CAF Champions League

CAF Champions League

Mtaani imekuwa kero..
mashabiki wa simba wanaibeza yanga kutolewa.
na wanabaki kuongelea historia yao ya kumtoa bingwa mtetezi.
sasa cha kujiuliza je walipomtoa bingwa mtetezi walichukua kombe au hata kufika final?
 
hivi Yanga walipoifunga Al Ahly goli moja pale Taifa waliendelea mbele au hata kufika hatua ya mtoano?
 
yanga yatupwa nje michuano ya club bingwa afrika , yeeeee oyeeee yeyeyeye. Polen sana watanganyika, mpira c fani yenu.

nimeamini washabiki wa simba ni washamba saaaaaaanaaaaaaaaaaaaaaaa, wanaishi kutegemea uchaaaaaawiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Waongelee yao ,maharage anawapa shida wanakomaa yanga yanga.sikuhizi mnashabikia yanga nini? Tuacheni na Yanga yetu
 
hivi yule mzee anayepayuka sana wanamwita Akilimali mbona simsikii tena?napenda aje na agenda ya umuondoa mwenyekiti maana ndiye aliyewauza kwa waarabu wenzake
 
Mkuu wasikilize na uwapuuze tu...ndio ushabiki na utani wa jadi huo.Mafanikio ya SImba au Yanga baada ya mfumo huu mpya wa Ligi ya Mabingwa sote tumeishia ngazi inayofafanana.
 
hakuna ubaya kwa watani wa jadi..huwa wanapenda ku-discuss weakness za mpinzani. usihuzunike broo
 
Mashabiki wa Yanga na Simba wa miaka hii hovyo kweli...

Zamani Simba au Yanga zikicheza mechi za kimataifa zilikuwa zinasaidia kuanzia ufundi hadi ushabiki...

Ujadi wa timu hizi ulikuwepo ndani ya nchi tu au ligi ya muungano au kombe la EAC na ni hadi pale zinapokutana zenyewe...

Leo hii Yanga kapoteza kwa waarab, kuna vimburukutu wanaojiita mashabiki wa Simba wanashangilia kwa mbwembwe kama makalio yanayoshusha uharo...

Sijui utaifa wenu upo wapi? Sijui utani wenu wa jadi upo wapi?
 
Mimi ni Simba na nilikuwa nawaombea wafungwe hapo jana, nilitegemea watakula kichapo cha haja. lkn kama wamefika mpaka kupigiana penati basi watani wamejitahidi tena sana wanahitaji pongezi aisee

Al Ahly wabovu sana...timu mbovu kama yanga haikutakiwa kuwapeleka hadi kwenye matuta....Yanga mbovu sana...Al Ahly mbovu pia...Ingekuwa simba kwa Al Ahly hii...tungewapiga 5 hapa nyumbani tukienda kule tunamalizia kwa kuwapiga tatu...wana bahati sana kukutana na timu mbovu ya Tanzania
 
Mara baada ya mapumziko golikipa nguli wa timu ya wananchi wa tanzania aka yanga alionekekana akimwaga kitu mithili ya unga kama si kutandaza uzi mwembamba golini kwake kuashiria kwamba anaamini utamsaidia kuzuia mabao. Mmoja kati ya wachezaji wa kiarabu baada ya kuona hivyo alifanya kitendo kilichoashiria kwamba alikuwa akitegua imani hiyo ya kishirikina. Juzi hawa wananchi walipiga kelele sana kwa watani wao kwamba ni washirikina. sasa nashangaa ni kwa nini wanayarudia yale walokuwa wakiyapigia kelele. Sina uhakika kama CAF wana vipengele vinavyohusu imani hizi. Dida naona umepaisha imani za kishirikina katika anga za kimataifa
 
nina presha mpk kusema siwezi yaa lalmaulaa elyuum yanga abkaaniy bukaa a laa ansaa kikweli sijafurahia matokeo km vile ambavyo sijajutoa kupoteza nauli kwenda misri na kurudi
 
Back
Top Bottom