BRELA inakimbiza wawekezaji

Inasikitisha sana kwa kweli BRELA Mimi binafsi niliwahi kuongea na kiongozi mmoja mwandamizi wa BRELA alichonijibu ulikua ujinga maana alikua anaongea na mimi kama vile anaongea na mimi kama mtu ambaye hajui chochote katika dunia hii. Yaani kwa kifupi alishindwa kutatua shida yangu, akashindwa kunipa majibu na kubaki anarukaruka tuu sababu anajua anachokifanya sio sawa ila anazidi kukitetea.

Tunajua mmekatiwa mirija ya seminar na safari zisizokua na tija, overtime na pesa nyingine nyingi mlizokua mnaidhinishiana. Mnachotakiwa kujua ni kwamba mirija haijakatwa kwenu tuu bali ni kwa kila mtanzania aliyekua anakula haramu aliyoihalalisha kwa tamaa zake.
Sasa msiendelee kuwakwamisha wawekezaji sababu hawa ndio wanakuja kuwapa watu ajira na kuongeza pato la taifa

BRELA sio kwamba hawajui hili tatizo, wanalijua sana na wanajua likitatuliwa hawatapata mwanya wa kupata chochote kitu kwa wateja.
Na kitu ninachojua mimi ni kwamba huu uhujumu unafanywa wale maofficer wa chini wanawasiliana moja kwa moja na wateja wakisaidia na supervisors wao.
Hiyo online system yenu mnayopambana kui customize ili muendelee kuwabana wateja inawaumiza wao leo lakini itakuja kuwaumiza nyie kesho. Acheni hizo mambo

Wakurugenzi, Makatibu wakuu, Mawaziri wengi hawajui hii michezo wanaamini wanayokubaliana kwenye vikao ndiyo yanayotekelezwa kumbe huku chini wateja wanaumia sana.... wa kuweza kuvumilia usumbufu wa kusajili kampuni miezi6 hadi mwaka wanavumilia, na wasioweza wanapeleka mitaji yao nchi zingine zisizokua na hii bureaucracy

Inasikitisha sana kuona serikali inatumia nguvu na pesa nyingi ku automate systems ila wajuzi wa yale mambo ya kitukidogo wanashauri parts za system ziwe manual kwa sababu za hovyo kabisa. Ukweli ni kwamba hawataki kulifanyia kazi maana system ikikaa vizuri itawanyima ulaji wamekua Mamlaka nyingi zimegeuka kuwa vijiwe vya kuhujumu juhudi za serikali.

Yaani baada ya rais John Pombe Magufuli kuwashinda wahujumu wa nje ya system, sasahivi wale anaowajali na kuwapa kazi, na kuwalipa mishahara tena mapema kabisa tarehe 21 ya kila mwezi ndio wamegeuka wahujumu wakuu.

Taasisi zilizokua zinaongoza kuitukanisha serikali kwa wawekezaji wageni na wazawa 2020 ni BRELA, TRA, TIC, ARDHI-Uwekezaji na Halmashauri zetu. Yaani ingekua wakupewa medal hawa ndio top5 ya wanaoongoza kutuhujumu watanzania, wageni, mamlaka ya rais na nchi kwa ujumla.

Hebu fanyeni kazi buana. Mnatukwaza wenzenu maana bila uwekezaji sio sisi wala nchi inaweza kuendelea.

fundi25 nasema uongo ndugu yangu?

Cylia
Mm nina kz yangu toka mwaka jana May hadi leo kila mara marekebisho hayyaishi
 
Naunga mkono hoja hata mm nimezungushwa sana na hao BRELA zaidi ya mwezi.
Ni ukanjanja sio professional zinazofanya kazi.
 
Umeandika kwa ufasaha sana nadhani wahusika watalifanyia kazi.
Kila ofisi ya Serikali hivi sasa ni UKIRITIMBA tu. Nadhani wanamhujumu Magufuli kiaina, itachukua muda sana Magufuli kugundua watendaji wanamhujumu and infact wanaoihujumu taifa, Magu yupo leo lakini kuna siku ataondoka eidha kikatiba au kwa mapenzi ya Mungu. Lakini damage ambayo watumishi wataacha itakula vizazi na vizazi
 
Kila ofisi ya Serikali hivi sasa ni UKIRITIMBA tu. Nadhani wanamhujumu Magufuli kiaina, itachukua muda sana Magufuli kugundua watendaji wanamhujumu and infact wanaoihujumu taifa, Magu yupo leo lakini kuna siku ataondoka eidha kikatiba au kwa mapenzi ya Mungu. Lakini damage ambayo watumishi wataacha itakula vizazi na vizazi
Unafikiri ni kwanini wanamhujumu. Kwa maoni yangu nadhan wanahujumiana.
 
Inasikitisha sana kwa kweli BRELA Mimi binafsi niliwahi kuongea na kiongozi mmoja mwandamizi wa BRELA alichonijibu ulikua ujinga maana alikua anaongea na mimi kama vile anaongea na mimi kama mtu ambaye hajui chochote katika dunia hii. Yaani kwa kifupi alishindwa kutatua shida yangu, akashindwa kunipa majibu na kubaki anarukaruka tuu sababu anajua anachokifanya sio sawa ila anazidi kukitetea.

Tunajua mmekatiwa mirija ya seminar na safari zisizokua na tija, overtime na pesa nyingine nyingi mlizokua mnaidhinishiana. Mnachotakiwa kujua ni kwamba mirija haijakatwa kwenu tuu bali ni kwa kila mtanzania aliyekua anakula haramu aliyoihalalisha kwa tamaa zake.
Sasa msiendelee kuwakwamisha wawekezaji sababu hawa ndio wanakuja kuwapa watu ajira na kuongeza pato la taifa

BRELA sio kwamba hawajui hili tatizo, wanalijua sana na wanajua likitatuliwa hawatapata mwanya wa kupata chochote kitu kwa wateja.
Na kitu ninachojua mimi ni kwamba huu uhujumu unafanywa wale maofficer wa chini wanawasiliana moja kwa moja na wateja wakisaidia na supervisors wao.
Hiyo online system yenu mnayopambana kui customize ili muendelee kuwabana wateja inawaumiza wao leo lakini itakuja kuwaumiza nyie kesho. Acheni hizo mambo

Wakurugenzi, Makatibu wakuu, Mawaziri wengi hawajui hii michezo wanaamini wanayokubaliana kwenye vikao ndiyo yanayotekelezwa kumbe huku chini wateja wanaumia sana.... wa kuweza kuvumilia usumbufu wa kusajili kampuni miezi6 hadi mwaka wanavumilia, na wasioweza wanapeleka mitaji yao nchi zingine zisizokua na hii bureaucracy

Inasikitisha sana kuona serikali inatumia nguvu na pesa nyingi ku automate systems ila wajuzi wa yale mambo ya kitukidogo wanashauri parts za system ziwe manual kwa sababu za hovyo kabisa. Ukweli ni kwamba hawataki kulifanyia kazi maana system ikikaa vizuri itawanyima ulaji wamekua Mamlaka nyingi zimegeuka kuwa vijiwe vya kuhujumu juhudi za serikali.

Yaani baada ya rais John Pombe Magufuli kuwashinda wahujumu wa nje ya system, sasahivi wale anaowajali na kuwapa kazi, na kuwalipa mishahara tena mapema kabisa tarehe 21 ya kila mwezi ndio wamegeuka wahujumu wakuu.

Taasisi zilizokua zinaongoza kuitukanisha serikali kwa wawekezaji wageni na wazawa 2020 ni BRELA, TRA, TIC, ARDHI-Uwekezaji na Halmashauri zetu. Yaani ingekua wakupewa medal hawa ndio top5 ya wanaoongoza kutuhujumu watanzania, wageni, mamlaka ya rais na nchi kwa ujumla.

Hebu fanyeni kazi buana. Mnatukwaza wenzenu maana bila uwekezaji sio sisi wala nchi inaweza kuendelea.

fundi25 nasema uongo ndugu yangu?

Cylia
Mkuu ni aibu sana,hapo CHADEMA watakuwa wanahusika kuhujumu UWEKEZAJI 🤣🤣🤣🤣 M-5 TENA 😃😃😁😁🤣🤣🙏🙏🙏
 
Mkuu ni aibu sana,hapo CHADEMA watakuwa wanahusika kuhujumu UWEKEZAJI 🤣🤣🤣🤣 M-5 TENA 😃😃😁😁🤣🤣🙏🙏🙏
Utakua unawaongelea wale kina Lord waliotupostia picha hapa wakati wa kupiga kuru wakatuonyesha kadi ya CCM na pembeni kura kwa Tundu
 
Kuna ujinga sana ....online karibia zote hata Latra wanakuzingua hivyo hivyo ili uende ..usajili magari wakiona yako mengi kidogo lazima uende ........ili muende sawa
 
BRELA INAKIMBIZA WAWEKEZAJI.

Na Bashir Yakub, WAKILI.
+255 714 047 241

Mfumo kama mfumo wa kusajili kampuni ni mzuri na unarespond haraka ila watendaji bado kabisa.

Nitatoa mfano na sina shaka kila mdau ambaye anasajili ama amewahi kusajili kampuni au biashara kupitia mfumo mpya wa Brela atakubaliana nami.

Ni hivi, unakamilisha docmnts na kusubmit online Brela. Unasubiri majib na baada ya muda unajibiwa ufanye marekebisho(Additional Information/correction is required.....,).

Unafanya marekebisho yote uliyoelekezwa na unasubmit upya. Baada ya siku au siku mbili dcmnt zinarejeshwa tena kuwa ufanye tena marekebisho(Additional Information/correction is required......).

Kinachouma sana na kukera sana ni kwamba haya marekebisho unayoambiwa ufanye kwa hii mara ya pili ni MAPYA. Kwa maana dcmnt zilivyorejeshwa mara ya kwanza hayakuwa matatizo ila mara ya pili yameonekana ni matatizo.

Unarekebisha mara ya pili na kusubmit tena. Unasubiri tena siku ama siku mbili au zaidi. Inarudishwa tena ikihitaji marekebisho(Additional Information/correction is required.....,).

Haya ya mara ya tatu nayo unakuta ni MAPYA. Maana yake hayakuonwa uliporudishwa mara ya kwanza, hayakuona uliporudishwa mara ya pili yameonwa mara ya tatu.

Unarekebisha tena na kusubmit. Unasubiri tena siku ama siku mbili au zaidi. Inarudishwa tena ikihitaji marekebisho(Additional Information/correction is required......,).

Haya ya mara ya nne nayo ni marekebisho MAPYA.
Maana yake hayakuonwa uliporudishwa mara ya kwanza, hayakuona uliporudishwa mara ya pili, hayakuona uliporudishwa mara ya tatu, sasa yameonwa mara ya nne.

Mchezo unaendelea hivyo mpaka mwezi au zaidi. Halafu unasikia Mtendaji Mkuu wa Brela inaiambia Serikali, Dunia, na Wawekezaji kuwa sasa Tanzania Brela inasajili Kampuni na Biashara ndani ya saa 24. Ni aibu sana.

Hoja sio kwamba marekebisho yasifanywe ama usajili ufanyike bila sifa kutimia, Laa hasha.

Hoja ni kwamba, huyu anayesoma dcmnt na kuzirejesha anashindwaje kupitia dcmnt nzima yote kwa umakini, akaorodhesha yoooote yanayotakiwa kufanyiwa marekebisho, ukairudisha ili yote yafanyike kwa pamoja.

Inakuwaje marekebisho yasionwe dcmnt ziliporudishwa mara ya kwanza yaje kuonwa mara ya pili na ya tatu na kuendelea.

Na bora ingekuwa kwamba kile ulichoambiwa kurekebisha umekirekebisha vibaya kwahiyo unatakiwa ukirekebishe vizuri zaidi, hapana. Hiki ulichoambiwa kurekebisha kinaachwa kwa maana kuwa umekirekebisha vizur unaletewa kipya kabisa ambacho hakikuwa kimeonwa mara ya kwanza, ama ya pili, ama ya tatu. Ni kero, usumbufu, na aibu kwa watendaji.

Msichojua ni kwamba wengi wanaosajili Makampuni na biashara ni Wawekezaji.

Anakuja mwekezaji kutoka nje unamuhakikishia kuwa ndani ya siku moja,mbili,tatu utakuwa umemsajilia Kampuni. Anasubiri siku, wiki, wiki mbili, tatu, mwezi mwezi na zaidi hakuna kitu.

Mimi kama Wakili, ama mtu mwingine aliyepewa kazi ya kusajili siwezi kukubali kuaibika kwa mteja wangu. Nitamwita, nitamuonesha majibu ya Brela kwenye system. Nitamuonesha marekebisho mapya ambayo hayakuwa yameletwa mwanzoni yanavyoletwa kila baada ya siku mbili au wiki.

Ataelewa kosa sio langu ni la BRELA. Ataondoka sababu hawez kusubiri zaidi anaingia gharama kubwa za Malazi. Ataenda kufungua Kampuni Rwanda au Kenya ambako kwa dhati yake kampuni inasajiliwa ndani au chini ya Saa 24. Hivi ndivyo tunavyopoteza wawekezaji kupitia Brela.

Lakini ni kero zaidi sababu kila marekebisho yanahitaji wanahisa ama wakurugenzi wasaini. Utawaita kusaini mara ngapi. Na vipi kama walisaini wakaondoka na kwenda mbali.

Kuna mda unawaza labda pengine aliyepitia kazi mara ya kwanza siye aliyeipitia mara ya pili, na siye aliyepitia mara ya tatu, pengine ndo maana kila mtu ametaka marekebisho yake tofauti.

Kama ndivyo, basi hiki ndicho kirusi chenyewe. Ina maana Brela haina STANDARD moja ya kazi kiasi kwamba kila mtu ana marekebisho yake. Yaani marekebisho sio STANDARD bali mtazamo wa mtendaji. Utumishi wa hovyo na wa Kijima kabisa.

Inakuwaje jambo ambalo jana mtendaji fulani alipitia na kuliona sio la marekebisho, mtendaji aliepitia leo akaona ni la marekebisho, na mwingine anayepitia kesho kutwa akaona jingine ambalo wa jana hakuona, na mwingine wa mtondogoo akaona jingine ambalo wa juzi hakuona, hivyo na hivyo na kuendelea. Wallah kazi haziwezi kufanyika hivyo. Huu ni mchezo na masihala.

Au mpaka mtu amuone mtu, ujinga mtupu. Waulizeni wadau wa usajili hasa Mawakili na Wanasheria kama hiki nilichoeleza ni tatizo ama hapana mtapata majawabu.

Tunataka mtu akisubmit kazi, mtendaji anayeshika hiyo kazi aipitie kwa umakini na kuainisha marekebisho yooote lwa pamoja(kama yapo), na asiache hata moja.

Kisha arejeshe hiyo kazi ili yafanyiwe marekebisho na mhusika. Kama yamerekebishwa vizur mpatie Certificate. Kama sio mrejeshee tena yale yale yamaliziwe na sio umletee mapya.

Ukileta mapya tafsiri yake ni kwamba ile mara ya kwanza hukupitia kwa umakini. Ulizembea na hiki ndicho tunachopinga kwa nguvu zote. Kampuni itachukua mwezi na zaidi kusajiliwa.

Pengine hamjui umuhimu wenu katika Uwekezaji Tanzania. Ni hivi, Brela ndio mlango ama hodi ya uwekezaji. Sababu mwekezaji hawezi kwenda hata TIC au Immigration kama hana certificate ya Brela. Mwekezaji lazima aanzie Brela kwanza ndo aende kwingine.

TAFADHALI Brela Acheni Kukimbiza Wawekezaji.
kuna madogo ukitoa kitu kidogo siku 2 tu unapata usajiri wapo pale chini Brela.mimi mpaka sasa maombi 3 tofauti nimelipa .mpaka leo akuna kitu
 
BRELA imekuwa taasisi ya ovyo kabisa wakati huu! Ni bora enzi huko nyuma tunapanda lifti zao zilizokuwa na dereva pale ushirika!
Kwa uchungu nasema hivi nilianza ku- update taarifa za kampuni yangu toka mwaka jana tarehe 11/04/2020 ! Kila niki- submit document wanaleta issue mpya ! Unasubmit baada ya siku tatu wanarudisha na wana- rise issue mpya hadi mwaka ukaisha nikachelewa ku- submit documents za kuomba leseni mahali.

January hii wameniletea invoice baada ya kufanya assessment nikajua nimekamilisha nikalipa karibia milioni 1.5 wakaniambia ni- upload pay in slip ya malipo nikafanya hivyo!

Baada ya siku 3 naangalia ili niendelee na hatua nyingine nakuta wananiambia ni- upload company consolidation form nimewambia nilishafanya hivyo mpaka nimefanyiwa assessment na nimelipa hawataki kunielewa kabisa! Niameanza mchakato upya! BRELA ni taasisi ya HOVYOOOOOOOOOOOOOOO KABISA!
 
Aisee iyo rudisha ondoa ongeza inakera sana hawapo kwaajili ya kusaidia watu wenye nia ya kuanzisha biashara hawa jamaa hawajui maaana ya muda kabisa!

Unaweza cheza nao miezi zaidi ya miwili

Kwa mtu ambaye alisha wahi kusajili anajuwa kabisa apo umesema 100% ukweli
 
Hii nchi Kuna watumishi wanaihujumu. Brela ni namba moja.

Kama mheshimiwa raisi anasoma hii meseji nakuomba uwafunge mtendaji mkuu wa Brela na Watumishi wengine wa brela. Wasihamishwe kazi ila wafungwe gerezani.

Mimi nilisajiri kampuni kwa miezi mitatu na kulikuwa Hakuna sababu yoyote ya msingi. Imagine eti unarudishiwa ufanye marekebisho kwa kutokuweka mkato kwenye sentence. Najua watakuja humu kujitetea ila serikali siku moja itume watu wa usalama pale Brela makao makuu wavhunguze vilio vya watu.

Hivi watu wa usalama hawayaoni yanayoendelea Brela? Kwanini wasifungue kampuni feki walau 5 waone tunayoyasema Kama ni kweli au si kweli?

Huduma kwa wateja ni mbovu unaweza kupiga simu ukiwabishia Kitu wanakata simu. Customer service department ya Brela ni ya hovyo kabisa kusahi kutokea duniani.

Bila watu kuwa wanafungwa kwa kuisababishia serikali hasara Kama hizi sidhani Kama huu uzembe utakuja kuisha serikalini.

IMG_20210124_143329.jpeg
 
Mwaka Jana nilitaka kufungua kampuni Marekani kupitia Jimbo la Delaware Kama domestic company.

Ila kilichonishangaza ni jinsi mfumo wao ulivyokua direct, yaani kama una documents zote ambazo zinatakiwa ndani ya siku moja unakamilisha kila kitu under usd 400.

Ila ukija BRELA utasumbuliwa sana kuna saa najiuliza tunakwama wapi, tunasundwaje kuwa na mfumo ambao uko direct kama nchi za wenzetu.
 
Kwanini unapenda kuifananisha Marekani na Tanzania? Hao jamaa wapo very advanced kuliko nchi nyingi sana hapa duniani.

Marekani wanapiga kura ya Veto huko UNSC. Tanzania wanazo hizo nguvu za kisiasa?

Matatizo ya Afrika yanahitaji ufumbuzi wa kiafrika na sio kila kitu kuiga kutoka Ulaya na Marekani.
 
Ninaowateua Wameshindwa Kufikiria Nje Ya Box. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
 
Ninaowateua Wameshindwa Kufikiria Nje Ya Box
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
 
Kwanini unapenda kuifananisha Marekani na Tanzania? Hao jamaa wapo very advanced kuliko nchi nyingi sana hapa duniani.

Marekani wanapiga kura ya Veto huko UNSC. Tanzania wanazo hizo nguvu za kisiasa?

Matatizo ya Afrika yanahitaji ufumbuzi wa kiafrika na sio kila kitu kuiga kutoka Ulaya na Marekani.
Huzijui kero za brela
 
Back
Top Bottom