Bosi wangu ananuka mdomo, nifanyeje?

Bosi wangu ananuka mdomo, nifanyeje?

Kuna magonjwa kama constipation na halitosis....
Haya hata upige mswaki mara 20 kwa siku, tatizo halikuachi na linazidi kuwa kubwa kila uchao......
Kwani constipation ina affect vipi kinywa? Mimi nadhani labda wakati wa kucheua. Labda wewe ni Dr. unaweza kutusaidia kutueleza hili.
 
Hyo hali inaitwa halitosis.
Inasbabishwa na kutopiga mswaki kisahihi na pia uchafu unaoganda kwenye meno(calculi) mara nyingi hapa meno ya mbele taya ya chini wengi unakuta kuna layer imeganda na watu wanachukulia kawaida kumbe ni uchafu unaokuwa unaganda kwa mda mrefu na unatoa harufu kali sana.
Solution moja inabd watu tukumbuke kufanya dental cleaning(hospitali hii) kutoa calculi zote kwenye meno alafu kupiga mswaki kwa usahihi iwe ni kila siku.
Mtu anapiga mswaki meno ya mbele tu tena kwa nje huyo karud! Lazima mdomo unuke. Inatakiwa meno uyasafishe na mswaki both side kwa usahihi then na ulimi uisisahau.Pia fanya flossing inasaidia kutoa particles ambazo hazijafikiwa na mswaki. Na unaweza pata kamba ya flossing pharmacy.
Hayo hapo juu kwa ujumla yatakusaidia sana kutunza kinywa chako na ukawa na harufu nzuri.

Kuhusu boss wako mkuu mtumie sms hata kwa namba ngeni ukieleza kinaga ubaga juu ya jambo lake nadhan ataufanyia kazi hata aki mind hatajua nani katuma.
 
Nawewe anza kunuka tu kwani hujui kama bosi akicheka na wewe inakubidi ucheke?
 
Ugonjwa wa kunuka mdomo unaongezeka, ukitaka kuthibitisha chunguza ndani ya daladala au mwendokasi, na hata wakati mwingine makanisani.

Sijajua watu wanaugua hivi kwanini lakini nijuacho ni kwamba hakuna watu wakorofi kama wanaonuka mdomo hasa ukiwaambia wananuka mdomo.

Sasa ugonjwa huu umeanza kuvamia na maofisini. Bosi wangu ananuka mdomo, sijui ni kwa sababu hapigi mswaki au ana matatizo ya kiafya.

Nimesema walivyo wakorofi wanaonuka mdomo. Sasa kama bosi ukimwambia kuwa ananuka mdomo, basi ndiyo kabisa, afadhali na wale wa kwenye daladala.

Nisaidieni jinsi ya kumfanya bosi wangu ajijua kuwa ananuka mdomo, maana inanikera.
Akikuongelesha ziba pua
 
kama kuna sanduku la maoni kazini kwenu mchane huyo boss ila huku ukimpa solution,kama hakuna sanduku tegea hayupo ofisin andika barua halafu pitisha mlangoni kwake chini ataipata tu na kusoma na hatojua nani kaandika na ujumbe utakua umemfikia barabara

cha kuongezea ni kwamba watu wengi hawajijui kama wananuka midomo,kuna uwezekano hata wewe boss wako anaweza akawa anakuona unanuka mdomo vile vile ila anashindwa kukuambia vile vile
 
Pole mkuu, hata nyinyi humu JF wapo wanaonuka midomo nadhani. Siyo hiyo tu hata vikwapa.

Midomo kunuka inabidi kupiga mswaki kila unapomaliza chakula iwe asubuhi, mchana na jioni. Mswaki si meno bali gums na hasa ulimi maana ndo unabeba uchafu mwingi. Vikwapa ni kununua Deodorants kama huwezi basi tumia limau au hakikisha huna nywele kwenye vikwapa na utumie sabuni inayonukia. Mimi siyo daktari ila ni uzoefu wangu tu.
ongezea na kufanya flossing kila siku na pia kutumia dawa za kusukutua kama medi oral kama mara mbili kwa week,usitumie kila siku kuna bacteria utakua unawaua ambao wana manufaa mdomoni
 
Ni wachache Sana wanaijua harufu ya midomo Yao
Naona watu wanajimwaga Tu, si ajabu na wao Wana haalllufu haallluuffu Kali Tu

Afya ya kinywaji inahitaji msaada wa fakitari wa Meno
Fakitari wa meno?
 
Ofisini kwenu hakuna sanduku la maoni mpka uje ulalamike huku si mwambie ata boyifurendi wako aandike unacholalamika mpka na anuani ya boss akifika tu unajifanya kumwambia kuna barua yako nmeikuta kwenye sanduku la maoni
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] piga kazi mkuu.... Harufu yamdomo muachie muhusika
 
Kuna kunuka mdomo kunakosababishwa na Kisukari.

Inawezekana kuna ongezeko la Kisukari kutokana na lifestyle changes, watu kunywa pombe na kula nyama sana, kutofanya mazoezi, kuongezeka uzito etc.
Mbona etoa sababu aa obesity?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom