Cabinet reshuffle: This is a disgustingly bad joke, Mr President

Cabinet reshuffle: This is a disgustingly bad joke, Mr President

Hivi Tanzania tumelogwaaaaa au ni Jk na ccm bado wanaota ndoto.. Uchumi wetu hoi baraza la mawaziri hihaaaa linakua siku hata siku sasa ni kulipa fadhilaaaa ni kukosa busara au ni kulipiza kisasi.. Kisasi hiki kinatuumiza sisi Watanzania tulio wengi.. Hivi huyu mtu huwa anashawishika kirahisi hivi au ni jeuri tu.. Kikwete kweli kweli kutuliza namna hii Watanzania tulikukosea nini? Tuambie tujue tujirekebishe. Inauma inaumiza inaliza inasikitisha... Mkulu unaacha kuzingatia shida za Watanzania Elimu mbovu barabara mbovu maji safi hakuna hospitali hakuna kweli kweli hii dhambi itaisha lini Tanzania yangu??????
 
Kamundu,

..wako wa-Tz wengi tu ambao ni competent wangeweza kuteuliwa kutumikia wizara ya fedha.

..nadhani JK mwenyewe haamini kama wizara ya fedha ni muhimu kiasi hicho kulazimisha kuteua watu wenye solid track record kutumikia pale.

NB:

..halafu kitendo cha waandishi wa habari kucheka na kuguna kuhusu baadhi ya teuzi za Raisi, kinaleta taswira isiyo nzuri kwa mteuliwa, washauri wa Raisi, pamoja na Raisi mwenyewe.

cc Mchambuzi, Mdondoaji, NasDaz
Mkuu JokaKuu,
Hivi kweli watu tuna hoja za msingi za kupinga uteuzi wa Mwigulu Nchemba au tu ni kutokana na ukweli kwamba wana-CHADEMA wengi hawampendi Mwigulu Nchemba? Na nani asiyefahamu kwamba wana-CHADEMA wana kila sababu ya kutompenda Nchemba kutokana na ukweli kwamba Nchemba anafanya exactly the same politics CHADEMA does...kinachotokea kwenye chuki za wana-CHADEMA dhidi ya Nchemba ni ule msemo wa kiswahili kwamba Mkuki kwa Nguruwe...Nchemba's and CHADEMA's political operations are Twins brother and sister...tatizo hapo ndipo linapoanzia otherwise mtu alete hapa ushahidi ni namna Nchemba ali-under perform alipokuwa BOT kama Economist I for Four Years. In addition to that, niliwahi kumsikia Nchemba akielezea historia yake...kwa maneno yake mwenyewe; alisema wakati anaanza darasa la kwanza alikuwa hata Kiswahili hafahamu! Nchemba alifika mjini kwa mara ya kwanza baada ya kufaulu form IV, na alikuja Dar wakati akishakuwa mkubwa....anakiri kwamba alishangazwa sana uwingi wa watu jijini! Nimetoa angalizo hilo kuonesha kwamba kuna kila uwezekano kwamab hata kuajiriwa kwake BOT hakukutokana na kubebwa bali alipata ajira kwa halali! Sasa, tuache siasa za CCM na CHADEMA pembeni; je kuna yeyote anayeweza kutueleza utendaji wa Nchemba alipokuwa BOT?
 
Last edited by a moderator:
Ndugu zangu watanzania wengi mitaani walikua na hamu ya kusikia wanaoingia na watokao kwenye baraza jipya la JK. Lakini najaribu kujiuliza kuna jipya kweli kutoka kwa hawa jamaa, yaani tembo watasalimika? wananchi watakuwa salama na hili jeshi la polisi ambalo badala ya kulinda raia lina ua na kunyanyasa? elimu itaboreka kweli? umeme, maji vitapatikana ? au tunabadilishiwa majina tu! na wao wanabadilishana vijiti kwenye kutafuna mali za Taifa?
 
Ndugu zangu watanzania wengi mitaani walikua na hamu ya kusikia wanaoingia na watokao kwenye baraza jipya la JK. Lakini najaribu kujiuliza kuna jipya kweli kutoka kwa hawa jamaa, yaani tembo watasalimika? wananchi watakuwa salama na hili jeshi la polisi ambalo badala ya kulinda raia lina ua na kunyanyasa? elimu itaboreka kweli? umeme, maji vitapatikana ? au tunabadilishiwa majina tu! na wao wanabadilishana vijiti kwenye kutafuna mali za Taifa?
Mkuu jitahidi mara nyingine usiandike pumba sana kama ulizoandika hizi.
 
Mkuu JokaKuu,
Hivi kweli watu tuna hoja za msingi za kupinga uteuzi wa Mwigulu Nchemba au tu ni kutokana na ukweli kwamba wana-CHADEMA wengi hawampendi Mwigulu Nchemba? Na nani asiyefahamu kwamba wana-CHADEMA wana kila sababu ya kutompenda Nchemba kutokana na ukweli kwamba Nchemba anafanya exactly the same politics CHADEMA does...kinachotokea kwenye chuki za wana-CHADEMA dhidi ya Nchemba ni ule msemo wa kiswahili kwamba Mkuki kwa Nguruwe...Nchemba's and CHADEMA's political operations are Twins brother and sister...tatizo hapo ndipo linapoanzia otherwise mtu alete hapa ushahidi ni namna Nchemba ali-under perform alipokuwa BOT kama Economist I for Four Years. In addition to that, niliwahi kumsikia Nchemba akielezea historia yake...kwa maneno yake mwenyewe; alisema wakati anaanza darasa la kwanza alikuwa hata Kiswahili hafahamu! Nchemba alifika mjini kwa mara ya kwanza baada ya kufaulu form IV, na alikuja Dar wakati akishakuwa mkubwa....anakiri kwamba alishangazwa sana uwingi wa watu jijini! Nimetoa angalizo hilo kuonesha kwamba kuna kila uwezekano kwamab hata kuajiriwa kwake BOT hakukutokana na kubebwa bali alipata ajira kwa halali! Sasa, tuache siasa za CCM na CHADEMA pembeni; je kuna yeyote anayeweza kutueleza utendaji wa Nchemba alipokuwa BOT?


..kwa mtizamo wangu wizara ya fedha ni taasisi nyeti mno. siwezi kumshauri mheshimiwa Raisi kuteua mbunge mwenye vitimbi kama Mwigulu Nchemba ku-serve ktk taasisi nyeti kama wizara ya fedha.

..CCM ina wanachama milioni 6, na miongoni mwao naamini wako wenye weledi, na waliotulizana, tofauti na Mwigulu Nchemba, ambao wanaweza kutumikia taifa kama manaibu waziri ktk wizara ya fedha.

..tabia, mihemko, na vitimbi vya Mwigulu Nchemba vinaweza kuvumilika kwa mbunge ambaye ni backbencher. lakini sina uhakika kama ni OK kwa Naibu Waziri wa Fedha kuwa mtu mwenye vitimbi na vituko kiasi kile.

..Now, I know kwamba Mwigulu ni 1st class economics graduate wa UDSM, na pia alikuwa BOT kama mchumi daraja la kwanza. Je, mamlaka za ushauri na uteuzi zimezingatia rekodi hiyo tu na ku-ignore mwenendo wake, na rekodi yake kama mbunge na naibu katibu mkuu wa CCM?

..I mean huu uteuzi unajenga picha gani??
Mdondoaji, Kubwajinga, Nguruvi3, Kilasara, Jasusi
 
Last edited by a moderator:
This a notorious joke...tatizo ni mfumo wa kishkaji, kifisadi na kulindana. Tutegemee maumivu zaidi ndani ya hii miaka 2 iliyobaki kwenye utawala wa JK. Nadhani sasa wananchi wanapaswa kuamka na kubadilisha uomgozi come 2015 general election. Watanzania tusikubali kuendelea kufanywa misukule kwa manufaa ya mafisadi na watumia tumbo wachache. Tuamkeeeee...saa ya ukombozi ni sasa! Kitendo cha kujikomboa kipo ndani ya uwezo wetu, tusije tukafanya mokosa tena kwa kuwaruhusu hawa wanyonyaji kuendelea kufilisi rasilimali za taifa. Tafakari, chukua hatua!
 
Ndugu wana Jf....
Rais Kikwete katika uteuzi wa mawaziri amewaacha katika nafasi zao Mawaziri waliodaiwa au al maarufu "mawaziri mizigo" tena kauli zilizotolewa na Katibu mkuu wa chama Bw Kinana na Katibu mwenezi Bw Nape ambao ni watu wa juu sana katika chama
je, huu ni usikivu? Kama katibu wa Chama anapuuzwa je, sisi wananchi?
Huu ni mtihani mkubwa kwa Kinana na Nape na inadhihirisha kauli ya Msigwa kwamba CCM sasa ni CHAMA CHAKAVU.
 
Wajitathmini kama wanastahili kuendelea kushika nyadhifa hizo wachukue hatua stahiki
 
Ndugu wana Jf....
Rais Kikwete katika uteuzi wa mawaziri amewaacha katika nafasi zao Mawaziri waliodaiwa au al maarufu "mawaziri mizigo" tena kauli zilizotolewa na Katibu mkuu wa chama Bw Kinana na Katibu mwenezi Bw Nape ambao ni watu wa juu sana katika chama
je, huu ni usikivu? Kama katibu wa Chama anapuuzwa je, sisi wananchi?
Huu ni mtihani mkubwa kwa Kinana na Nape na inadhihirisha kauli ya Msigwa kwamba CCM sasa ni CHAMA CHAKAVU.
kuwa na heshima na chama tawala.
 
..kwa mtizamo wangu wizara ya fedha ni taasisi nyeti mno. siwezi kumshauri mheshimiwa Raisi kuteua mbunge mwenye vitimbi kama Mwigulu Nchemba ku-serve ktk taasisi nyeti kama wizara ya fedha.

..CCM ina wanachama milioni 6, na miongoni mwao naamini wako wenye weledi, na waliotulizana, tofauti na Mwigulu Nchemba, ambao wanaweza kutumikia taifa kama manaibu waziri ktk wizara ya fedha.

..tabia, mihemko, na vitimbi vya Mwigulu Nchemba vinaweza kuvumilika kwa mbunge ambaye ni backbencher. lakini sina uhakika kama ni OK kwa Naibu Waziri wa Fedha kuwa mtu mwenye vitimbi na vituko kiasi kile.

..Now, I know kwamba Mwigulu ni 1st class economics graduate wa UDSM, na pia alikuwa BOT kama mchumi daraja la kwanza. Je, mamlaka za ushauri na uteuzi zimezingatia rekodi hiyo tu na ku-ignore mwenendo wake, na rekodi yake kama mbunge na naibu katibu mkuu wa CCM?

..I mean huu uteuzi unajenga picha gani??
Mdondoaji, Kubwajinga, Nguruvi3, Kilasara, Jasusi
JokaKuu,
Kwa hakika nakubaliana na maelezo yako moja kwa moja ingawaje napata shaka pale unaposema kwa kuangalia mwenendo wake bila shaka ukimaanisha kisiasa!! Sasa hebu nisaidie wewe mkuu wangu hususani linapokuja hili suala la siasa za CCM na CHADEMA!! Kwa maelezo yako, Mwigulu Nchemba hafai kabisa lakini unajikita na hoja za minyukano ya kisiasa....siasa zile zile ambazo upande mwingine wa shilingi tunaambiwa Dr. Slaa ana uovu huu, ana uovu ule; Mbowe nae tunaambiwa ana uovu huu, ana uovu ule....Zitto ana uovu huu ana uovu ule; Lema nae ana uovu huu ana uovu....list ni ndefu lakini ukiangalia kwa makini unakuta ni siasa maji taka zilizojikita sana upande wa CCM na CHADEMA!!! Na kimsingi, hilo neno "UOVU" limefunika tuhuma mzito mzito na za kutisha kama vile wizi, ufisadi na mambo mengine!! Tuje hilo la siasa za Kisavimbi tunazoambiwa Mwigulu anatumia....je, viongozi wa CHADEMA wamesalimika katika tuhuma kama hizi? Je, unataka kuniambia kwamba wote hao hawafai au upande mwingine tuchukulie na siasa za majitaka na upande mwingine tu-conclude kwamba huyo ni hasidi asiyefaa kwa Alif wala Be hata kama wote tuhuma zao zinafanana ambazo kimsingi zinatokana na minyukano ya kisiasa??!!
JokaKuu, binafsi nilitarajia ungejikita kwenye hoja ya nini Nchema alifanya alipokuwa Mweka Hazina wa CCM kwavile hiyo post inafanana fanana na jukumu lake hili la sasa....Labda tufahamu ni kwanini alitolewa kule...je, ali-under perform au ni mabadiliko tu ya kawaida? Kupata jibu la moja kwa moja inaweza kuwa ngumu; lakini tunaweza tu kuwa curious kwamba hivi kweli kule angefanya mambo makubwa ya kuimarisha uchumi wa CCM, je kweli angeondolewa mapema vile? Labda hoja ijikite hapo lakini haya mambo ya siasa za CCM na CHADEMA hayawezi kuwa kigezo!
 
Last edited by a moderator:
Inasikitisha Sana, Mtu kama Mwigulu ama Mkamia amefanya nini hasa cha maana kwa Nchi ama yeye binafsi kinachompa sifa ya kuteuliwa Unaibu waziri,
Mh. Mwigulu zaidi ya kufanya BOT mwaka 2006 hadi 2010 (tunaongelea uzoefu wa miaka minne) kama Economist 1 zaidi ya hapo ni siasa tu, ataleta jipya gani kwenye wizara nyeti kama ya Fedha?
Imefikia kipindi sasa katika katiba mpya RAISI apunguziwe nguvu (maana wana zi ABUSE) tuwe na BUNGE imara kwa ajili ya Vetting , candidates wahojiwe maswali magumu walichofanya na kufanikisha katika nafasi zao za awali na wanachotegemea kufanya katika nafasi mpya ikiwezekana wasainishwe Performance Contract, ambapo akiunder perform BUNGE liwe na uwezo wa ku msummon na kumpiga chini pamoja na kufanyiwa backround check za maana .
Tukiendelea kumuachia RAISI (wa chama chochote) kufanya hizi teuzi za kisiasa Tanzania tutabaki kulalamika tu wakati majirani zetu wanasonga mbele.

RAISI Umetuangusha
 
Ndugu wana JF mfumo wa uteuzi wa mawaziri hapa Tanzania umekuwa mfano wa uongozi wa timu za mpira kwani baraza la mawaziri la awali ni mfano wa kikosi tegemezi cha wachezaji wa mpira wa miguu sasa kimeboronga uwanjani na sasa tuna Reserve kuna changes?.
 
Mwigulu ndo naibu waziri KIBUYU wao na NYALANDU..JK katushangaza kwa hawa.
 
..kwa mtizamo wangu wizara ya fedha ni taasisi nyeti mno. siwezi kumshauri mheshimiwa Raisi kuteua mbunge mwenye vitimbi kama Mwigulu Nchemba ku-serve ktk taasisi nyeti kama wizara ya fedha.

..CCM ina wanachama milioni 6, na miongoni mwao naamini wako wenye weledi, na waliotulizana, tofauti na Mwigulu Nchemba, ambao wanaweza kutumikia taifa kama manaibu waziri ktk wizara ya fedha.

..tabia, mihemko, na vitimbi vya Mwigulu Nchemba vinaweza kuvumilika kwa mbunge ambaye ni backbencher. lakini sina uhakika kama ni OK kwa Naibu Waziri wa Fedha kuwa mtu mwenye vitimbi na vituko kiasi kile.

..Now, I know kwamba Mwigulu ni 1st class economics graduate wa UDSM, na pia alikuwa BOT kama mchumi daraja la kwanza. Je, mamlaka za ushauri na uteuzi zimezingatia rekodi hiyo tu na ku-ignore mwenendo wake, na rekodi yake kama mbunge na naibu katibu mkuu wa CCM?

..I mean huu uteuzi unajenga picha gani??
Mdondoaji, Kubwajinga, Nguruvi3, Kilasara, Jasusi

Joka Kuu,

Hizi ndio hasara za kulazimisha mbunge awe waziri matokeo mnateua hadi watoto kuongoza wizara muhimu za nchi. Tukirudi katika cabinet ya Mstahiki Rais ni dalili kuwa ameshachoka anachosubiria ni kumaliza uongozi atuachie nchi. Kwasababu gani nasema hayo mfano Wizara ya Fedha inataka mtu mwenye deep understanding ya uchumi na sio elimu ya utawala na biashara. Utawala na biashara ni branches za economics, kuna branches fedha, masoko ya mitaji, mabenki, uchumi wa baharini, uchumi wa watu (labour economics). Sasa unapomteua mtu anajua a small fraction of uchumi sijui unamaanisha nini?

Na wasaidizi wake ni watu hawana experience ya kutosha katika sekta ya uchumi na fedha. Washauri hawa tunawategemea wamsaidie waziri kwenye kufanya maamuzi. Mwigulu na mwenzie ni kama hakuna msaidizi wote ni junior hawana experience ya kutosha kushika cabinet position. Hata hivyo kwakuwa sheria inaruhusu hakuna makosa ya kiufundi yaliyofanyika.

Ah tukisema tunaambiwa tuna wivu ila alichokisema Professa Lipumba kwa mwenye kuona mbali ataelewa kwanini kasema vile. Mfano mkiwa katika negotiation table washauri watakupa opinion zao wewe kama waziri mwisho wa siku unatakiwa ufanye maamuzi ya msingi yenye manufaa kwa nchi yako. Sasa kama huna weledi wa kutosha katika mambo hayo kitakachotokea utaburuzwa tu. Na ndio maana mawaziri wenye weledi wao kama akina Professor Muhongo au Dr Magufuli wanafanya vizuri kwani wanafanya decision zilizoambatana na ufahamu wa nini kinatarajiwa kutokea in future.

Nilikuwapo!!!!
 
JokaKuu,
Kwa hakika nakubaliana na maelezo yako moja kwa moja ingawaje napata shaka pale unaposema kwa kuangalia mwenendo wake bila shaka ukimaanisha kisiasa!! Sasa hebu nisaidie wewe mkuu wangu hususani linapokuja hili suala la siasa za CCM na CHADEMA!! Kwa maelezo yako, Mwigulu Nchemba hafai kabisa lakini unajikita na hoja za minyukano ya kisiasa....siasa zile zile ambazo upande mwingine wa shilingi tunaambiwa Dr. Slaa ana uovu huu, ana uovu ule; Mbowe nae tunaambiwa ana uovu huu, ana uovu ule....Zitto ana uovu huu ana uovu ule; Lema nae ana uovu huu ana uovu....list ni ndefu lakini ukiangalia kwa makini unakuta ni siasa maji taka zilizojikita sana upande wa CCM na CHADEMA!!! Na kimsingi, hilo neno "UOVU" limefunika tuhuma mzito mzito na za kutisha kama vile wizi, ufisadi na mambo mengine!! Tuje hilo la siasa za Kisavimbi tunazoambiwa Mwigulu anatumia....je, viongozi wa CHADEMA wamesalimika katika tuhuma kama hizi? Je, unataka kuniambia kwamba wote hao hawafai au upande mwingine tuchukulie na siasa za majitaka na upande mwingine tu-conclude kwamba huyo ni hasidi asiyefaa kwa Alif wala Be hata kama wote tuhuma zao zinafanana ambazo kimsingi zinatokana na minyukano ya kisiasa??!!
JokaKuu, binafsi nilitarajia ungejikita kwenye hoja ya nini Nchema alifanya alipokuwa Mweka Hazina wa CCM kwavile hiyo post inafanana fanana na jukumu lake hili la sasa....Labda tufahamu ni kwanini alitolewa kule...je, ali-under perform au ni mabadiliko tu ya kawaida? Kupata jibu la moja kwa moja inaweza kuwa ngumu; lakini tunaweza tu kuwa curious kwamba hivi kweli kule angefanya mambo makubwa ya kuimarisha uchumi wa CCM, je kweli angeondolewa mapema vile? Labda hoja ijikite hapo lakini haya mambo ya siasa za CCM na CHADEMA hayawezi kuwa kigezo!

Nas,

Mara nyingi nimekuwa nakubaliana na wewe ila kwa hili naomba nikukatalie kwasababu mmoja. Kule akiwa kama mweka hazina wa chama siasa ile ni taasisi isiyo ya kiserikali na hivyo model au system ya uendeshaji wake ni tofauti kabisa na position aliyopewa sasa hivi. Naibu Waziri ni cabinet position yenye mamlaka fulani na maamuzi yake yanatuathiri mimi na wewe kwa namna moja nyengine. Position hii inataka mtu mwenye extensive experience katika sekta ya fedha na uchumi. Haya niambie Mwigulu kafanya kazi BOT kama Director hata miaka 3? Adam je? Au alishakuwa MD wa Benki yeyote hapa jijini? Au kuna mmoja wao ashawahi kufanya kazi World Bank? Au Hata kufanya researches nyingi kwenye sekta za uchumi na fedha?

Tuweni serious jamani ndio maana nchi yetu ipo ipo tu!!!!:angry:
 
Sijakubaliana na tamko la ikulu kuwa wananchi hawana sababu juu ya uteuzi wa viongozi mbalimbali hasa baraza la mawaziri unaofanywa na rais! Ukweli ni kuwa wananchi wanayo haki hii kutokana na ukweli kuwa wao ndio wanaomwajiri rais. Kauli hii inaweza kutolewa kwa taifa kama letu tu! ambalo wananchi wake ni bhululu. TAFAKARI.
 
Nas,

Mara nyingi nimekuwa nakubaliana na wewe ila kwa hili naomba nikukatalie kwasababu mmoja. Kule akiwa kama mweka hazina wa chama siasa ile ni taasisi isiyo ya kiserikali na hivyo model au system ya uendeshaji wake ni tofauti kabisa na position aliyopewa sasa hivi. Naibu Waziri ni cabinet position yenye mamlaka fulani na maamuzi yake yanatuathiri mimi na wewe kwa namna moja nyengine. Position hii inataka mtu mwenye extensive experience katika sekta ya fedha na uchumi. Haya niambie Mwigulu kafanya kazi BOT kama Director hata miaka 3? Adam je? Au alishakuwa MD wa Benki yeyote hapa jijini? Au kuna mmoja wao ashawahi kufanya kazi World Bank? Au Hata kufanya researches nyingi kwenye sekta za uchumi na fedha?

Tuweni serious jamani ndio maana nchi yetu ipo ipo tu!!!!:angry:
Mkuu Mdondoaji, hujachunguza kwa makini tu otherwise ungegundua kwamba hata hili nao unaniunga mkono in other way round! Hayo uliyosema ndiyo yanayotakiwa kujadiliwa na lakini wengi wetu tunam-judge Nchemba from hizi political blah blah za CCM na CHADEMA! Tukitaka kumtathimini mtu kwa kuangalia siasa za CHADEMA na CCM basi hakuna hata mmoja aliye msafi anayepaswa kupewa japo uhasibu wa kata! Wakati CHADEMA wanamuona Dr. Slaa na Mbowe ndio wakombozi wa kweli nchi hii; wana-CCM wanawaona watu hao kinyume chake! Wakati CCM wanawaona akina Lowasa,Membe na wengine kwamba ndio wakombozi, wana-CHADEMA wanawaona kinyume chake! Sasa basi, tunapotakiwa kuwatathimini watu tunatakiwa kuangalia ufanisi wao outside political cycle lakini ukiangalia michango ya wengi hapa inajikuta kwa kuangalia inside political ring!
 
Last edited by a moderator:
Akiwa jimboni Busega, katibu mkuu wa Chadema Dr. W. Slaa amemshambulia mbunge wa jimbo hilo Dr. Titus Kamani ambaye pia ni waziri mpya wa wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi akimtaja kuwa ni mzigo mwingine katika baraza jipya. Waziri Kamani alifananishwa kama mzigo wa (furushi la)misumari kwani ni miongoni mwa watu walioshindwa kutekeleza vyema majukumu yao.


Chanzo: Tanzania Daima J. Pili 02/02/1014
 
Back
Top Bottom