Bukoba vs Moshi

Bukoba vs Moshi

Status
Not open for further replies.
Kwaka jana mwezi wa nne
Ulitembea bk yote au ulifika standi ukarudi stendi na soko na one way ndo pabaya subiri wamalizie stendi kule nyanga na soko uje uone na je ulienda milimani achana na bk
 
e42166aff63862d6ba88cb2090d38e96.jpg
huu haupo moshi
Basi itakuwa chumbani kwako
e42166aff63862d6ba88cb2090d38e96.jpg
huu haupo moshi
Basi itakuwa chumbani kwako
 
Yote ni Tanzania...hizi ligi za kikanda kila siku, zimezidi sasa..na always inakuwa ni Moshi/Arusha vs Somewhere else, kisha makabila yanaanza kushambuliwa...huu ni upuuzi


waache tuu waanzishe, washambulie ina kuna Uwazi kabisaa... wakubali wasikubali WACHAGA WAPO JUU na ndio maana kila utani unaohusu pesa Wanaongelea wachaga.....Chezea mchaga na kutafuta tangu enzi za ukoloni....
 
Bk huwezi linganisha na Moshi wewe..Moshi pako juu sana kwakuwa watu wa moshi wanapapenda sana kwao kiliko watu wa bk na wamepajenga vyema kuliko bk .alafu mzunguko wa pesa huko juu sana .bk mpaka wasubiri senene msimu wake na kipindi cha uvuvi ndo utaona pesa
 
Bukoba the worst place I've ever seen,sehemu ya kula Hamna ,mjini katikati majengo yote au by 90 percent Ni ya serikali.
 
nimetembelea mikoa yote hii miwili tena kiundani yaani mpaka vijijini.
mtazamo wangu: Moshi town kama mji ni msafi na una infrustructure nzuri za kuridhisha ukilinganisha na BK town

BK kwakweli mandhari ni nzuri sana kutokana na uwepo wa ziwa. hali ya hewa pia ni nzuri ila infrustructure ni mbovu mno kwakweli. ukiangalia stand na soko na barabara ni vumbi tupu.

Ukija upande wa vijijini Kilimanjaro nimefika maeneo ya kibosho, Marangu, na Rombo. kwa mtazamo wangu bado huu mkoa una barabara nzuri za lami ukilinganisha na mkoa wa Kagera. watu wa kilimanjaro wana umeme na maji ya bomba hadi vijijini. kwenye ubora wa makazi yaani majengo naona ngoma ni draw kwa kiasi kikubwa.

kwa kufupi mkoa wa kilimanjaro una maendeleo interms of infrustrure na hii nafikiri ni sababu serikali iliona ni muhimu kupromote utalii while Kagera watu binafsi wamejitahidi kujijengea makazi mazuri lakini hawana miundombinu mizuri.

kwa swala la mzunguko wa hela kwakweli mimi sijui. lakini kwa akili ya kawaida Kilimajaro inaweza kuwa juu sababu ya utalii, na ukiangalia utalii unachangia kiasi kikubwa kwenye pato la taifa.

huo ndio mtazamo wangu.
 
Bukoba the worst place I've ever seen,sehemu ya kula Hamna ,mjini katikati majengo yote au by 90 percent Ni ya serikali.

inabidi pia uangalie na utamaduni wa eneo husika. kule hawana utamadunu wa kula kwenye mabarabara. watu wanapenda zaidi kula chakula kilichoandaliwa nyumbani. ni aibu mtu kula kwa hotel. kwa hiyo biashara ya hotel kwa ujumla kule si nzuri
 
Bk huwezi linganisha na Moshi wewe..Moshi pako juu sana kwakuwa watu wa moshi wanapapenda sana kwao kiliko watu wa bk na wamepajenga vyema kuliko bk .alafu mzunguko wa pesa huko juu sana .bk mpaka wasubiri senene msimu wake na kipindi cha uvuvi ndo utaona pesa

sikubaliani na wewe kuhusu kujenga nyumbani. watu wa bukoba wanajenga sana pia nyumbani, tatizo ni miundombinu. na kwakweli watu wengi wanaosagia mkoa wa kagera ni wale ambao hawajafika vijijini. watu wa kule wanapenda kujenga nyumbani yaani vijijini.
pia issue ya gharama kubwa kufika nyumbani inachangia sana mahudhurio kuwa dhaifu.
 
Mimi sio mwenyeji wa mikoa yote miwili, ila nimeishi katika miji yote miwili kwa muda tu wa kutosha mjini na vijijini. Moshi ni mji mzuri na mkubwa kulinganisha na Bukoba. Hata idadi ya watu Bukoba inazidiwa na Moshi na sababu kubwa ni upande wa usafiri, hakuna ruti zozote za daladala katika mji wa Bukoba. Kila unapokwenda lazima upande Bodaboda labda kama unaenda wilayani.
Bukoba mzunguko wa hela ni mdogo sana kulinganisha na Moshi.
Kwa upande wa miundombinu Moshi wapo juu sana.
Kwa mandhari, Bukoba yaweza kuvutia kwa sababu ya Ziwa na vilima kuwa vingi.
Kuna mdau alielezea kuhusu majengo mazuri yapo zaidi katika wilaya za Kagera kuliko Bukoba mjini. Kama huamini hivyo nenda Karagwe(Kayanga mji) na eneo la Bunazi (Missenyi) watu wanapajenga sana.

Kwa mpangilio wa mji bado Moshi inaizidi Bukoba.

Moshi ni mji mdogo kwa eneo lakini ni mzuri na msafi.
Hata kwa idadi ya vyuo vikuu vyenye kuheshimika vipo Moshi;KCMCo,Mwenge,Ushirika nk.
 
Mimi sio mwenyeji wa mikoa yote miwili, ila nimeishi katika miji yote miwili kwa muda tu wa kutosha mjini na vijijini. Moshi ni mji mzuri na mkubwa kulinganisha na Bukoba. Hata idadi ya watu Bukoba inazidiwa na Moshi na sababu kubwa ni upande wa usafiri, hakuna ruti zozote za daladala katika mji wa Bukoba. Kila unapokwenda lazima upande Bodaboda labda kama unaenda wilayani.
Bukoba mzunguko wa hela ni mdogo sana kulinganisha na Moshi.
Kwa upande wa miundombinu Moshi wapo juu sana.
Kwa mandhari, Bukoba yaweza kuvutia kwa sababu ya Ziwa na vilima kuwa vingi.
Kuna mdau alielezea kuhusu majengo mazuri yapo zaidi katika wilaya za Kagera kuliko Bukoba mjini. Kama huamini hivyo nenda Karagwe(Kayanga mji) na eneo la Bunazi (Missenyi) watu wanapajenga sana.

Kwa mpangilio wa mji bado Moshi inaizidi Bukoba.

Moshi ni mji mdogo kwa eneo lakini ni mzuri na msafi.
Hata kwa idadi ya vyuo vikuu vyenye kuheshimika vipo Moshi;KCMCo,Mwenge,Ushirika nk.
Wala hawatakuelewa
 
waache tuu waanzishe, washambulie ina kuna Uwazi kabisaa... wakubali wasikubali WACHAGA WAPO JUU na ndio maana kila utani unaohusu pesa Wanaongelea wachaga.....Chezea mchaga na kutafuta tangu enzi za ukoloni....
Ina maana moshi ni ya wachaga tuu bkb kuna wanyarwanda,waganda, na wahaya hivyo sio mji Wa kabila fulani
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom