Asiyewajibika na asiyejiamini ndiye anaogopa Wananchi kumuona alivyowadanganya au kutaka wasifahamu ni kiongozi wa namna gani kulinganisha anayojitangaza au kudai kusimamia.
Mimi ningependa iwe sehemu ya kanuni zetu, kila Mbunge awe na column ktk website ya Bunge ikiorodhesha yote aliyoahidi Mbunge na taarifa ya utekelezaji wake in real time.
Kila Halmashauri inatakiwa kuchapisha taarifa zake za robo mwaka na kuzisambaza bure kwa wananchi wa maeneo yao wakionyesha waziwazi mapato na matumizi ya fedha pamoja na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya mendeleo iliyopangwa ndani ya mwaka wa fedha na hatua iliyofikiwa kwa wakati huo.
Hata Usalama wa Taifa (UwT) unatakiwa sasa uwe na tovuti (for public consumption) na kuweka wazi yale yote yanayotakiwa kuwa wazi (makusudi ya jumla, idara na vitengo, nafasi wazi, jaribio la AWALI la binafsi (preliminary self-appraisal) kutathmini kama una sifa za awali za kujiunga na UwT, Tafiti na Machapisho yao mbalimbali na rangi kama ishara za hali ya Usalama wa nchi yetu, link ambapo mtu anaweza kutoa credible info zinazohusu hatari ya usalama wetu na ufisadi mkubwa nchini na usiri wa mtoa habari ukahakikishwa n.k.
Huu ni muda wa uwazi na ukweli.