RWAYA: BOMU
Mwandishi; Halfani Sudy
Simu 0652 212391
Sehemu ya Ishirini na sita
Daniel Mwaseba na Adrian Kaanan Kaanan kwa tahadhari kubwa sana walielekea kule nyuma ya ile nyumba ya kulala wageni ya Platnumz.
Daniel alikuwa mbele, Adrian akifuatia nyuma. Bastola mikononi mwao. Macho yakizunguka kila upande kwa umakini na kasi. Yakiitafuta hatari!. Yakimsaka adui!.
Kule porini alipokuwa David bado alikuwa anaangaza huku na kule. Lakini hakuambua lolote, michirizi ya damu ilikuwa imeishia palepale, na kutengeneza kidimbwi kidogo cha damu.
"Nini kilitokea hapa?. Mbona hii michirizi ya damu hakuna inapoelekea. Kwanini michirizi hii iishe ghafla. Au walipofika hapa waligundua kwamba hii michirizi ya damu itakuwa tatizo kwao?. Na kuamua kuidhibiti?" David alikuwa anajiuliza mwenyewe, lakini hakuwa na jibu hata moja.
Alikata shauri kuwasubiri kina Daniel Mwaseba watafute majibu kwa pamoja.
***
Martin Hisia, mwanaume mwenye Hisia zake nd'o alikuwa anaingia Vikindu. Kichwani mwake alikuwa anawaza kitu kimoja tu, kuhakikisha mpenzi wake, Felisia, anakuwa salama.
Leo hii aliamini usahihi wa hisia zake tangu siku ya kwanza aliyokutana ba Felisia. Alikumbuka kila kitu kilivyotokea siku ile katika klabu ya Bilcanas. Lakini kwa sasa hakujari hayo. Alikuwa anataka kitu kimoja tu, kuhakikisha Felisia anakuwa salama. Alitambua sana matokeo ya kitendo cha hatari alichokifanya Felisia. Huku akijua kwamba adhabu yake ni moja tu endapo atastukiwa.
Kifo!!
Na yeye hakutaka hata kidogo Felisia afe kwa namna yoyote ile.
Felisia Nyenyembe. Mwanamke waliyekutana kama bahati tu katika klabu ya usiku ya Bilcanas...
Siku hiyo Martin alikuwa ametoka kukamilisha misheni moja ya hatari sana. Misheni ambayo iliisha kwa mafanikio makubwa sana kwake, na kuhakikisha bilioni sita zilizoibwa kutoka katika benki ya wakulima zinarudi salama katika benki hiyo. Huku watu wote waliohusika na wizi katika benki hiyo wakitiwa katika mikono ya dola.
Siku hiyo jioni ndipo alipoenda katika klabu ya muziki ya Bilcanas kujipongeza kwa kazi kubwa aliyoifanya.
Baada ya kunywa sana pombe, ndipo alipoamua kuingia sehemu ya kuchezea naye aoneshe ujuzi wake katika fani hiyo. Wimbo uliokuwa unapigwa ni 'Fool again' wa kundi la muziki la West life.
Martin aliucheza haswa wimbo huo, akichagizwa na pombe zilizokuwa zimejaa pomoni kichwani mwake.
"Tunaweza cheza pamoja?" Sauti ya kike nyembamba ilipenya katika masikio yake. Martin alimwangalia mmiliki wa sauti hiyo aliyekuwa mbele yake.
Blauzi nyeupe yenye kung'aa, suruali ya jeans fupi iliyombana vyema na viatu vya mchuchumio kwa chini vilikuwa ni vitu alivyovitazama kwa haraka.
"Huyu ni mtoto haswa" Alijisemea kimoyomoyo.
Martin hakuwa na nguvu za kukataa ombi la binti huyo, ingawa hisia zake zilimwambia kwamba hakuwa mtu mzuri.
Kwa mara ya kwanza katika maisha yake Martin Hisia alipingana na Hisia zake. Hisia zilizoanza tangu akiwa mtoto mdogo na kuaminiwa na kila mtu.
Ilikuwa Martin alikuwa akihisi kitu basi lazima kitatokea. Na hili lilimfanya jina la babaye mzazi liondoke na kuitwa Martin Hisia.
"Usijari dada. Twaweza cheza, tena hadi majogoo ukitakaa" Martin alisema kwa sauti ya kilevi.
Na DJ alibadili wimbo. Sasa ulikuwa unaimbwa wimbo wa 'My love' toka katika kundi hilohilo la West life.
DJ kama alijua kuweka wimbo huo. Maana penzi jipya ndio lilikuwa linazaliwa mjini. Hadi wimbo laini wa 'My love' ulipoisha Martin alikuwa ameshadadisi kila kitu. Sasa alikuwa analijua jina la yule binti, mahali anapoishi na kazi anayoifanya hapa mjini. Yote hayo waliulizana wakati wimbo wa 'My love' ukikita katika spika za klabu ya Bilcanas.
Martin alihisi lakini hakutilia maanan. Pombe, ukichanganya na hisia kali za mapenzi basi zilimfanya aendelee kuzidharau hisia zake. Hakujua kwamba yule alikuwa ni wakala wa Imma Ogbo aliyetumwa kwake kwa kazi maalum.
Tangu siku hiyo Felisia akawa mpenzi wa Martin Hisia, huku akipeleka taarifa mbalimbali za Martin kwa Imma Ogbo.
Katika moyo wa Martin Hisia alitokea kumpenda sana Felisia. Felisia alikuwa mwanamke aliyekamilika haswa. Wa kupendwa na kila mtu. Hata wewe...
Ukiacha weupe wake wa asili sio wa kuchanganya na carotone na maji ya diana, sura nzuri na shepu ya kufa mtu, Felisia alikuwa na ya zaidi. Alikuwa mpishi mzuri sana jikoni. Alikuwa anajua kupika kila aina ya chakula na kuwa kitamu sana. Pia Felisia alikuwa malaya sana kitandani. Alikuwa anaweza kufanya mitindo ya kila aina ya mapenzi tena kwa umahiri wa ajabu sana. Huku akilia kwa milio ya kushangaza. Hili la kitandani lilimmaliza sana Martin. Akawa hana uthubutu wa kumuacha hata kidogo ingawa alikuwa anamtilia shaka mara kadhaa kwa matendo yake.
Siku moja, usiku wa manane wakiwa wamelala kitandani simu ya Felisia iliita. Felisia aliamka na kumwangalia Martin kama amelala. Martin alijifanya ametopea usingizini.
Kumbe haikuwa hivyo..
Martin alikuwa anasikia kila kitu!
Felisia alinyanyuka pale kitandani taratibu. Kuhakikisha hamuamshi Martin, alielekea bafuni na simu yake mkononi. Martin naye aliamka kitandani na kumfuata kwa nyuma Felisia hukohuko bafuni.
Kule bafuni Felisia alipiga simu yake kwa Imma Ogbo. Akawa anaongea kwa sauti ndogo sana. Martin alijaribu sana kusikiliza akiwa nje ya mlango wa bafu, lakini aliambulia maneno mawili tu.
Misheni na Daniel Mwaseba..
Felisia alikata simu, na kuelekea chumbani. Alimkuta Martin akiwa amelala vilevile. Akaamini kwamba maongezi yake na Imma Ogbo hayajasikiwa na kiumbe chochote kile hapa duniani.
Kumbe haikuwa hivyo.
Martin kichwa kilimuuma kwa mawazo, huku akiwa anatamani amfahamu huyo aliyekuwa anaongea na Felisia usiku wa manane. Hisia za wivu zilimtawala zaidi ya hisia za kipelelezi. Maneno mawili aliyoyasikia kwenye simu yalikuwa ya muhimu sana kwake kuyafanyia kazi, lakini alipotezea. Mapenzi yalikuwa yamemlevya. Akadharau kazi.
Asuhuhi kulikucha. Kabla hawajatoka kitandani wakafanya mapenzi ya asubuhi. Wenyewe walikuwa wanaita 'morning glory'.
Kwa utundu alioufanya Felisia asubuhi hii, yalimsahaulisha kila kitu Martin Hisia.
Kila siku mwanamke huyu alikuwa mpya kitandani, alikuwa anakatika kiajabu huku akitoa kilio mithili ya ndege chiriku.
Alivyotoka hapo alimpikia chai yenye viungo mbalimbali na chapati zilizokaangwa kikike. Huku pembeni kukiwa na supu ya kuku iliyopikwa ikapikika. Hapo alikuwa tayari katoka kuogeshwa kwa maji ya moto na kusuguliwa kila sehemu ya mwili wake.
Unafikiri hata alikumbuka simu ya jana usiku?
Alichokumbuka ni kumweka kifaa kidogo maalum mithili ya punje ya mchele, katikati ya nywele za Felisia zilizosukwa kwa mtindo wa yebo fasta, kifaa hiko kikimwezesha Martin kujua uelekeo wa Felisia..
Yote hayo ulikuwa ni wivu tu..
***
Imma Ogbo na Dr Louis walikuwa katika nyumba ya balozi wa Nigeria hapa nchini. Walitoka kule Vikindu kwa mtindo wa ajabu wakisaidiwa na balozi Agdir na kusalimika kutiwa mkononi na wakina Daniel Mwaseba.
Felisia yeye, alikuwa katika stoo ndogo iliyopo ndani ya nyumba hiyo, akiwa uchi wa mnyama huku akiwa amefungwa kamba ngumu mikononi na miguuni.
Mwili mzima ukiwa umevimba huku akiwa anabubujikwa na damu sehemu kadhaa. Jicho lake moja lilikiwa likiwa limetolewa na kubaki shimo baya na la kutisha! huku mkono wake wake wa kulia akiwa hana kidole cha mwisho. Kilikuwa kimekatwa!
Hiyo ilikuwa kazi ya Imma Ogbo katika kumfanya Felisia aseme alikuwa anampigia nani simu kule chooni.
Lakini pamoja na mateso yote hayo bado Felisia alikuwa mgumu kufunguka, huku akidai alienda bafuni kujisaidia sio kupiga simu. Utetezi huo haukuingia hata kidogo katika kichwa cha Imma Ogbo na kumuahidi atarejea tena!
Na hapo ndipo atasema hata asivyoulizwa.
Je nini kitatokea?
Lako Jicho.
Hadithi hii itapatikana yote kwa njia ya whatsapp siku ya jumanne kwa sh 3000 tu.