Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,768
- 49,934
Serikali ya Tanzania kama zilivyo serikali nyingi za kiafrika zimejaa dhulma. Ni aheri hata hapo zamani utasema kuwa haki za binadamu karibu Dunia nzima zilikuwa zimefifshwa na watawala. Angalia Waarabu walivyowadhulmu waafrika kwenye biashara ya utumwa, Wamarekani dhidi ya Waafrika, Makaburu dhidi ya watu weusi, Urusi, China, Yugoslavia, Romania dhidi ya wananchi wao, n.k.
Kinachoumiza zaidi ni kwamba wenzetu katika mataifa mengine, dhulma hizo za kale zimefutika lakini kwetu zimeendelezwa na kuoteshwa mizizi. Angalia utawala wa Kikwete ulivyowadhulmu watu haki ya kuishi, rejea mauaji ya Mwangosi, kutolewa watu kucha na meno, miswada ya kugandamiza haki za habari, kukataa mamlaka ya wananchi kwa kupitia katiba ya CCM dhidi ya ile ya wananchi, n.k.
Nadhani wakati tunakiri dhulma zilizofanyika zamani, tuangalie kwa umakini juu ya hizi za sasa ambazo kuna wapumbavu wachache mpaka sasa wanazishabikia kisa tu zinafanywa na wapendwa wao dhidi ya mahasimu wao.
Kinachoumiza zaidi ni kwamba wenzetu katika mataifa mengine, dhulma hizo za kale zimefutika lakini kwetu zimeendelezwa na kuoteshwa mizizi. Angalia utawala wa Kikwete ulivyowadhulmu watu haki ya kuishi, rejea mauaji ya Mwangosi, kutolewa watu kucha na meno, miswada ya kugandamiza haki za habari, kukataa mamlaka ya wananchi kwa kupitia katiba ya CCM dhidi ya ile ya wananchi, n.k.
Nadhani wakati tunakiri dhulma zilizofanyika zamani, tuangalie kwa umakini juu ya hizi za sasa ambazo kuna wapumbavu wachache mpaka sasa wanazishabikia kisa tu zinafanywa na wapendwa wao dhidi ya mahasimu wao.
Safi sana kwa kukubali kuwa uhujumu uchumi wa wakati wa Nyerere na Sokoine kuna dhulma ilifanyika.
Wewe ni kati ya wachache sana, kuna watu hawaamini kabisa kama wakati wa utawala Nyerere kungeweza kuwa kumefanyika dhulma na serikali ikaja kukiri bungeni.
Ni ajabu kubwa sana.