Wambandwa
JF-Expert Member
- Dec 3, 2006
- 2,249
- 833
Nimekua nikijiuliza kila siku bila kupata majibu sababu za wabunge hususan wa chadema wakiongozwa na mbowe kutoonesha dhana ya uwajibikaji wa pamoja kwa vitendo;....
Wakati mbunge kijana ZITTO KABWE alipogomea kupokea posho ya kukaa kitako kwa vitendo licha ya vitisho vya spika kwamba atapoteza ubunge wake kwa kutoweka saini ya kupokea pesa hizo haramu wabunge wengine wa chama cha ZITTO wakiongozwa na kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni wamekua wakionekana kwenye dirisha la mhasibu wa bunge wakipanga foleni dirishani hapo kuchukua fedha hizo haramu.
Je ni kwanini mbowe hakuitumia kofia yake ya kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni kumuunga mkono Zitto na kushawishi kambi nzima ya upinzani kugomea posho hiyo haramu na badala yake kusisitiza pesa hiyo kama ipo na haina kazi ipelekwe kwenye sekta ya afya inakohitajika sana?
Nawasalisha.
Huu utumbo mleta mada ameisha uleta neno kwa neno humu jamvini, he MUST be under influence of somthing: banghe, mdudrushwa, mapowder, gubeli, mirungi n.k