Bunge kusitisha uuzwaji UDA? 270 Milioni zaingizwa akaunti ya Idi Simba

...........Natoa mwito kwa wananchi wa Dar es salaam kutuunga mkono katika kulifuatilia kwa karibu suala hili na kuchukua hatua zinazostahili kila mmoja kwa nafasi yake.

Wenu katika utumishi wa umma,

John Mnyika (Mb)Bungeni-Dodoma31 Julai 2011

Mh. Mnyika nina mambo mawili tu ningependa kufahamu toka kwako, na bila shaka leo ndio bajeti ya wizara ya uchukuzi inajadiliwa;

Je umejaribu kutafuta nafasi ya kuchangia ili kuliweka wazi suala hili ambalo inaonekana masaburi amejitahidi kuwahi kuwahadaa wananchi ilihali kumbe naye ni mnufaika wa ufisadi huu?

Kama ikitokea serikali imeng'ang'ania msimamo wake wa kuifisadi UDA, mmejiandaaje kukabiliana na uamuzi huo?
 
Wana JF,

Mwl.Nyerere aliwasema sana ile May Mosi 1995 kule mbeya viongozi wa serikali wanauza mashirika ya UMMA alishangaa sana, hii nikutokana viongozi kuwa na tamaaa za ajabu, Kuipinga azimio la Arusha, urafi wa madaraka, kutokuwa waadilifu, wazalendo, kadri siku zinavyo kwenda maozo yote aliyoyasema baba wa Taifa yatajitokeza huyo mzee aliwaachia raana hawa viongozi wetu, tena enzi hizo hawa viongozi walikuwa ni vijana kabisa sasa ndio worse kabisa wanazeeka na watakufa na vitu vyote vya UMMA"[QUOTE

Jethro, wakati Nyerere anaongea , Basil Mramba ndo alikuwa mwenyeji wake pale Mbeya , maana alikuwa Mkuu wa mkoa wa Mbeya. Kila alipoongea, aligeuka na kumuuliza Basi " eti Basil, mnauza hata vitu vyenye faida? "
Baada tu ya kufariki Baba wa taifa , Basil aliyapuuza maneno yale, lakini leo hii bila shaka yanavuma masikioni mwake kama radi. Pesa anayo, lakini heshima ameipoteza. Kila siku kuishi kwa kutumia mashushu ili ajue kesi yake ataimalizaje: I WAPI FURAHA YA UPORAJI ALIOUFANYA KWA UMA WA WATANZANIA?
Na wote akina Mkapa , wana raha gani sasa hivi, kila mtu anakunyooshea kidole.
Hili liwe somo hata kwa vijana wanaotaka kupata utajiri wa haraka haraka kwa njia hizi za kuwaibia masikini, waache hayo mawazo mara moja. Guys Working hard and objectively is the only way utaenjoy maisha yako na utajiri bila kuwa na hofu ya kukamatwa one day! it is a WARNING!
 
FwViYlzUn++xAAAAAElFTkSuQmCC


busexplorer.com

440 × 281 - Ikarus 280 Articulated Articulated Bus -



Nayakumbuka sana mabasi haya Ikarus enzi za uhai wa UDA, hii ilikuwa ni kazi nzuri ya Baba wa Taifa lakini tangu awakabidhi nchi hawa manyang'au kazi ni kuuza tu mbwa kabisa hawa.
 
Mh. Mnyika nina mambo mawili tu ningependa kufahamu toka kwako, na bila shaka leo ndio bajeti ya wizara ya uchukuzi inajadiliwa;

Je umejaribu kutafuta nafasi ya kuchangia ili kuliweka wazi suala hili ambalo inaonekana masaburi amejitahidi kuwahi kuwahadaa wananchi ilihali kumbe naye ni mnufaika wa ufisadi huu?

Kama ikitokea serikali imeng'ang'ania msimamo wake wa kuifisadi UDA, mmejiandaaje kukabiliana na uamuzi huo?


Asante. Sitapata nafasi ya kuchangia kwa kuzungumza kuwa wanachaguliwa waliochangia mara chache. Nitachangia kwa maandishi na nitatafuta wasaa wa kushika vifungu. Pia, tumekutana wabunge wa CHADEMA na CCM wa DSM na wa baadhi ya mikoa wenye kuguswa na suala hili na tumekubaliana kulipinga. Hivyo, natarajia wachangiaji wengine wataendelea kuchukua msimamo wa kunusuru hisa, mali na mwelekeo wa UDA.

Nafikiria kutoa taarifa ya ziada leo kwa kuwa Simon group walitoa tamko kuhusu maelezo yangu ambayo nawajibika kujibu; kuna wengi wengine wenye mgogoro wa maslahi katika suala hili ikiwepo Kapuya.

JJ
 
Mh. Mnyika nina mambo mawili tu ningependa kufahamu toka kwako, na bila shaka leo ndio bajeti ya wizara ya uchukuzi inajadiliwa;

Je umejaribu kutafuta nafasi ya kuchangia ili kuliweka wazi suala hili ambalo inaonekana masaburi amejitahidi kuwahi kuwahadaa wananchi ilihali kumbe naye ni mnufaika wa ufisadi huu?

Kama ikitokea serikali imeng'ang'ania msimamo wake wa kuifisadi UDA, mmejiandaaje kukabiliana na uamuzi huo?
Usiwe na wasiwasi mkuu, hakuna mali ya Umma itakayoondoka na bajeti wizara ya uchukuzi haipiti hata kwa dawa. Take my word.
 
Asante. Sitapata nafasi ya kuchangia kwa kuzungumza kuwa wanachaguliwa waliochangia mara chache. Nitachangia kwa maandishi na nitatafuta wasaa wa kushika vifungu. Pia, tumekutana wabunge wa CHADEMA na CCM wa DSM na wa baadhi ya mikoa wenye kuguswa na suala hili na tumekubaliana kulipinga. Hivyo, natarajia wachangiaji wengine wataendelea kuchukua msimamo wa kunusuru hisa, mali na mwelekeo wa UDA.

Nafikiria kutoa taarifa ya ziada leo kwa kuwa Simon group walitoa tamko kuhusu maelezo yangu ambayo nawajibika kujibu; kuna wengi wengine wenye mgogoro wa maslahi katika suala hili ikiwepo Kapuya.

JJ

Hivi hawa wazeeeeeee, hawatosheki tu jamani, mpaka tumechoka sasa. Daaaaaaa
 
Inaonekana bado CHC haijaeleweka kwa wawekezaji,wafanyabiashara na hata watumishi katika potfolio husika ! Hili linaweza kuwa kosa la kitaasisi
 
Mwanakijiji hii sinema bado sana na nashauri watanzania wasishangilie.

UDA ni kama EPA wakiingia vibaya ni aibu tupu. Hii kitu pamoja kwamba inamhusisha mtu kwenye 1st family, yumo kigogo toka Tabora amepata kuwa waziri, pia yumo kigogo wa CRDB bank. Waziri wa fedha analifahamu hili kwa karibu sana kuliko mtu mwingine - huyo msajili atahukumiwa bure tu.
Hivi sasa mazungumzo yalikuwa yanaendelea kumshawishi Mkulo aachie hisa za serikali zilizobakia nadhani watatulia kidogo vumbi litulie.

Mwekezaji anashikilia title deeds za UDA kwa sasa na sioni wa kumnyang'anya vinginevyo serikali itaishia kulipa mabilioni.
Leo wanazungumzia kwamba wameshajipanga kuagiza mabus 26 kwa gharama ya Paundi zaidi ya laki moja kwa kila bus (sh6.5 billion) hii yote ni kujiweka kwenye mazingira ya kuramba mapesa pindi mkataba ukivunjwa watadai fidia ya hasara.

Bahati mbaya haya yanafanyika machoni pa mkuu wa nchi hivyo kufanya vita yetu kuwa ngumu zaidi

Hapo ndipo huwa namhurumia sana Kikwete, kwa sababu mie nilidhani kwa kujikampenia mwenyewe atakuja kivingine safari hii , kume do amekuja na kasi zaidi. Namhrumia kwa sababu ameshindwa kabla ya wakati. Chama amekigawa, nchi anaiendesha atakvyo yeye na marafiki zake. Hii kwa bahati nzuri bila yeye kujua anajenga uhasama na serikali yake mwenyewe, hivyo hatojua nani atamwangusha lini. He is a confused man. It is a real pity, hata watoto wake wanashindwa kuliona hili na wanahangaika na ujuha wa kusema ni zamu yetu kula. I tell you before this term ends, Tanzania itakuwa kwenye hali tete sana, na nahofia uasi kwenye nchi hii tunayoipenda sana. Hili gamba wanalojaribu kulivua , litang'ang'a nia ngozi na litayumbisha hii nchi vile isivyoweza tabirika.
 
Kwa kuwa Bunge limetoa support ya kusitishwa kwa kuuzwa huko ebu Mr John Mnyika wasilisha maendeleo ya kina kwa swala hilo zima tupate list ya watu wote walioshiriki kila stage, wamwageni hapa jamvini,tiba yake ni hapa hapa jamvini kama ulivyokwisha lianza tutaliendeleza mpaka mwisho wake UDA iludi kwa Wananchi.Na hao wote wajanja wa kudandia pasipo kutafakari.
 
Tunahitaji CRITICAL SURGERY KWENYE SERIKALI......TUNAHITAJI KIONGOZI AMBAYE ATAFANYA MAAMUZI MAGUMU NA HATA YAKILETA MACHUNGU KWA BAADHI YA WATU LAKINI YANANUFAISHA TAIFA...HATA AKIITWA DIKTETA NI SAWA TU.......VINGINEVYO NCHI ILIPOFIKIA NI PABAYA NA HALI ITAKUWA MBAYA ZAIDI......

KWA HILI LA AKINA SIMBA KUJITWALIA PESA ZILIZOLIPWA KWA AJILI YA KUNUNUA SHIRIKA LA UMMA (UDA), NI ISHARA YA KUWEPO UOZO USIOMITHIRIKA NDANI YA SERIKALI YETU..... INAUMIZA SANA......
 
Asante. Sitapata nafasi ya kuchangia kwa kuzungumza kuwa wanachaguliwa waliochangia mara chache. Nitachangia kwa maandishi na nitatafuta wasaa wa kushika vifungu. Pia, tumekutana wabunge wa CHADEMA na CCM wa DSM na wa baadhi ya mikoa wenye kuguswa na suala hili na tumekubaliana kulipinga. Hivyo, natarajia wachangiaji wengine wataendelea kuchukua msimamo wa kunusuru hisa, mali na mwelekeo wa UDA.

Nafikiria kutoa taarifa ya ziada leo kwa kuwa Simon group walitoa tamko kuhusu maelezo yangu ambayo nawajibika kujibu; kuna wengi wengine wenye mgogoro wa maslahi katika suala hili ikiwepo Kapuya.

JJ

Ahsante sana kwa maelezo yako, naamini sasa kwamba kama hali ndo hii basi UDA haitaangukia mikononi mwa wanyang'anyi.

Kama wabunge wa ccm hawatakuwa vigeugeu nadhani UDA inarudi mahali pake na kama ni ubinafsishaji basi utafuata utaratibu unaokubalika kisheria.

Usiwe na wasiwasi mkuu, hakuna mali ya Umma itakayoondoka na bajeti wizara ya uchukuzi haipiti hata kwa dawa. Take my word.

Nimekusoma kiongozi, naamini maneno yako mara nyingi hubahatishi hasa kwa masuala nyeti kama hili!!
 
Mali ya umma inauzwa pesa zinakwenda kwa account binafsi ya Mwenyekiti wa Bodi, Duh! kweli ili ni fumbo lenye maswali mengi kuliko majibu.
Huyu Mwenyekiti wa Body Iddi Simba si ndiye aliyeuwa Waziri wa Viwanda na Biashara na kulazimishwa kujiuzulu mwaka 2002 kwa kashfa ya kutoa vibali vya kuingiza sukari Tanzania?, baadae akapewa Shilrika la Umma la Wakala wa Meli Tanzania (NASACO ) akaliuwa chap-chap. Baada ya hapo kumbe safari iliendelea na kupewa shirika lingine la Umma - UDA. Sasa nalo analiuza na pesa kutia kwapani (akaunti yake binafsi). anyway nitarudi baadae.

Ndiye huyu huyu Iddi Mohamed Simba Ndume, mzaliwa wa Buyenzi kule Burundi na ambaye utata wa uraia wake haujatatuliwa hadi leo. Ndiye huyu huyu Iddi Mohamed Simba Ndume aliyefurushwa katika uwaziri kwa kashfa ya sukari. Ndiye huyu huyu Iddi Mohamed Simba Ndume ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki M ambayo mwenyekiti wake ni Nimrod Mkono. Ndiye huyu huyu Iddi Mohamed Simba Ndume ambaye ni Mwenyekiti wa Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam. Ni huyu huyu Iddi Mohamed Simba Ndume, muasisi wa harakati za uzawa, aliyetaka kugombea urais 2005, uzawa kwake ukiwa na maana wizi wa mtu mweusi dhidi ya mweusi mwenzie as opposed to wizi wa ma********* dhidi ya weusi. Ndiye huyuhuyu Iddis Mohamed Simba Ndume ambaye kwa kushirikiana na swhiba yake Thabiti Katunda waliasisi na kuratibu wizi wa mabilioni ya EPA kwa kumtumia Rajab Shabani Maranda na binamu yake Farjalla Hussein, ambao sasa wanakula dona gerezani Ukonga. Ndiye huyu huyu Iddi Simba wa UDA!
 
Hivi Iddi Simba ni mjinga hivi?? Nilikuwa namuona mtu wa maana na sera zake za uzawa kumbe ana lake! Kweli nimeamini hata kwenye CCM wapinga ufisadi si kweli wanapinga ufisadi bali wana ajenda yao nyingine!

Hivi kwa nini waTanzania tunadanganyika kirahisi sana namna hii?
 
Hee maskini Tanzania nchi yangu, jamani eeh! Yaani nafikiri nipite tu, haya mambo kadiri unavyozidi kuyajua ndio roho inauma.
 
Swala kubwa zaidi ya hii incident hapa ni.

Kwa nini mtu ambaye kaondolewa uwaziri kwa rushwa apewe bodi ya shirika la umma kuendesha?
 
"Nilihoji suala hilo kama sehemu ya hitaji la kuwa na mfumo thabiti wa Usafiri wa Halaiki wa Umma (Mass Public Transit) ambao utachangia kwa kiwango kikubwa kupunguza adha ya usafiri katika jiji la Dar es salaam.Hatahivyo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika majumuisho ya bajeti yake tarehe 1 Julai 2011 hakutoa kauli wala kuchukua hatua za haraka za kunusuru hali ya mambo pamoja na kuwa yeye ndiye mwenye dhamana ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) hivyo ana wajibu wa kufuatilia masuala ya kisheria, kinanuni na kimikataba ya Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam kama ilivyo kwa halmashauri zingine."

Mnyika,
Hivi hakuna sheria inayoweza kutumika kuomba bungu limwondoe huyu Waziri Mkuu kwa kutokuwa na imani naye? Maana siku hizi yeye ndo punch ya kuficha maovu kwa kisingizio cha mtoto wa mkulima wakati he is a useless person! Huyu amekuwa TAMISEMI kabla ya kuwa waziri mkuu, anashindwa nini kukemea uozo huu ambao anaujua fika?
Ndiyo maana Mbowe leo kwenye mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi, amehoji iwapo hata yeye Pinda na Kikwette wanakuwepo kwenye Balraza la Mawaziri wanaopitisha bajeti hovyo. Ni tusi kubwa hili japo Pinda atadharau, maana yeye hawezi kwepa lawama za bajeti hii kukwama.
WAZIRUI MKUU mwoga kama huyu tunamtaka wa nini?

 
Swala kubwa zaidi ya hii incident hapa ni.

Kwa nini mtu ambaye kaondolewa uwaziri kwa rushwa apewe bodi ya shirika la umma kuendesha?
Ndio utaratibu wetu tuliojiwekea, maana hata RC kilaza huwa anapangiwa kuongoza mikoa iliyo nyuma kimaendeleo ili aende kuzidisha umaskini. mfano Dittopile RIP, Lindi & Pwani.
 
Ahsante "Vikwazo"
Hapa ndio mgoto wa fikra za "uongozi" wa nchi yetu....
Tulipowekewa wimbo wa kubinafsisha na "wakubwa wa dunia"

Tukakoma kujiangalia kama sisi pia ni watu na taifa lenye mazingira yake na asili yake,
Ok hiyo sawa basi tumeshindwa hata kuangalia tu wenzetu wanavyofanya katika huo "ubinafsishaji"??
Na bado kila siku tunashinda kwenye nchi hizi za wakubwa na tunaona tafsiri yao ya "huduma za umma" na hatujifunzi kitu!

Mkuu inatia hasira sana kila siku
viongozi wetu wanasafiri kwenda ng'ambo lakini hakuna wanachorudi nacho
hawa tunaowaita wahisani shughuli za usafiri zinafanywa na halimashauri wakienda sana
watauza hisa au kushirikiana na makampuni makubwa ya usafiri yaani TRAIN maana hizo nyingi
ni kampuni binafsi lakini lazima UMMA unakuwa na hii huduma na mifano hiko wazi TAJA mji wowote mkubwa
dunia kwenye nchi zilizoendelea kama usafirishaji unafanya na watu binafsi tu!!!!

kwanza biashara ya usafiri uwezi kuifanya kama mradi wa kuchuma pesa ni kiwa na maana inafaa kufanywa kwa bei nafuu
yaani ya kujiendesha tu na faida yake ni shughuli zile watu wanazokwenda kufanya pamoja na bidhaa kusafirishwa kirahisi
hii ina manufaa makubwa sana kiuchumi kwa taifa na kwa mtu mmoja mmoja
 
Back
Top Bottom