Bongo Star Search ni janga la kitaifa

Bongo Star Search ni janga la kitaifa

Kuna wengine wanaenda kujazia foleni tu. Hata ukimuuliza mazoezi amefanya lini na ni nani kamsikiliza hana.
Ila wale wanaoonekana serious wanapokatwa inauma
 
Hao Master Jay na salama wamesoma wapi huo muziki? Ni wahuni kama wahuni wengine tu wenye njaa kama ilivyo ada Bango!

kama majaji wangekua lady jaydee. mwana fa na alikiba. Hao wanafaham mziki ni nini.

Master jay yeye ni producer .salama janja ya mjini.ile.
kidogo madam lita yupo vizuri kwenye mziki
 
Umeongea Ukweli Ndugu, Mimi Huwa Ni Mtu Wa Kukosoa Humu Jukwaani, Ila Nimekuunga Mkono Bss Ni Janga La Taifa Wanawakatisha Tamaa Vijana, Ntaleta Andiko Langu Katika Ubora Wangu Baada Ya Nusu Saa Nikimaliza Hii Castle Charles Glass Kuwahusu Hawa Majaji Uchwara Wa Bss
 
Utakuta mtu anaimba eti,maua mazuri yapendezaaaaa.sasa hapo unategemewa apewe majibu gani.
 
dilemma

Salama Jabir si mwanamuziki na hajawahi kuwa mwanamuziki, Master J ni dj japo anajiita a producer. So in theory hawana lolote. Tatizo kubwa la watanzania huwa tunapenda sana kuiga watu na vitu toka nje bila hata uzingatiaji. Hii star search mimi ni muda mrefu huwa siiangalii hata kidogo, ni upuuzi mtupu.
 
Last edited by a moderator:
Jana tu niliwaza hilo huyo master j ni mibangi ndo inayomtia kiburi huyo salama ni stress za Maisha tu
 
Hiyo ni show tu wenzako wanatafuta hela na kuongelewa kama wewe unavoongelea,yani wanaweka na drama humohumo kwahyo wewe chukulia poa kua wameambiana wewe uwe mtu wa aina hii na sisi tuwe watu wa aina hii.
 
Ungekuwa 'intellectual' ungetumia hata nukta ya akili yako kujikumbusha hata wanamuziki walotusua wanavyopigwa mawe mbaya kila kukicha!kwenye muziki LAZIMA ukaze,vinginevyo katunge shanga.,nayo ni kazi pia!
 
kiukweli kila nikiangalia hiki kipindi sijaweza kutambua ni vigezo gani wanatumia . Mshiriki hajamaliza hata line moja ya wimbo tayari anaambiwa toka nje, hujui kuimba, wasalimie nyumbani n.k inakatisha tamaa
 
Hivi Kuna msanii anayevuma ambaye ni zao la BSS

Wapo, Kala jeremaya na Peter Msechu kama sikosei

Ila ni kweli salama na master J wanawashushua sana wale vijana but wale vijana nao wengine hawako serious kabisa
 
Kumbe Msechu sio zao la BSS, ni Tusker what waht ile ya Kenya.............

niltaka kumsahau ndo hapo kwenye mashaka maana naye hukuwa mshindi wa kwanza..Mimi walakin wangu ni pale washindi wao kuto fanya vile ilivyokusudiwa maana hupewa karibu kila kitu mpaka promo sasa kwanini hawa zai matunda??
 
Ulitaka wasifiwe hata kama hawana uwezo wo wote wa kuimba?

Hizo sifa zisizo na mpango ndizo zinazowalegeza watanzania.

Mimi huwa naangalia na kuna wengine wanaimba kama kobe, wengine kama ngamia na wengine hawana hata idea nini wanatakiwa kufanya. Sasa wapewe sifa za nini?

wengine hawaimbi kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom