BOMU: Riwaya ya kipelelezi (1)

BOMU: Riwaya ya kipelelezi (1)

RIWAYA; BOMU
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU 0652 212391

Sehemu ya Ishirini na Tano

Daniel akagonga mlango wa chumba cha Lion kwa kutumia mdomo wa bastola.

Ngo ngo ngo..

Mlango ulikuwa kimya. Kimya cha kaburi.

Akagonga tena.

Ngo ngo ngo..

Ikawa kimya tena kama awali. Hakuna aliyejibu.

Kwa mbali, akasikia sauti za miguu kutoka mlango alioingilia. Akajua pale si mahali salama. Alipiga hatua tano kubwa kukimbilia ule upande lilipo bafu. Akabana katika kona moja. Macho yake yote mawili yakiwa katika mlango wa chumba cha Lion..
Je ni nani alikuwa anakuja?

Zile kelele za miguu alizozisikia zikaishia katika chumba cha Lion. Kutoka pale alipokuwa Daniel aliwaona vizuri watu wale wawili.

Alikuwa Adrian Kaanan na yule dada Mhudumu.

Daniel alimwona Adrian akigonga ule mlango kama alivyokuwa anagonga yeye. Sasa mlango ule uligongwa kwa mara ya tatu na watu wawili tofauti.

Daniel na Adrian..

Adrian akagonga tena. Huku hofu dhahiri ikionekana katika sura ya yule mhudumu kila mlango ulipokuwa unagongwa. Bila shaka alikuwa anahisi kwamba walikuwa wanaibishia hodi hatari.

Adrian akashika kitasa cha mlango. Akakizungusha. Kikazunguka taratibu. Na mlango ukaanza kufunguka.

Adrian alikuwa anausukuma taratibu mlango kwa mkono wa kushoto. Huku mkono wa kulia ukiwa umeshikilia bastola iliyoondolewa usalama. Tayari kufanya shambulio!!

Tayari kwa kumfyatua Imma Ogbo!

Kwa mwendo wa taratibu akajitosa mle chumbani. Huku akimwacha yule mhudumu kwa nyuma. Ngoja sasa tumtambue jina lake, alikuwa anaitwa Merina.

Adrian alikutana na chumba kisichokuwa na mpangilio. Godoro lilokuwa chini huku kabati kubwa likiwa limeegeshwa upande. Chandarua kilikuwa kimekatwa. Runinga ikionesha picha bila sauti.

Macho ya kipelelezi ya Adrian yalitazama kila mahali mle ndani. Kwasasa wala hakukuwa na mtu, lakini kwa mazingira waliyoyakuta ilionesha kwamba kulikuwa na watu, tena wamefanya vurugu ya kutosha.

Alitumia dakika tano kupekuapekua mle ndani. Hakuna chochote cha maana alichokipata.

"Nipo chumba cha Lion. Chumba kimevurugwa hasa. Hakuna mtu yeyote humu ndani" Adrian alisema kupitia kile kifaa cha mawasiliano.

"Nipo karibu na hiko chumba. Nakuja" Daniel alijibu.

"Mimi nipo pembeni hapa. Sehemu ambapo kuna jiko la hii guest. Nimeona michirizi ya damu. Nimejaribu kuichunguza, sio damu ya mnyama ni damu ya binadamu. Tena ya moto!" David alisema.

"Angalia mwelekeo wa hiyo damu. Inaweza kuwa damu ya adui" Daniel alisema.

"Nafanya hivyo Daniel" David alijibu.

Wakati huo Daniel alikuwa anarudi kuelekea chumba cha Lion. Huku akiwa makini kama awali.

Alifika.

Aliusukuma mlango na kuingia ndani, Merina akiwa nyuma yao. Naye aliushuhudia mvurugano akiousema Adrian. Chumba kilikuwa kimevurugwa haswa!!

"Nini hiki?" Merina alishangaa.

Hakuna aliyejibu.

Daniel kwa kutumia macho yake ya kipelelezi alianza kukichunguza kile chumba. Naye hakugundua kitu chochote kipya. Macho yake yalitembea mlemle yalipotembea macho ya Adrian.

"Tunyanyue godoro" Daniel alishauri.

Kwa kushirikiana na Adrian walilinyanyua lile godoro na kuliweka mahala pake.

Hapo ndipo walipoona kitu cha kushangaza..

Pale mahali lilipokuwa godoro walikutana na damu!

Kengele za hatari zikagonga kichwani mwao. Na maelezo ya David yaliwarejea vichwani mwao.


"Mimi nipo pembeni hapa. Sehemu ambapo kuna jiko la hii guest. Nimeona michirizi ya damu. Nimejaribu kuichunguza, sio damu ya mnyama ni damu ya binadamu. Tena ya moto!" Hayo yalikuwa maneno ya David.

"Damu!! Ina maana kuna mtu amejeruhiwa humu?" Adrian aliuliza.

"Bila shaka. Hii ni damu ya mwanadamu..kuna mtu alijeruhiwa humu ndani kabla hawa watu hawajatoroka" Daniel alisema.

"Tumechelewaa" Adrian alisema akiwa amekata tamaa.

"Usikate tamaa Adrian. Amini tunaenda kuwakamata hawa watu. Tupo karibu nao sana hivi sasa kuliko wakati wowote tangu sakata hili lianze" Daniel alisema.

Adrian alishusha pumzi kwa nguvu.

Mara sauti ilisikika katika vile vifaa vya masikioni. Ilikuwa ni sauti ya David.

"Hii michirizi ya damu imeenda hadi huku nyuma kabisa ya hii guest, porini huku. Hapa nimeikuta damu nyingi zaidi, inaonesha walipumzika hapa" David alisema.

"Baada ya hapo inaonesha hiyo michirizi ya damu ilielekea wapi?" Adrian aliuliza.

"Imekomea hapahapa. Hii michirizi haiendi sehemu yoyote tena.." David alisema.

"Tusubiri. Tunakuja hapohapo" Daniel alisema.

"Merina, hapa mlipangisha watu hatari sana. Kuweni makini sana msiruhusu guest yenu kuwa kichaka cha wahalifu" Adrian alisema.

Merina aliitikia kwa kichwa. Huku akijitahidi kuzuia machozi yakiyoanza kujenga ujirani na macho yake.

"Adrian twenzetu mahali alipo David. Tukiwa watatu bila shaka tutagundua kitu hapo.." Daniel alisema.

"Na Merina hakikisha hamumpangishi mtu chumba hiki. Pengine tutarudi tena na kukihitaji kukitumia kikiwa hivihivi. Pia usiwaambie chochote wahudumu wenzako wala wale wateja, fanya kama hakijatokea kitu. Lakini kama watakuja tena hao watu, piga mara moja namba hii" Daniel alisema huku akimpa business kadi Merina. Wakati akimpa akamtekenya kidogo katikati ya mkono. Merina alistuka kidogo na kumlegezea jicho Daniel. Daniel akalifinya jicho lake la upande wa kulia pia. Merina akalainika..

"Tutawasiliana" Daniel alimtoa katika mawazo Merina kwa kauli hiyo.

Kisha wakaondoka.

Je kina Daniel wataenda kukutana na nani huko? Je michirizi ya damu ni ya nani? Vipi tena Daniel na Merina, umewaelewa?
 
Story nzuri Sana,sema unachelewa Sana kuiweka, kiasi kwamba inafika muda tunasahau tulipotoka
 
RWAYA: BOMU
Mwandishi; Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Ishirini na sita

Daniel Mwaseba na Adrian Kaanan Kaanan kwa tahadhari kubwa sana walielekea kule nyuma ya ile nyumba ya kulala wageni ya Platnumz.

Daniel alikuwa mbele, Adrian akifuatia nyuma. Bastola mikononi mwao. Macho yakizunguka kila upande kwa umakini na kasi. Yakiitafuta hatari!. Yakimsaka adui!.

Kule porini alipokuwa David bado alikuwa anaangaza huku na kule. Lakini hakuambua lolote, michirizi ya damu ilikuwa imeishia palepale, na kutengeneza kidimbwi kidogo cha damu.

"Nini kilitokea hapa?. Mbona hii michirizi ya damu hakuna inapoelekea. Kwanini michirizi hii iishe ghafla. Au walipofika hapa waligundua kwamba hii michirizi ya damu itakuwa tatizo kwao?. Na kuamua kuidhibiti?" David alikuwa anajiuliza mwenyewe, lakini hakuwa na jibu hata moja.

Alikata shauri kuwasubiri kina Daniel Mwaseba watafute majibu kwa pamoja.

***

Martin Hisia, mwanaume mwenye Hisia zake nd'o alikuwa anaingia Vikindu. Kichwani mwake alikuwa anawaza kitu kimoja tu, kuhakikisha mpenzi wake, Felisia, anakuwa salama.

Leo hii aliamini usahihi wa hisia zake tangu siku ya kwanza aliyokutana ba Felisia. Alikumbuka kila kitu kilivyotokea siku ile katika klabu ya Bilcanas. Lakini kwa sasa hakujari hayo. Alikuwa anataka kitu kimoja tu, kuhakikisha Felisia anakuwa salama. Alitambua sana matokeo ya kitendo cha hatari alichokifanya Felisia. Huku akijua kwamba adhabu yake ni moja tu endapo atastukiwa.
Kifo!!

Na yeye hakutaka hata kidogo Felisia afe kwa namna yoyote ile.

Felisia Nyenyembe. Mwanamke waliyekutana kama bahati tu katika klabu ya usiku ya Bilcanas...

Siku hiyo Martin alikuwa ametoka kukamilisha misheni moja ya hatari sana. Misheni ambayo iliisha kwa mafanikio makubwa sana kwake, na kuhakikisha bilioni sita zilizoibwa kutoka katika benki ya wakulima zinarudi salama katika benki hiyo. Huku watu wote waliohusika na wizi katika benki hiyo wakitiwa katika mikono ya dola.

Siku hiyo jioni ndipo alipoenda katika klabu ya muziki ya Bilcanas kujipongeza kwa kazi kubwa aliyoifanya.

Baada ya kunywa sana pombe, ndipo alipoamua kuingia sehemu ya kuchezea naye aoneshe ujuzi wake katika fani hiyo. Wimbo uliokuwa unapigwa ni 'Fool again' wa kundi la muziki la West life.

Martin aliucheza haswa wimbo huo, akichagizwa na pombe zilizokuwa zimejaa pomoni kichwani mwake.

"Tunaweza cheza pamoja?" Sauti ya kike nyembamba ilipenya katika masikio yake. Martin alimwangalia mmiliki wa sauti hiyo aliyekuwa mbele yake.

Blauzi nyeupe yenye kung'aa, suruali ya jeans fupi iliyombana vyema na viatu vya mchuchumio kwa chini vilikuwa ni vitu alivyovitazama kwa haraka.

"Huyu ni mtoto haswa" Alijisemea kimoyomoyo.

Martin hakuwa na nguvu za kukataa ombi la binti huyo, ingawa hisia zake zilimwambia kwamba hakuwa mtu mzuri.

Kwa mara ya kwanza katika maisha yake Martin Hisia alipingana na Hisia zake. Hisia zilizoanza tangu akiwa mtoto mdogo na kuaminiwa na kila mtu.

Ilikuwa Martin alikuwa akihisi kitu basi lazima kitatokea. Na hili lilimfanya jina la babaye mzazi liondoke na kuitwa Martin Hisia.

"Usijari dada. Twaweza cheza, tena hadi majogoo ukitakaa" Martin alisema kwa sauti ya kilevi.

Na DJ alibadili wimbo. Sasa ulikuwa unaimbwa wimbo wa 'My love' toka katika kundi hilohilo la West life.

DJ kama alijua kuweka wimbo huo. Maana penzi jipya ndio lilikuwa linazaliwa mjini. Hadi wimbo laini wa 'My love' ulipoisha Martin alikuwa ameshadadisi kila kitu. Sasa alikuwa analijua jina la yule binti, mahali anapoishi na kazi anayoifanya hapa mjini. Yote hayo waliulizana wakati wimbo wa 'My love' ukikita katika spika za klabu ya Bilcanas.

Martin alihisi lakini hakutilia maanan. Pombe, ukichanganya na hisia kali za mapenzi basi zilimfanya aendelee kuzidharau hisia zake. Hakujua kwamba yule alikuwa ni wakala wa Imma Ogbo aliyetumwa kwake kwa kazi maalum.

Tangu siku hiyo Felisia akawa mpenzi wa Martin Hisia, huku akipeleka taarifa mbalimbali za Martin kwa Imma Ogbo.

Katika moyo wa Martin Hisia alitokea kumpenda sana Felisia. Felisia alikuwa mwanamke aliyekamilika haswa. Wa kupendwa na kila mtu. Hata wewe...

Ukiacha weupe wake wa asili sio wa kuchanganya na carotone na maji ya diana, sura nzuri na shepu ya kufa mtu, Felisia alikuwa na ya zaidi. Alikuwa mpishi mzuri sana jikoni. Alikuwa anajua kupika kila aina ya chakula na kuwa kitamu sana. Pia Felisia alikuwa malaya sana kitandani. Alikuwa anaweza kufanya mitindo ya kila aina ya mapenzi tena kwa umahiri wa ajabu sana. Huku akilia kwa milio ya kushangaza. Hili la kitandani lilimmaliza sana Martin. Akawa hana uthubutu wa kumuacha hata kidogo ingawa alikuwa anamtilia shaka mara kadhaa kwa matendo yake.

Siku moja, usiku wa manane wakiwa wamelala kitandani simu ya Felisia iliita. Felisia aliamka na kumwangalia Martin kama amelala. Martin alijifanya ametopea usingizini.
Kumbe haikuwa hivyo..
Martin alikuwa anasikia kila kitu!

Felisia alinyanyuka pale kitandani taratibu. Kuhakikisha hamuamshi Martin, alielekea bafuni na simu yake mkononi. Martin naye aliamka kitandani na kumfuata kwa nyuma Felisia hukohuko bafuni.

Kule bafuni Felisia alipiga simu yake kwa Imma Ogbo. Akawa anaongea kwa sauti ndogo sana. Martin alijaribu sana kusikiliza akiwa nje ya mlango wa bafu, lakini aliambulia maneno mawili tu.

Misheni na Daniel Mwaseba..

Felisia alikata simu, na kuelekea chumbani. Alimkuta Martin akiwa amelala vilevile. Akaamini kwamba maongezi yake na Imma Ogbo hayajasikiwa na kiumbe chochote kile hapa duniani.

Kumbe haikuwa hivyo.

Martin kichwa kilimuuma kwa mawazo, huku akiwa anatamani amfahamu huyo aliyekuwa anaongea na Felisia usiku wa manane. Hisia za wivu zilimtawala zaidi ya hisia za kipelelezi. Maneno mawili aliyoyasikia kwenye simu yalikuwa ya muhimu sana kwake kuyafanyia kazi, lakini alipotezea. Mapenzi yalikuwa yamemlevya. Akadharau kazi.

Asuhuhi kulikucha. Kabla hawajatoka kitandani wakafanya mapenzi ya asubuhi. Wenyewe walikuwa wanaita 'morning glory'.

Kwa utundu alioufanya Felisia asubuhi hii, yalimsahaulisha kila kitu Martin Hisia.
Kila siku mwanamke huyu alikuwa mpya kitandani, alikuwa anakatika kiajabu huku akitoa kilio mithili ya ndege chiriku.

Alivyotoka hapo alimpikia chai yenye viungo mbalimbali na chapati zilizokaangwa kikike. Huku pembeni kukiwa na supu ya kuku iliyopikwa ikapikika. Hapo alikuwa tayari katoka kuogeshwa kwa maji ya moto na kusuguliwa kila sehemu ya mwili wake.

Unafikiri hata alikumbuka simu ya jana usiku?

Alichokumbuka ni kumweka kifaa kidogo maalum mithili ya punje ya mchele, katikati ya nywele za Felisia zilizosukwa kwa mtindo wa yebo fasta, kifaa hiko kikimwezesha Martin kujua uelekeo wa Felisia..

Yote hayo ulikuwa ni wivu tu..

***

Imma Ogbo na Dr Louis walikuwa katika nyumba ya balozi wa Nigeria hapa nchini. Walitoka kule Vikindu kwa mtindo wa ajabu wakisaidiwa na balozi Agdir na kusalimika kutiwa mkononi na wakina Daniel Mwaseba.

Felisia yeye, alikuwa katika stoo ndogo iliyopo ndani ya nyumba hiyo, akiwa uchi wa mnyama huku akiwa amefungwa kamba ngumu mikononi na miguuni.

Mwili mzima ukiwa umevimba huku akiwa anabubujikwa na damu sehemu kadhaa. Jicho lake moja lilikiwa likiwa limetolewa na kubaki shimo baya na la kutisha! huku mkono wake wake wa kulia akiwa hana kidole cha mwisho. Kilikuwa kimekatwa!
Hiyo ilikuwa kazi ya Imma Ogbo katika kumfanya Felisia aseme alikuwa anampigia nani simu kule chooni.

Lakini pamoja na mateso yote hayo bado Felisia alikuwa mgumu kufunguka, huku akidai alienda bafuni kujisaidia sio kupiga simu. Utetezi huo haukuingia hata kidogo katika kichwa cha Imma Ogbo na kumuahidi atarejea tena!
Na hapo ndipo atasema hata asivyoulizwa.

Je nini kitatokea?

Lako Jicho.

Hadithi hii itapatikana yote kwa njia ya whatsapp siku ya jumanne kwa sh 3000 tu.
 
Dah Imma Igbo Martin hisia akikukamata utakunya kokoto haki ya nani
 
martin hisia namkumbuka sana ndani ya mkanda wa siri lakini uku amelala kupita kiasi
 
RWAYA: BOMU
Mwandishi; Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Ishirini na sita

Daniel Mwaseba na Adrian Kaanan Kaanan kwa tahadhari kubwa sana walielekea kule nyuma ya ile nyumba ya kulala wageni ya Platnumz.

Daniel alikuwa mbele, Adrian akifuatia nyuma. Bastola mikononi mwao. Macho yakizunguka kila upande kwa umakini na kasi. Yakiitafuta hatari!. Yakimsaka adui!.

Kule porini alipokuwa David bado alikuwa anaangaza huku na kule. Lakini hakuambua lolote, michirizi ya damu ilikuwa imeishia palepale, na kutengeneza kidimbwi kidogo cha damu.

"Nini kilitokea hapa?. Mbona hii michirizi ya damu hakuna inapoelekea. Kwanini michirizi hii iishe ghafla. Au walipofika hapa waligundua kwamba hii michirizi ya damu itakuwa tatizo kwao?. Na kuamua kuidhibiti?" David alikuwa anajiuliza mwenyewe, lakini hakuwa na jibu hata moja.

Alikata shauri kuwasubiri kina Daniel Mwaseba watafute majibu kwa pamoja.

***

Martin Hisia, mwanaume mwenye Hisia zake nd'o alikuwa anaingia Vikindu. Kichwani mwake alikuwa anawaza kitu kimoja tu, kuhakikisha mpenzi wake, Felisia, anakuwa salama.

Leo hii aliamini usahihi wa hisia zake tangu siku ya kwanza aliyokutana ba Felisia. Alikumbuka kila kitu kilivyotokea siku ile katika klabu ya Bilcanas. Lakini kwa sasa hakujari hayo. Alikuwa anataka kitu kimoja tu, kuhakikisha Felisia anakuwa salama. Alitambua sana matokeo ya kitendo cha hatari alichokifanya Felisia. Huku akijua kwamba adhabu yake ni moja tu endapo atastukiwa.
Kifo!!

Na yeye hakutaka hata kidogo Felisia afe kwa namna yoyote ile.

Felisia Nyenyembe. Mwanamke waliyekutana kama bahati tu katika klabu ya usiku ya Bilcanas...

Siku hiyo Martin alikuwa ametoka kukamilisha misheni moja ya hatari sana. Misheni ambayo iliisha kwa mafanikio makubwa sana kwake, na kuhakikisha bilioni sita zilizoibwa kutoka katika benki ya wakulima zinarudi salama katika benki hiyo. Huku watu wote waliohusika na wizi katika benki hiyo wakitiwa katika mikono ya dola.

Siku hiyo jioni ndipo alipoenda katika klabu ya muziki ya Bilcanas kujipongeza kwa kazi kubwa aliyoifanya.

Baada ya kunywa sana pombe, ndipo alipoamua kuingia sehemu ya kuchezea naye aoneshe ujuzi wake katika fani hiyo. Wimbo uliokuwa unapigwa ni 'Fool again' wa kundi la muziki la West life.

Martin aliucheza haswa wimbo huo, akichagizwa na pombe zilizokuwa zimejaa pomoni kichwani mwake.

"Tunaweza cheza pamoja?" Sauti ya kike nyembamba ilipenya katika masikio yake. Martin alimwangalia mmiliki wa sauti hiyo aliyekuwa mbele yake.

Blauzi nyeupe yenye kung'aa, suruali ya jeans fupi iliyombana vyema na viatu vya mchuchumio kwa chini vilikuwa ni vitu alivyovitazama kwa haraka.

"Huyu ni mtoto haswa" Alijisemea kimoyomoyo.

Martin hakuwa na nguvu za kukataa ombi la binti huyo, ingawa hisia zake zilimwambia kwamba hakuwa mtu mzuri.

Kwa mara ya kwanza katika maisha yake Martin Hisia alipingana na Hisia zake. Hisia zilizoanza tangu akiwa mtoto mdogo na kuaminiwa na kila mtu.

Ilikuwa Martin alikuwa akihisi kitu basi lazima kitatokea. Na hili lilimfanya jina la babaye mzazi liondoke na kuitwa Martin Hisia.

"Usijari dada. Twaweza cheza, tena hadi majogoo ukitakaa" Martin alisema kwa sauti ya kilevi.

Na DJ alibadili wimbo. Sasa ulikuwa unaimbwa wimbo wa 'My love' toka katika kundi hilohilo la West life.

DJ kama alijua kuweka wimbo huo. Maana penzi jipya ndio lilikuwa linazaliwa mjini. Hadi wimbo laini wa 'My love' ulipoisha Martin alikuwa ameshadadisi kila kitu. Sasa alikuwa analijua jina la yule binti, mahali anapoishi na kazi anayoifanya hapa mjini. Yote hayo waliulizana wakati wimbo wa 'My love' ukikita katika spika za klabu ya Bilcanas.

Martin alihisi lakini hakutilia maanan. Pombe, ukichanganya na hisia kali za mapenzi basi zilimfanya aendelee kuzidharau hisia zake. Hakujua kwamba yule alikuwa ni wakala wa Imma Ogbo aliyetumwa kwake kwa kazi maalum.

Tangu siku hiyo Felisia akawa mpenzi wa Martin Hisia, huku akipeleka taarifa mbalimbali za Martin kwa Imma Ogbo.

Katika moyo wa Martin Hisia alitokea kumpenda sana Felisia. Felisia alikuwa mwanamke aliyekamilika haswa. Wa kupendwa na kila mtu. Hata wewe...

Ukiacha weupe wake wa asili sio wa kuchanganya na carotone na maji ya diana, sura nzuri na shepu ya kufa mtu, Felisia alikuwa na ya zaidi. Alikuwa mpishi mzuri sana jikoni. Alikuwa anajua kupika kila aina ya chakula na kuwa kitamu sana. Pia Felisia alikuwa malaya sana kitandani. Alikuwa anaweza kufanya mitindo ya kila aina ya mapenzi tena kwa umahiri wa ajabu sana. Huku akilia kwa milio ya kushangaza. Hili la kitandani lilimmaliza sana Martin. Akawa hana uthubutu wa kumuacha hata kidogo ingawa alikuwa anamtilia shaka mara kadhaa kwa matendo yake.

Siku moja, usiku wa manane wakiwa wamelala kitandani simu ya Felisia iliita. Felisia aliamka na kumwangalia Martin kama amelala. Martin alijifanya ametopea usingizini.
Kumbe haikuwa hivyo..
Martin alikuwa anasikia kila kitu!

Felisia alinyanyuka pale kitandani taratibu. Kuhakikisha hamuamshi Martin, alielekea bafuni na simu yake mkononi. Martin naye aliamka kitandani na kumfuata kwa nyuma Felisia hukohuko bafuni.

Kule bafuni Felisia alipiga simu yake kwa Imma Ogbo. Akawa anaongea kwa sauti ndogo sana. Martin alijaribu sana kusikiliza akiwa nje ya mlango wa bafu, lakini aliambulia maneno mawili tu.

Misheni na Daniel Mwaseba..

Felisia alikata simu, na kuelekea chumbani. Alimkuta Martin akiwa amelala vilevile. Akaamini kwamba maongezi yake na Imma Ogbo hayajasikiwa na kiumbe chochote kile hapa duniani.

Kumbe haikuwa hivyo.

Martin kichwa kilimuuma kwa mawazo, huku akiwa anatamani amfahamu huyo aliyekuwa anaongea na Felisia usiku wa manane. Hisia za wivu zilimtawala zaidi ya hisia za kipelelezi. Maneno mawili aliyoyasikia kwenye simu yalikuwa ya muhimu sana kwake kuyafanyia kazi, lakini alipotezea. Mapenzi yalikuwa yamemlevya. Akadharau kazi.

Asuhuhi kulikucha. Kabla hawajatoka kitandani wakafanya mapenzi ya asubuhi. Wenyewe walikuwa wanaita 'morning glory'.

Kwa utundu alioufanya Felisia asubuhi hii, yalimsahaulisha kila kitu Martin Hisia.
Kila siku mwanamke huyu alikuwa mpya kitandani, alikuwa anakatika kiajabu huku akitoa kilio mithili ya ndege chiriku.

Alivyotoka hapo alimpikia chai yenye viungo mbalimbali na chapati zilizokaangwa kikike. Huku pembeni kukiwa na supu ya kuku iliyopikwa ikapikika. Hapo alikuwa tayari katoka kuogeshwa kwa maji ya moto na kusuguliwa kila sehemu ya mwili wake.

Unafikiri hata alikumbuka simu ya jana usiku?

Alichokumbuka ni kumweka kifaa kidogo maalum mithili ya punje ya mchele, katikati ya nywele za Felisia zilizosukwa kwa mtindo wa yebo fasta, kifaa hiko kikimwezesha Martin kujua uelekeo wa Felisia..

Yote hayo ulikuwa ni wivu tu..

***

Imma Ogbo na Dr Louis walikuwa katika nyumba ya balozi wa Nigeria hapa nchini. Walitoka kule Vikindu kwa mtindo wa ajabu wakisaidiwa na balozi Agdir na kusalimika kutiwa mkononi na wakina Daniel Mwaseba.

Felisia yeye, alikuwa katika stoo ndogo iliyopo ndani ya nyumba hiyo, akiwa uchi wa mnyama huku akiwa amefungwa kamba ngumu mikononi na miguuni.

Mwili mzima ukiwa umevimba huku akiwa anabubujikwa na damu sehemu kadhaa. Jicho lake moja lilikiwa likiwa limetolewa na kubaki shimo baya na la kutisha! huku mkono wake wake wa kulia akiwa hana kidole cha mwisho. Kilikuwa kimekatwa!
Hiyo ilikuwa kazi ya Imma Ogbo katika kumfanya Felisia aseme alikuwa anampigia nani simu kule chooni.

Lakini pamoja na mateso yote hayo bado Felisia alikuwa mgumu kufunguka, huku akidai alienda bafuni kujisaidia sio kupiga simu. Utetezi huo haukuingia hata kidogo katika kichwa cha Imma Ogbo na kumuahidi atarejea tena!
Na hapo ndipo atasema hata asivyoulizwa.

Je nini kitatokea?

Lako Jicho.

Hadithi hii itapatikana yote kwa njia ya whatsapp siku ya jumanne kwa sh 3000 tu.

Una mana gani mkuu. Siku ya jumanne ? Ndo siku hiyo tu wanaotaka kununua wanaweza fanya hivyo au and if that is true, kwa namba gani malipo Hayo yanafanyika na jina gani linatumika kwenye hiyo namba ya malipo. Muhimu kwa kuwa sisi wa nje tunawatuma watu watulipie huko lakini Hadithi tunataka tutumiwe sisi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom