Bunge Lisirushe Matangazo yake 'LIVE' - Nape

Bunge Lisirushe Matangazo yake 'LIVE' - Nape

Ama kweli magamba wamefilisika Hoja.

Kwa kiongozi anayetegemewa na chama kutoa taarifa za kichama kama huyu Nape, ni aibu kwa yeye na chama chake.

Suala la TV siku hizi zipo maofisini muda wa kazi tunaangalia TV huku kazi zinaenda. Mwambieni atembelee ofisi nyingi mjini na hata mabenki kuna TV, na wanafuatilia vipindi vya Bunge.

Nape yupo Dunia gani huyu!!!!!!!!! Mbona mshamba hivi!!!!!


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!!
 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nauye, amesema kuwa jambo lolote ambalo linaleta heshima kwa Bunge analiunga mkono.

“Suala la Bunge kurushwa ‘live’ halirushwi kwa wakati ambao watu wanafuatilia kwani wakati wa asubuhi watu wanakuwa maofisini, wakati wa mchana wao wanakuwa wako mapumziko wanakula na Bunge nalo linakuwa mapumziko, sasa wanaangalia saa ngapi?” alihoji Nape.
Alisema hawezi kupinga suala ambalo linaonekana lina faida na kuleta heshima kwa Bunge hivyo anaafiki uamuzi huo.

Source:Nipashe Ijumaa

kwa mtazamo huo, redio na TV zote zianze matangazo jioni, si anasema mchana watu wanakuwa kazi...
 
Hawa wanataka kufanya watanzania ni wajinga kiasi gani naona wao wanaweka mbele maslahi ya chama kuliko utaifa na watu wake watafute njia nyingine ya kujinusuru sio kuzuia bunge lisionyeshwe live na 2015 mtatukuta tu mtaani maana sis ndio wapiga kura wenu.
 
Kwa kuwa Tanzania siyo kisiwa, ninawaomba Nape na Kashililah waniambie ni nchi zipi za Afrika Mashariki bunge lao halioneshwi 'live'. Hawa watu kwa nini wanaongea kabla hata ya kutafuta ushauri? I never expected Nape's reasoning capacity to be that low. Poor guy! Ni lazima bunge lioneshwe 'live' ili wabunge wakawajibike kwa wapiga kura wao. Kuna mwaka fulani mbunge mmoja aliwahi kuuliza kama ni kweli pembe za kifaru zinaongeza nguvu za kiume. Hivi kweli wapiga kura wake ndiyo walimtuma kuuliza swali la namna hiyo? Tunataka tuwasikie hao wanaouliza upuzi bungeni ili tuwape hukumu ya haki. :fencing:Wakati wenzao wakiuliza habari za mazao, elimu na miundo mbinu, yeye alikazania nguvu za kiume.
 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nauye, amesema kuwa jambo lolote ambalo linaleta heshima kwa Bunge analiunga mkono.

“Suala la Bunge kurushwa ‘live’ halirushwi kwa wakati ambao watu wanafuatilia kwani wakati wa asubuhi watu wanakuwa maofisini, wakati wa mchana wao wanakuwa wako mapumziko wanakula na Bunge nalo linakuwa mapumziko, sasa wanaangalia saa ngapi?” alihoji Nape.
Alisema hawezi kupinga suala ambalo linaonekana lina faida na kuleta heshima kwa Bunge hivyo anaafiki uamuzi huo.

Source:Nipashe Ijumaa

Kweli kwa maneno haya ni dhahiri kuwa NAPE anaanza kuchanganyikiwa. anakuja na hoja mpya kabisa, mwanzoni walituambia kwamba wanataka kuchakachua habari za bunge kwa sababu wabunge wanafanya fujo na kujenga twasira mbaya ya chombo hicho kwa wananchi. leo Nape anatuambia kwamba wananchi huwa hawatazami Bunge. Namshauri Nape na wenzake wakakae na wajipange Upya. Mbinu ya kumtumia katibu wa Bunge imeshindikana. HAKUNA ANAEWEZA KUZIMA NGUVU YA MABADILIKO TANZANIA. Mtakaaa sana kwenye vikao vyenu vya hila vinavyofanyika uwani ili kutumia Bunge kuhalalisha matendo yenu dhalimu na ya kifisadi, lakini mjue ya kwamba mtaishia kunawa tu.
 
Nape haisaidii kuua upinzani hizo mbinu nizakitoto huwezi kuwapangia watu muda wa kutizama kipindi. dawa ya kuua upinzani nikuwatumikia wananchi na kuumaliza ubinafsi unaotawala chama chakoi ccm na magamba yake
Katibu wa Itikadi na
Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nauye, amesema kuwa jambo
lolote ambalo linaleta heshima kwa Bunge analiunga mkono.

“Suala la Bunge kurushwa ‘live’ halirushwi kwa wakati ambao watu
wanafuatilia kwani wakati wa asubuhi watu wanakuwa maofisini, wakati wa
mchana wao wanakuwa wako mapumziko wanakula na Bunge nalo linakuwa
mapumziko, sasa wanaangalia saa ngapi?” alihoji Nape.
Alisema hawezi kupinga suala ambalo linaonekana lina faida na kuleta
heshima kwa Bunge hivyo anaafiki uamuzi huo.

Source:Nipashe Ijumaa
 
hivi huyu anafikiri bado yupo enzi zile za babu yake nini? Au ndiyo upeo wake wa akili ulipofiki? bora kuishi na chizi fresh kuliko msomi anayejipumbaza
Eh mkuu ninamkumbuka Moses Nnauye akiwa na Umri wa Babu bado alijipeleka tamasha la Vijana Pyongyang! Akapambana na makamanda wa wakati huo UDSM eti anataka kukaa first class!! alitolewa mkuku wa mbwa!!Hao ndio the Napes!! Alitumia USHUSHUSHU watu wakaswekwa lupango ya Korea lakini poa sasa tunamwona NEPI original na tunadeal naye!! Kiukweliiiiiiiiiiii
 
Kumekuwepo na Uvumi na upotoshaji mkubwa unaoendelea katika mitandao ya kijamii hasa hapa JF kuhusu kauli ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM ndugu Nape Nnauye.

Upotoshaji huo umejitokeza kufuatia Nukuu ya gazeti moja la kila siku la Nipashe kunukuu kauli ya Nape juu ya mjadala unaoendelea hivi sasa kuhusu kuonyeshwa ama kutooneshwa kwa Bunge la Jamhuri. Kilichojitokeza ni kuwa Mwandishi wa Gazeti hili aliwasiliana na Mwenezi kutaka maoni yake juu ya suala hilo na ndipo Nape alipofafanua kuwa hawezi kupinga suala la kuonyeshwa kwa Bunge live na kueleza kuwa tunalo tatizo la msingi la kushuka kwa nidhamu ndani ya vyombo vyetu vya maamuzi wakati mwingine lakini lazima tufikiri katika njia sahihi zaidi katika kutatua matatizo hayo bila kuzalisha matatizo mengine zaidi.

Hakuna maana wala tafakuri iliyo sawa inayoweza kukubaliana na uamuzi wa kutoonyesha bunge ili kukuza nidhamu ya wawakilishi bali ni lazima kanuni zilizopo zifuatwe na zipewe makali zaidi ya kuwashughulikia wale wenye kufanya makosa.

Ninachokisema ni kuwa tunahitaji muda zaidi wa kuonyesha bunge letu, ili kuwapa fursa wananchi kulifuatilia kwa umakini zaidi na kwa namna hiyo kuwaongezea ushiriki wao katika vyombo hivi vya kimaamuzi, lakini pia kuwaongezea hoja na vigezo vya maamuzi juu ya wawakilishi wao kwa yale wanayoyasema bungeni. Lakini pia hili la kutoonesha linakinzana na kanuni za utawala bora ambazo tunazifuata na kuzidumisha.

Hata hivyo Nape ameendelea kufafanua juu ya mjadala huo kupitia mitandao yake ya Kijamii, ambapo kwenye facebook ameeleza.
Naunga mkono juhudi za kulifanya bunge letu liwajibike zaidi kwa wananchi na kuwa na heshima zaidi. Lakini naamini kutolionyesha "live" si moja ya juhudi hizo!

Lakini ni muhimu kujadili pia muda wa kurusha bunge ambapo wananchi wengi wanapata muda wa kuliangalia badala ya utaratibu wa sasa ambapo naamini watu wengi wapo/wanapaswa kuwa kazini.

Nape Nnauye
NILICHOKISEMA ni kuwa ni vizuri zaidi bunge likipewa airtime ya ziada hasa kwa muda ambao watu wengi wanakuwa majumbani.

Wakati mwingine ni makosa yanayojitokeza kwa waandishi wetu, lakini mara nyingine hayawi makosa halisi bali makosa yanayokusudiwa.
 
Mimi nadhani dhambi haiwezi kuondolewa kwa kufunikwa bali ni kwa kuitubia na kuwa na nia ya dhati ya kutoirudia. Kutoonyesha Bunge "live" hakuwezi reta heshima ya bunge, bali ni kuzuia haki ya wananchi kupata habari kwa manufaa ya watu wachache wanaojilinda maovu yao kwa kisingizio kama hicho, tene wakati huu wa sasa bunge limekuwa likisikilizwa na watanzania wengi sana kuliko miaka ya nyuma, Mimi naona Mbunge wa Vunjo alikosea sana kusema hivyo maana tusipoona bunge linavyoondelea Bunge litashindwa kujikosoa na kujirekebisha, lakini wakijua kwamba tunawaona watajisahihisha, naomba hawa wanasiasa watuachi bunge, halafu mi nawashangaa sana hawa wanasiasa kunawakati wanasema watanzania hawafanyikazi lakini sasa wanasema watanzania watakuwa kazini sijui ukweli ni upi mi nathani juu ya jmbo hili la matangazo ya Bunge kuna hila nyuma yake.
 
Hahahahahahahahahahhahahhahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahahhahahaahhahahahahahahahahahah

Nnape bwana hamnazo kweli yeye amebakia Anologia hajui habari za Digitali, TV hata kwenye simu tunazo na tunaona hata kama tuko chooni wacha makazini
 
Asante Afisa Mwandamizi wa Nape kwa ufafanuzi.

Bunge lazima lioneshwe live na madudu yote tuyaone bila chenga. Kama angekuwa mkweli eti nia ilikuwa "kuboreshwa..." kama Nape alivyodai sasa Kashilila ni nani na kwa mamlaka gani alisema alichokisema?

Spinning aside, mmepima kina cha maji mkagundua wananchi hawatakubali so rudini tu studio. Tena mkome kuyumbisha-yumbisha wananchi. Tuna mambo ya muhimu ya kuyafikiria na kufanya kuliko hizi pox-spinning zenu.
 
HIVI HII IMEKUWA KAMA FASHENI, WANASIASA UCHWARA KUTOA KAULI, THEN WANAKUJA TENA KUZIKANA WAKIONA WALICHEMKA.kwanini basi usitulie kwanza organise your thought kabla ya kulipuka matamko ya hovyohovyo bila kufikiria ,then unaingia gharama tena ya kuyakanusha?? shame NAPE
 
siku zote mtu alie na njaa hata akiwa anaongea,hoja zake zinakuwa za kinjaanjaa! Kwa maana hii simshangai nape kulopoka hayo aliyosema.
 
katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi (ccm), nape nauye, amesema kuwa jambo lolote ambalo linaleta heshima kwa bunge analiunga mkono.

“suala la bunge kurushwa ‘live’ halirushwi kwa wakati ambao watu wanafuatilia kwani wakati wa asubuhi watu wanakuwa maofisini, wakati wa mchana wao wanakuwa wako mapumziko wanakula na bunge nalo linakuwa mapumziko, sasa wanaangalia saa ngapi?” alihoji nape.
Alisema hawezi kupinga suala ambalo linaonekana lina faida na kuleta heshima kwa bunge hivyo anaafiki uamuzi huo.

Source:nipashe ijumaa

yani huyu nape kweli anachekesha, sidhani kwa sbbu muenezi ndio basi unalazimika kuongea tu kila kitu hata km hauna mantiki ya jambo husika. Hivi bunge ni kwa ajili wananchi wafanyakazi tu jamani??? Hata huku maofisini ndio tv zimejaa mno. Nafkiri nape ungekaa kimya tu kaka na hili la bunge halikubaliki popote pale hata kama mtalipika vp??????
 
Asubuhi ni muda wa kazi. Ukienda ofisini halafu usihudumiwe kisa mfanyakazi yupo busy kwa kuangalia bunge utajisikiaje?

Bunge lisionyeshwe live, wawe wanaonyesha marudio yake yote saa tano na nusu usiku.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

ili wamwonyeshe nani saa hizo?
 
Umeona eeh. Hiyo, Id nimeshalishtukia hata mimi siku nyingi. However, it does not matter, cha msingi ameona maji yanazidi unga sasa anatafuta kurekebisha. Bunge lazima lioneshwe live. That is the bottom line. Kauli ya Mnyika pia ni mwafaka.

Ni jambo la ajabu sana kuwa na wanasiasa vijana wenye maono primitive kama aliyotoa.Nimeshangaa kweli kweli na mbaya zaidi yeye ni graduate wa kwenye Journalism.Katika jambo baya zaidi ambalo mwanasiasa makini analoweza kufanya ni ku-compromise taaluma yake kukidhi haja za kisiasa
 
Back
Top Bottom