niltaka kumsahau ndo hapo kwenye mashaka maana naye hukuwa mshindi wa kwanza..Mimi walakin wangu ni pale washindi wao kuto fanya vile ilivyokusudiwa maana hupewa karibu kila kitu mpaka promo sasa kwanini hawa zai matunda??
dilemma
Salama Jabir si mwanamuziki na hajawahi kuwa mwanamuziki, Master J ni dj japo anajiita a producer. So in theory hawana lolote. Tatizo kubwa la watanzania huwa tunapenda sana kuiga watu na vitu toka nje bila hata uzingatiaji. Hii star search mimi ni muda mrefu huwa siiangalii hata kidogo, ni upuuzi mtupu.
only Kala wengine wote na walio pata milioni hamsini hawajulikani
Mi ndo ningekuwa mmiliki wa BSS ningeweka na askar wa kukamata wazembe maana kuna wengine wanaenda kuleta masihara.
Ila kiukweli kadri siku zinavyokwenda ndio inazidi kupoteza mvuto kwanza kwa sie naona wanatupotezea muda bora wangetuachia ile tamthilia yetu pendwa tuendelee kuitazama .
Kwa nini wenye mawazo tofauti msianzishe shindano mbadala? Dunia haiwezi kuendelea kwa kulalamika. Hii ni opportunity, seize it man!
Kwa hili ulilosema, nilitegemea mjadala ungefungwa watu wangeenda kuandaa shindano lao.
Watz tuna safari ndefu sana.
Dar City, to seize opportunity is not simple! Unaanza vipi kama unatoka katika familia masikini kama za kwetu! Hawa unaowaona kuna mahali walianzia tena usiseme kama ni wanawake- men are at work. Ila nakubaliana na wewe kuwa na mawazo mbadala na kuwa na wazo la kukattaa udhalilishaji. Kama ulivyosema ni vizuri kuwa-encourage vijana kuthubutu. Jay na Salama ni wadhalilishaji wa vijana masikini wanaotafuta pa kuponea
Unajua watanzania tunalia lia sana kiasi kwamba huwezi kujua tunaweza nini na kipi hatuwezi.