Kaka acha tu,nna hasira kufanya uwaziri majaribio..Nkamia ataban magazeti mengi,Mwigulu umeshataja atakayofanya but uteuzi wake ni COMEDY tosha,Malima anapozwa ktk nafasi iliyomletea baba yake shida,Mbona mizigo imebaki? Lazaro Nyalandu yeye anakwenda kumalizia kuhujumu utalii..long live KAGASHEKI.
Hii nchi inaendeshwa kihuni sana..
Wizara nyeti kama hiyo huwezi ukamweka mtu kama Mwigulu. Sina ubaya na Jakaya lakini hapo ameweka siasa mbele zaidi ya weledi
I agree. Mwigulu Nchemba's choice for Naibu W.F. is a bad joke'
Mimi nashukuru amewekwa, na atakuwa anapewa nafasi kubwa ya kujibu maswali ya wabunge, tutarajie matusi.
yeyote anayetetea huu uteuzi lazima ana maslahi binafsi, uteuzi wa ajabu kabisa!
Kuna thread niliandika hapa jf nikizungumzia tetesi za Mwigulu kupewa uwaziri. Niliadika kuwa kutokana na tuhuma kibao zinazomwandama Mwigulu ikiwa ni pamoja na mabomu ya Arusha, umwagiaji watu tindikali, ubambikiaji watu makosa ya kigaidi nk..nk... Nikasema ikiwa JK hakika atamteuwa mtu huyu katika baraza la mawaziri basi itakuwa ni kweli isiyo na shaka kwamba Mwigulu ametuhumiwa kwa matendo aliyotumwa na mwenyekiti wake. Bahati mbaya thread hiyo ilizimwa juu kwa-juu.
Nimalizie kwa kusema CCM na muungano wa Tanzania unaenda kupasukia mikononi mwa J.Kikwete. Huyu rais amekuwa na mzaha mno hata panapohitaji umakini, kama katika kipindi hiki. Uteuzi wake huu wa kuwaingiza Mwigulu Nchemba, Juma Mkamia na kuiacha mizigo mingine ambayo hata Katibu Mkuu wa CCM ameibainisha kuwa inakipotezea umaarufu CCM. Rais amekidharau chama chake na kawadharau watanzania.
Kama rais analeta mzaha kwenye uteuzi wa baraza lake la mawaziri wa inayoitwa Serikali ya Muungano, Je! Ana nia njema kwa muungano wenyewe?
Aidha, uteuziu huu wa Baraza hili la mawaziri umewakatisha tamaa wana CCM na watanzania; pamoja na Abdalahman Kinana na Nape ambao walizunguka Tanzania yote wakiungana na watanzania kwamba baadhi ya mawaziri ni mizigo. Kwa JK hiyo sio mizigo. Mh.Kinana na Nape mpo hapoooo?