Bungeni: Serikali yakiri kudhulumu watu

Bungeni: Serikali yakiri kudhulumu watu

Soma post namba moja halafu wewe jibu upendalo lililopo kwenye hiyo post. Waliodhulumiwa wakati wa uhujumu uchumi, Viongozi wakati huo walikuwa akina nani? labda wewe unawajuwa zaidi utujuze.
Viongozi walikuwa lazima walikuwa watekeleza Ilani ya CCM,sidhani kama walikuwa NLD? Nadhani mdau alitaka kusema hiyo dhulma isiishie huko tu kwenye uhujumu uchumi ije hata kwenye dhulma za Sasa isije ikatokea watawala wa sasa wakafa baada ya miaka arobaini au ishirini watu waanze kulalamika kuwa walidhulmiwa
 
Nilikuwa nafikiri we ni perfect 100% kumbe nawe shule ulienda kusomea ujinga

Kuna typo na kuna kukosea "R" na "L" kama ulivyofanya wewe huko juu, tatizo lako ni kubwa sana Tanzania, nnajuwa sababu shule ulienda kusomea ujinga na si tatizo la typo.
 
Kuna typo na kuna kukosea "R" na "L" kama ulivyofanya wewe huko juu, tatizo lako ni kubwa sana Tanzania, nnajuwa sababu shule ulienda kusomea ujinga na si tatizo la typo.
Hilo lako ni ukosefu wa umakini,yaani hakuna proof reading.Huo ni ujinga pia kutuma kazi bila kuhakiki
 
Hilo lako ni ukosefu wa umakini,yaani hakuna proof reading.Huo ni ujinga pia kutuma kazi bila kuhakiki

Sawa kabisa wala hujakosea. Sasa hebu nieleze, unaonaje hili:

Kwanza nnaisifu sana Serikali ya awamu hii kwa kukiri hilo bungeni "live" kuwa kweli kuna dhuluma ilitendeka. Kwa hakika Serikali kukiri hilo kosa ni ujasiri mkubwa sana na ni njia nzuri sana ya wananchi waliodhulumiwa kuweza kurudisha imani kwa Serikali yao na sasa wapokelewe na kurudishiwa mali zao na kusiwe na hili suala la kuchelewa.
 
Sawa kabisa wala hujakosea. Sasa hebu nieleze, unaonaje hili:Kwanza nnaisifu sana Serikali ya awamu hii kwa kukiri hilo bungeni "live" kuwa kweli kuna dhuluma ilitendeka. Kwa hakika Serikali kukiri hilo kosa ni ujasiri mkubwa sana na ni njia nzuri sana ya wananchi waliodhulumiwa kuweza kurudisha imani kwa Serikali yao na sasa wapokelewe na kurudishiwa mali zao na kusiwe na hili suala la kuchelewa.
Nitaisifu serikali siku wakipata haki yao sio siku ya ahadi tulishazichoka hizo ahadi.
 
Nitaisifu serikali siku wakipata haki yao sio siku ya ahadi tulishazichoka hizo ahadi.

Wapo waliokwisha lipwa, ndiyo maana nikakwambia kwenye post namba moja, pitia hansard kwa kuyaelewa zaidi.

Jee, na hilo la watu kudhulumiwa wakati wa uhujumu uchumi (Nyerere na Sokoine) unalilaani au kwako ni sawa tu?
 
Wapo waliokwisha lipwa, ndiyo maana nikakwambia kwenye post namba moja, pitia hansard kwa kuyaelewa zaidi.Jee, na hilo la watu kudhulumiwa wakati wa uhujumu uchumi (Nyerere na Sokoine) unalilaani au kwako ni sawa tu?
Hakuna mtu anayefurahia dhulma
 
Hivi alikuwa specific kuwa waende waliodhulumiwa awamu ya Kwanza tu?je,waliodhulumiwa kuanzia 2006?
 
Naam, hata ichukuwe miaka migapi, dhulma hailipi, na kilichoafanyika bungeni ni kitendo cha kijasiri sana kwa waziri kukiri hilo. Ansatahiki sifa.

Jee, wewe huoni kuwa ni kitu chema?

mwizi hana jema,anarudisha shilingi kumi huku akiiba elfu moja
 
Sasa mimi na Nyerere inahusu nini wakati hilo jambo limeongelewa bungeni?

Hivi unaelewa unachokisoma?

Sidhani kama kuna anayepinga sana usemacho bali dhamira yako iliyofichika. Hii serekali unayoisifia leo ndio imeingia madarakani? Wazee wa A. Mashariki si walikuwa wanapigwa na serekalj hiihii kisa madai yao? Mwaka huu wa uchaguzi wabunge wote wa ccm wanaongea kama wa upinzani, serekali inajifanya malaika kwa umma. Bado unadhani watu ni wajinga mama? Mahakama iliamua kuwe na mgombea binafsi serekali ikagoma, je leo iko tayari kutekeleza? Unafiki kwa umri huo haupendezi.
 
Jee, UKAWA ikitokea bahati mbaya mkachukuwa nchi mtaendeleza hili la kurudishia watu mali zao walizodhulumiwa?
SIO BAHATI MBAYA KWA ALIYE NA NIA YA KUONDOA DHURUMA ukawa kuchukua nchi.!
na kura yako tunaitaka UKAWA na kwa sababu hatuungi mkono dhuruma, kila aliyeathirika na hili should be promptly and fairly compasated the same regardless who are you! Lete kura yako ukawa na kwa kuwa dhuruma zilifanya na ccm they should be answerable and liable regardless time bared!
 
SIO BAHATI MBAYA KWA ALIYE NA NIA YA KUONDOA DHURUMA ukawa kuchukua nchi.!
na kura yako tunaitaka UKAWA na kwa sababu hatuungi mkono dhuruma, kila aliyeathirika na hili should be promptly and fairly compasated the same regardless who are you! Lete kura yako ukawa na kwa kuwa dhuruma zilifanya na ccm they should be answerable and liable regardless time bared!

= dhuluma / dhulma
= dhuluma / dhulma
= dhuluma / dhulma

Hebu waambie wakubwa wako wa ukawa waliweke kwenye sera zao au japo waliongelee kama walivyoliongelea mbunge na waziri wa CCM.
 
Kuna dhuruma Kwa waliokuwa watumishi. Waliodhurumiwa na serikali kwa kuwaondoa ktk ajira ghafla Kwa ujira kidogo na kuwatelekeza. Hili ilikuwa wakati wa maboresho ya serikali za mitaa na serikali kuu.Walikuja na operation iliyokuwa na jina retrenchment. Kukafuatia na kuanzishwa kwa idara za serikali kuwa wakala. Malaki ya watumishi waliondolewa ktk ajira zao bila hiari zao na bila malipo mazuri. Waliokuwa Kwa mkataba wa kudumu wakaingzwa ktk mfumo wa kulipwa pesheni ambapo hadi sasa wanalipwa kutoka hazina pesa kiduchu zsizo endana na maisha pamoja na uzee wao.
 
Kuna dhuruma Kwa waliokuwa watumishi. Waliodhurumiwa na serikali kwa kuwaondoa ktk ajira ghafla Kwa ujira kidogo na kuwatelekeza. Hili ilikuwa wakati wa maboresho ya serikali za mitaa na serikali kuu.Walikuja na operation iliyokuwa na jina retrenchment. Kukafuatia na kuanzishwa kwa idara za serikali kuwa wakala. Malaki ya watumishi waliondolewa ktk ajira zao bila hiari zao na bila malipo mazuri. Waliokuwa Kwa mkataba wa kudumu wakaingzwa ktk mfumo wa kulipwa pesheni ambapo hadi sasa wanalipwa kutoka hazina pesa kiduchu zsizo endana na maisha pamoja na uzee wao.

= dhuluma
= waliodhulumiwa.

Hayo ni mambo ya ajira. Mada hii haiyaongelei hayo kabisa. Jee unajuwa "uhujumu uchumi" ilikuwa ni nini?

Hakuna ambae anaajiriwa Serikalini au popote pale akaambiwa hii ni kazi ya maisha yako yote labda wale wa dikteta wanosema wao ni Marais wa maisha na wao wenyewe hawana uhakika, lini watapinduliwa.

Na hakuna anaeajiriwa seikali ya Tanzania hii asiyejuwa pensheni za serikali zikoje. kKwa hio apo hakuna dhuluma hapo kuna maelewano tu.

Mada hapa ni nyingine kabisa.
 
Sidhani kama kuna anayepinga sana usemacho bali dhamira yako iliyofichika. Hii serekali unayoisifia leo ndio imeingia madarakani? Wazee wa A. Mashariki si walikuwa wanapigwa na serekalj hiihii kisa madai yao? Mwaka huu wa uchaguzi wabunge wote wa ccm wanaongea kama wa upinzani, serekali inajifanya malaika kwa umma. Bado unadhani watu ni wajinga mama? Mahakama iliamua kuwe na mgombea binafsi serekali ikagoma, je leo iko tayari kutekeleza? Unafiki kwa umri huo haupendezi.

Sasa umekuwa Mungu (astaghafurullah) unaejuwa dhamira za watu?

Wazee wa Afrika Mashariki kama kudhulumiwa walidhulumiwa na nani? ni utawala upi Afrika Mashariki ilikufa? sasa kasome tena mada uone ni utawala upi uliofanya dhuluma inayoonegelewa kwenye hii mada, kisha utajaza mwenyewe.

Mgombea binafsi kama mahakama imeamuwa, Jee, wewe umeshatangaza kugombeaa binasi ukakataliwa? na utapokatakiwa nendaa tena mahakamani, ulizuwiliwa na nani?

Vipi lakini unaonaje wewe, dhuluma ilifanyika kweli wakati wa uhujumu uchumi katika utawala wa Nyerere na Sokoine au awamu hii inawaonea tu kwa kukiri kweli watu walidhulumiwa?
 
Hakuna mtu anayefurahia dhulma

Safi sana kwa kukubali kuwa uhujumu uchumi wa wakati wa Nyerere na Sokoine kuna dhulma ilifanyika.

Wewe ni kati ya wachache sana, kuna watu hawaamini kabisa kama wakati wa utawala Nyerere kungeweza kuwa kumefanyika dhulma na serikali ikaja kukiri bungeni.

Ni ajabu kubwa sana.
 
Jee, UKAWA ikitokea bahati mbaya mkachukuwa nchi mtaendeleza hili la kurudishia watu mali zao walizodhulumiwa?

Dhuluma bado ni kubwa serikali yako unayoipenda bado inatudhulumu wananchi kwenye huduma kama vile maji na hospital yaaani ukienda hospital hakuna Dawa wala nini Pesa za umma wanagawana tu kwenye ma ufisadi yao wanasamehe kodi huku nyuma ya pazia wanapiga 10% sijui kama unaliona hilo serikali ya ccm ya sasa ni tofauti sana na ile ya nyerere najua ndani ya moyo wako utaelewa hilo ndio maana tofauti ya pato kati ya walionacho na wasionacho ni kubwa mno na linadhidi kuongezeka.
 
Back
Top Bottom