Boris Johnson akashifu wanawake wavaa hijab

Boris Johnson akashifu wanawake wavaa hijab

okay thanks a bunch, sasa kwamba hiyo ni kashfa kwa wavaa hijab ni mawazo yako wewe! Hakuna mahala rasmi pameandikwa Boris Johnson awakashifu wavaa hijab. Kwa sababu hawakubaliani Waingereza wote kwamba hijab ni njema, wapo wanaomtetea Boris Johnson.

tamaduni za Magharibi ni tofauti na utamaduni wa waarabu, tusilazimishe kuwamezesha kooni matamaduni ya kigeni wenyeji wanapotukaribisha tuishi kwao.

hakuna mahala Quran Takatifu imeongelea kuvaa hijab, niqab wala burka

in fact, hakuna mahala popote kwenye Quran Takatifu pameongelewa uvaaji wa Muislam period.

kwa hiyo ukiona mtu Kariakoo kavaa suruali ya dont-tachi na barakashia na kanzu, huo sio uislam, ni ma-utamaduni ya Uarabuni tumeyabuguia jumla. On the other hand huwezi kwa miaka milioni kukuta muarabu kavaa kitenge cha Mswahili au lubega la Mmasai...

facial expression, eye contact and positive identification of who the hell you are in public space are time-honored values of the western culture...

Hijab, Niqab, Burka zimepigwa marufuku Morocco, Cameroon, Chad, Republic of the Congo, Gabon, Austria, Denmark, France, Belgium, Tajikistan, Latvia, Netherlands pamoja na China
Hivi kumbe Qur'an haijaelekeza kuvaa hijabu,nilikuwa sijui
 
Ulichotakiwa kuongelea ni utamaduni na sio imani. HAKUNA IMANI BILA MATENDO
Basi endelea kuabudu bila kuzingatia tamaduni na taratibu za jamii husika uone kitakachokupata.
 
mwee... nchi ina hanki ya kuchagua vile wageni wanavaa. ukienda saudi arabia mbona unalazimishwa kujifunika? so kama wao waingereza hawataki they have every right to decide so. hupendi basi ondoka.
 
unaharibu vipi utamaduni wa watu kwa mavazi yako!?..na usipokula wanavyokula wao pia utakua inaharibu
Kwamba hujui maana na uapana wa tamaduni katika jamii? Hizi ndo hupelekea kuwepo kwa sheria zinazopitishwa na jamii husika.

Sasa kama jamii inaamini kuvaa ninja ni vibaya kwao unalazimishaje ukavae ninja?

Sasa subiri wakushughulikie.
 
Hujui Nguvu ya Imani
Hehe nguvu ya imani kwenye mazingira ambayo hayakuruhusu!

Kafuge nguruwe maeneo wanakokaa watu wanaoamini nguruwe ni wabaya kwao, ndo utajua imani yako ilivyo na nguvu.

Mfano mzuri ni zanzibar, watu wanapigwa kula hadharani wakati wa ramadhani ilihali wanajua sio wa imani hiyo na kufunga ni hiali.
 
Kwamba hujui maana na uapana wa tamaduni katika jamii? Hizi ndo hupelekea kuwepo kwa sheria zinazopitishwa na jamii husika.

Sasa kama jamii inaamini kuvaa ninja ni vibaya kwao unalazimishaje ukavae ninja?

Sasa subiri wakushughulikie.
unaleta ushabiki tu unaoshawishiwa na udini..kama hutaki watu wa tamaduni zingine usiruhusu waingie
 
Hehe nguvu ya imani kwenye mazingira ambayo hayakuruhusu!

Kafuge nguruwe maeneo wanakokaa watu wanaoamini nguruwe ni wabaya kwao, ndo utajua imani yako ilivyo na nguvu.

Mfano mzuri ni zanzibar, watu wanapigwa kula hadharani wakati wa ramadhani ilihali wanajua sio wa imani hiyo na kufunga ni hiali.
Haya na mawazo ya mtu anayetazama mambo kwa macho ya nyama na sio ya Rohoni
 
Aliyekuwa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Uingereza bwana Boris Johnson yuko kwenye mgogoro na chama chake cha Conservative kufuatia ujumbe wake kwenye gazeti kuhusu wanawake wavaa hijabu na baibui.
Mjadala wa kamati ya maadili ya Conservative unafikiria kumwajibisha bwana Johnson kwa kumtaka kuomba msamaha hadharani. Hata hivyo wanawake wavaa hijab wamepinga adhabu ya bwana Johnson kuomba msamaha hadharani wakidai kuwa adhabu hiyo ni ndogo sana. Wanawake hao wameweka shinikizo bwana Johnson avuliwe uwanachama.

Wengi wanasema kumvua bwana Johnson uwanachama kutaleta mgawanyiko mkubwa katika chama. Bwana Johnson ni chaguo la wengi ndani ya chama kuwa mrith wa Theresa May ambae ni waziri mkuu wa sasa.
Maneno aliyoandika bwana Johnson yaliyomletea matatizo ni kuwa wanawake wavaa hijab hufanana na masanduku ya kupostia barua au wezi wa benki “.
Bwana Boris Rafiki yangu sana wakati nikiwa london nikifanya field kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza bwana John Major. Namkumbuka Boris tulivyokuwa tukipiga naye bia aina ya TOBOG pale Zone 3 London
 
Haya na mawazo ya mtu anayetazama mambo kwa macho ya nyama na sio ya Rohoni
Hehe sawa mkuu, endelea kukinzana na hili kuna siku utaweka banda la nguruwe pembeni ya msikiti na watakuonesha nini maana ya kuheshimu taratibu na imani za wenzako!
 
mbona wanafuga tu na mabucha yapo sehemu ambazo wala nguruww ni wa kuhesabu..njoo kigogo sambusa
Hehe sasa unasemea huko uswazi ambako hawako serious, nenda kayafanye huko nchi za kiislamu hata hapo zanzibar kaweke banda la nguruwe kando kando ya msikiti halafu utaniletea mrejesho!
 
Back
Top Bottom