuvunja sheria lakini wahanga wa uvunjifu huo wa sheria, Chadema hajachukua hatua za kisheria. Sasa hapo tatizo si katiba bali ni kupuuza sheria inayoweza kutoa haki stahili.
Logic ya wakati huo kwa Chadema: zama za Mwendazake, ingekuwa sawa na kupoteza muda kwa Chadema kwenda mahakamani kudai haki yao.
Logic ya sasa: huhitaji kuwa na upeo mkubwa wa kinachoendelea Tanzania kubaini kuwa zama zimebadilika haswa. Japo utaambiwa "kutenguliwa hukumu ya Mbowe na Mdude kuachiwa huru ni suala la kimahakama," ukweli wa wazi ni kuwa haya yasingewezekana katika zama za Mwendazake.
Kwa maana hiyo: kwa vile mazingira yaliyopo ni rafiki kudai haki, angalau kwa kigezo cha kesi hizo mbili, kwanini Chadema wasiiburuze mahakamani Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kosa la kufoji majina 19 ya wabunge wa viti maalum?
Katiba mpya inaingiaje hapa?: Naam kuna haja ya marekebisho ya sheria mbalimbali kandamizi. Endapo mabadiliko hayo ni lazima yafanyike kwa njia ya Katiba mpya, ni sawa. Endapo badala ya katiba mpya tunaweza kufanya marekebisho tu ya katiba, ni sawa pia. However, iwe ni marekebisho ya katiba au ujio wa katiba mpya, kasumba ya kupuuza sheria itafanya marekebisho ya katiba/katiba mpya kuwa tatizo kama ilivyo sasa.
Kama alivyosema Askofu Bagonza kuwa wanaovunja Katiba hii wanaweza pia kuvunja katiba mpya, nami nahitimisha kuwa wanaopuuzia kudai haki zao kipindi hiki cha "katiba yenye mapungufu" wanaweza pia kupuuzia kudai haki zao katika zama za "Katiba mpya."
Na mwisho kabisa, kama hatuwezi kuheshimiana sie wenyewe katika mjadala huu muhimu kwa mustakabali wa taifa letu, hiyo katiba mpya itaheshimiwa vipi maana asiye na heshima kwa mtu ana nafasi kubwa ya kutokuwa na heshima kwa kitu/vitu (eg Katiba).
Mfano hai wa "kukoseana heshima" ni pale nguli wa sheria Prof Issa Shivji alipotoa angalizo kuhusu katiba mpya na kutanabaisha kuwa sio mwarobaini wa kutatua changamoto mbalimbali, baadhi ya "wasiopenda mawazo tofauti na yao" wamedai profesa huyo anazeeka vibaya. Wengine wameenda mbali na kumtusi kuwa "nafasi za u-DC zimejaa."
I stand to be corrected 🙏
Chahali chadema wamejaa majukumu kwa kuwafukuza uanachama na kutoa kauli kuwa hawahusiki na hiyo barua,wamefoji na kulidanganya bunge,chadema hapo ni shahidi shahidi ataendaje kufungua kesiEvarist Chahali,
..hoja yako ni nzuri, lakini naona umeichanganya na mfano mbaya ulipoleta suala la Chadema kutokwenda mahakamani kuhusiana na waliokuwa wanachama wao kujipeleka bungeni.
..mimi nadhani ungekuwa sahihi kama ungewashinikiza wabunge 19 ni kwanini wanahudhuria bungeni wakati chama chao kimewafukuza uanachama.
..Yuko mbunge mmoja alikiri bungeni kwamba amefukuzwa uanachama, na kitu cha kushangaza Naibu Spika akamkatiza hotuba yake na kumuelekeza afute kauli kuwa amefukuzwa uanachama.
..Pia wanaoweza kwenda mahakamani sio Chadema peke yao. Hata wabunge 19, Tume ya uchaguzi, Ofisi ya Spika, Msajili wa vyama vya siasa, wanayo dhima ya kulipeleka suala hili mahakamani ili liamuliwe kisheria.
..Kuhusu Chadema kutokwenda mahakamani inawezekana ni kutokana na UZOEFU wao na mahakama zetu. Kuna matukio mengi ya mahakama kuwaonea Chadema ama kwa kuwatia hatiani kwa makosa ya kubambikiwa, au kuamua mashauri kwa namna ya kukikandamiza chama hicho.
..Ni maoni yangu kwamba mhimili wa mahakama nao unapaswa kuhojiwa kama umekuwa ukitenda HAKI wakati wote. Kuna umuhimu wa mhimili huo kujitathmini utendaji wake na maadili yake.
..Naamini utendaji mbovu wa mahakama zetu ambazo zinashirikiana na wavunja sheria, na katiba, na hali hiyo imepelekea wananchi kukata tamaa kutafuta haki zao mahakamani.
Katiba kutoka kwa mwanasiasa ni ile inayompa favour yeye kwanza
So ukimkaribisha mwanasiasa akutengenezee katiba, tegemea mivutano isiyo na maana(kila mtu atatetea kinachompa favour)
Kazi ya kupiga ramli huiwezi, kaa kwa kutulia,
Kumbukumbu ya Magufuli ni chachu kwa viongozi wazalendo wajao
NB: tusiharibu mada ya katiba tafwadhari.
Kwa mujibu wa nani?Binadamu yoyote ni mwanasiasa.
Watu wa kijiji gani wanastahili zaidi kuwa na airport?Mzalendo anaweza kujenga airport kijijini kwake huku akiwaacha mamilioni ya watu bila maji safi ya kunywa?
Watu wa kijiji gani wanastahili zaidi kuwa na airport?
Kwa mujibu wa nani?
Kelele za nini sasa.Wa kwenu
Kama kina nani?Wasio wapumbavu.