baada ya kuzitazama picha za miji yote miwili ya bukoba na moshi,niseme tu kwamba kwa mujibu wa picha hizo,kimadhari bukoba inaonekana kuwa juu dhidi ya moshi.
bukoba inapata backup kutokana na picha za juu (aerial shot) ambazo zilipigwa na millard ayo(nadhani alipiga wakati wa tour ya fiesta).
nyingi ya picha za bukoba zinapatikana kiurahisi mitandaoni kiasi cha kurahisha zoezi la kuzi-share hapa.
moshi ina uhaba wa picha(hata uki-google hazipatkani) za kutosha kuweza kuishindanisha na bukoba.ndio maana mashabiki wake wengi wanaishia kurusha vijembe vingi bila picha.
nihitimishe tu kwamba,akina mangi ktk thread hii mmechezea za uso toka kwa kina nshomile.jamaa walijipanga,wana picha nyingi.
akina mangi inabidi mpige picha nyingi za mji wenu ili siku nyingine muweze kuzishindanisha na picha za miji mingine.otherwise ipo siku nitakuja na picha zangu za mji wa songea nilizopiga vizuri,nikaomba mpambano halafu nikawashinda.