Cabinet reshuffle: This is a disgustingly bad joke, Mr President

Cabinet reshuffle: This is a disgustingly bad joke, Mr President

Inawezekana bado ni mipango ya Mungu ili kila aliyekuwa bado hajaielewa vizuri CCM na utendaji wake,aijonee ili achukue uamuzi unaostahili.
Sometimes Unashindwa kuelewa kama JK anapata ushauri mzuri ili kufanya maamuzi au ni upeo wake mdogo sana vilevile wa kutoweza kupambanua nini cha kuamua.
Sioni tatizo sana kwa wale walioteuliwa ktk positions hizo pamoja na sifa zao na record zao mbovu zisizofaa.Tatizo ni au source ya matatizo yote na maamuzi mabovu yote ni kuwa na kiongozi asiyefaa ktk ngazi ya taifa. Na hili mbali na kuwaweka mahala pagumu wateule wake,nadhani inatoa taswira mbaya sana na kumuumbua rais wetu jinsi alivyo na upeo mdogo sana ktk post aliyonayo.
Taratibu mtaanza kumwelewa Kagame ni jinsi gani aliudhiwa na huyu jamaa kiasi cha kuazimia kumvizia na kumchapa akidhani hilo lingesaidia. Nahisi Kagame angemchapa,hali yetu ingekuwa na mabadiliko ambayo mimi na wewe hatujui.Ingeweza kusaidia au kuharibu zaidi.
Sina hakika kama anajua anachokifanya, na kama ni dhamira yake, basi kutokana na utendaji wake mbovu,jamaa ana dhamira mbaya sana kwa taifa lake.
Inatia uchungu sana kuwa na kiongozi wa namna hii katika ulimwengu wa sasa.Haihitaji kufika hata O level kuona mapungufu ya JK.
Ndiyo maana pamoja na mapungufu ya viongozi wa nchi jirani,bado wakikaa na JK kufanya maamuzi kwa manufaa ya nchi zao nadhani walishagundua jamaa ni kilaza fulani hivi na kuona atachelewesha mambo muhimu ktk maendeleo, bila kumficha wameamua kumweka kando.
To be honest the guy hafai kabisa na anapwaya sana kwenye post hiyo. Nchi yetu itakuwa imepita ktk kipindi cha giza ktk utawala wake. Hasara kubwa sana kwa Taifa.
Ndiyo maana nilianza kwa kusema huenda Mungu ameamua kulirehemu taifa letu kupitia utawala dhaifu ambao sijawahi kuona aina yake,ili kutokana na UBOVU wa ngwe hii ya utawala watz wajipange kutorudia kuchagua Msiba kama huu kwa taifa.
Ni dhahiri yote ambayo yameshatokea,yanayotokea na yatakayotokea kuhusu watu kama akina Nchemba kupewa post za hivyo, Ni udhaifu wa kiongozi asiye na dhamira njemba kwa taifa,na kama si udhaifu tu basi jamaa atakuwa ni jeuri na kiburi kisichokuwa na mfano. Huyu mtu hakustahili kuendelea kuwa madarakani. It's only in Tanzania.
 
Nndondo anza kutoka wewe barabarani si kubwatuka humu kumbe muoga wahedi eti siogopi hata mods wakitutaja, watakutaja vipi wakati wewe umeonekana barabarani? Namheshimu kijana mmoja pale UD mwaka jana aliandamana mwenyewe hadi Ikulu wewe je? Nchemba humuwezi hata mkipambanishwa kwa vita ya maneno achilia mbali utendaji. Amewaweza kwenye vyama vyenu mnaleta za kuleta hapa. Hatudanganyiki tena
 
mleta mada: Usisahau OKTOBA 2015 na bajeti inayohitajika ...
 
Hizi ni dharau na kejeli kwa watanzania...sijui kama tunawaelewa wanavyotuchukulia hawa jamaa.
Mtanzania alisha tafsiliwa na wanaccm kuwa ni bogus tu,hana uwezo wa ku argue chochote hata wangefanya madudu gani.Wao maisha ya Mtanzania siyo issue,mhimu ni wao tu kuwa madarakani basi.
 
Nyie acheni unoko na wivu Nchemba ni jembe, siasa tu zinawasumbua. Mtu mwenye MEconomics na sasa anchukua Phd amabaye aliwahi kufanya kazi Central Bank bado mnasema hatoshi. Mareh Mginwa alikuwa na Masters pia lakini, kabla ya hapo Mkuro elimu yake ilikuwa ndogo kuliko Mwigulu, tatizo nilionalo ni kwamba mnamwona kama mwanasiasa zaidi lakini ni mchapa kazi msomi.Kwa Nkamia kutajwa na waandishi kucheka unajua waandishi na Nkamia pamoja na kwamba ni mwenzaao huwa hawamwelewi awambiapo mkiandika nchi kwanza na mambo yenu baadaye; lakini cha mno ni kwamba Tido Mhando imekula kwake, kwani itabidi kwenda kwake kupiga hodi kikazi.
Elimu ya inayotolewa na ccm iliyooza nayo utaita elimu?mwanafunzi aliyesoma UDSM utamlinganisha na wa UNIVERSITY OF CAPE TOWN?
 
Nndondo anza kutoka wewe barabarani si kubwatuka humu kumbe muoga wahedi eti siogopi hata mods wakitutaja, watakutaja vipi wakati wewe umeonekana barabarani? Namheshimu kijana mmoja pale UD mwaka jana aliandamana mwenyewe hadi Ikulu wewe je? Nchemba humuwezi hata mkipambanishwa kwa vita ya maneno achilia mbali utendaji. Amewaweza kwenye vyama vyenu mnaleta za kuleta hapa. Hatudanganyiki tena
Wewe ni katika wale mashabiki zuzu hujui hata uchambuzi.huwazi hata watoto wako unawaza wewe namkeo tu.Hamjali maisha ya mwananchi maskini utafikiri mtaishi milele hapa duniani.Mabutu Seseseko wa Zabanga naye alikuwa na jeuri kama yako.Nusu ya utajiri wa Zaire ulikuwa wake binafsi na watoto wake.Kwa taarifa yako alizikwa na watu sita tu katika nchi ya kigeni.
 
Kamundu,

..wako wa-Tz wengi tu ambao ni competent wangeweza kuteuliwa kutumikia wizara ya fedha.

..nadhani JK mwenyewe haamini kama wizara ya fedha ni muhimu kiasi hicho kulazimisha kuteua watu wenye solid track record kutumikia pale.

NB:

..halafu kitendo cha waandishi wa habari kucheka na kuguna kuhusu baadhi ya teuzi za Raisi, kinaleta taswira isiyo nzuri kwa mteuliwa, washauri wa Raisi, pamoja na Raisi mwenyewe.

cc Mchambuzi, Mdondoaji, NasDaz

....Mkuu jamaa anaezeka paa la nyasi ...kuvuja kwa nyumba kupo pale pale!!!!
 
Taswira ya baraza la mawaziri jipya halitoi tumaini la mabadiliko ya aina yoyote ya kiutendaji badala yake walaji wapya wameingia ndani ya mfumo ule ule.Watu makini wameachwa na kuwekwa watu dhaifu kama Mwigulu Nchemba huyu ni mropokaji tu na mpanga mipango ya kuhujumu upinzani na wasi wasi sana na huyu jamaa kwani toka ameingia ktk ulingo wa siasa amekuwa Mbabaishaji na mlopokaji wala hana jipya anafanyia kazi tumbo lake.Kwa kifupi sina imani kabisa na baraza jipya la mawaziri kwamba litaleta mabadiliko yoyote yale kwa Wa
Tanzania wanaolia kila kukicha na ugumu wa maisha.Kilichofanyika nikubadilisha nguo kwa mtu yuleyule mwenye tabia zilezile.Hili baraza jipya nilakiulaji zaidi nasio kuleta mabadiliko ktk nchi yetu maana watu niwale wale wakiwa na mbinu zile zile za kifisadi za kutengeneza pesa za uchaguzi mkuu mwakani ndio maana nasema Baraza jipya hawana jipya ni dhaifu ndani ya mfumo dhaifu.
 
Ninauhakika sana sasa kuwa mshauri mkuu wa Kikwete ni mganga wa kienyeji!

Haiwezekani katika jopo la washauri wa5 tuseme halafu wenye akili timamu wakakaa chini na rahisi na kumshauri hio outcome! HAIWEZEKANI!! Wachagua randomly wanfunzi wa chuo kikuu wawe makada wa CCM halafu wagawe makundi ya wa5 wa5 then wape assignment ya kumshauri rahisi huyu kuhusu baraza la mawaziri, naamini hawawezi kuja na conclusion kama ya huyu jamaa angu! Ni lazima tu mganga wa kienyeji ndio mshauri wake pekee na mkuu!
 
Inawezekana bado ni mipango ya Mungu ili kila aliyekuwa bado hajaielewa vizuri CCM na utendaji wake,aijonee ili achukue uamuzi unaostahili.
Sometimes Unashindwa kuelewa kama JK anapata ushauri mzuri ili kufanya maamuzi au ni upeo wake mdogo sana vilevile wa kutoweza kupambanua nini cha kuamua.
Sioni tatizo sana kwa wale walioteuliwa ktk positions hizo pamoja na sifa zao na record zao mbovu zisizofaa.Tatizo ni au source ya matatizo yote na maamuzi mabovu yote ni kuwa na kiongozi asiyefaa ktk ngazi ya taifa. Na hili mbali na kuwaweka mahala pagumu wateule wake,nadhani inatoa taswira mbaya sana na kumuumbua rais wetu jinsi alivyo na upeo mdogo sana ktk post aliyonayo.
Taratibu mtaanza kumwelewa Kagame ni jinsi gani aliudhiwa na huyu jamaa kiasi cha kuazimia kumvizia na kumchapa akidhani hilo lingesaidia. Nahisi Kagame angemchapa,hali yetu ingekuwa na mabadiliko ambayo mimi na wewe hatujui.Ingeweza kusaidia au kuharibu zaidi.
Sina hakika kama anajua anachokifanya, na kama ni dhamira yake, basi kutokana na utendaji wake mbovu,jamaa ana dhamira mbaya sana kwa taifa lake.
Inatia uchungu sana kuwa na kiongozi wa namna hii katika ulimwengu wa sasa.Haihitaji kufika hata O level kuona mapungufu ya JK.
Ndiyo maana pamoja na mapungufu ya viongozi wa nchi jirani,bado wakikaa na JK kufanya maamuzi kwa manufaa ya nchi zao nadhani walishagundua jamaa ni kilaza fulani hivi na kuona atachelewesha mambo muhimu ktk maendeleo, bila kumficha wameamua kumweka kando.
To be honest the guy hafai kabisa na anapwaya sana kwenye post hiyo. Nchi yetu itakuwa imepita ktk kipindi cha giza ktk utawala wake. Hasara kubwa sana kwa Taifa.
Ndiyo maana nilianza kwa kusema huenda Mungu ameamua kulirehemu taifa letu kupitia utawala dhaifu ambao sijawahi kuona aina yake,ili kutokana na UBOVU wa ngwe hii ya utawala watz wajipange kutorudia kuchagua Msiba kama huu kwa taifa.
Ni dhahiri yote ambayo yameshatokea,yanayotokea na yatakayotokea kuhusu watu kama akina Nchemba kupewa post za hivyo, Ni udhaifu wa kiongozi asiye na dhamira njemba kwa taifa,na kama si udhaifu tu basi jamaa atakuwa ni jeuri na kiburi kisichokuwa na mfano. Huyu mtu hakustahili kuendelea kuwa madarakani. It's only in Tanzania.

Kaamua kuwasaidia watanzania kuijua CCM vizuri.......anania njema ya kuwafanya watz waharakishe kichagua mabadiliko........Anaifagilia njia chadema.
 
Watanzania bwana in less than 20 years shillingi imeporomoka kutoka £1 kwa sh800 leo £1 sawa na sh2700 bei ya kuuza.
Chini ya kikwete sasa anaenda mwaka wa tisa sh. imeporomoka kwa sh 400 tu, halafu bado mmnabeza na mawaziri wake. Mkapa ambae ana mchango mkubwa wala hakusakamwa na baraza la mawaziri uchwara.

Tangia tupate uhuru leo ndio wakulima wanafundishwa kulima kilimo cha mstari nje ya jembe hata kwa kutumia ng'ombe, matokeo yake wengi sasa wanavuna zaidi ya awali. Tuna uhuru miaka 50 eti walikuwa hawayajui hayo. Sikuhizi wakulima awalalamika mazao ya kula wao, bali wapewe soko, wenye bahati na soko wameanza kukarabati au kujenga nyumba mpya, leo wakulima wanaomba wajengewe vitu vingine kama viwanda vya kusindika, mitaji, kufundishwa ujasiriamali. JK keshawatoa wengi kwenye kilimo cha kujikidhi wao na sasa wanafikiria biashara in 9 years time.

Leo lami kwenda popote Tanzania na hakuna hata mkataba mmoja wa kinyonyaji umesainiwa chini ya JK yote kaicha Mkapa, kwenye chokochoko waziri anaondoka yote kwa sababu JK kaachia uhuru wa habari. Whistle blowers information sasa maelezo yanaandikwa kwenye magazeti.

Ametimiza hayo yote na mengi zaidi akiwa hayupo serious na kazi yake wakati amefanikisha mengi kuliko yeyote aliyemtangulia, huo ndio ukweli wenyewe. JK is not a good president but lets face it ameweka bench mark mpya ya mafanikio. Na mmawaziri hawa hawa tunao wabeza ndio wametufikisha well at least those who perform, unafiki wenu mmbaya sana watanzania waziri wa kilimo ni pigo kutolewa jamaa kajitahidi kushinda wote.

Leo nyie tena mko mstari wa mbele JK ajui kuchagua mbona tunasonga ingawa kazi yenyewe anaifanya kimza what if angekuwa serious. Ndo kusema huko nyuma jamaa waliokuwa wanajifanya serious kumbe walikuwa useless zaidi.
 
Mwigulu na Nkamia ni disappointment.....
 
Tatizo kubwa kwa JK ni kukosa watu wa kufanya nao kazi! Zile nafasi 10 alizopewa za kuteua wabunge Laiti angezitumia vizuri kwa kuwateua watu wenye uwezo kama akina Dr. Ali Mcharazo, Dr. Dau, Dr. Kimei, Dr. Rishedi, Nehemia Mchechu, Dr. Rashid, Dr. Salim, Lisu, Mbowe, Prof. Lipumba, Lyatonga, Lowassa na yule DC aliewacharaza waalimu viboko! kisha akaunda baraza dogo sana la mawaziri! Tanzania yenye neema ingonekana mapema sana
 
Mwigulu na Nkamia ni disappointment.....
Mwigulu kafanyakazi BoT ni experience tosha ya kufanya kazi katika wizara anajulikana kwa performance zake za awali, hilo linamfanya atambulike for his talents na wahusika wajuu kuwa ni option kwa hivyo unashangaa nini kuchaguliwa, timing is everything in life kuna wengi pia wanafahamika mpaka juu lakini wanabaki nyuma kwanza kupima maamuzi habari ndio hiyo.
 
Kuibuka kwa kashfa tena zilizosemwa kwa weledi w ahali ya juu km ilivokuwa report ya mwakyembe kwa chama chenye kupenda funga watu midomo kwa nguvu nyingi ,huku wahanga wa haya mazoezi kisiasa wakialalamika sana..na waliowawajibisha wengine hawana maelezo ya kutosha ni wazi ipo kazi.Wahanga halisi hawan awa kuwasemea kihivyo.


Mara zote Mawaziri wa CCM huwa wanajijua kuwa watakuwa mawaziri, na wengine hubaatika kuchagua wizara.Na pia hujua wakati wanatolewa ...na wanaowatoa ni wale wanaozivia hizo nafasi, achilia mbali maslahi ya wenye CCM.

Jk aliwahi ligusia hili kuwa kuna makuwadi wa uwaziri....CCM haiwezi kuwa stable tena kwani haya makundi na wapiga dili wa uwaziri wamekuwa wengi sana.

Ch akujiuliza ni lini huu umafia ktk nafasi za CCM utaisha?Chama cha mapinduzi kimeonyesha jinsi gani kilivyo cha mapinduzi si yale ya kimaendeleo ila yake Kuchukua madaraka.

Km CDM haikuwepo CCM wangekuwa wamefikia mahali pa kupindua rais...ila kwa sasa wana Too manya parameters to deal with.
 
Mimi nashangaa kwa nini hakumchagua LUSINDE JOSEPH LIVINGSTONE ili na yeye ashike wizara kwani naye anafaa sana kuwa waziri kwenye serikali ya awamu ya nne!
 
Dah kaka umenikumbusha mbali nilikosa somo la Physics likifundishwa na Grahams kisa laptop yake iliibwa na hawa jamaa ingawa najua walikuwa wanaiba data may b lakini baada ya kuchukua hayo makitu wangemrudishia laptop yake ili tufundishwe

Duh mbali sana nimekumbuka, Mwigu mbaya sana hata akiwa mazengo!
 
Usawa wa kuchukua mbawa za blue tuu huu, kwingine huko tunacheza.

I am sorry, uzalendo ushanishinda.
 
Back
Top Bottom