Bungeni: Serikali yakiri kudhulumu watu

Bungeni: Serikali yakiri kudhulumu watu

FaizaFoxy

Kwa hiyo bi mkubwa unataka kutuamisnisha kwamba Mwalimu Nyerere, mwasisi wa chama chako chako cha CCM aliwadhurumu watu mali zao ama? sasa bado unasubiri nini kwenye hicho chama cha DHURUMA, si uhamiye UKAWA? mpuuzi mkubwa wewe!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Last edited by a moderator:
samahani jamani,huko mirembe mmewahesabu vizuri wapo wote?isijekuwa kuna mmoja kachoropoka yuko huku anapiga bla bla,wanafiki utawajua tu.leo hii miaka kadhaa ndo wanajifanya kukiri bungeni,ili waonekane wema kwa watu.mbona hawakiri epa,escro,meremeta,kagoda etc?kwanini wasikiri kuwa wizi wao umesababisha watanzania wanaishi kwa tabu?

Naam, hata ichukuwe miaka mingapi, dhulma hailipi, na kilichofanyika bungeni ni kitendo cha kijasiri sana kwa waziri kukiri hilo. Anastahiki sifa.

Jee, wewe huoni kuwa ni kitu chema?
 
Jee, UKAWA ikitokea bahati mbaya mkachukuwa nchi mtaendeleza hili la kurudishia watu mali zao walizodhulumiwa?

Kuchukua nchi kwa UKAWA au opposition kamwe haiwezi kuwa ni BAHATI MBAYA kwanza uelewe hivyo. Kuna nchi kibao zilibadili uongozi ili kuleta mabadiliko,na hiyo ndo hulka ya binadamu. Sometimes binadamu jambo moja hilo hilo huwa linamkinai(kuchoshwa sijui lugha sahihi hapo),lakini ni katika kubadili ladha ya jambo, na hivyo haiwez kuwa ni bahati mbaya kamwe!

Dada FF ukiwa na vazi moja la kaniki kwa miaka kadhaa,ukiichoka na kuamua kununua kitenge cha wax nk haiwez kusemwa umenunua kitenge kwa bahati mbaya.

Nikija kuhusu uzi wako,basi iundwe tume ya maridhiano na usuluhishi ili kila aliyedhulumiwa nchi hii apate haki yake halali!
 
FaizaFoxy

We mama siku hizi umebadilika! Nataka kuamini kile ulichosema kua huna kambi.
 
Last edited by a moderator:
Kuchukua nchi kwa UKAWA au opposition kamwe haiwezi kuwa ni BAHATI MBAYA kwanza uelewe hivyo. Kuna nchi kibao zilibadili uongozi ili kuleta mabadiliko,na hiyo ndo hulka ya binadamu. Sometimes binadamu jambo moja hilo hilo huwa linamkinai(kuchoshwa sijui lugha sahihi hapo),lakini ni katika kubadili ladha ya jambo, na hivyo haiwez kuwa ni bahati mbaya kamwe!

Dada FF ukiwa na vazi moja la kaniki kwa miaka kadhaa,ukiichoka na kuamua kununua kitenge cha wax nk haiwez kusemwa umenunua kitenge kwa bahati mbaya.

Nikija kuhusu uzi wako,basi iundwe tume ya maridhiano na usuluhishi ili kila aliyedhulumiwa nchi hii apate haki yake halali!

Maelezo yako mazuri sana kwa muono wako, sasa jibu swali:

Jee, mtaendeleza hili la kurudishia watu mali zao walizodhulumiwa wakati wa Nyerere na Sokoine kama ilivyoelezwa bungeni, (soma post namba moja)?
 
kwa hiyo bi mkubwa unataka kutuamisnisha kwamba Mwalimu Nyerere, mwasisi wa chama chako chako cha CCM aliwadhurumu watu mali zao ama? sasa bado unasubiri nini kwenye hicho chama cha DHURUMA, si uhamiye UKAWA? mpuuzi mkubwa wewe!!!!!!!!!!!!!!!!

Hakuna langu hapo, hayo ni bungeni.

Jisomee wewe halafu uamini upendacho, mimi sina haja ya kukuaminisha kitu.

Amini upendacho, upo huru, lakini hayo ndiyo yaliyojiri bungeni na serikali imekiri wakati huo wa uhujumu uchumi watu walidhulumiwa. Wakati ho wa Uhujumu uchumi ulikuwa wa kiongozi yupi? Rais nani? na Waziri Mkuu nani?
 
Hilo nalo neno, tunataka nchi isiyodhulumu raia wake, na ikiwa leo wamekiri hili nililoandika nadhani na hayo uyaletayo ukiyawakilisha kwa mbunge wako kwa ushahidi kama alivyofanya huyo aliyetetewa na mbunge wake leo bungeni utakuwa umefanya la maana sana katika kupigania haki.
Serikali hii ya awamu ya nne ndiyo hasa imeweka dhuluma kupitia kodi za kero na zisizolipika kama kipaumbele chake. Nitatoa mifano michache:
1.Kupandisha Motor vehicle licence kutoka elfu 20 hadi laki 3 kwa mwaka
2.kuongeza gharama za fire tingisha kutoka elfu 5 hadi elfu 50 bila sababu yoyote
3. Land rent imeongezwa hadi 300% bila sababu yoyote ya msingi
4. Kunyanganya watu ardhi yao na kuwapa wawekezaji bila fidia au kwa fidia mbuzi
5. kutowalipa wafanyakazi salaries increaments au pesa za likizo
7. kuwabambika wafanya biashara kodi kubwa zaidi ya ile wangetakiwa kulipa kwa kiwango cha mitaji yao
8.kuwauzia wafanya biashara EFDs za elfu 30 kwa laki 8
9. kulipa wafanyakazi mishahara mbuzi
10. Kudhulumu haki ya watu kuandamana, kuchagua wanayempenda
11. etc
 
Hilo ni sawa Ila tatizo ni mleta mada.Kutokana na kile kilichoonekana kuwa ni personal attacks kutoka kwa mleta mada dhidi ya mwalimu hasa katika mlengo wa kidini kupitia nyuzi na comments mbalimbali alizowahi kuwasilisha jamvini,ni vigumu kuondoa hisia hizo sasa!
Nikumbushe pia kuwa dhuluma haikuwahi kukoma,tumeendelea kushuhudia watu wakiporwa maeneo yao na serikali kwa mgongo wa uwekezaji,watu wachache kunufaika na rasilimali za nchi,rushwa na kupeana madaraka kishkaji zote hizo ni dhuluma
 
Jee, UKAWA ikitokea bahati mbaya mkachukuwa nchi mtaendeleza hili la kurudishia watu mali zao walizodhulumiwa?
Hata waliodhurumiwa uhai walipwe tu,2001 Tanzania Visiwani,Akina Mwangosi waliouawa Kimya kimya Mtwara kwenye gesi,Wamasai huko Loriondo wote hawa wafidiwe tu,bila kuangalia dhuruma ilitokea muda gani
 
Hakuna langu hapo, hayo ni bungeni. Jisomee wewe halafu uamini upendacho, mimi sina haja ya kukuaminisha kitu.Amini upendacho, upo huru, lakini hayo ndiyo yaliyojiri bungeni na serikali imekiri wakati huo wa uhujumu uchumi watu walidhulumiwa. Wakati ho wa Uhujumu uchumi ulikuwa wa kiongozi yupi? Rais nani? na Waziri Mkuu nani?
Hii inaonyesha dhuruma chini ya utawala wa CCM haijaanza leo na bila kuing'oa CCM dhuruma haitaisha kwa sababu ilishakwepo na ipo ndani ya chama.Huyo Mbunge ilibidi amalizie kwa kusema CCM itoke ili dhuruma ikome
 
Hii inaonyesha dhuruma chini ya utawala wa CCM haijaanza leo na bila kuing'oa CCM dhuruma haitaisha kwa sababu ilishakwepo na ipo ndani ya chama.Huyo Mbunge ilibidi amalizie kwa kusema CCM itoke ili dhuruma ikome

= dhuluma / dhulma

Kikwete alishatangaza wakati anaongea na wazee wa Dar, hatodhulumiwa mtu.

Na hii siyo mbunge anaekiri kuwa Serikali wakati wa "uhujumu uchumi (Nyerere na Sokoine) ilidhulumu, ni waziri anaekiri hilo, soma vizuri mada. Mbunge alikuwa anamtetea mwananchi wa jimboni kwake.
 
Hata waliodhurumiwa uhai walipwe tu,2001 Tanzania Visiwani,Akina Mwangosi waliouawa Kimya kimya Mtwara kwenye gesi,Wamasai huko Loriondo wote hawa wafidiwe tu,bila kuangalia dhuruma ilitokea muda gani

= waliodhulumiwa
= Loliondo

Hivi una matatizo yepi na hizo "R" na "L"?

Hiyo shule ulienda kusomea ujinga?
 
= dhuluma / dhulmaKikwete alishatangaza wakati anaongea na wazee wa Dar, hatodhulumiwa mtu.Na hii siyo mbunge anaekiri kuwa Serikali wakati wa "uhujumu uchumi (Nyerere na Sokoine) ilidhulumu, ni waziri anaekiri hilo, soma vizuri mada. Mbunge alikuwa anamtetea mwananchi wa jimboni kwake.
Asante kwa.kunisahihisaha,Kutangaza tu haitoshi.Hii CCM ni janga la taifa just imagine toka Enzi za Nyerere wakati anatekeleza ilani ya CCM ilitokea dhuluma mpaka leo bado.Nasema tena kutangaza tu haitoshi kinachotakiwa ni utekelezaji.Wanaodhulumiwa wapo wengi ila hawana pa kusemea sababu ya unyonge wao.
 
Serikali hii ya awamu ya nne ndiyo hasa imeweka dhuluma kupitia kodi za kero na zisizolipika kama kipaumbele chake. Nitatoa mifano michache:
1.Kupandisha Motor vehicle licence kutoka elfu 20 hadi laki 3 kwa mwaka
2.kuongeza gharama za fire tingisha kutoka elfu 5 hadi elfu 50 bila sababu yoyote
3. Land rent imeongezwa hadi 300% bila sababu yoyote ya msingi
4. Kunyanganya watu ardhi yao na kuwapa wawekezaji bila fidia au kwa fidia mbuzi
5. kutowalipa wafanyakazi salaries increaments au pesa za likizo
7. kuwabambika wafanya biashara kodi kubwa zaidi ya ile wangetakiwa kulipa kwa kiwango cha mitaji yao
8.kuwauzia wafanya biashara EFDs za elfu 30 kwa laki 8
9. kulipa wafanyakazi mishahara mbuzi
10. Kudhulumu haki ya watu kuandamana, kuchagua wanayempenda
11. etc

Umeshasema kodi. Sasa kama unaona kodi ni kubwa mwambie mbunge wako akatetee kama alivyofanya huyo mbunge, soma post namba moja, alivyo mtetea mpiga kura wake.

Hilo namba 3 Land Rent leo zimeshushwa na Waziri Lukuvi.

Mada ya hapa ni waliodhulimwa wakato wa uhujumu uchumi, haiongelewi kodi hapa, ukitaka kuongelea kodi funguwa nyuzi tutakuja kujadili. Kumbuka hilo.

Jee, huoni kuwa Serikali imefanya la maana kukiri kuwa wakati wa uhujumu uchumi (Nyerere na Sokoine) kweli watu walidhulumiwa? Na jee, huoni kuwa haina haja ya kuweka limit ya watu kupeleka madai yao? Na pia hauoni kuwa wako waliodhulumiwa wakati wa Azimio la Arusha na wengi wameshindwa kudai kwani Mwinyi aliporuhusu wakadai wengi muda ulikwisha kabla ya kupata hata fursa ya kupata habari kuwa wanaweza kudai mali walizodhulumiwa.

Hebu jitahidi tusichanganye mada, dhulma zipo nyingi sana lakini hapa tujikite kwenye hizo za uhujumu uchumi na azimio la Arusha.
 
Umeshasema kodi. Sasa kama unaona kodi ni kubwa mwambie mbunge wako akatetee kama alivyofanya huyo mbunge, soma post namba moja, alivyo mtetea mpiga kura wake.Hilo namba 3 Land Rent leo zimeshushwa na Waziri Lukuvi.Mada ya hapa ni waliodhulimwa wakato wa uhujumu uchumi, haiongelewi kodi hapa, ukitaka kuongelea kodi funguwa nyuzi tutakuja kujadili. Kumbuka hilo.Jee, huoni kuwa Serikali imefanya la maana kukiri kuwa wakati wa uhujumu uchumi (Nyerere na Sokoine) kweli watu walidhulumiwa? Na jee, huoni kuwa haina haja ya kuweka limit ya watu kupeleka madai yao? Na pia hauoni kuwa wako waliodhulumiwa wakati wa Azimio la Arusha na wengi wameshindwa kudai kwani Mwinyi aliporuhusu wakadai wengi muda ulikwisha kabla ya kupata hata fursa ya kupata habari kuwa wanaweza kudai mali walizodhulumiwa.Hebu jitahidi tusichanganye mada, dhulma zipo nyingi sana lakini hapa tujikite kwenye hizo za uhujumu uchumi na azimio la Arusha.
Hapa mada ni ipi Dhulma au Nyerere na Sokoine?
 
Asante kwa.kunisahihisaha,Kutangaza tu haitoshi.Hii CCM ni janga la taifa just imagine toka Enzi za Nyerere wakati anatekeleza ilani ya CCM ilitokea dhuluma mpaka leo bado.Nasema tena kutangaza tu haitoshi kinachotakiwa ni utekelezaji.Wanaodhulumiwa wapo wengi ila hawana pa kusemea sababu ya unyonge wao.

Naam, na ndiyo maana unaona waziri kaseema kinaga ubaga bungeni aliyedhulumiwa apeleke madai yake kwake na atayafanyia kazi. Kutangaza hakutoshi na waziri ametangaza kuyafanyia kazi hususan kwenye hilo lililoibuliwa la watu waliodhulumiwa wakati wa uhujumu uchumi. Jee, huoni kuwa ni jambo jema hilo?
 
Umeshasema kodi. Sasa kama unaona kodi ni kubwa mwambie mbunge wako akatetee kama alivyofanya huyo mbunge, soma post namba moja, alivyo mtetea mpiga kura wake.

Hilo namba 3 Land Rent leo zimeshushwa na Waziri Lukuvi.

Mada ya hapa ni waliodhulimwa wakato wa uhujumu uchumi, haiongelewi kodi hapa, ukitaka kuongelea kodi funguwa nyuzi tutakuja kujadili. Kumbuka hilo.

Jee, huoni kuwa Serikali imefanya la maana kukiri kuwa wakati wa uhujumu uchumi (Nyerere na Sokoine) kweli watu walidhulumiwa? Na jee, huoni kuwa haina haja ya kuweka limit ya watu kupeleka madai yao? Na pia hauoni kuwa wako waliodhulumiwa wakati wa Azimio la Arusha na wengi wameshindwa kudai kwani Mwinyi aliporuhusu wakadai wengi muda ulikwisha kabla ya kupata hata fursa ya kupata habari kuwa wanaweza kudai mali walizodhulumiwa.

Hebu jitahidi tusichanganye mada, dhulma zipo nyingi sana lakini hapa tujikite kwenye hizo za uhujumu uchumi na azimio la Arusha.
Uko sahihi. Tuko pamoja. Lakini ujumbe wangu angalau umefika.
 
Hapa mada ni ipi Dhulma au Nyerere na Sokoine?

Soma post namba moja halafu wewe jibu upendalo lililopo kwenye hiyo post. Waliodhulumiwa wakati wa uhujumu uchumi, Viongozi wakati huo walikuwa akina nani? labda wewe unawajuwa zaidi utujuze.
 
Uko sahihi. Tuko pamoja. Lakini ujumbe wangu angalau umefika.

Ujumbe wako umefika wrong place, laiti ungeliufungulia nyuzi ungekuwa na mashiko zaidi. Kwa kuuweka hapa inaonekana kama unataka kuibadili mada na kututaka tuachane na hii mada ya waliodhulumiwa wakati wa uhujumu uchumi. Labda hauna uwajuao waliodhulimiwa wakati huo ndiyo maana haikugusi.
 
Back
Top Bottom