Case study kuhusiana na mjadala wa Katiba Mpya

Katiba kutoka kwa mwanasiasa ni ile inayompa favour yeye kwanza

So ukimkaribisha mwanasiasa akutengenezee katiba, tegemea mivutano isiyo na maana(kila mtu atatetea kinachompa favour)
Katiba inatekelezwa na wanasiasa.

Kila kilichomo kwenye katiba kinalenga kutekeleza sera zitokanazo na siasa.

Huwezi kuondoa siasa kwenye mambo ya sheria na sera.

Mivutano hiyo ya kisiasa ndiyo huzaa mustakabali wa kesho ya taifa.

Kabla hujaendelea kuniquote jielimishe kidogo juu ya mifumo ya utawala na sheria.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Lengo na madhumuni ya chama cha siasa ni kuikosoa serikali sio ku deal na Raisi. Chadema hawajawahi kujenga shule, zahanati au hospitali toka chama kianzishwe. Watu wanataka chadema wafanye kazi yao kuisimamia serikali. Hakuna ufisadi wowote uliovumbuliwa na chadema watu tuna maswali kuhusiana na ulinzi wa rasilimali za taifa kama ujenzi wa bandari ya bagamoyo mpaka sa hivi chadema hawana nakala ya mkataba. Kama mkiangalia naona mamlaka ya raisi juu ya sheria ya ardhi ni makubwa kuliko hata katiba. Nilitegemea chadema kutoa msimamo wao lakini ukimya wao kwa mtazamo wa wengi wameweka mkazo sana kutawala sio shida za wananchi. Wakiendelea na tamaa ya madaraka watakosa vyote. Nawashauri waweke nguvu kubwa sana kwenye kuisimamia serikali kuliko kudai katiba hiyo inawafanya waonekane wana tamaa ya madaraka. Waanze kuchukua ruzuku kwanza wqsipo chukua ruzuku chama chao kitqhusishwa na ufadhili wa wazungu.
 
Mleta mada unachanganya baina ya vitu vitatu; Katiba mpya, katiba bora na kuheshimu katiba. Vyote hivyo ni vitu vitatu tofauti na tusilazimishe kuwa kitu kimoja, wala tusilazimishe kimoja kuwa mbadala wa kingine. Mtawala wa sasa akiheshimu katiba iliyopo sasa hiyo haina maana hii katiba itakuwa bora au kuwa mbadala wa kuwepo katiba mpya.

Swali, Je, Tanzania ya leo inahitaji katiba mpya? Na huo ndio mjadala unaopaswa kujadiliwa.

Kwa maoni yangu, kwa kuzingatia haya, kwanini ni lazima tudai Katiba mpya sasa;

1. Tanzania kama taifa hatujawahi kutunga katiba yetu sisi wenyewe toka kuumbwa kwa ulimwengu (Katiba iliyopo sasa ni urithi wa katiba ya kikoloni ya serikali ya Tanganyika tuliyoifanyia mabadiliko mengi mnoo, mara kwa mara tangu tunapata uhuru mpaka leo hii kiasi cha katiba yenyewe kupoteza taswira yake halisi ya mwanzo)

2. Mabadiliko ya kisiasa, kijamii na kiuchumi yaliyofanyika miaka 1990s hususani kuruhusu mfumo wa vyama vingi vya kisiasa, uchumi huria na uhuru wa kijamii, hayawezi kuhimilika kwa katiba iliyopo sasa hata tuifanyie mabadiliko kiasi gani.

3. Mabadiliko makubwa yaliyofanyika kwenye katiba ya Zanzibar hayawezi kubebwa na katiba iliyopo sasa hata kama tutaifanyia mabadiliko makubwa.

4. Udhaifu mwingi na nyufa nyingi zilizomo kwenye katiba hii ya sasa (jambo ambalo wanasiasa wa pande zote wanakiri hivyo) kiasi ambacho sote tunajiuliza na kushangaa zilikuwaje zikawepo kwenye katiba yetu, ni kielelezo tosha cha kudai kuwepo kwa katiba mpya.

5. Kelele na fukuto la kijamii na kisiasa la kutaka kuwepo kwa katiba mpya itakayokidhi mahitaji ya kizazi cha sasa limekuwepo kwa zaidi ya miaka 30 sasa bila kunyamaza wala kuchoka, hakuna namna tunaweza kulikwepa, kulipuuzia au kulifuta. Dawa ni kulifanyia kazi.

NOTE
Katiba yoyote ikifanyiwa mabadiliko mengi, makubwa au mara kwa mara inapoteza sura, muundo na mantiki ya kuendelea kuwa katiba iliyotungwa na walengwa. Katika ya Tanzania iliyopo sasa, haijarishi ni nzuri au mbaya, imepoteza uhalali wa kuendelea kuwa katiba iliyotungwa na walengwa (watanzania!) kwa sababu ya utitiri wa viraka vya mabadiliko uliofanywa na serikali kupitia bunge.
 
Lengo na madhumuni ya chama cha siasa ni kuikosoa serikali sio ku deal na Raisi. Chadema hawajawahi kujenga shule, zahanati au hospitali toka chama kianzishwe. Watu wanataka chadema wafanye kazi yao kuisimamia serikali. Hakuna ufisadi wowote uliovumbuliwa na chadema watu tuna maswali kuhusiana na ulinzi wa rasilimali za taifa kama ujenzi wa bandari ya bagamoyo mpaka sa hivi chadema hawana nakala ya mkataba. Kama mkiangalia naona mamlaka ya raisi juu ya sheria ya ardhi ni makubwa kuliko hata katiba. Nilitegemea chadema kutoa msimamo wao lakini ukimya wao kwa mtazamo wa wengi wameweka mkazo sana kutawala sio shida za wananchi. Wakiendelea na tamaa ya madaraka watakosa vyote. Nawashauri waweke nguvu kubwa sana kwenye kuisimamia serikali kuliko kudai katiba hiyo inawafanya waonekane wana tamaa ya madaraka. Waanze kuchukua ruzuku kwanza wqsipo chukua ruzuku chama chao kitqhusishwa na ufadhili wa wazungu.
Na wanaoweka msimamo kuwa katiba siyo kipaumbele chao ilihali wameshindwa kutatua hayo matatizo unayoyasema lengo lao siyo kutawala ?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Katiba sio kipaumbele cha wanannchi walio wengi wa Tanzania .

Kama wao wanataka katiba mpya waunde ya kwao na waitumie wao kama wao .

..ndugu yangu Tz ni yetu sote.

..kwa hiyo katiba yetu inapaswa kutatua mahitaji ya makundi mbalimbali ambayo ni sehemu ya Watz.

..kwa mfano, hatuwezi kukataa kusikiliza maombi ya wafanyakazi ambao ni percent ndogo ktk nchi yetu, kwasababu wakulima, wafugaji, na wavuvi, ambao wako wengi zaidi ktk jamii yetu, hawajatoa maombi yoyote kuhusu katiba.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Katiba inatekelezwa na wanasiasa.

Kila kilichomo kwenye katiba kinalenga kutekeleza sera zitokanazo na siasa.

Huwezi kuondoa siasa kwenye mambo ya sheria na sera.

Mivutano hiyo ya kisiasa ndiyo huzaa mustakabali wa kesho ya taifa.

Kabla hujaendelea kuniquote jielimishe kidogo juu ya mifumo ya utawala na sheria.
Kama unakubaliana na utengenezwaji wa katiba kupitia wanasiasa hupaswi kuwa mmoja wa wanaoipinga katiba tuliyonayo,

Wewe ndio ulianza kuniquote, so unaweza nipuuza.
 
mada nzuri sana hii

wachangiaji tusiharibu huu mjadala

maoni yangu
katiba ya sasa haitufai tena kwasababu imeshindwa kwenda sambamba na mabadiliko ya kiuchumi,kiteknologia,kimazingira na kiutawala.
 
Wewe ni mmoja kati ya wale waliolewa na utawala na "mama" wengi wenu mmekuwa mnatawaliwa na hisia zaidi ya uhalisia.

Unazungumzia mambo ya kudai Katiba kistaarabu wakati hao watawala hawaujui huo ustaarabu, unaonaje kama ungeanza kumwambia Samia afute ile kauli yake aliyoitoa Mbeya kuwa hata kama CCM isipochaguliwa itatangazwa mshindi?

- Kuhusu kuheshimu sheria, unadai kwamba hata kama Katiba Mpya ikija bado kuna uwezekano sheria nazo zitavunjwa.

Unasahau au hujui kwamba Katiba Mpya (Rasimu ya Warioba) iliweka miongozo kwa kila mtendaji kwenye ofisi ya serikali kuanzia Rais kwa nafasi yake atakuwa responsible kwa kila kosa atakalofanya, nini afanye akiwa ofisini na kipi kitampata asipotekeleza majukumu yake kisheria, wakati hii Katiba ya sasa inamzuia Rais kushtakiwa, Rais ni kama mfalme/ malaika.

Zaidi umeenda kutupia malalamiko yako kwa Chadema kwamba hawakwenda mahakamani licha ya wao kudai kwamba palikuwepo na forgery kwenye lile suala la wale Covid 19, hapa umenishangaza, unataka Chadema waende mahakama ipi haki ikatendeke wakati mahakama sasa zimewekwa mfukoni na watawala?

- Rais hajawahi kuzungumza lolote kuhusu wale wanawake, yupo kimya licha ya nguvu na ushawishi alionao kwenye siasa za nchi, kitendo chake cha kukaa kimya kwenye hili suala kinaacha tafsiri kwamba anaridhika na uwepo wa wale wanawake kule bungeni kinyume cha sheria, licha ya kujinadi ni mpenda HAKI.

- Kule bungeni nako, Ndugai kila siku anawalinda wale wanawake licha ya kujua fika anavunja sheria inayotaka wabunge watoke kwenye chama cha siasa, licha ya Chadema kudai mara zote kwamba tayari walishamuandikia Ndugai barua kumjulisha kuhusu kuvuliwa uanachama wale wanawake 19.

Ndugai anadai Chadema hawajafuata taratibu wakati taratibu kam hizo zimewahi kufuatwa miaka ya nyuma na waliokuwa wabunge kufutwa uanachama.

Hapa tunaona kumbe ni watawala ndio wanaongoza kupuuza sheria zilizopo badala ya Chadema kama unavyodai wewe, hivyo Katiba Mpya ni muhimu ije kuwawajibisha viongozi wa aina hii na kuleta usawa kwa wote.

Wakati kwa "individuals" wa nchi hii na wapinzani wakishindwa kutii sheria, au wakati mwingine wakifuata sheria kinyume na mapenzi ya watawala hupelekwa mahakamani au jela kabisa ( sababu wameziweka mahakama mfukoni), kitendo chako cha kushindwa ku - address hii problem ni udhaifu mkubwa kwenye andiko lako.
Je una uhakika gani hiyo katiba mpya haitakanyangwa iwapo unadai iliyopo imekanyagwa!
 
Unategemeo gani ukipata hiyo katiba mpya?
Katiba mpya itapatikana haijalishi ni leo au kesho.

Lengo kubwa la katiba mpya ni kurejesha madaraka kwa wananchi ili waweze kujiamulia mambo yao wenyewe badala ya watawala wezi.

Huwezi kuvipata ulivyovitaja hapo bila kwanza kuwarejeshea madaraka wananchi wenyewe kutoka kwa watawala na hilo itawezekana tu kupitia katiba mpya
 
Katiba mpya itapatikana haijalishi ni leo au kesho.

Lengo kubwa la katiba mpya ni kurejesha madaraka kwa wananchi ili waweze kujiamulia mambo yao wenyewe badala ya watawala wezi.

Huwezi kuvipata ulivyovitaja hapo bila kwanza kuwarejeshea madaraka wananchi wenyewe kutoka kwa watawala na hilo itawezekana tu kupitia katiba mpya

Power to the people ndo malengo yako. Nimazuri kwa kweli lakini kila kizuri hakikosi kasoro. Katiba za mrengo wa power to the people zinamapungufu yake. Je unayajua??
 
Power to the people ndo malengo yako. Nimazuri kwa kweli lakini kila kizuri hakikosi kasoro. Katiba za mrengo wa power to the people zinamapungufu yake. Je unayajua??
Yataje wewe unayeyajua mimi nitakuambia suluhisho la hayo mapungufu.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Hoja: la muhimu zaidi ni heshima kwa sheria, na kwa vile Katiba ni sheria mama, basi heshima husika iwe kwenye sheria zilizomo kwenye katiba.

Hali ilivyo sasa: ni kweli katiba iliyopo ina mapungufu mengi. Na ni kweli kuwa mapungufu hayo yanaathiri maeneo mbalimbali hususan haki za kisiasa/kidemokrasia.

Katiba yote ya sasa ina mapungufu?: Hapana. Kuna sheria nyingi tu katika katiba ya sasa ambazo ni mwafaka. Tatizo ni kwamba heshima kwa sheria ni changamoto kubwa kwa Watanzania. Kwahiyo hata sheria hizo "nzuri" zaishia kuonekana "mbaya" kwa sababu zinapuuzwa

Case study: kwa mujibu wa maelezo ya Chadema, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilifoji majina wa wabunge 19 wa viti maalum wa chama hicho. Kufoji ni kosa la jinai. Hadi muda huu Chadema hawajafungua mashtaka dhidi ya tume ya Taifa ya Uchaguzi kutokana na forgery hiyo.

Tatizo lipo wapi? Ukisikiliza mjadala kuhusu Katiba mpya, focus ipo kwa watawala. Nguvu kubwa za Rais, Tume ya uchaguzi kutokuwa huru, nk. Lakini pengine kwa makusudi au kutojua, hakuna mjadala kuhusu "mapungufu ya watawaliwa." Mfano hai hapa ni huo wa NEC kuvunja sheria lakini wahanga wa uvunjifu huo wa sheria, Chadema hajachukua hatua za kisheria. Sasa hapo tatizo si katiba bali ni kupuuza sheria inayoweza kutoa haki stahili.

Logic ya wakati huo kwa Chadema: zama za Mwendazake, ingekuwa sawa na kupoteza muda kwa Chadema kwenda mahakamani kudai haki yao.

Logic ya sasa: huhitaji kuwa na upeo mkubwa wa kinachoendelea Tanzania kubaini kuwa zama zimebadilika haswa. Japo utaambiwa "kutenguliwa hukumu ya Mbowe na Mdude kuachiwa huru ni suala la kimahakama," ukweli wa wazi ni kuwa haya yasingewezekana katika zama za Mwendazake.

Kwa maana hiyo: kwa vile mazingira yaliyopo ni rafiki kudai haki, angalau kwa kigezo cha kesi hizo mbili, kwanini Chadema wasiiburuze mahakamani Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kosa la kufoji majina 19 ya wabunge wa viti maalum?

Katiba mpya inaingiaje hapa?: Naam kuna haja ya marekebisho ya sheria mbalimbali kandamizi. Endapo mabadiliko hayo ni lazima yafanyike kwa njia ya Katiba mpya, ni sawa. Endapo badala ya katiba mpya tunaweza kufanya marekebisho tu ya katiba, ni sawa pia. However, iwe ni marekebisho ya katiba au ujio wa katiba mpya, kasumba ya kupuuza sheria itafanya marekebisho ya katiba/katiba mpya kuwa tatizo kama ilivyo sasa.

Kama alivyosema Askofu Bagonza kuwa wanaovunja Katiba hii wanaweza pia kuvunja katiba mpya, nami nahitimisha kuwa wanaopuuzia kudai haki zao kipindi hiki cha "katiba yenye mapungufu" wanaweza pia kupuuzia kudai haki zao katika zama za "Katiba mpya."

Na mwisho kabisa, kama hatuwezi kuheshimiana sie wenyewe katika mjadala huu muhimu kwa mustakabali wa taifa letu, hiyo katiba mpya itaheshimiwa vipi maana asiye na heshima kwa mtu ana nafasi kubwa ya kutokuwa na heshima kwa kitu/vitu (eg Katiba).

Mfano hai wa "kukoseana heshima" ni pale nguli wa sheria Prof Issa Shivji alipotoa angalizo kuhusu katiba mpya na kutanabaisha kuwa sio mwarobaini wa kutatua changamoto mbalimbali, baadhi ya "wasiopenda mawazo tofauti na yao" wamedai profesa huyo anazeeka vibaya. Wengine wameenda mbali na kumtusi kuwa "nafasi za u-DC zimejaa."

I stand to be corrected 🙏
Huathiri hata uchumi ,Sera ambazo hazina muelekeo (ineffective policies)
 
Je una uhakika gani hiyo katiba mpya haitakanyangwa iwapo unadai iliyopo imekanyagwa!
Haitakanyagwa kwasababu itaweka mipaka kati ya mhimili mmoja na mwingine, na zaidi, itaainisha ni yapi majukumu ya kila ofisi ya serikali, na kipi kitatokea kwa atakae kwenda kinyume na taratibu za ofisi yake, hii ni kianzia kwa Rais mpaka wabunge, mahakimu na majaji.

Iliyopo inakanyagwa kwasababu watawala wameigeuza kichaka cha kujifichia wakifanya maovu yao.

Mfano, Rais akishaingia madarakani kwa kuiba kura, matokeo yake hayaruhusiwi kupingwa popote, na Tume ya uchaguzi imepewa mamlaka ya kuwa chombo pekee cha kutangaza washindi wa uchaguzi wakati wajumbe na mwenyekiti wake ni wanateuliwa na mwenyekiti wa CCM..
 
Raisi ni alama ya nchi, kutumia pesa ya umma kujenga sanamu yake ni kutaka akumbukwe,

Ingekuwa tunatumia pesa ya umma kutaka kujenga sanamu la mjomba wako au bibi yako, ndo yangekua matumizi mabaya ya pesa

Maana hakuna cha maana wameifanyia hii nchi,

NB: tusiharibu mada ya katiba tafwadhari.
Yaani nilikua nakuona una akili,kumbe amuna kitu.
 
Katiba ni nini?nani anahitaji katiba mpya??katiba ni ya nani??kwa nini tinahitaji katiba mpya??ukijibu haya maswali kwa ufasaha utapata kujua kwa nn ccm wanasema mbowe dikteta
 
Ukisema katiba mpya,

Tutajiuliza nani anayeidai,

Kwa interest zipi.
 
Back
Top Bottom