Leo kila kijiwe cha ubishi maongezi yanayosikika ni 'YANGA WAMTOA ULIMI MWARABU'. Eti baada ya Yanga kunyolewa na mwarabu, wamebaki kujisifia kwa sifa za kijinga za 'KUFUNGA WATUFUNGA LAKINI CHENGA TWAWALA'. Maajabu haya!!!
Watu wanatafuta kushinda halafu wengine wanatafuta sifa za kijinga? Wakati waarabu wanapiga mpira wa kitabuni, Yanga wanaweka uchawi golini!!
Rudini nyumbani bongo mje mkacheze mpira wenu wa kichawi. Mpira wa kichawi hauchezwi uarabuni bali huchezwa katika 'majaruba' yenu ya bongo.
Kuna wanayanga wanamlaumu Twite kwa kukosa penati ya mwisho na kusahau kwamba yule aliyekosa ya kwanza ndiye aliyewakatisha tamaa wenzake. Mchezaji aliyefanya kazi nzuri ni Dida, wengine wote mbwela tu, hawakuwa na lolote. Tuache kucheza mpira wa mdomoni na wa kishirikina. Mpira hauchezwi hivyo. Mbona ushirikina wa Dida haukuwasaidia kushinda? Tubadilike.