Miaka ya zamani sana, TPDF ilikua inafanya direct recruitment kutoka uraiani lakini baadae ikaja kusitisha baada ya kuibuka layer ya askari/maafisa wasio na weledi. Unakuta mtu alikua jambazi, changudoa, mwizi etc. lakini anavumilia miezi minne ya depo tayari anakua muajiriwa. Hakuna kipindi kinachopima uvumilivu kama cha u-service man. Tena kwa sisi tuliopitia vikosi vya malezi kama 837KJ kipindi hiko, fatiki za shamba ni za kutosha hadi wengine wakaanza kujiengua mmoja mmoja kwa kutoroka. Kwa msoto unaopitia JKT, ukibahatika kuajiriwa lazima uwe na weledi na nidhamu ya hali ya juu tofauti na mtu aliyepitia moja kwa moja uraiani. Somehow hata kwa maafisa , unaweza ukaona tofauti kati ya afisa aliyepitia JKT, akapitia maisha ya uaskari na baadae kwenda officer cadet, na wale madogo wa BMS ambao wanachukuliwa mujibu wa sheria wanaenda miaka 3 TMA wanapewa kamisheni. Wengi wao hua wana lack leadership skills, hata uwapeleke exposure popote wakirudi kwenye loc zao wanaonesha unanga wao.