Mzalendo_Mwandamizi
JF-Expert Member
- Dec 12, 2007
- 1,117
- 4,764
Hoja: la muhimu zaidi ni heshima kwa sheria, na kwa vile Katiba ni sheria mama, basi heshima husika iwe kwenye sheria zilizomo kwenye katiba.
Hali ilivyo sasa: ni kweli katiba iliyopo ina mapungufu mengi. Na ni kweli kuwa mapungufu hayo yanaathiri maeneo mbalimbali hususan haki za kisiasa/kidemokrasia.
Katiba yote ya sasa ina mapungufu?: Hapana. Kuna sheria nyingi tu katika katiba ya sasa ambazo ni mwafaka. Tatizo ni kwamba heshima kwa sheria ni changamoto kubwa kwa Watanzania. Kwahiyo hata sheria hizo "nzuri" zaishia kuonekana "mbaya" kwa sababu zinapuuzwa
Case study: kwa mujibu wa maelezo ya Chadema, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilifoji majina wa wabunge 19 wa viti maalum wa chama hicho. Kufoji ni kosa la jinai. Hadi muda huu Chadema hawajafungua mashtaka dhidi ya tume ya Taifa ya Uchaguzi kutokana na forgery hiyo.
Tatizo lipo wapi? Ukisikiliza mjadala kuhusu Katiba mpya, focus ipo kwa watawala. Nguvu kubwa za Rais, Tume ya uchaguzi kutokuwa huru, nk. Lakini pengine kwa makusudi au kutojua, hakuna mjadala kuhusu "mapungufu ya watawaliwa." Mfano hai hapa ni huo wa NEC kuvunja sheria lakini wahanga wa uvunjifu huo wa sheria, Chadema hajachukua hatua za kisheria. Sasa hapo tatizo si katiba bali ni kupuuza sheria inayoweza kutoa haki stahili.
Logic ya wakati huo kwa Chadema: zama za Mwendazake, ingekuwa sawa na kupoteza muda kwa Chadema kwenda mahakamani kudai haki yao.
Logic ya sasa: huhitaji kuwa na upeo mkubwa wa kinachoendelea Tanzania kubaini kuwa zama zimebadilika haswa. Japo utaambiwa "kutenguliwa hukumu ya Mbowe na Mdude kuachiwa huru ni suala la kimahakama," ukweli wa wazi ni kuwa haya yasingewezekana katika zama za Mwendazake.
Kwa maana hiyo: kwa vile mazingira yaliyopo ni rafiki kudai haki, angalau kwa kigezo cha kesi hizo mbili, kwanini Chadema wasiiburuze mahakamani Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kosa la kufoji majina 19 ya wabunge wa viti maalum?
Katiba mpya inaingiaje hapa?: Naam kuna haja ya marekebisho ya sheria mbalimbali kandamizi. Endapo mabadiliko hayo ni lazima yafanyike kwa njia ya Katiba mpya, ni sawa. Endapo badala ya katiba mpya tunaweza kufanya marekebisho tu ya katiba, ni sawa pia. However, iwe ni marekebisho ya katiba au ujio wa katiba mpya, kasumba ya kupuuza sheria itafanya marekebisho ya katiba/katiba mpya kuwa tatizo kama ilivyo sasa.
Kama alivyosema Askofu Bagonza kuwa wanaovunja Katiba hii wanaweza pia kuvunja katiba mpya, nami nahitimisha kuwa wanaopuuzia kudai haki zao kipindi hiki cha "katiba yenye mapungufu" wanaweza pia kupuuzia kudai haki zao katika zama za "Katiba mpya."
Na mwisho kabisa, kama hatuwezi kuheshimiana sie wenyewe katika mjadala huu muhimu kwa mustakabali wa taifa letu, hiyo katiba mpya itaheshimiwa vipi maana asiye na heshima kwa mtu ana nafasi kubwa ya kutokuwa na heshima kwa kitu/vitu (eg Katiba).
Mfano hai wa "kukoseana heshima" ni pale nguli wa sheria Prof Issa Shivji alipotoa angalizo kuhusu katiba mpya na kutanabaisha kuwa sio mwarobaini wa kutatua changamoto mbalimbali, baadhi ya "wasiopenda mawazo tofauti na yao" wamedai profesa huyo anazeeka vibaya. Wengine wameenda mbali na kumtusi kuwa "nafasi za u-DC zimejaa."
I stand to be corrected 🙏
Hali ilivyo sasa: ni kweli katiba iliyopo ina mapungufu mengi. Na ni kweli kuwa mapungufu hayo yanaathiri maeneo mbalimbali hususan haki za kisiasa/kidemokrasia.
Katiba yote ya sasa ina mapungufu?: Hapana. Kuna sheria nyingi tu katika katiba ya sasa ambazo ni mwafaka. Tatizo ni kwamba heshima kwa sheria ni changamoto kubwa kwa Watanzania. Kwahiyo hata sheria hizo "nzuri" zaishia kuonekana "mbaya" kwa sababu zinapuuzwa
Case study: kwa mujibu wa maelezo ya Chadema, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilifoji majina wa wabunge 19 wa viti maalum wa chama hicho. Kufoji ni kosa la jinai. Hadi muda huu Chadema hawajafungua mashtaka dhidi ya tume ya Taifa ya Uchaguzi kutokana na forgery hiyo.
Tatizo lipo wapi? Ukisikiliza mjadala kuhusu Katiba mpya, focus ipo kwa watawala. Nguvu kubwa za Rais, Tume ya uchaguzi kutokuwa huru, nk. Lakini pengine kwa makusudi au kutojua, hakuna mjadala kuhusu "mapungufu ya watawaliwa." Mfano hai hapa ni huo wa NEC kuvunja sheria lakini wahanga wa uvunjifu huo wa sheria, Chadema hajachukua hatua za kisheria. Sasa hapo tatizo si katiba bali ni kupuuza sheria inayoweza kutoa haki stahili.
Logic ya wakati huo kwa Chadema: zama za Mwendazake, ingekuwa sawa na kupoteza muda kwa Chadema kwenda mahakamani kudai haki yao.
Logic ya sasa: huhitaji kuwa na upeo mkubwa wa kinachoendelea Tanzania kubaini kuwa zama zimebadilika haswa. Japo utaambiwa "kutenguliwa hukumu ya Mbowe na Mdude kuachiwa huru ni suala la kimahakama," ukweli wa wazi ni kuwa haya yasingewezekana katika zama za Mwendazake.
Kwa maana hiyo: kwa vile mazingira yaliyopo ni rafiki kudai haki, angalau kwa kigezo cha kesi hizo mbili, kwanini Chadema wasiiburuze mahakamani Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kosa la kufoji majina 19 ya wabunge wa viti maalum?
Katiba mpya inaingiaje hapa?: Naam kuna haja ya marekebisho ya sheria mbalimbali kandamizi. Endapo mabadiliko hayo ni lazima yafanyike kwa njia ya Katiba mpya, ni sawa. Endapo badala ya katiba mpya tunaweza kufanya marekebisho tu ya katiba, ni sawa pia. However, iwe ni marekebisho ya katiba au ujio wa katiba mpya, kasumba ya kupuuza sheria itafanya marekebisho ya katiba/katiba mpya kuwa tatizo kama ilivyo sasa.
Kama alivyosema Askofu Bagonza kuwa wanaovunja Katiba hii wanaweza pia kuvunja katiba mpya, nami nahitimisha kuwa wanaopuuzia kudai haki zao kipindi hiki cha "katiba yenye mapungufu" wanaweza pia kupuuzia kudai haki zao katika zama za "Katiba mpya."
Na mwisho kabisa, kama hatuwezi kuheshimiana sie wenyewe katika mjadala huu muhimu kwa mustakabali wa taifa letu, hiyo katiba mpya itaheshimiwa vipi maana asiye na heshima kwa mtu ana nafasi kubwa ya kutokuwa na heshima kwa kitu/vitu (eg Katiba).
Mfano hai wa "kukoseana heshima" ni pale nguli wa sheria Prof Issa Shivji alipotoa angalizo kuhusu katiba mpya na kutanabaisha kuwa sio mwarobaini wa kutatua changamoto mbalimbali, baadhi ya "wasiopenda mawazo tofauti na yao" wamedai profesa huyo anazeeka vibaya. Wengine wameenda mbali na kumtusi kuwa "nafasi za u-DC zimejaa."
I stand to be corrected 🙏