Bungeni: Mwigulu Nchemba achafua hali ya hewa!

Bungeni: Mwigulu Nchemba achafua hali ya hewa!

Kweli kama mwigulu ndio mashine yenue tegemezi subirini makubwa, mtachanganyikiwa soon msijue pa kushika. maana kwa akifanyacho kaeni mjue anawaimarisha wapinzani kwenye kuchambua kwa kina udhaifu wa serikali ya CCM.

Chama washwa washwa, Wabunge washwa washwa, viongozi washwa washwa, wanachama washwa washwa na hoja washwa washwa . Mh Mnyika aka Mh. Washwa washwa ndio ameileta jina jipya la cdm na kuwa washwa washwa
 
ni tishio kwa watoto wetu wanaposikiliza bunge na yeye anapokuwa live,watoto baada ya bunge kupita watakuja kutuulize vip yule jamaa alikuwa nafuka mle kwenye vit vyekundu kwanini asiungane na akina masanja na akina jito
 
1. GeniusBrain, kwanini wabunge wa CCM wanatumia nguvu kubwa kuzuia report ya kamati ya bunge isiwekwe wazi kwa bunge zima?

2. Siku ya 6 leo, hakuna mtu yoyote aliyekamatwa na kuhojiwa kuhusu mkasa wa Dr Ulimboka. Kwanini wabunge wa CCM hawaonekani kushtushwa na hilo?

bunge lina ratiba zake na kanuni sake, wabunge wa upinzani wameonyesha ni vilaza wakutupa wa kujua kanuni na ndio maana wanaona wanaonewa, kumbe ni kutojua kanuni Ndio maana nasema haya mawazo yenu ya washwa washwa yanahitaji dawa, na dawa sasa mnaipata bungeni kupitia wajuzi wa mambo na kanuni
 
Pole sana ndugu yangu,inatakiwa kutambua kuwa wanachi wamekutuma ili uzichambue kwa makini hoja za serikali na kuangalia vipaombele vilivyopo kwa jimbo lako na jinsi gani ya kuviboresha.Ila nashukuru kwa akili yako na shoga yako nchemba mmekubali kuwa hoja zinazojadiliwa ktk bunge hili la bajeti ni za upinzani tu na sio zile zinazoletwa na wizara zenu kwa maana nyingine mmekubali kuwa wanaotawala kifikra nchi hii ni hao unaowataja na sio wengine.

Kweli ukiisha pend a unakuwa kipofu aisee, cdm wenyewe haya unayosema hawayafanyi , mtu Sugu alichangia nn sasa pale jana ? mie na wasiwasi na nyie wote, washwa washwa mna akili wote saw a hakuna zaidi ya kulaumu na kutafuta umaarufu wa kirahisi
 
mzinzi hawezi kuwa tishio kwa wapinzani labda kwa mke wako
 
Kwa kweli mchemba ni tishio kama ndio vijana ccm inawategemea lazima awe tishio toka ameingia bungeni sijawahi msikia akaongea ishu yenye manufaa kwa taifa zaidi ya upotoshaji kama leo nimemfananisha na mkiristo aliyesoma bibilia wokorito ule mstari unaosema msinyimane peaneni ane akawa malaya wa kugawa kwa kutosoma mstari unaofuata.
 
Siku zote ukiisha ona wabunge, wanachama, wapenzi na viongozi wa chama cha washwa washwa wana lalamika kama hivi ujue jamaa amewashika pabaya aisee na hakamatiki, sio siri Mwigulu ameisha pabaya cdm kila siku wanamuwaza jinsi yakumdhibiti jamaa hawapati majibu na yeye amewaonyesha watanzania udhaifu wa bajeti ya upinzani na kuiita ni ya harusi na si ya nchi, kuna ubaya gani nae kuwaelimisha watanzania?

Pole sana naona hapo ndo mwisho wa uelewa wako, wananchi hatuhitaji mipasho ya kitoto bungeni tunataraji kusikia kile ambacho wawakilishi wetu tumewatuma. Hajishughulishi kutafuta hoja zenye mashiko hayo ndo matunda.
 
Mwigulu is insignificant and useless piece of shit...and frankly he doesn't belong to the CCM elite class.
 
Mbunge wa Iramba Mashariki, Mwigullu Nchemba anaonekana kuwanyima usingizi Wapinzani na mashabiki wao.
Je inawezekana Mbunge huyu akawa tishio kwa wapinzani?
Kwa maoni yangu mimi naona kama NI kweli wapinzani wanamgwaya Mwigullu, kwani kama siyo tishio, basi wasingehangaika naye.

Si wabunge tu wa Upinzani wanaohaha kuhakikisha CCM haufuruki kupitia kwa Mwigullu, bali hata mashabiki wao, kupitia vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na wengine wanaonekana kutumia muda mrefu kumponda Mbunge huyo machachari wa CCM.

Lakini swali la msingi ni , je Anayoyasema Mwigullu hayana msingi au sasa Wapinzani nao wanaona kama wanashikwa pabaya na wanajaribu kutapatapa? Na kama wanatapatapa, wanaogopa nini? kwani nao wana madhambi? Ni mabaya gani hayo?




That is pipe dream-Gamba mkubwa
 
nafichua siri

siasa ni mchezo mchafu. ccm walichoamua safari hii ni kutumia siasa ya distabilisation bungeni. wameamua kuwabana wapinzani ili wasipumue. kwa sasa hivi hadi baadhi ya wabunge wa upinzani wanaogopa kuongea ili wasishambuliwe na akina nchemba. mabingwa wa kujenga hoja akina zitto , mnyika, mdee ................... kila wakisimama unaombwa mwongozo wa spika. lengo ni kuwapandisha hasira na kuwatoa kwenye hoja.


ndugu zanguni siasa ndivyo ilivyo. asilaumiwe nchemba. kuhusu maendeleo jimboni kwake, nchemba ni mjumbe wa kamati kuu ya nec kwa nafasi yake kama mtunza fedha za ccm. lazima maendeleo yatapelekwa jimboni kwake. hata mawaziri huwa hawaongelei majimbo yao bungeni lkn huwa wanaonana wenyewe na kupanga namna ya kupelekeana maendeleo.

ushauri wangu kwa vyama vingine ni kujipanga na kuweka mkakati wa kupambana na makombora ya akina nchemba. otherwise ccm wanalitawala bunge sana kwa ss. kama ungekua mpira naweza kusema ball possession ni 70% kwa 30%. ccm wana 70%
 
bunge lina ratiba zake na kanuni sake, wabunge wa upinzani wameonyesha ni vilaza wakutupa wa kujua kanuni na ndio maana wanaona wanaonewa, kumbe ni kutojua kanuni Ndio maana nasema haya mawazo yenu ya washwa washwa yanahitaji dawa, na dawa sasa mnaipata bungeni kupitia wajuzi wa mambo na kanuni


GeniusBrain, ninakuuliza tena kwa mara ya pili;
1. Kwa nini wabunge wa CCM wanatumia nguvu kubwa kuzuia kuwekwa wazi report ya kamati ya bunge iliyokutana na pande mbili yaani serikali na madaktari?

2. Leo ni siku 6, Dr Ulimboka ametekwa, ameteswa usiku mzima, ameumiwa vibaya lakini hakuna mtu yoyote aliyekamatwa na kuhojiwa kuhusu unyama huo! Wabunge wa ccm pamoja na kumuita Dr Ulimboka "Hitler' wanatumia nguvu kubwa kwenye chombo cha kutunga sheria kuziba watu mdomo. Kuna nini?
 
Kama kawa gamba kwao ni matusi na makofi tu, nashindwa kuelewa anowawakilisha wanamchukuliaje
 
GeniusBrain, ninakuuliza tena kwa mara ya pili;
1. Kwa nini wabunge wa CCM wanatumia nguvu kubwa kuzuia kuwekwa wazi report ya kamati ya bunge iliyokutana na pande mbili yaani serikali na madaktari?

2. Leo ni siku 6, Dr Ulimboka ametekwa, ameteswa usiku mzima, ameumiwa vibaya lakini hakuna mtu yoyote aliyekamatwa na kuhojiwa kuhusu unyama huo! Wabunge wa ccm pamoja na kumuita Dr Ulimboka "Hitler' wanatumia nguvu kubwa kwenye chombo cha kutunga sheria kuziba watu mdomo. Kuna nini?


mbinu ambayo wameitumia wabunge wa ccm na spika, ni kusema kuwa suala la madaktari lipo mahakamani. kulijadili ni kudharau mhimili wa mahakama. siasa ndivyo ilivyo. ni kama mchezo wa draft. ukipata njia ya kukufanya umdhibiti mwenzako, unaitumia haraka sana. ccm kwa siasa chafu wabaya sn.
 
We mdirii acha fikra potofu, huko kwenu mbulu kuna nini? kila siku mnakimbilia arusha kutafuta vibarua. Ungefikiria zaidi kabla hujalileta kwenye public.Ni wananchi wangapi wamakabila mbalimbali wanaoenda sehemu mbalimbali kutafuta ajira.Umeishia darasa la ngapi wewe?
 
umesahau baa zote na madanguro mikoa ya kasakazini na kati huwakosi.Wanaongoza kuamzisha makazi sehemu na kuishi kwa ulevi na umalaya.Si haba kukuta wakilala chumba kimoja, bibi,mama, mjukuu na kila mtu akiwa na bwana ke.Hapo wakiwa juu ya ulabu wao al maarufu buzaa+dadii.
 
KWA NINI CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM KILIMDHULUMU MWIGULU NCHEMBA HIVI KWA KUTOKUMFANYA AFANANE NA ALAMA ZA KI-TAALUMA HIZO ANAZOZIIMBA SANA?

Laiti Mwalimu wa Mwigulu Nchemba, pale Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, angefanikiwa kumrekebishia kijana huyu SPIDI ya kufikiri ikawa kubwa zaidi kuliko SPIDI ya kuongea sana mitaani, pengine hiyo 'A' yake anayoitembeza kila jukwaa ingepata maana na kutambulika zaidi hata bila ya yeye kulazimika kutumia nguvu nyingi mno kulitangaza katika jamii ya Tanzania...

huyu jamaa tumeshahakikisha harudi tena mjengoni, mchakato mkali unaendelea, lazima tumngoe!!!! wala msiwe na wasiwasi
 
We mdirii acha fikra potofu, huko kwenu mbulu kuna nini? kila siku mnakimbilia arusha kutafuta vibarua. Ungefikiria zaidi kabla hujalileta kwenye public.Ni wananchi wangapi wamakabila mbalimbali wanaoenda sehemu mbalimbali kutafuta ajira.Umeishia darasa la ngapi wewe?

Ukweli haubishaniki Iramba kuna umaskini wa kutisha. CCM haioni kama huko kuna wananchi wanaohitaji maendeleo. Hakuna wa kuwasemea. Miaka yote 50 Iramba haijawahi kupata mbunge makini na mtetezi wa watu.

Ni kweli kuwa kuna wimbi kubwa la watu wa Iramba wamehama maeneo yao na wapo mikoa ya jirani kukimbia umaskini. Nchemba akiwa msomi na mfanyakazi toka benki kuu alipojitokeza wananchi wa Iramba walisikika wakisema kuwa huyo ataliletea jimbo maendeleo.

Kumbe ni kinyume chake. Maeneo kama Mbulu japo bado kuna umaskini, lakini watu wana mwamko wa kisiasa jambo linaloleta afya katika kujadili changamoto za kuleta maendeleo. Iramba pamoja na wilaya mpya ya Mkalama inahitaji wawakilishi wa wananchi makini la sivyo umaskini utaendelea kukita mizizi sehemu hizo wakati maeneo mengine yanazidi kusonga mbele kwa kutetewa na wawakilishi makini.
 
Back
Top Bottom