CAF yamfungia mechi 8 Kocha wa Taifa Stars, huku TFF ikimsimamisha. Aliishutumu Morocco kwa kupanga mechi

Cicadulina

JF-Expert Member
Sep 8, 2015
961
2,345
Shirikisho la soka barani Afrika CAF limemfungia mechi nane Kocha wa timu ya Taifa ya Tanzania Adel Amrouche kwasababu ya shutuma zake alizozitoa dhidi ya Morocco

Adhabu hiyo ulitolewa jana na Kamati ya Nidhamu ya CAF baada ya malalamiko yaliyowasilishwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Morocco (RMFF) ikimlalamikia Kocha huyo kwa kauli zake kuwa Morocco inaushawishi ndani ya CAF katika kupanga mechi pamoja na waamuzi.

Katika hatua nyingine, Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemsimamisha Kocha Adel Amrouche

Kutokana na uamuzi huo na imemteua Hemed Morocco kuwa Kaimu Kocha Mkuu akisaidiwa na Juma Mgunda.

IMG_9084.jpeg
 
Duuuh
Hebu andika kwa utulivu basi tuelewe
TAARIFA Kutoka @tanfootball

Shirikisho la soka barani Afrika CAF limemfungia mechi nane Kocha wa timu ya Taifa ya Tanzania Adel Amrouche kwasababu ya shutuma zake alizozitoa dhidi ya Morocco

Adhabu hiyo ulitolewa jana na Kamati ya Nidhamu ya CAF baada ya malalamiko yaliyowasilishwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Morocco (RMFF) ikimlalamikia Kocha huyo kwa kauli zake kuwa Morocco inaushawishi ndani ya CAF katika kupanga mechi pamoja na waamuzi.

Katika hatua nyingine, Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemsimamisha Kocha Adel Amrouche.

Kutokana na uamuzi huo na imemteua Hemed Morocco kuwa Kaimu Kocha Mkuu akisaidiwa na Juma Mgunda.

#sokaonlineupdates
 
Back
Top Bottom