Bungeni: Serikali yakiri kudhulumu watu

Bungeni: Serikali yakiri kudhulumu watu

Muongo akishazoeleka kwa kusema uwongo, basi siku akisema ukweli kuna watu wanadhani anatakiwa kupongezwa.. Kupongezwa atapongezwa endapo tu ... Atalipa waliodhurumiwa kwenye kila nyanja
- Uhujumu uchumi,
- Mabomu ya mbagala na gongolamboto
- Waliofukiwa na kutolipwa fidia kwenye uanzishwaji wa mgidi wa Bulyanhulu
- Walionyang'anywa haki ya ardhi sehemu mbalimbali hapa TZ


= waliodhulumiwa
 
Watu hawa sina hamu nao kabisa,hata mimi walinidhulumu pension yangu.MUNGU NDIYE ATAKAYEKUWA MWAMUZI.
FaizaFoxy

DHULUMA ZINGINE PIA ZIFIDIWE, DHULUMA ILIYOTENDEKA ZANZIBAR mwaka 1995 na mwaka 2000 Nazo ziangaliwe Upya zisiwe tu za kuhujumu Uchumi. Hata Kuhujumu Haki ya Mpiga Kura wa zanzibar lazima ifidiwe.
 
Last edited by a moderator:
Hapa wana CCM wenzako wanakukimbia, ni kweli unachokinena na ndiyo maana huwa nasema kuna dhuluma kubwa sana chini ya utawala wa CcM
 
Leo nimeona "live" katika bunge wakati wa majumuisho ya bajeti ya Wizara ya fedha, kuna mbunge (sikumbuki jina) alisimama kumtetea mtu wa jimboni kwake kuwa alidhulumiwa wakati wa "uhujumu uchumi" na amekuwa anahangaishwa kulipwa madai yake na mwisho akaambiwa amechelewa. Mbunge huyo alisema kama kuchelewa alikuwa hajachelewa kwani anadai siku zote na ushahidi upo. Ndipo aliposimama Naibu Waziri wa Fedha na kumtaka huyo mbunge kuwa awasilishe madai yake yote kwake na karatasi zake zote na anaahidi kushughulikia hilo na kuhakikisha haki inapatikana kwani ni kweli wengi walidhulumiwa wakati wa (operesheni) ya Uhujumu Uchumi.

Ikumbukwe kuwa hii operesheni ilifanyika wakati marehemu Nyerere akiwa Rais na marehemu Sokoine akiwa Waziri Mkuu.

Huyo mbunge alisema kuwa wapo pia waliolipwa kwa kuonekana kweli walidhulumiwa.

Sasa nnajiuliza, na tusichangie hili kwa jazba, Ikiwa serikali inakiri tena bungeni, watu walidhulumiwa, jee ni hatua gani wale waliodhulumiwa wazee ambao wameshakufa ili kudai haki zao, si kurudishiwa tu mali zao na hukumu ipi "posthumous" inayoweza kutolewa kwa waliodhulumu?

Tukumbuke watu walidhulumiwa si katika uhujumu uchumi tu, kama Serikali ilivyokiri leo bungeni bali pia kuna watu waliodhulumiwa wakati wa Azimio la Arusha. Nao wakati wa Mwinyi waliambiwa wakadai lakini kwa kuwa haikutangazwa sana wengine walipoenda wakaambiwa wamechelewa, hivi haki ya mtu kweli ina kuchelewa katika kuidai?

Kwanza nnaisifu sana Serikali ya awamu hii kwa kukiri hilo bungeni "live" kuwa kweli kuna dhuluma ilitendeka. Kwa hakika Serikali kukiri hilo kosa ni ujasiri mkubwa sana na ni njia nzuri sana ya wananchi waliodhulumiwa kuweza kurudisha imani kwa Serikali yao na sasa wapokelewe na kurudishiwa mali zao na kusiwe na hili suala la kuchelewa.

Naipongeza Serikali kwa hilo, na lisiishie hapo watutangazie tuanzie wapi? Kwani nnaamini si wengi waliosikia hilo bungeni kwani si wengi wanaotazama bunge.

Nawaomba na waandishi wa habari walitangaze hili, kwani ni jambo la kheri kubwa sana, hakuna dua inayopokelewa haraka kama ya mwenye kudhulumiwa, pengine haya majanga yote yanayotupata Tanzania ni kwa hizo dhuluma zilizofanywa na viongozi wetu huko nyuma, ni wakati muafaka Serikali kukiri hilo na kuanza kufanya toba na kurudisha imani ya wananchi kwa Serikali yao.

Hansard zitakuwa zipo kwa wanaotaka kuelewa zaidi.

Ahsante Serikali kwa kuliweka wazi hilo.
Hivi wale wafanyakazi wa iliyokuwa juuia ya afrika mashariki wamelipwa?
 
Leo nimeona "live" katika bunge wakati wa majumuisho ya bajeti ya Wizara ya fedha, kuna mbunge (sikumbuki jina) alisimama kumtetea mtu wa jimboni kwake kuwa alidhulumiwa wakati wa "uhujumu uchumi" na amekuwa anahangaishwa kulipwa madai yake na mwisho akaambiwa amechelewa. Mbunge huyo alisema kama kuchelewa alikuwa hajachelewa kwani anadai siku zote na ushahidi upo. Ndipo aliposimama Naibu Waziri wa Fedha na kumtaka huyo mbunge kuwa awasilishe madai yake yote kwake na karatasi zake zote na anaahidi kushughulikia hilo na kuhakikisha haki inapatikana kwani ni kweli wengi walidhulumiwa wakati wa (operesheni) ya Uhujumu Uchumi.

Ikumbukwe kuwa hii operesheni ilifanyika wakati marehemu Nyerere akiwa Rais na marehemu Sokoine akiwa Waziri Mkuu.

Huyo mbunge alisema kuwa wapo pia waliolipwa kwa kuonekana kweli walidhulumiwa.

Sasa nnajiuliza, na tusichangie hili kwa jazba, Ikiwa serikali inakiri tena bungeni, watu walidhulumiwa, jee ni hatua gani wale waliodhulumiwa wazee ambao wameshakufa ili kudai haki zao, si kurudishiwa tu mali zao na hukumu ipi "posthumous" inayoweza kutolewa kwa waliodhulumu?

Tukumbuke watu walidhulumiwa si katika uhujumu uchumi tu, kama Serikali ilivyokiri leo bungeni bali pia kuna watu waliodhulumiwa wakati wa Azimio la Arusha. Nao wakati wa Mwinyi waliambiwa wakadai lakini kwa kuwa haikutangazwa sana wengine walipoenda wakaambiwa wamechelewa, hivi haki ya mtu kweli ina kuchelewa katika kuidai?

Kwanza nnaisifu sana Serikali ya awamu hii kwa kukiri hilo bungeni "live" kuwa kweli kuna dhuluma ilitendeka. Kwa hakika Serikali kukiri hilo kosa ni ujasiri mkubwa sana na ni njia nzuri sana ya wananchi waliodhulumiwa kuweza kurudisha imani kwa Serikali yao na sasa wapokelewe na kurudishiwa mali zao na kusiwe na hili suala la kuchelewa.

Naipongeza Serikali kwa hilo, na lisiishie hapo watutangazie tuanzie wapi? Kwani nnaamini si wengi waliosikia hilo bungeni kwani si wengi wanaotazama bunge.

Nawaomba na waandishi wa habari walitangaze hili, kwani ni jambo la kheri kubwa sana, hakuna dua inayopokelewa haraka kama ya mwenye kudhulumiwa, pengine haya majanga yote yanayotupata Tanzania ni kwa hizo dhuluma zilizofanywa na viongozi wetu huko nyuma, ni wakati muafaka Serikali kukiri hilo na kuanza kufanya toba na kurudisha imani ya wananchi kwa Serikali yao.

Hansard zitakuwa zipo kwa wanaotaka kuelewa zaidi.

Ahsante Serikali kwa kuliweka wazi hilo.
Wewe dada huwa unaipendelea sana CCM na hata sasa bado unaisifu serikali kwa kukiri dhuruma. suala hapa si kukiri bali hatua wanazochukua dhidi ya dhuruma hizo. CCM na serikali zake wamezoea kudhurumu watu, awamu zote. Wakati wa uhuru na azimio la arusha taasisi zetu za kikristo zilitaifishwa na baada ya miaka mingi wakarudisha baadhi ya magofu waliyoshindwa kuyaendeleza. Mwaka 1974-1975 tulibobolewa nyumba zetu na kulazimishwa kwenda mbugani tukiacha nyuma mashamba na malizingine. Wengine waliuawa Enzi zile za chama kushika hatamu. Mwaka 1977 jumuia ya afrika mashariki ilivunjwa na nchi zingine waliwalipa wadai wao isipokuwa kwetu. Kaka yangu kafa mwaka 2005 hajapata haki zake kutoka serikali hizi sikivu na chama kikongwe kwa mizengwe. Kabla ya mwaka 1992 serikali na chama vilitulazimisha kufanya kazi kadhaa na kutoa michango ya lazima kama ujenzi wa shule,ofisi na viwanja vya michezo na leo hii wanadai ni vya CCM ilhali wametudhurumu tu. baada ya kulipa kodi na kuitumia kujenga chuo cha tanesco, serikali ikaamua kutudhurumu watu wa dini zingine na wakawakabidhi wa wa dini moja taasisi tuliyoitolea jasho sote, hata wasio na dini. Kodi inatolewa na wote lakini hata sasa ufadhili wa kielimu na mikopo hutolewa kwa upendeleo kwa wa daraja la kwanza (na pili kwa watu wa jinsia moja na kuiacha nyingine ikose haki ya kikatiba ya kupata elimu)Muda hautoshi kusema vile CCM na serikali yake walivyokubuhu kwa dhuruma kwani hata askali wake wa polisi walipomlipua pasipo huruma yule mwandishi Daudi Mwangosi haijakiri kuhusika kwakena kuifidia familia ya marehemu ila kamanda akapadishwa cheo. Hongera CCM, hongera Faizafox.
 
Leo nimeona "live" katika bunge wakati wa majumuisho ya bajeti ya Wizara ya fedha, kuna mbunge (sikumbuki jina) alisimama kumtetea mtu wa jimboni kwake kuwa alidhulumiwa wakati wa "uhujumu uchumi" na amekuwa anahangaishwa kulipwa madai yake na mwisho akaambiwa amechelewa. Mbunge huyo alisema kama kuchelewa alikuwa hajachelewa kwani anadai siku zote na ushahidi upo. Ndipo aliposimama Naibu Waziri wa Fedha na kumtaka huyo mbunge kuwa awasilishe madai yake yote kwake na karatasi zake zote na anaahidi kushughulikia hilo na kuhakikisha haki inapatikana kwani ni kweli wengi walidhulumiwa wakati wa (operesheni) ya Uhujumu Uchumi.

Ikumbukwe kuwa hii operesheni ilifanyika wakati marehemu Nyerere akiwa Rais na marehemu Sokoine akiwa Waziri Mkuu.

Huyo mbunge alisema kuwa wapo pia waliolipwa kwa kuonekana kweli walidhulumiwa.

Sasa nnajiuliza, na tusichangie hili kwa jazba, Ikiwa serikali inakiri tena bungeni, watu walidhulumiwa, jee ni hatua gani wale waliodhulumiwa wazee ambao wameshakufa ili kudai haki zao, si kurudishiwa tu mali zao na hukumu ipi "posthumous" inayoweza kutolewa kwa waliodhulumu?

Tukumbuke watu walidhulumiwa si katika uhujumu uchumi tu, kama Serikali ilivyokiri leo bungeni bali pia kuna watu waliodhulumiwa wakati wa Azimio la Arusha. Nao wakati wa Mwinyi waliambiwa wakadai lakini kwa kuwa haikutangazwa sana wengine walipoenda wakaambiwa wamechelewa, hivi haki ya mtu kweli ina kuchelewa katika kuidai?

Kwanza nnaisifu sana Serikali ya awamu hii kwa kukiri hilo bungeni "live" kuwa kweli kuna dhuluma ilitendeka. Kwa hakika Serikali kukiri hilo kosa ni ujasiri mkubwa sana na ni njia nzuri sana ya wananchi waliodhulumiwa kuweza kurudisha imani kwa Serikali yao na sasa wapokelewe na kurudishiwa mali zao na kusiwe na hili suala la kuchelewa.

Naipongeza Serikali kwa hilo, na lisiishie hapo watutangazie tuanzie wapi? Kwani nnaamini si wengi waliosikia hilo bungeni kwani si wengi wanaotazama bunge.

Nawaomba na waandishi wa habari walitangaze hili, kwani ni jambo la kheri kubwa sana, hakuna dua inayopokelewa haraka kama ya mwenye kudhulumiwa, pengine haya majanga yote yanayotupata Tanzania ni kwa hizo dhuluma zilizofanywa na viongozi wetu huko nyuma, ni wakati muafaka Serikali kukiri hilo na kuanza kufanya toba na kurudisha imani ya wananchi kwa Serikali yao.

Hansard zitakuwa zipo kwa wanaotaka kuelewa zaidi.

Ahsante Serikali kwa kuliweka wazi hilo.

Utakufa kibudu kushindana na Hayati Mwl JK Nyerere ww mwana mama.
 
unawadhulumu watu halafu unajidai kuwalipa uonekane mzuri,kweli utawala ni mtamu
 
FaizaFoxy, talking of dhulma, je unaonaje ukiishauri Serikali kuhakikisha mali za wananchi zilizodhulumiwa na CCM (nyumba, viwanja, mashirika ya Umma hadi vyombo vya dola) zinarudishwa? Oops! nilikuwa nasahau, serikali yenyewe inamilikiwa kiharamu na hilo hilo genge la wezi, Chama cha Mapinduzi.
 
Last edited by a moderator:
Nyerere atabaki kuwa ndo baba wa taifa hili, hizo chuki zako utaingia nazo kaburini. Nakusifu kwa jitihada zako za kumkweza vasco dagama
 
Leo nimeona "live" katika bunge wakati wa majumuisho ya bajeti ya Wizara ya fedha, kuna mbunge (sikumbuki jina) alisimama kumtetea mtu wa jimboni kwake kuwa alidhulumiwa wakati wa "uhujumu uchumi" na amekuwa anahangaishwa kulipwa madai yake na mwisho akaambiwa amechelewa. Mbunge huyo alisema kama kuchelewa alikuwa hajachelewa kwani anadai siku zote na ushahidi upo. Ndipo aliposimama Naibu Waziri wa Fedha na kumtaka huyo mbunge kuwa awasilishe madai yake yote kwake na karatasi zake zote na anaahidi kushughulikia hilo na kuhakikisha haki inapatikana kwani ni kweli wengi walidhulumiwa wakati wa (operesheni) ya Uhujumu Uchumi.

Ikumbukwe kuwa hii operesheni ilifanyika wakati marehemu Nyerere akiwa Rais na marehemu Sokoine akiwa Waziri Mkuu.

Huyo mbunge alisema kuwa wapo pia waliolipwa kwa kuonekana kweli walidhulumiwa.

Sasa nnajiuliza, na tusichangie hili kwa jazba, Ikiwa serikali inakiri tena bungeni, watu walidhulumiwa, jee ni hatua gani wale waliodhulumiwa wazee ambao wameshakufa ili kudai haki zao, si kurudishiwa tu mali zao na hukumu ipi "posthumous" inayoweza kutolewa kwa waliodhulumu?

Tukumbuke watu walidhulumiwa si katika uhujumu uchumi tu, kama Serikali ilivyokiri leo bungeni bali pia kuna watu waliodhulumiwa wakati wa Azimio la Arusha. Nao wakati wa Mwinyi waliambiwa wakadai lakini kwa kuwa haikutangazwa sana wengine walipoenda wakaambiwa wamechelewa, hivi haki ya mtu kweli ina kuchelewa katika kuidai?

Kwanza nnaisifu sana Serikali ya awamu hii kwa kukiri hilo bungeni "live" kuwa kweli kuna dhuluma ilitendeka. Kwa hakika Serikali kukiri hilo kosa ni ujasiri mkubwa sana na ni njia nzuri sana ya wananchi waliodhulumiwa kuweza kurudisha imani kwa Serikali yao na sasa wapokelewe na kurudishiwa mali zao na kusiwe na hili suala la kuchelewa.

Naipongeza Serikali kwa hilo, na lisiishie hapo watutangazie tuanzie wapi? Kwani nnaamini si wengi waliosikia hilo bungeni kwani si wengi wanaotazama bunge.

Nawaomba na waandishi wa habari walitangaze hili, kwani ni jambo la kheri kubwa sana, hakuna dua inayopokelewa haraka kama ya mwenye kudhulumiwa, pengine haya majanga yote yanayotupata Tanzania ni kwa hizo dhuluma zilizofanywa na viongozi wetu huko nyuma, ni wakati muafaka Serikali kukiri hilo na kuanza kufanya toba na kurudisha imani ya wananchi kwa Serikali yao.

Hansard zitakuwa zipo kwa wanaotaka kuelewa zaidi.

Ahsante Serikali kwa kuliweka wazi hilo.
Hii ni mipango yote ya CCM ya CHUKUA CHAKO MAPEMA maana wengi wao ni kizazi cha wale walokuwa wamesubiri mwalimu afe waanzishe tungo za kumnadi Vibaya mwalimu. Tunawajua na hii yote haiwezi kubadilisha dhumuni la taifa alotaka kulijenga.

Hata hivi leo Maskini WAKULIMA na WAFANYAKAZI wanadhulumiwa na wanasiasa kwa kila hali na hatuelewi watarudishiwa vipi nchi yao. Unadhani kama mwalimu angekuwepo leo Lowassa angepata hata nafasi ya kuhubiria UFISADI na akapata wafuasi?
 
Hii ni mipango yote ya CCM ya CHUKUA CHAKO MAPEMA maana wengi wao ni kizazi cha wale walokuwa wamesubiri mwalimu afe waanzishe tungo za kumnadi Vibaya mwalimu. Tunawajua na hii yote haiwezi kubadilisha dhumuni la taifa alotaka kulijenga.

Hata hivi leo Maskini WAKULIMA na WAFANYAKAZI wanadhulumiwa na wanasiasa kwa kila hali na hatuelewi watarudishiwa vipi nchi yao. Unadhani kama mwalimu angekuwepo leo Lowassa angepata hata nafasi ya kuhubiria UFISADI na akapata wafuasi?

Kwani hayupo? Membe anasema kamuona alivyoenda Mwitongo na kamkabidhi viatu vyake.

Hapo sasa!
 
Sina haja ya kumwuliza baba yangu, nilikuwepo.

Kujua kusoma na kuandika vizuri ndiyo iliepusha njaa vijijini au unakataa kulikuwa hamna njaa kwa kuwa nimeleta picha ya juzi Kama mfano wa njaa?

Tumia ubongo kidogo.

Nilikuwa najibu hoja yako kuwa Nyerere "aliwakomesha" warabu koko. Mjinga ndiyo hajui Tanzania bado kuna njaa vijijini.Mimi nilikuwa sipo hapo kabisa.

Nataka kukuonyesha njaa ya kijijini. Unitafutie ya wahindi na "warabu koko" wa Tanzania "waliokomeshwa" kama hawa baada ya kudhulumiwa mali zao na Nyerere.

Siku nyingine nikitaka kuonyesha mfano wa kahawa, nitaitafuta kahawa ya Africafe, kwa sababu huenda utaikata kahawa ya Nescafé kama mfano wa "kahawa".

Kazi ipo.


Fool at 40,
Ubongo wako unafikiria kukomeshwa ni kufa njaa? Nyerere alikuwa mtu wa Mungu na alichofanya ni kuwapunguzia wale wenye ziada ya kukufuru na kuwapelekea wasionacho, bahati mbaya najaribu kumwelewesha mtu uliyekulia mtaani ktk nyumba za msajili hivyo maisha real ya kijijini huyajui mpaka uombe picha. Kwa taarifa yako ni Nyerere pekee aliyeweza kuweka usawa wa kusomesha waTZ wote, mradi uko bright. Nyie k.oko si hamjui hata faida ya kusoma?
 
FaizaFoxy

Samahani jamani,huko mirembe mmewahesabu vizuri wapo wote?isijekuwa kuna mmoja kachoropoka yuko huku anapiga bla bla,wanafiki utawajua tu.leo hii miaka kadhaa ndo wanajifanya kukiri bungeni,ili waonekane wema kwa watu.mbona hawakiri epa,escro,meremeta,kagoda etc?kwanini wasikiri kuwa wizi wao umesababisha watanzania wanaishi kwa tabu?

Je wizi unao fanywa na vyuo vikuu upande wa ada?.
Vyuo vya serikali ada tofauti na wanategemea kufanya kazi yenye kipato sawa,je huu si wizi?.
Vyuo vya private ada ni mara mbili ya vyuo vya serikali,na ajira ni aina moja na mshaara ni uleule je huu nao si wizi?.
TAFAKALI,SERIKALI INAIBA KILA SIKU/INARUHUSU WIZI KILA SIKU.
 
Je wizi unao fanywa na vyuo vikuu upande wa ada?.
Vyuo vya serikali ada tofauti na wanategemea kufanya kazi yenye kipato sawa,je huu si wizi?.
Vyuo vya private ada ni mara mbili ya vyuo vya serikali,na ajira ni aina moja na mshaara ni uleule je huu nao si wizi?.
TAFAKALI,SERIKALI INAIBA KILA SIKU/INARUHUSU WIZI KILA SIKU.

Hapa mada ni Serikali kukiri ilidhulumu awamu hiyooooooooo, soma utaijuwa tu.
 
Huna jipya, ni chuki yako kwa Mwalimu Nyerere (R.I.P Mwalimu);
Na mahaba yako ya dini ndivyo unavyovichambua hapa.
 
Hakuna aliyedhulumiwa na hata leo serikali ya Makongoro ikiingia Madarakani nyie wote wenye Mali za ufisadi jiandaeni tena Kukimbilia Canada( sijui kwa nini hamkimbilii Saud Arabia) maana Kwa Mara nyingine tena Tutawafunga na kutaifisha Mali zenu zote za ufisadi, mlizozipata awamu hii ya sheikh wenu dhaifu J.K
 
Fool at 40,
Ubongo wako unafikiria kukomeshwa ni kufa njaa? Nyerere alikuwa mtu wa Mungu na alichofanya ni kuwapunguzia wale wenye ziada ya kukufuru na kuwapelekea wasionacho, bahati mbaya najaribu kumwelewesha mtu uliyekulia mtaani ktk nyumba za msajili hivyo maisha real ya kijijini huyajui mpaka uombe picha. Kwa taarifa yako ni Nyerere pekee aliyeweza kuweka usawa wa kusomesha waTZ wote, mradi uko bright. Nyie k.oko si hamjui hata faida ya kusoma?

Ubongo wako umejaa nazi, huna uwezo wa kufikiri. Mko wengi kama wewe hapa, mpaka narudia mara nne kumwelewesha mtu kitu kidogo.

Kawadanganye wenzio. Hunidanganyi mimi. Mimi nimeuza chakula cha ration na nimewasaidia wazawa chungumzima chakula na nguo. Hiyo propaganda yako kapeleke hukoooo kwa wenzako.

Na kama unataka kujuwa, sijaishi hata siku moja nyumba za Msajili. Umeshawahi kusikia mwenye Mali anakuwa mpangaji?

Maisha niliyoishi wakati wa Nyerere na sokoine ni mara mia kuliko walioishi ndugu zako vijijini. Kumbuka hilo!

Wewe unayojuwa faida ya kusoma, mbona unaandika matapishi kama hujamaliza darasa la saba?

Faida yangu ya kusoma ni kuweza kuongeza mali aliyotudhulumu Nyerere mara 250 ya thamani yake leo.

Wewe unayojitia umesoma, unatowa ajira ngapi Tanzania?

Wewe umeitumia elimu yako ya bure kuandika uharo.

Eti, Nyerere alikuwa "Mtu wa Mungu",
Ninyi mnafikiri huko Vatikan ni vilaza kama ninyi?

Nyerere is supposed to go through Two Miracles not Two Tragedies Verification. If it was the later, you would have started worshipping him as your Saint loooooong time ago.
 
Back
Top Bottom